Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Swala la masoko ya mayai na broiler . na pia kama soko likiwa halitoshelez inakuaje? naomba ushauri wako katika hili.
 
Kutatua tatizo hilo ni vyema kufuga kuku aina ya CROWLER ambao unaweza kuwafungulia wakajiokotea kama kuku wa kienyeji (ikiwa kama una eneo la kutosha) na ukawaongezea na chakula.

Pia wanakua haraka na kutaga mayai yakutosha kwa mwaka .
 
Nauza kuku wa kienyej mbegu za malaw ..sh 1000..,wanataga sana nipigie 0743158800
 
Nina uzoefu mdogo katika hili. Nilienda nikanunua majike 10 ya kienyeji, kwa nyakati tofauti nikawafungia bandani kwa kuwapa mchanganyo wa pumba, mashudu, dagaa na vingine kama vinavyoelezwa kwenye majalida ya Ufugaji.

Kuna jike aliyekuwa akiwa anataga, na aliendelea kwa siku 5 kisha akaacha, wengine kama 4 hivi wakaanza kutaga, akitaga Leo anakaa wiki anataga tena, hali hiyo ilidumu kwa miezi mitatu, hakuna wa kutaga mfululizo hata kwa siku 2 wala wa kuhatamia.

Nikapata hasira nikawafungulia, kwa maana nikawaacha wazurure, wiki moja tangu kuwaachia huru, yule alikuja anataga most ezi mitatu iliyopita akaanza kutaga mfululizo, imepita wiki moja tena wengine watano wakaanza kutaga kwa pamoja na mfululizo na wakahatamia na kutotoa!

Ushauri wa kuwapa majani na kuwaachia nje ndani ya uzio japo kwa jioni au Masaa machache kwa siku ili kufanya mazoezi inaweza kukusaidia.
 
Nafikiri anaendelea kuomba akimaliza atauliza hilo swali, na sisi tutaendelea kusubiri swali, au wewe Hamorapa nini?
 
Wapendwa habari pasaka mim niko poa ila nimekuja kwenu kuomba msaada wa mawazo na ufundi kama kunamtu anajua kutengeneza mashine ya kutotoreshea vifaranga vya kuku bila kutumia umeme anisaidie na ikiwezekana anifundishe jinsi ya kuvitunza bila kuwa na kuku wa kuviatamia
 
Habari ndugu zangu, ninaomba kufaham kama suala la kufuga kuku wa kienyeji kwa muda mfupi kama wanavyofugwa kuku wa kisasa wa nyama linawezekana?. Nahitaji kufuga kuku wa kienyeji kuanzia wakiwa wana siku moja na wakifika wiki 6 au 8 nianze kuwauza. Tafadhali kwa yoyote mwenye uwelewa naomba anisaidie
 
Kuku wa kiwnyeji? Unawafahamu vizuri lakini, labda ujaribu chotara.
 
habari wana jamvi! kwanza nimshukuru Mungu kwa neema zake pia nitoe shukrani kwa @Kubota,@chasha poultry farmer na wadau wote walio wahi changia uzi wa mh.kubota ule wa ''zijue mbinu zangu za ufugaji wa kuku'' kwani ni uzi ulio nihamasisha kwa kiasi kikubwa hadi kujitosa kwenye ufugaji wa kuku lakini pia na mimi nikawa mbunifu kidogo nikaongezea na ujanja wangu ni kabuni mbinu zangu.

Nimeona Leo nieleze mbinu zangu ninazo tumia kufuga kuku wa kienyeji pia nitaeleza faida na hasara za mbinu hizi.

Lengo la Uzi huu ni kutoka elimu ya ufugaji wa kuku wa kienyeji pia kujadili mapungufu/kuboresha mahali ambapo unaona panahitaji maboresho ya mbinu hizi.Karibu sana.

kwanza,nina mabanda manne,pamoja na uzio wa chicken wire.Banda la kwanza ni kwaajiri ya kukuzia vifaranga wadogo kabisa,banda la pili ni lakukuzia vifaranga wenye umri wa kuanzia wiki nne(mwezi ),banda la tatu ni kwaajiri ya kuku wazazi na wengine ,banda la nne ni kwaajiri ya kutenga kuku wagonjwa na uzio wa chicken wire ni kwaajiri ya kufungia kuku wa kuanzia miezi miwili nitaelezea mbele kwanini nimetenganisha hivyo.mabanda yote ni yale yenye sifa za banda bora.

pili,nina kuku wazazi ambao ni mitetea ya kienyeji halisi/pure na majogoo mbegu nzuri ya chotara uwiano wao ni mitetea kumi kwa jogoo moja.hawa kuku wazazi wanalala kwenye lile banda la kuku wazazi ambalo ndani yake nimetengeneza na viota vya kutagia mayai.gharama ya kulisha hawa kuku wazazi inatokana na kuuza mayai yanayobaki baada ya kuchagua mayai yanayofaa kulaliwa na kuku nitakao wateua kulalia nitaelezea mbele namna ninavyo zalisha vifaranga.

tatu,hapa ni namna ninavyo zalisha vifanga,lishe na namna ninavyo tunza na kuhudumia makundi yangu ya kuku kiujumla.

naona bimkubwa ananiita hapa kupata lunch ya pasaka.nitarudi baadae kidogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…