Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Mm naomba ushauri ,nimenunua kuku wa mayai 26 size ya miezi mitatu cha kushangaza nimewaweka ktk chumba ambacho muna godoro ukutani leo nimeamka wamelitoboatoboa wanakula je hakuna madhara yeyote?

wataalamu wanakuja na jibu rasmi lakini kwa kuchangia tu inaonekana hawakuwa na maji ya kutosha
 
Asante Mkuu kwa mchanganuo huu, Je wewe umeshaanza kufuga au unaelezea nadharia? Katika uwekezaji au biashara yeyote kuna changamoto zake, kwa hiyo usijekuingia katika uwekezaji au biashara kwa mahesabu haya; mambo yakienda tofauti unaweza kukata tamaa. Unaweza kuona ufugaji wa kuku wa kienyeji ni rahisi, lakini siyo rahisi kama wengi wamavyofikiria (kwa uzoefu wangu). Nami nilikuwa na mahesabu kama haya nikanunua kuku zaidi ya 35, lakini zilianza changamoto za magonjwa na walibaki wachache sana. Unaweza kusema tumia dawa. Kwa sasa kuku wa kienyeji nimeweka kwa ajili ya matumizi binafsi lakini kwa biashara niliamua kufuga kuku wa nyama (broiler). Nimetoa comment kutokana na uzoefu niliopata lakini wengine wanaweza kuwa na uzoefu wa tofauti na michango zaidi inaweza kutolewa.

Ifikapo mwezi Jan 2013 nitaweka hesabu za wazi na mchanganuo mzima wa ufugaji wa kuku wa kienyeji unavyolipa + changamoto zilizopo.
 
je juna mtu anjua kuhusu kuku aina ya KROIRER? ni high bread ya local chicken and muzungu wametoka kenya,

nimeamua kuanza na kuku 10 tu, na kesho ndo nawapokea na maandalizi yako kwenye gear no 5, na haya yote ni juu ya kusoma saaana huu mtandao wa ujasiriamali ndani ya jamii forum, nimeamua kuyavulia woga maji na kujitumbukiza mzimamzima
its ssaid that FAILURE IS PART OF SUCCESS

umeishaanza kuwafuga au? tupe changamoto za hao kuku ziko vipi?
 
Ufugaji wa kuku wa kienyeji ni mzuri na wenye manufaa sana. Unauwezo wa kumnyanyua mtu mwenye kipato cha kuanzia Tsh. 6,000 hadi10,000/= (nunua kuku mmoja) na kuwa milionea. Ni kuwa serious, determined, mvumilivu na mwenye kutumia ufugaji wa kisasa. Tatizo la wengi vijijini they don't take it seriously, wanafuga tu kimtindo kama supplement ya kazi zao za mashambani au ufugaji wa ng'ombe. Tatizo lingine kubwa kwao ni Kideri/mdondo (New castle disease), hawachanji kuku dhidi ya gonjwa hili plus magonjwa mengine. Serikali ingewasadia kuchanja kuku dhidi ya kideri ingewasaidia sana. Dawa yenyewe ni cheap sana, by 2012 tube ya kuchanja kuku 400 ilikuwa Tsh. 5,000. Ukiwa kasehemu kakuwafanya wawe huru kidogo hata mijini au pembezoni mwa miji unaweza wafuga. Lakini siku hizi kuna watu wanawafungia ndani kama wa kisasa either kwa kukosa enough space au ili kufuga wengi zaidi kibiashara.
 
Haya ni moja kati ya mazuri ya mapinduzi ya teknolojia, natamani wadogo zangu wa sekondari na vyuo vikuu wangekuwa wanatumia mitandao ya kijamii positively kama uzi huu na mingine kama hii. Bravo jf, bravo wadau wote.
 
ndio mzee nilishaanza ninao 14 wana miezi 3.5 na wanaendlela vizuri, maana wakiwa wadogo ndo shida lakini wakifikisha miezi2 hapo inakuwa lahisi, kwani hawana tofauti na wakienyeji ila wao wanakua halaka sana na wanpata uzito wakutosha
 
Mimi jukwaa la siasa halina faida kwangu.,napenda sana hili jukwaa wa wajasiriamali,bsness &econmy.
I like it,yani mtu unapat vitu vya kukukomboa,afu hili jukwaa watu wapo serious na kazi,halina waropokaji na wazozaji kama kuuule politics forum.
Umesema vema mkuu, WaTz tumekuwa watu wa porojo na mabishano ya kisiasa yasiyo hata na tija ktk maisha yetu ya kila siku. Ukienda JUKWAA LA SIASA utakuta ni Chadema na CCM tu! Comments za kizushi hadi inachefua, kisa anatetea chama chake. Huku hata mm naona kwanifaa atiii...
 
