Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Naamini soko lipo, pigana Kaka! Jiingize kwenye magroup, post Facebook, zunguka kwenye maofisi. Utafanikiwa, kama ni kweli ukishindwa njoo niuzie. Nina mpango wa kuweka kuku wa kienyeji 600
yah that is what am doing now bro, na faida ipo sana tu.
 
trey natotolesha sh 10000 tu, pia napatikana Kimara Temboni Dar es salaam..
karibu sana
Ahsantee kwa taaarifa mkuu ila nimepitia source yako vitu vingi umeelezea juu juu tu me nadhani ungetoa ufafanuzi hata hapa kuhusu gharama za Yale matangazo yako kule kuhusu hizo heater incubator vifaranga na mengine
 
Ahsantee kwa taaarifa mkuu ila nimepitia source yako vitu vingi umeelezea juu juu tu me nadhani ungetoa ufafanuzi hata hapa kuhusu gharama za Yale matangazo yako kule kuhusu hizo heater incubator vifaranga na mengine


MASHINE ziko za viwango tofauti tofauti, mfano kuna mashine ya kuanzia mayai 48, 88, 144 ,264, 432, 528 ,726, 1056 , 2112.. na zingine za viwango tofauti..

samahani mara nyingi huwa swala la bei hatuweki mitandaoni kwa sababu tunatoa mizigo yetu nje, na kama unajua huwa dolla unabadilika unaweza leo ukaweka kiasi fulani na dolla ikapanda au kushuka.


Na kuhusu VIFARANGA , Kifaranga mmoja ni shilingi 1500/=( huyo ni wa siku ya kwanza).
Na pi vyote vilivyoandikwa hapo na kule kwenye Blog vipo, ukija kujifunza unaonyeshwa kwa vitendo.
 
Ahsantee kwa ufafanuzi uluosimama kuhusu kutotolesha mayai ya siku saba inawezekana kupata vifaranga vingapi kwa trei moja na bei ya incubator hiyo ya mayai 48 maana bado mtaji mdogo kwa kweli ningekua naku-pm ila bado sina uzoefu na hii app
 
Umekata tamaa mapema mno.
Huwezi kuongeza idadi ya kuku halafu ukawa unauza hayo mayai mikoa jirani?
 


Mkuu pole kwa changamoto za ufugaji, nisingependa kukukatisha tamaa ila ni vyema nikupe ushauri utakaokusaidia kama ukiamua kuufanyia kazi. binafsi niko katika sekta ya ufugaji na nimejipatia uzoefu mkubwa kidogo tangu nianze hii shughuli. ukweli uliomchungu ni kwamba, kibiashara, hasa ya mayai na nyama, kuku wa kienyeji pure hawalipi. kwanini nasema hawalipi.

Biashara ya Mayai.
kwa asili ya kuku wa kienyeji,huwa wanatabia ya utagaji mara nyingi ni siku kwa siku 10 mfululizo, utamiaji -siku 21, na uleaji wa vifaranga -siku 50-60. hii inampelekea kwa kuku mmoja kuweza kutaga wastani wa mayai 35-50 kwa mwaka. Idadi hii ya mayai haina tija kibiashara kwani kuku mmoja anaweza kukuzalishia tray 1 mpka mbili kasoro pekee kwa mwaka ambayo kwa bei ya soko si Zaidi ya shilingi za kitanzania 20,000 tu kwa mwaka.

Changamoto kwenye soko la mayai ya kienyeji. nilianza kusambaza mayai ya kienyeji kwenye supermarkets miaka mitatu iliyopita.. Haya mayai yako fertilized, (yamerutubishwa na majogoo) hivyo storage yake ni ngumu Zaidi ukilinganisha na mayai ya kuku wa kisasa kwa vile hayana mbbegu. nilipata sana tatizo la mayai kuharibika hasa yasipotoka ndani ya kipindi cha week moja au Zaidi kutegemeana na hali ya joto.

