Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Ndugu. Kwanza tatizo lako ni Dogo Sana. Kuangalia watu wanasemaje. Pili kukata tamaa.

Yakupasa ujue kwamba biashara ni vita, na yakupasa uishinde.

Watanzania wengi wamekuwa na kasumba ya kukosoa bidhaa hasa za watanzania wenzao na kuthamini bidhaa za nje.

Mimi ni mfanyabiashara. Na ninazungumza kitu ninachojikua kwa tabia mbaya walionao baadhi ya watanzania, ni kudhara vya ndani na kutukuza vya nje.

Chamsingi.
Nikutokukata tamaa. Chapakazi kwa bidii Endelea na Ufugaji wako uo huo na kuku Hao Ao.

Fungua macho mikoani, maana hakuna mafanikio bila changa moto.

Changa moto zipo ili ufanikiwe zaidi. Kama hapo mtaani kwako wana yakataa mayai yako, inua Macho Kwingine Pata hasira ya kutafuta Masoko.

Nenda kwenye Mahotel. Vioski vya chips. Nenda madukani, Fungua Duka la kuuza Mayai kwa Bei ya Jumla.

Panuka kimawazo, usiazie Eneo 1 la hao wanao kukatisha Tamaa.

Huwezi kufanikiwa kwa kuangalia watu wanasemaje au wanakusemeaje biashara yako. Fuata Ndoto zako Ona picha ya Kupanuka na kuongezeka sana.

Ukisha Jenga Picha Hii hakika hakuna mtu atakukwamisha katika safari yako ya mafanikio.

Ona unaudumia Africa Nzima Mayai na Kuku wa kienyeji, alafu kila siku jiambie wewe ni mfanyabiashara Mkubwa ulimwenguni.

Alafu anza kutenda mambo yako kwa ufanisi na kutokukatishwa tamaa na mtu Awaye yote.
 
Wana Jf,

Kuna maandiko mengi JF ya ufugaji Kuku wa Kienyeji! Nawasilisha kwenu wadau wa JF mbinu ambazo kwa mikono yangu nimezitumia kutatua changamoto za kuku wa kienyeji! Nimeandika kuwalenga wajasiliamali ambao hawana nguvu kifedha kujenga mabanda kisasa, mashine kutotolesha vifaranga, kutibu magonjwa wala kujenga wigo (fence) n,k. Naomba mzijue mbinu hizi nisije kufa nazo, huu ni mchango wangu kwenu watanzania wenzangu wale ambao mtakuwa hamjawahi kuzisikia mbinu hizi. Mbinu hizi baadhi nilisoma vitabuni nikazijaribu na kuziboresha kwa mazingira yangu duni! Mbinu zingine niliziona kwa wakulima duni kama mimi nikazitumia na kuleta mafanikio makubwa, mbinu zingine nilizigundua mwenyewe na nikafanikiwa sana. Hizi mbinu hazijafanyiwa utafiti rasmi lakini nimeweza kufanikiwa kuwa na kundi kubwa la kuku kwa haraka sana kupitia ujanja huu!!

Mdau wa JF nakualika utembelee uzi huu mara kwa mara kila upatapo fursa ili uweze kufuatilia simulizi yangu maana itakwenda kwa vipande vipande. Mnakaribishwa kuchangia uzoefu wenu ili tuboreke zaidi.

Mbinu hizi zitagusia zaidi: Utotoreshaji vifaranga vingi kwa mara moja bila kutumia mashine! Ukuzaji wa vifaranga vingi kwa njia rahisi na kwa haraka zaidi, ulinzi wa kuku dhidi ya wanyama maadui, kudhibiti kuku wasizurule, magonjwa niliyofanikiwa kuyadhibiti, ujenzi wa vibanda wenye kukidhi mahitaji mbali mbali. Ni utaalamu nilioupata kwa gharama kubwa na mahangaiko ya muda mrefu, nauleta kwenu ili sote tuendelee kukua pamoja kiujasilia mali.

