Ufugaji wa kisasa wa Nyuki: Faida, Utaalam na Masoko

Ufugaji wa kisasa wa Nyuki: Faida, Utaalam na Masoko

Kuna njia mbalimbali za kuwavutia nyuki waweze kuinhabit mizinga mipya. Njia kubwa kabisa na ya kisasa ambayo mimi huwa natumia ni matumizi ya nta (wax sheets). Hapa huwa naweka wax sheets kwenye vibao vya ndani ya mizinga yangu na harufu yake huwavutia nyuki na kuwafanya waingie kwenye mzinga. Njia nyingine ambayo pia husaidia nyuki waingie kwenye mzinga ni matumizi ya majani ya mchai chai (unapaka kidogo sehemu ya mlango wa mzinga na ndani ya mzinga). Pia unaweza tumia "majani ya kufukuzia mbu" na kuyasmear ndani ya mzinga, harufu yake inavutia sana nyuki.

Kama unakuwa na mzinga mingi na ufugaji wa kisasa, ukipata makundi kwenye mzinga michache unaweza kufanya colony division na kumultiply makundi yako kwenye mizinga mingine. Mfano, kama una mizinga kumi na umepata nyuki kwenye mitano, colony division itakusaidia kupata makundi kwenye mizinga mitano liliyobaki ndani ya muda mfupi. Hii njia inahitaji utaalam kidogo ila ni rahisi na haina gharama.
mkuu shukrani kwa elimu unayotoa, mimi napenda kujua kwa wastani mzinga mmoja unaweza ukavuna mara ngapi kwa mwaka kwa eneo lenye vegetation kwa wingi?
 
Ndugu,

Ufugaji nyuki kisasa una mambo mengi ya kuzingatia, kwa uchache mambo hayo ni:
  • Uchaguzi bora wa eneo la kufugia nyuki - liwe na chakula kwa ajili ya nyuki (ingawaje nyuki hujitafutia wenyewe chakula hata maeneo ya jirani), kuwe na maji (ya asili au ya kuwekwa), liwe na utulivu, liwe mbali na makazi ya watu na liwe linafikika.
  • Aina ya mizinga ya kutumia - Ili uwe ufugaji wa kisasa, mizinga ya kutumia pia iwe ya kisasa. Kuna aina nyingi ya mzinga kama traditional hives, modern top bar hives na commercial hives. Bei hutofautiana kulingana na eneo ulilopo na ubora. Kwa eneo nilipo mzinga wa modern top bar ni kati ya Tshs 60k na 70k, commercial beehive ni kati ya Tshs 120k na 150k. Ushauri wangu kwako kama uwezo unaruhusu nunua commercial beehives kwani inakuhakikishia kumantain makundi ya nyuki na mavuno ni mara nyingi kwa mwaka (utapata asali nyingi) na hutoa asali bora.
  • Vitendea kazi vya kisasa - hapa nazungumzia vifaa vya ukaguzi, mashine ya uvunaji pamoja na vifaa vya kuhifadhia asali. Mfano mavazi ya kujikinga na nyuki, smoker, mashine ya kurina asali n.k. Cha kuzingatia hapa ni kuwa na vifaa vya kutosha na bora.
  • Usimamizi wa shamba na nyuki wenyewe - hapa ndio wafugaji wengi wanakwama. Wengi hudhani nyuki hawahitaji ukaguzi. Ukweli ni kwamba usimamizi bora wa shamba na ukaguzi wa angalau mara 1 - 2 kwa mwezi husaidia kujua hali ya mzinga, maendeleo ya kundi, lini utarajie kuvuna n.k. Pia husaidia kuondoa wadudu waharibifu wa nyuki na vihatarishi vingine.
Nafikiri nimekusaidia kidogo mahali pa kuanzia ufugaji wako wa kisasa wa nyuki. Mimi pia ni mfugaji, kwa msaada zaidi tuwasiliane.
 
