Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Nitaweka picha hapa baadae, majuzi tu hapa nimenyoosha mikono kuhusu biashara ya ufugaji wa kuku wa kienyeji! Nilinunua majike ambayo tayari yanataga. nikajengea mabanda safi, hadi mlinzi nikaweka, wakataga mayai yanawateja sana, mengine wakaatamishia nilikuwa kwenye mpango wa kununua incubator, magonjwa nkayadhibiti hakuna vifo cha kuku vya kutisha!

Wamefika kuku 200+ ikaja changamoto ya CHAKULA.....kuku wanakula hadi mshahara wangu mapato kiduchuuu! Kwa ufupi nimekula HASARA.....sijuhi haya mabanda yangu mazuri nifugie nini! Kuku wa kienyeji sio wa kuchezea, naomba wafugaji wazoefu waniambie wanawalisha nini ....

Ungenunua pumba nyingi ukamix na mashudu kidg plus multivitamins . ...kuku kienyeji sio kwa biashara aisee..
 
Ungenunua pumba nyingi ukamix na mashudu kidg plus multivitamins . ...kuku kienyeji sio kwa biashara aisee..
Hayo yote nimefanya, pumba nilianza nanunua kwa bei ya sh. 300@kg sasa pumba ni 400 hadi 420shs, mashudu pia premix niliweka....kumbuka hapa kwangu hapajawa na msongamano wa watu hivyo kama sio msimu wa kilimo nilikuwa nawaacha wajitafutie chakula...ila wanakula hao! kibaya zaidi kuku wa kieneyji utagaji wao sijuhi unategemea nini maana leo atage apitishe siku mbili, mwingine akitaga mayai 5 anataka kuatamia...nikasema nifuge chotara jamaa yangu akasema nao wa ankula na ubaya wao mayai yao watu wanayachukulia kama ni ya kisasa!
 
Watu wengi hapa naona ni bendera fata upepo sooooo negative nna uwakika 99% ata kufuga hawajawahi ama iyo elimu tu ya ufugaji hawana siku wazee kuna chanjo za ayo maradhi ukiwa serious kuku mbn unatoboa tu, maradhi yatakayosumbua ni ya kawaida tu ambayo yanatibika poa tu, njoeni field mpambane acheni uwoga kila kazi ina changamoto zake muhimu ni kujifunza kupambana kukomaa na kuwa serious, si unajua unachotaka basi kila sekunde ishi hiyo sababu eroo
 
Mbona hata 1000 (buku) unatajirika? Ingia sokoni majira ya jioni au alfajiri bei ya bidhaa iko chini.

DAY1
Nunua Tikiti zima la 1000 ( buku), nenda sehemu yenye uhitaji katakata pata vipande 5. Jero isevu.

500× 5= 2500

DAY2
Nunua matikiti 2 kwa 2000 na mia tano itumie tu.

Katakata tena safari hii utakuwa na vipande 10.

500× 10 = Sh. 5000

DAY3
Nenda nunua tikiti 5.

Hapa kila tikiti 1 vipande 5 ×5 = 25
500×25 =7,500

DAY 4
Tikiti 8 kwa nikimaanisha 7500 + 500 uliyosevu DAY1 = 8000.

This time tikiti 8 utapata vipande 40
40 × 500 = 20,000

DAY 5
Tikiti 20
Utapata vipande 100

100×500= 50,000

DAY6
Tikiti 50
Utapata vipande 5 × tikiti 50= 250
Vipande 250 × 500 = 75,000

DAY 7
Nenda kachukue tikiti 75 na fungua kijiwe kingine weka kijana afanye internship.

Hapo utakuwa na vipande 375 ukiuza kwa bei yetu 500 unapata Sh. 187500/=

Wiki inayofuata kuwa constant tu kwamba

Kila siku unachukua tikiti 100 za bukubuku kwa Sh. 100,000. Ile 87,500 isevu.

Tikiti 100 kwa wastani wetu wa kila tikiti moja vipande 5 na unauza kwa 500.

Kila siku utakuwa unauza vipande 500 unapata Sh. 250,000/=.

250,000 × siku 30 (mwezi1) = 7,500,000

7,500,000 × mara miezi 12= 90,000,000

Kipato chako kwa mwaka kitakuwa Sh. 90,000,0000.

Huna mtaji wa 1000 (Buku!) Unasubiri nini kuanza.
Motivational soeakers bana.
 