Stay tuned and keep on visiting this thread!!


===============
UPDATE
===============



Mkubwa tunakusubiria bila shaka kabisa Kubota; kwani hakika ni na imani ni mbinu mbadala kabisa unakuja nayo mkubwa wangu! Hii uzi ninaisave left kabisa nikitegemea newz toka kwako! Asante sana! Hapa ndiyo Jf jamani!






Safari yangu ilianza baada ya kukutana na mhamasishaji aliyenitia chachu kwamba 10 x10 x 10 you become a millionea! Kwamba ukianza na kuku 10 kila mmoja akazaa 10 na hao watoto na mama zao wakazaa kila mmoja 10 unakuwa millionea! Wakubwa kuongea ni rahisi utekelezaji ukawa mgumu sana! Changamoto kuu aipatayo mfugaji wa kuku wa kienyeji ni kuzalisha vifaranga wengi na kuweza kuwakuza! Bila hivyo kundi haliwezi kukua na kukupa kipato cha uhakika!

Safari ya ufugaji niliianza kwa kununua mitetea 30 na jogoo watatu! Ilibidi nisubiri muda hadi kuku waanze kutaga! Muda ukafika kuku wakaanza kutaga kwa fujo sana! Nilikuwa na banda moja tu ambamo kuku wote walikuwa wakilala humo. Nilitengeneza viota vingi kwa ajili ya kuku kutagia. Asubuhi nilikuwa nawafungulia! Changamoto nilizoanza kupambana nazo kwanza kama mjuavyo kuku tofauti walikuwa wanataga kwenye kiota kimoja! Ilipofika wakati wa kuatamia ikawa kila kwenye kiota kimoja kuna kuku kadhaa wamebanana wanaatamia! Hali hii haipaswi kutokea kwani kuku mmoja anaweza kuwa amejilundikia mayai mengi ambayo hawezi kuyapajoto la kutosha na kuku mwingine anakuwa amekaa kando tu hana hata yai moja. Hii ilibadilika ikawa kero kubwa! Nilijua utotoaji unaweza kuathirika sana!

Ili utotoreshe vifaranga vingi kwa wakati mmoja badala ya kutumia incubator, tumia hao hao kuku. Wakianza kutaga kila siku okota mayai na kuyahifadhi mahali salama ili kuku wasiyatie joto! Kuku wengi wanapotaga kwa pamoja hufikia wakati mayai huishatumboni unakuta wamelala kwenye viota wakiwa wameatamia mayai yaliyopo au udongo tu! Kuku anaekuwa amefikia kuatamia utamjua kwani ukimshitua haondoki kwenye kiota. Kuku anaetaga ukimshitua hukimbia! Kwa hiyo kama nimepanga kutotolesha vifaranga 100 kwa mara moja nikishagundua kuwa kuna kuku 8 wameanza kuonesha dalili ya kuatamia hapo husubiri usiku ninawawekea mayai amabayo nilikuwa nimeyahifadhi. Ambapo mimi huwekea kila kuku mayai 15. Kwa hiyo kuku 8 hufanya jumla ya mayai 120. Kwa kuwa banda langu ni hilo moja tu kuku wengine wanaoendelea kutaga walikuwa wanaendelea kutagia kwenye viota ambavyo kuku wengine walikuwa wanaatamia! Hali hii ilikuwa inaleta tabu sana kwani ilikuwa si rahisi kutambua mayai mapya na yenye siku nyingi. Kuondoa shida hii nilinunua MARKER PEN (rangi yoyote) na siku ya kuwawekea mayai kuku ili waatamie niliyachora mduara kuzunguka yai ili iwe rahisi kuyatambua mayai mapya. Huo mchoro hauwatishi kuku na hakuna dosari yoyote. Kwa hiyo kila siku jioni ninapokuja kuokota mayai yaliyotagwa nilikuwa pia nakagua kila kiota cha kuku walioatamia na kuondoa mayai mapya. Kumnyenyua kuku anaeatamia na kuondoa yai haileti shida yoyote!