Mwiaho ni gharama za mayai husika, bei ya mayai ya kienyeji iko juu ukilinganisha na gharama za mayai ya kuku wa kisasa. soko kubwa la mayai ni pamoja na vibanda vya chips, migahawa na hoteli. hawa wanauhitaji mkubwa sana wa mayai na soko liko juu muda wote wa mwaka. Soko la mayai ya kienyeji lipo Zaidi kwenye households. (soko la familia) hasa kwa vigezo vya kuzingatia afya Zaidi. Soko hili la familia sio kubwa, ni soko dogo na mara nyingi hutumia tray moja kwa kipindi cha wiki mbili au Zaidi. kwa mzalishaji mkubwa wa mayai ya kienyeji ni lazma awe na soko la familia pana Zaidi kuweza kupata faida ndogo, nasema faida ndogo maana ili kuzalisha mayai tray kumi (mayai 300) kwa siku, utahitaji Zaidi ya matetea 700 mpaka 1000 ya kienyeji pure. idadi ambayo ni kubwa kuliko idadi ya mayai yanayopatikana.

Biashara ya Nyama.
Na declare interest, mimi pia ni msambazaji wa nyama ya kuku wa kienyeji, hivyo naongea kwa uzoefu, na niko tayari kukosolewa. Pamoja na kufugwa katika misingi ya kijani (organic rearing), iyo pekee haitoshi kumpa thamani inayostahili huyu kuku sokoni. Thamani ya kuku sokoni ni uzito alio nao, organic component ni jambo la ziada lililo muhimu pia. tunavyo jadili bei ya soko ya kuku huyu ni lazma tumliganishe na gharama za bidhaa pinzani zilizoko sokoni. Haitawezekana kumuuza kuku mwenye kilo moja au pungufu kwa bei ambayo tunashawishiana humu ya 15000-20000 wakati bidhaa pinzani (nyama nyeupe) kama samaki sato toka mwanza wanauzwakwa 7500 kwa kilo, au kitimoto, numa ya ngombe ambazo nazo kilo ni 7500-8000. Hivyo basi. hoja yangu hapa ni uzito wa kuku husika. Ukiachana na jamii chache za kuku wa kienyeji (kuchi etc) wenye uzito mzuri, majority ya kuku pure wa asili/kienyeji kwa majogoo huwa na pungufu ya kilo moja na nusu. Kumbuka uzito wa kuku hawa sio kwasababu ya malisho duni, laah hasha, bali ni kutokana na vinasaba (genes) vyao kuwafanya kuwa na maumbo madogo madogo. kwa kuku wa aina hii, sitegemei mfugaji kama atafanikiwa kuwapeleka sokoni na kuweza kupata bei nzuri toka kwa mlaji wa mwisho.

Nini kifanyike.
ili ufugaji uwe wenye tija kibiashara ufanyike, ni lazma wafugaji tuamke na kuachana na ufugaji wa kuku hawa asilia kwani hawana tija. Nikisema hivi simaanishi watu waache kufuga, hapana, ila wafuge aina /breeds za kuku zenye tija kibiashara. Kuku pekee unaoweza kuwafuga kwa mbinu za kienyeji na bado wakakuletea mfugaji faida nzuri kibiashara, ni kuku aina ya chotara (cross breeds). hii ni aina ya kuku wenye sifa zote za ukienyeji kwa misingi ya mbinu zao za kuwafuga pamoja na namna walivyo nauwezo wa kuhimili mazingira hasa ya vijijini. Kuna aina mbalimbali ya kuku hawa ikiwamo Black/ white australorps, kroiller, Rhodes island red, red hamshire, Sussex etc. Hawa ni kuku ambao wanaserve purpose zote za mayai na za nyama. Mfano kuku aina ya black/white australorps wao wanauwezo wa kutaga mpaka mayai 250 kwa mwaka, tofauti na wa kienyeji, mayai ya kuku hawa huwa makubwa na yenye kasha jeupe na kiini cha njano kama utawafuga kwenye mazingira na mbinu asilia (za kienyeji). Ukilinganisha uwezo wa utagaji wa kuku hawa utagundua utagaji wao ni Zaidi ya asilimia 500% ukilinganisha na ule wa kienyeji pure. Idadi hii ya mayai toka kwa kuku mmoja kwa mwaka, anaweza kumwezesha mfugaji kuzalisha mayai kwa wingi na kushusha Zaidi bei ya mazao yake (mayai) kuwa chini kuweza kuliteka soko kwa urahisi Zaidi. Kumbuka, bei ya juu ya mayai ya kienyeji ni kwaajili ya kulipia gharama kubwa za utunzaji wa kuku huyu ilihali utagaji wake ni hafifu.