Asante mkuu, sikuwepo nilikua kwenye mihangaiko nimerudi ndo nimekuta barua ya wito na namba ya simu.
Nimempigia uyo afisa ananiambia niende kesho asubuhi na laki tatu za faini, nimemuuliza kosa ni nini eti sheria za manispaa zinataka niwe na kibali cha ufugaji nimemuuliza kuwa Rais alisema nikiwa na mtaji wa chini ya milioni nne na nimenunua kitambulisho nisisumbuliwe inakuaje tena? akasema we fika ofisini tuyajenge ni kama anatengeneza mazingira ya rushwa.
Tanzania ya viwanda kesho asubuhi badala niamke mapema kwenda kujenga nchi naenda kuitikia wito wa kufuga kuku bila kibali.
Kwa hiyo ilikuwaje?
 
Kwa hiyo ilikuwaje?
Asubuhi walinipigia simu tuonane sehemu nyingine nje ya ofisi ya kata nilipofika wakataka niwapoze ili issue ife pale nisifikishwe ofisini wakanihakikishia kuwa nikifika kule ni faini tu hakuna maelezo nikagoma kutoa hata mia wakampigia simu bibi afya wakaniambia niende kwake wao wakasepa.

Nikaenda kwa bibi afya ni mdada wa makamo kidogo na ni muungwana kweli kweli alinipa elimu nzuri ni namna gani naweza kufuga bila usumbufu especially kwenye kuhifadhi mbolea na hapo alitilia mkazo sana kuhusu tetanus.
Baada ya kuongea mambo mawili matatu tukagundua kuwa tumekulia sehemu moja na mama yake aliwahi kufanya kazi na baba yangu kabla hajahamishwa kwenye miaka ya 90 basi kesi ikaishia hapo hapo nikaondoka kuendelea na ujenzi wa taifa.
 
Asubuhi walinipigia simu tuonane sehemu nyingine nje ya ofisi ya kata nilipofika wakataka niwapoze ili issue ife pale nisifikishwe ofisini wakanihakikishia kuwa nikifika kule ni faini tu hakuna maelezo nikagoma kutoa hata mia wakampigia simu bibi afya wakaniambia niende kwake wao wakasepa.

Nikaenda kwa bibi afya ni mdada wa makamo kidogo na ni muungwana kweli kweli alinipa elimu nzuri ni namna gani naweza kufuga bila usumbufu especially kwenye kuhifadhi mbolea na hapo alitilia mkazo sana kuhusu tetanus.
Baada ya kuongea mambo mawili matatu tukagundua kuwa tumekulia sehemu moja na mama yake aliwahi kufanya kazi na baba yangu kabla hajahamishwa kwenye miaka ya 90 basi kesi ikaishia hapo hapo nikaondoka kuendelea na ujenzi wa taifa.
Hukumueleza habari za wale WAPUUZI?
 
Nitaweka picha hapa baadae, majuzi tu hapa nimenyoosha mikono kuhusu biashara ya ufugaji wa kuku wa kienyeji! Nilinunua majike ambayo tayari yanataga. nikajengea mabanda safi, hadi mlinzi nikaweka, wakataga mayai yanawateja sana, mengine wakaatamishia nilikuwa kwenye mpango wa kununua incubator, magonjwa nkayadhibiti hakuna vifo cha kuku vya kutisha!

Wamefika kuku 200+ ikaja changamoto ya CHAKULA.....kuku wanakula hadi mshahara wangu mapato kiduchuuu! Kwa ufupi nimekula HASARA.....sijuhi haya mabanda yangu mazuri nifugie nini! Kuku wa kienyeji sio wa kuchezea, naomba wafugaji wazoefu waniambie wanawalisha nini ....
Nikodishie hayo mabanda au tuingie ubia tufanye kazi
0718151415
 
Hizi mada ni tamu mnooo zikiwa kwenye maandiko kama hivi yani utajiri unauona nje nje...
 
Kuku was kienyeji so mchezo kwenye ufugaji,fuga 3 tu uone mtiti wake,wakianza taga,huyu anataga hapa akimaliza na mwenzie anataga kwenye mayai ya mwenzie.
 
Ingekuwaga rahisi hivi mimi ningetajirika toka niko primary. Niliendaga fresh nikafikisha kuku 50+
Kilichokuja kutokea ni hadithi.
 
Back
Top Bottom