Kuku akifikia wakati wa kuatamia ukamnyima mayai hawa wanatabia kuendelea kung'ang'ania kuatamia, hapo ilibidi kutengeneza JELA! Watu wengine wanambinu tofauti kumwachisha kuku asiatamie! Mbinu ya kumtia kuku stress inafanya kazi nzuri sana! Jela inaweza kuwa ni Tega, au Box kubwa au chumba kidogo kilichopo. Ukimfungia kuku JELA bila maji wala chakula kwa kutwa mbili siku ukimfungulia akili yake huwa ni kutafuta chakula tu hakumbuki kurudi kwenye kiota! Njia hii ilifanikiwa sana na ilifanya kuendesha shughuri zangu bila bughudha! Kuna wakati JELA ilikuwa na kuku kibao hivyo unapaswa kutengeneza kibanda cha JELA. Hawa kuku wakitoka JELA hutaga mapema sana amabapo bila hivyo wangekuwa wanaatamia. Pia kuku wakishaatamia kwa muda wa siku 10 nilikuwa nayapima mayai ili kubaini kama kuna mayai yasiyoweza kuanguliwa! Ni rahisi sana kama una Tochi! Ukimulika yai Kwa kulizungushia vidole kiganjani kama ni yai zima linakuwa na giza kama ni yai bovu linapitisha mwanga kama yai lililotagwa siku hiyo! Jinsi ya kuzungushia vidole yai, tengeneza duara kwa vidole vyako na dole gumba kisha pachika yai katikati ya duara ili mwanga wa tochi upenye kwenye yai! Kwahiyo unaweka tochi inayowaka chini ya yai na hii ifanyike gizani au ndani ya chumba chenye mwaga mdogo. Kadri ya yai linavyokaribia kutotolewa ukilimulika huwa na giza zaidi! Ukimulika mayai toa mayai yasiyoweza kutotolewa maana hayo hutumia joto la Mama bure!

Ndugu zangu wana JF naendelea kuelezea utotoleshaji bado sijamaliza hebu niwarushie hii kwanza maana nimeona nimechelewesha kuwakilisha na nimewaudhi, poleni, mwenzenu nilikuwa nahangaika kufukia tanuru la mkaa nimekuta limefunguka! Si mnajua maisha jamani!
 
Kiukweli kumufuga kuku wa kienyeji kwa njia ya commercial feeding utegemee kupata faida ni ngumu kidogo,
Nimefuga sana hao kuku, ili upate faida nzur lazima ufuge sehemu ambayo una eneo la kutosha kiasi kwamba muda mwingi utawafungulia wajitafutie wenyewe chakula.
Kwa njia hio pia inaboresha ubora wa mayai utakayopata.
Ukimufungia ndani muda wote kwa kuwalisha vyakula vya kisasa uwezekano wa kupata mayai yenye uharisia wa ukienyeji inakuwa mdogo sana.
 
Kiukweli kumufuga kuku wa kienyeji kwa njia ya commercial feeding utegemee kupata faida ni ngumu kidogo,
Nimefuga sana hao kuku, ili upate faida nzur lazima ufuge sehemu ambayo una eneo la kutosha kiasi kwamba muda mwingi utawafungulia wajitafutie wenyewe chakula.
Kwa njia hio pia inaboresha ubora wa mayai utakayopata.
Ukimufungia ndani muda wote kwa kuwalisha vyakula vya kisasa uwezekano wa kupata mayai yenye uharisia wa ukienyeji inakuwa mdogo sana.
Mpwa wangu anawafuga shambani, wako huru kutembea na pia gharama ya chakula si sawa na kuwafungia, wanajitafutia ingawa anawawekea pumba zilizochanganywa na unga wa dagaa pamoja na maji ya kunywa asubuhi wakiwa wanatoka na jioni wakirudi. Matatizo ni vicheche na mwewe. Lakini bado anaona faida.
 