Pili, kuku hawa wana nyama nyingi Zaidi kuliko hawa wa kienyeji kwa majogoo hufikia mpaka uzito wa kilo 3-3.5. huku matetea hufikia kilo 2-2.5 na huwa na nyama nzuri, iliyokomaa vyema na yenye ladha. kwa uzito huu kwa majogoo, kuku hawa uuzwa kwa bei ya 20,000 - 25,000 wakiwa hai. bei ambayoni kwa mujibu wa bei ya soko kwa makadirio ya shilingi 8,000 kwa kilo kwa nyama nyeupe.

Mapungufu.
Pamoja na ubora wa kuku hawa katika ufugaji wa kibiashara, kuku hawa pia wanachangamoto mbali mbali ikiwemo kutokuwa na uwezo wa kutamia. Pamoja na hii kuwa changamoto pia ni fursa kwani kwa yeye kutotamia kunamwongezea nafasi ya yeye kuendelea kutaga mara nyingi Zaidi bila kupumzika. hivyo changamoto hii ni faida kwa mfugaji anaelenga kufuga kwa tija. kwa vile mayai haya huwa yamerutubishwa na majogoo, nirahisi kwa mfugaji kuongeza idadi ya kuku kwa kupitia kutotolesha kwa mshine za kuangulia vifaranga au kumpa kuku mwingine ayatamie kwa niaba.

kwa ushauri Zaidi kuhusu shughuli za ufugaji, tuwasiliane kwa namba 0755815174. pia pata fursa kusoma ya Makala mbali na utaalamu kutoka kwenye mtandao wetu www.backyard.co.tz
 
Ahsante mkuu kwa maelezo yako mazuri,tupo pamoja.
 
ufugaji ni hatua ya kwanza na masoko ni hatua ya pili, jitahidi kutafuta soko utapata tu wateja wanayoyaelewa
 
Kuku wa kienyeji ni yule anayejitafutia mwenyewe....kuku wa kienyeji ukimfungia ndani na kumpa chakula na madawa huyo ni "wakisasa"
Asante kwa comment yenye akili: Watu wengi hawaelewi hili na wanadanganywa sana sana. Wanadhani kuku wa kienyeji ni yule anayetaga mayai madogo na ya rangi fulani. Lakini ukweli ni kwamba, kuku anakuwa wa kienyeji au wa kisasa kutokana na anavyofugwa. Wa kienyeji akifungiwa kama wa kisasa huyo ni wa kisasa. Wa kisasa akiachiwa ajitafutie huyo ni wa kienyeji.
 
Sidhani kama hii ndio tafsiri halisi ya kuku wa kienyeji na wa kisasa... mfumo wa ufugaji haibadilishi maana ya kuku wa kienyeji..hii ni sawa na kusema ukienda ulaya unakua mzungu
 
HII QUATATION IMENIGUSA lakini pia somo lako nimelielewa vema mkuu,popote uliko nakupa hongera
 

Ebana GAZETI shukran sana elimu imefika na kuelewa hakuna mwisho kwa yaliobakia ni juhudi binafsi pale mtu atapohitaji kuendelea zaidi ila DIRA tumeiona...
 
nataka nianzi upugaji huo wa kuku ila cjafagamu aina ya banda zuri la kufugia
 
Ahsantee kwa ufafanuzi uluosimama kuhusu kutotolesha mayai ya siku saba inawezekana kupata vifaranga vingapi kwa trei moja na bei ya incubator hiyo ya mayai 48 maana bado mtaji mdogo kwa kweli ningekua naku-pm ila bado sina uzoefu na hii app
hamna shida hata hapa tunaweza kuwasiliana vizuri na ple kwa late reply.. kuhusuhiyo mashine ya mayai 48 unaweza kupiga sim namba 0754 467423 na ukapata ufafanuzi na maelez mazuri,,.
na kuhusu mayai kutoka mangapi kwa tray inategemea ratio ya matetea yako na mjogoo bandani pia na hayo mayai kukaa muda mrefu kwenye joto, ila kwa uzoefu wangu huwa trey ina mayai 30, lakini yakiaribika huwa ni matatu au manne, kwa hiyo unaweza kupata vifaranga kwenye 25 mpaka 27.
NB:UKIZINGATIA RATIO YA MAJOGO NA MATETEA NA MAYAI KUTOKAA SANA MAHALI PENTE JOTO.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…