DOKEZO Ufisadi wa kutisha ndani ya CHADEMA: Namba ya simu iliyokuwa ikitumika kukusanya pesa za “Join the Chain” siyo ya Chama!

DOKEZO Ufisadi wa kutisha ndani ya CHADEMA: Namba ya simu iliyokuwa ikitumika kukusanya pesa za “Join the Chain” siyo ya Chama!

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Aisee, nani angeweza kujua kuwa ndani ya CHADEMA kuna ujambazi wa kutisha wa fedha za wanachama na wananchi. Hiki kinyang'anyiro cha kugombea uenyekiti wa chama umeibua mambo mazito na kukianika wazi hiki chama kuwa ndani yake kuna mijizi kwelikweli.

Leo katika press conference ya Lema, aliyekuwa mjumbe wa Technical team ya chama aliyehusika kusajili namba ya chama iliyotumika kwa ajili ya kukusanyia pesa za Join the Chain, akijibu swali la mwandishi wa habari ameuhabarisha umma kuwa kulikuwa na namba nyingine ambayo wananchi walipewa wachangie lakini namba hiyo siyo ya chama na haijulikani ni ya nani.

Bwana huyo akasema kuwa namba rasmi ya chama ilikuwa ni 0744446969 ambayo mzungumzaji aliisajili yeye kwa niaba ya chama na alama za vidole ni za kwake, na hii namba ilisajiliwa pindi viongozi wa CHADEMA wamefungwa na wakawa wanatafuta namna ya kuwatoa. Lakini cha ajabu zilitengenezwa vest za kuhimiza watu kuchangia kupitia "join the chain" zenye namba ambayo "kiujanja" ni tofauti na hiyo yaani 0744444969.

Akasema kuwa yeye binafsi haijui namba hiyo nyingine, na akawaomba waandishi wamuulize katibu Mkuu wa CHADEAM aeleze hiyo namba nyingine ilikujajekujaje kwenye kukusanya michango.

Hili suala zima la Join the Chain mwanzoni lilianza vizuri sana likiwa na lengo la kukifanya chama kiweze kujiendesha lakini tangu Mbowe alivyotoka gerezani, zoezi likahujumiwa na hata mapato na matumizi ya hilo zoezi yalikuwa hayatolewi wazi mpaka jana Mnyika alivyoeleza pesa zilizopatikana.

Kabla ya Mnyika kuzielezea hizo pesa bwana Wenje alidai eti hizo pesa zilikuwa zinakusanywa na akina Lissu na Lema ili kumpindua Mbowe kitu ambacho Mnyika alikipinga kwa ufafanuzi wake wa jana. Hata hivyo maswali bado yangalipo katika ishu nzima ya pesa za join the Chain hasa kuhusiana na namba hiyo feki ya kukusanyia pesa
 
Yote haya kayataka dalali Wenje, na kila akifanya press anamuachia shuzi Sultan. Ngoja Msigwa naye sijui atakuja na bomb 💣 gani kesho,walahi hawa watamuua mwamba huu moto siyo wa kitoto

FB_IMG_1737030202896.jpg
FB_IMG_1737030098799.jpg
 
Lema ndio amejua leo kwamba hiyo namba haikuwa ya Chama?

Sasa wanapotaka chama na hela hawana si watauwana kwa kula michango ya wananchi..

Fikiria hii ni collection ua mil 100 tu, pesa ndogo kuliko mauzo ya duka la mangi...Wakipewa Biiiz si kila siku itafanyika press
 
Lema ndio amejua leo kwamba hiyo namba haikuwa ya Chama?

Sasa wanapotaka chama na hela hawana si watauwana kwa kula michango ya wananchi..

Fikiria hii ni collection ua mil 100 tu, pesa ndogo kuliko mauzo ya duka la mangi...Wakipewa Biiiz si kila siku itafanyika press
Muulize Mbowe alivyotoka gerezani ilikuwaje akasajili namba nyingine ya kukusanya michango?
Lema ana busara sana, kaamua kumlinda Mbowe ili angalau abaki na kiheshima kidogo.
 
Muulize Mbowe alivyotoka gerezani ilikuwaje akasajili namba nyingine ya kukusanya michango?
Lema ana busara sana, kaamua kumlinda Mbowe ili angalau abaki na kiheshima kidogo.
Amlinde wa Nini,

Kama ni ufisadi waseme..

Hivyo vihela anavyozungumzia nilijua ni bilion mia huko..

Hizo si Mauzo duka la mangi Mbagala..
 