Habari za saizi wapendwa, Mimi ni mtanzania mwenzenu niliyebahatika kukua katika FAMILIA ya kiufugaji,(KUKU WA KIENYEJI).
Tuna kampuni yetu iitwayo SHITINDI POUTRY FARM AND HATCHER.

Hii kampuni inajihusisha hasa katika...

  • UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI.
  • UTOTOLESHAJI WA MAYAI.
  • UUZAJI WA INCUBATOR(MASHINE ZA KUTOTOLESHEA VIFARANGA).
  • UUZAJI WA VIFARANGA.
Zaidi tunatoa fursa za kutoa SEMINA za bure kabisa bila malipo ya aina yeyote kwa vikundi yva ujasiliamali na kwa mtu mmoja mmoja pia.


Zaidi ya yote madhumuni yangu ya kuja humu na kuandika jambo hili ni kwamba watu wengi na watanzania wenzangu jambo hili liwafikie, nimeiona watu wengi wakifanikiwa kupitia semina zinazoendelea mara kwa mara bilia kukoma.


kwa maelezo na mawasiliano tembelea blog yetu SHITINDI POULTRY FARM AND HATCHER

au kwa simu namba
  • +255 713 071 701
img-20160816-wa0084-jpg.384003
img-20160817-wa0021-jpg.384005
 
malalamiko ya wateja wako kuhusu mayai yako baadhi yana hoja. kuku wa kienyeji kwa mjini tatizo kubwa ni eneo. wanahitaji eneo kubwa wawe huru na kupata vyakula asili, kama wadudu, majani nk. kuwafungia ndani bila kuwalisha 'formula', uasili wake hupungua. la ukubwa na rangi ya mayai si hoja. ukubwa na rangi ya kuku huamua ukubwa na rangi ya yai. kuna kuku asili wakubwa hutaga mayai makubwa mpaka gm 56, ukubwa ambao ni yaidi ya wastani wa mayai ya kuku wa kisasa. waelimishe wateja na kuongeya mbinu za ulishaji.
 
Ahsante kwa wazo,mimi nauza kwa 12,000 nilichojifunza kwako suala la bei.Nadhani natakiwa nipunguze bei kidogo ili niwe kwenye mzunguko wa haraka.

Sio lzm kupunguza,mm nauza hivyo kwa sababu wateja wangu wengi wanakwenda kuuza lkn wale wachache wa kula nawauzia 12,000.
 
Habari za saizi wapendwa, Mimi ni mtanzania mwenzenu niliyebahatika kukua katika FAMILIA ya kiufugaji,(KUKU WA KIENYEJI).
Tuna kampuni yetu iitwayo SHITINDI POUTRY FARM AND HATCHER.

Hii kampuni inajihusisha hasa katika...

  • UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI.
  • UTOTOLESHAJI WA MAYAI.
  • UUZAJI WA INCUBATOR(MASHINE ZA KUTOTOLESHEA VIFARANGA).
  • UUZAJI WA VIFARANGA.
Zaidi tunatoa fursa za kutoa SEMINA za bure kabisa bila malipo ya aina yeyote kwa vikundi yva ujasiliamali na kwa mtu mmoja mmoja pia.


Zaidi ya yote madhumuni yangu ya kuja humu na kuandika jambo hili ni kwamba watu wengi na watanzania wenzangu jambo hili liwafikie, nimeiona watu wengi wakifanikiwa kupitia semina zinazoendelea mara kwa mara bilia kukoma.


kwa maelezo na mawasiliano tembelea blog yetu SHITINDI POULTRY FARM AND HATCHER

au kwa simu namba
  • +255 713 071 701
img-20160816-wa0084-jpg.384003
img-20160817-wa0021-jpg.384005
Unapatikana wapi unatotoa kwa gharama gani kwa trei bei ya hiyo incubator pia
 
Morogoro wateja wengi sana mpaka mayai yanashindwa kukidhi uhitaji. Wengi wanataka yenye jogoo kwa ajili ya kutotolesha
 
Back
Top Bottom