Nakushauri ufuge wa kisasa - Layers. wa kienyeji it takes time na faida si kubwa vile unavyodhani - nitafute nikupe ushauri wa bure - meanwhile angalia kazi hii hapa

attachment.php


Hawa wako 900, wanatoa Tray 24 kila siku kila Tray 5000- Chakula chao ni kilo 125 approx Tshs 55,000/-

Mtaji wa kuanzia unahitaji kuwa na not less than 6m before you start production. Kama unataka mchakato mzima sema nitakutumia database yangu.
nami najipanga ili niingie kwenye hii biashara kichwa kichwa nimeshachoka kutumwa.
 
Habari ya majukumu wakuu! Wandugu nilikuwa naomba kujuzwa kuhusu masoko ya kuku wa kienyeji hapa Dar, nahitaji kuwauza kuku kuanzia 100
 
Habari ya majukumu wakuu! Wandugu nilikuwa naomba kujuzwa kuhusu masoko ya kuku wa kienyeji hapa Dar, nahitaji kuwauza kuku kuanzia 100
karibu mkuu soko lipo, unatoka nao wapi, lini umewachanja Kideri/mdondo? Kuna wadau wamekuwa wakiulizia hata hapa JF sana hawa kuku hivyo sio lazima ummuzie mmoja wote ila tupo tunaotaka 20, 50 nk. Jieleza majogoo wangapi na tetea wangapi na bei ya jumla shilingi na utawafikishia wapi kwa hapa Dar tukutafute, cc faiz jr, wazo langu
 
karibu mkuu soko lipo, unatoka nao wapi, lini umewachanja Kideri/mdondo? Kuna wadau wamekuwa wakiulizia hata hapa JF sana hawa kuku hivyo sio lazima ummuzie mmoja wote ila tupo tunaotaka 20, 50 nk. Jieleza majogoo wangapi na tetea wangapi na bei ya jumla shilingi na utawafikishia wapi kwa hapa Dar tukutafute, cc faizajr, wazo langu

'kweli kabisa maelezo yake hayajitoshelezi hata kidogo kwa kweli...'
 
'kweli kabisa maelezo yake hayajitoshelezi hata kidogo kwa kweli...'
ni kweli watu tunakimbia kuku wanaouzwa masokoni sababu mtu akiona wagonjwa anaamua kuuza. Pia wengi hawapatiwi chanjo ikitokea wamesafirishwa toka mbali wanafika wanaanza kuumwa aidha kudhoofu na hali ya hewa au kuambukizwa njiani. Tunategemea hapa JF itakuwa gulio la wasomi kutokana na darasa zinazotolewa hapa na kupigiwa mfano.
 
Elezea vzr mkuu wanapatikana wapi na kwa bei gani? Na kama wamepata chanjo

Sent from my BlackBerry 9790 using JamiiForums
 
karibu mkuu soko lipo, unatoka nao wapi, lini umewachanja Kideri/mdondo? Kuna wadau wamekuwa wakiulizia hata hapa JF sana hawa kuku hivyo sio lazima ummuzie mmoja wote ila tupo tunaotaka 20, 50 nk. Jieleza majogoo wangapi na tetea wangapi na bei ya jumla shilingi na utawafikishia wapi kwa hapa Dar tukutafute, cc faiz jr, wazo langu

kweli kabsa mama joe atutajie atapatikana wapi au atuwekee mawasiliano
 
Huyu mdau analeta masikhara kwenye siriasi issue. Mbona haji kujibu maswali ya wadau.
 
Huyu mdau analeta masikhara kwenye siriasi issue. Mbona haji kujibu maswali ya wadau.

Ndio tatizo la baadhi ya waafrika, nadhani alitaka kujua tu soko la kuku likoje, pamoja na hayo soko la kuku ukiwa na usimamizi mzuri hutajuta kufuga kuku"
 
Back
Top Bottom