Lema ndio amejua leo kwamba hiyo namba haikuwa ya Chama?

Sasa wanapotaka chama na hela hawana si watauwana kwa kula michango ya wananchi..

Fikiria hii ni collection ua mil 100 tu, pesa ndogo kuliko mauzo ya duka la mangi...Wakipewa Biiiz si kila siku itafanyika press
Mkuu, ilikuwa siri ya kambi hadi pale wengi walipoanza kung'oa koki wakidai si wao wamehusika.

Sijui unaelewa kweli? Yaani safari moja imeanzisha nyingine.
 
Amlinde wa Nini,

Kama ni ufisadi waseme..

Hivyo vihela anavyozungumzia nilijua ni bilion mia huko..

Hizo si Mauzo duka la mangi Mbagala..
Mkuu, kwani idadi kamili unaijua? Nani atakwambia alikusanya 10B???
 
Lema kailieleza vizuri sana hili jambo la join the chain.

Tatizo lilianza pale Mwenyekiti aliptoka jela na kisha yeye akawa ndiye yuko incharge ya operation ya join the chain. Hapo ndipo kizungumkuti kilipoanza
 
Lema ndio amejua leo kwamba hiyo namba haikuwa ya Chama?

Sasa wanapotaka chama na hela hawana si watauwana kwa kula michango ya wananchi..

Fikiria hii ni collection ua mil 100 tu, pesa ndogo kuliko mauzo ya duka la mangi...Wakipewa Biiiz si kila siku itafanyika press
Ndo hivyo, huo mzigo atakufa nao mmiliki wa Saccos
 
Mkuu, ilikuwa siri ya kambi hadi pale wengi walipoanza kung'oa koki wakidai si wao wamehusika.

Sijui unaelewa kweli? Yaani safari moja imeanzisha nyingine.

..wamtaje tu mhusika.

..majizi yote Chadema yaondoke.

..watu wamekuwa vilema, wengine wamekufa, halafu kuna watu wanapiga hela?
 
Aisee, nani angeweza kujua kuwa ndani ya CHADEMA kuna ujambazi wa kutisha wa fedha za wanachama na wananchi. Hiki kinyang'anyiro cha kugombea uenyekiti wa chama umeibua mambo mazito na kukianika wazi hiki chama kuwa ndani yake kuna mijizi kwelikweli.

Leo katika press conference ya Lema, aliyekuwa mjumbe wa Technical team ya chama aliyehusika kusajili namba ya chama iliyotumika kwa ajili ya kukusanyia pesa za Join the Chain, akijibu swali la mwandishi wa habari ameuhabarisha umma kuwa kulikuwa na namba nyingine ambayo wananchi walipewa wachangie lakini namba hiyo siyo ya chama na haijulikani ni ya nani.

Bwana huyo akasema kuwa namba rasmi ya chama ilikuwa ni 0744446969 ambayo mzungumzaji aliisajili yeye kwa niaba ya chama na alama za vidole ni za kwake, na hii namba ilisajiliwa pindi viongozi wa CHADEMA wamefungwa na wakawa wanatafuta namna ya kuwatoa. Lakini cha ajabu zilitengenezwa vest za kuhimiza watu kuchangia kupitia "join the chain" zenye namba ambayo "kiujanja" ni tofauti na hiyo yaani 0744444969.

Akasema kuwa yeye binafsi haijui namba hiyo nyingine, na akawaomba waandishi wamuulize katibu Mkuu wa CHADEAM aeleze hiyo namba nyingine ilikujajekujaje kwenye kukusanya michango.

Hili suala zima la Join the Chain mwanzoni lilianza vizuri sana likiwa na lengo la kukifanya chama kiweze kujiendesha lakini tangu Mbowe alivyotoka gerezani, zoezi likahujumiwa na hata mapato na matumizi ya hilo zoezi yalikuwa hayatolewi wazi mpaka jana Mnyika alivyoeleza pesa zilizopatikana.

Kabla ya Mnyika kuzielezea hizo pesa bwana Wenje alidai eti hizo pesa zilikuwa zinakusanywa na akina Lissu na Lema ili kumpindua Mbowe kitu ambacho Mnyika alikipinga kwa ufafanuzi wake wa jana. Hata hivyo maswali bado yangalipo katika ishu nzima ya pesa za join the Chain hasa kuhusiana na namba hiyo feki ya kukusanyia pesa
Hebu tuwekee ile namba feki!! Hii uliyoweka inasoma CHADEMA HQ
 
Back
Top Bottom