Mheshimuwa ninahitaji kujua ni miti au maua ya aina gani ni mizuri kupanda kwenye shamba la nyuki
 
Ni vema pia kuwa na Kalenda ya ufugaji nyuki ( Beekeeping Calendar ) ya eneo husika , hiyo itakuwa mwongozo mzuri wa kuongoza kifanyike na kwa Wakati upi, mf. Kuandaa eneo la manzuki,kuandaa mizinga, kuambika, usimamizi na ukaguzi wa mizinga,kurina na kuchakata makao ya nyuki n.k
 
Mkuu,

Kiukweli kuna aina nyingi sana za miti na maua / mimea yenye maua yapendayo na nyuki. Upandaji pia unategemea sana mipango yako ya muda mfupi na muda mrefu katika mradi wako wa ufugaji nyuki, pia eneo ulipo.

Naomba nitaje michache na rahisi kupanda;

Miti: Miembe, Milonge, mizambarau, michungwa, mipera, papai, mi-passion, minazi, miparachichi, kahawa, karafuu, eucalypts n.k

Maua: Aina zote, ikiwemo maua pori kama bidens pilosa (manata nguo)....

Mazao: Alizeti (pollen kwa wingi), mbaazi, mahindi, karanga, carrots, maharage, mpunga n.k


Kibiashara, uchaguzi wako wa miti / mazao ya kupanda shambani ufanyike kwa kuangalia mimea ambayo utakuwa unavuna na ikawa sehemu ya kipato.



Mheshimuwa ninahitaji kujua ni miti au maua ya aina gani ni mizuri kupanda kwenye shamba la nyuki
 
Real G,

Kuna tofauti kubwa sana kati ya mzinga na mzinga kwenye uvunaji kutegemea na aina / design hata kama yote itawekwa kwenye eneo moja lenye mazingira sawa.

Kujibu swali lako vizuri, frequency ya uvunaji kwa mzinga kama eneo lina vegetation kwa wingi linaweza kuwa zaidi ya mara sita kwa mwaka (yaani unaweza kuuvuna mzinga mmoja zaidi ya mara sita kwa mwaka). Lakini, wingi wa vegetation kwenye eneo haudetermine sana frequency ya uvunaji bali "rotational flowering" ya vegetation husika. Mfano, ukiwa na eneo lenye alizeti kwa wingi na hiyo alizeti inatoa maua mara mbili tu kwa mwaka, tafsiri yake ni utavuna mara mbili. Lakini ukiwa na eneo lenye alizeti kwa wingi, milonge, maembe, maua mbali mbali n.k basi utavuna mara nyingi.

Niliwahi kumtembelea mfugaji nyuki anayefanya rotational farming na kuhakikisha kila kipindi cha mwaka ana maua, kila mzinga anavuna mara 15 kwa mwaka.


mkuu shukrani kwa elimu unayotoa, mimi napenda kujua kwa wastani mzinga mmoja unaweza ukavuna mara ngapi kwa mwaka kwa eneo lenye vegetation kwa wingi?
 
Karibu sana mkuu.

Kwa sasa ninafanya hizi shughuli za ufugaji nyuki Saadan, Morogoro na Kisarawe.


Salute kwako Allan,nimejifunza mengi sana...kama hutojali kutuambia Shamba la nyuki wako lilipo angalau siku moja tukatembeleana.
 
Real G,

Kuna tofauti kubwa sana kati ya mzinga na mzinga kwenye uvunaji kutegemea na aina / design hata kama yote itawekwa kwenye eneo moja lenye mazingira sawa.

Kujibu swali lako vizuri, frequency ya uvunaji kwa mzinga kama eneo lina vegetation kwa wingi linaweza kuwa zaidi ya mara sita kwa mwaka (yaani unaweza kuuvuna mzinga mmoja zaidi ya mara sita kwa mwaka). Lakini, wingi wa vegetation kwenye eneo haudetermine sana frequency ya uvunaji bali "rotational flowering" ya vegetation husika. Mfano, ukiwa na eneo lenye alizeti kwa wingi na hiyo alizeti inatoa maua mara mbili tu kwa mwaka, tafsiri yake ni utavuna mara mbili. Lakini ukiwa na eneo lenye alizeti kwa wingi, milonge, maembe, maua mbali mbali n.k basi utavuna mara nyingi.

Niliwahi kumtembelea mfugaji nyuki anayefanya rotational farming na kuhakikisha kila kipindi cha mwaka ana maua, kila mzinga anavuna mara 15 kwa mwaka.
mkuu shukrani tena, soko la asali kwa sasa hivi likoje, maana uzi ni wa tangu mwaka 2013, soko linaweza kuwa limebadilika
maana changamoto kubwa kwenye kilimo ni soko la uhakika
 
Mkuu,

Kiukweli kuna aina nyingi sana za miti na maua / mimea yenye maua yapendayo na nyuki. Upandaji pia unategemea sana mipango yako ya muda mfupi na muda mrefu katika mradi wako wa ufugaji nyuki, pia eneo ulipo.

Naomba nitaje michache na rahisi kupanda;

Miti: Miembe, Milonge, mizambarau, michungwa, mipera, papai, mi-passion, minazi, miparachichi, kahawa, karafuu, eucalypts n.k

Maua: Aina zote, ikiwemo maua pori kama bidens pilosa (manata nguo)....

Mazao: Alizeti (pollen kwa wingi), mbaazi, mahindi, karanga, carrots, maharage, mpunga n.k


Kibiashara, uchaguzi wako wa miti / mazao ya kupanda shambani ufanyike kwa kuangalia mimea ambayo utakuwa unavuna na ikawa sehemu ya kipato.
Salute
 
Nataka Kujiunga na Chuo cha Nyuki Tabora!Nina Ufaulu wa Geography=B,Biology=D,English=C!
A-level:
Geography=E,English=S!
Naweza Kupokelewa?
Na Ada Zake Zikoje?
Kama Kuna Mtu Mwenye Mawasiliano Naomba Anipe!
 
ninataka kuanzisha ufugaji wa nyuki ninawaomba mwenye uzoefu busness plan anisaidie
 
Shamba la kufugia nyuki, linapaswa kuwa na ukubwa gani, mf: ekari moja inakaa mizinga mingapi!? Halafu kwenye mzinga unajuaje kama asali imejaa?
 
Idadi ya mizinga inategemea upatikanaji wa maua na maji. Hivyo ni very critical. Kama hivyo sio tatizo, unaweza kuwa na mizinga.kati ya 100-200 kutegemeana na jinsi unavyoitundika. Njia ya vichanja inabeba mizinga.mingi zaidi.

Kuhusu kujua kama mizinga.imejaa, ni suala la calendar.
 
JE UNATAKA KUFUGA NYUKI KWA NJIA YA KISASA NA KIBIASHARA ZAIDI

THE HIVE LTD TANZANIA WANASHUGHULIKA NA MAMBO HAYA

MPIGIE MENEJA MIRADI BW. Nicas Mbeikya 0653 930 391 au 0653242627 Kwa maelezo ya kupatikana kwa soko,mizinga na vifaa vyake vya kisasaaa.
 

Attachments

  • 13932736_1167722699965536_1271352412995484818_n.jpg
    13932736_1167722699965536_1271352412995484818_n.jpg
    53 KB · Views: 264
  • 14022270_1167718709965935_861364356177463643_n.jpg
    14022270_1167718709965935_861364356177463643_n.jpg
    125.4 KB · Views: 297
  • 14045772_1167719939965812_4200483841395713158_n.jpg
    14045772_1167719939965812_4200483841395713158_n.jpg
    118.3 KB · Views: 291
  • 14046035_1167720653299074_2808127119109415584_n.jpg
    14046035_1167720653299074_2808127119109415584_n.jpg
    109.6 KB · Views: 276
Back
Top Bottom