Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Kwa hesabu ya mtoa mada, jaribu uone mziki wake, jamaa hakusema vifaranga wangapi watakufa, gharama za dawa kwa kuku. Kideli kiki ingia kwenye banda lako, utakimbia! Heasbu haziendi hivyo la sivyo kila mtu angekuwa millionea!

Haswaaaa! Niulizeni mie mfugaji wa hao kuku. But sio vema kuwakatisha wengine tamaa, jaribu ukipenda na ujiandae kwa mengi.
 
Reactions: 3D.

Mkuu hii topic nimeiona leo lakini nimo kwenye mkakati wa kuanzisha hiyo project ya kuku wa kienyeji. Very soon naanza kutayarisha mabanda, kuanza kufuga Mungu akiweka mkono nina hakika nitatokea tuu!!!!!!!!! Good advise. UBARIKIWE!!!!!!!!!!
 
Mkuu hii topic nimeiona leo lakini nimo kwenye mkakati wa kuanzisha hiyo project ya kuku wa kienyeji. Very soon naanza kutayarisha mabanda, kuanza kufuga Mungu akiweka mkono nina hakika nitatokea tuu!!!!!!!!! Good advise. UBARIKIWE!!!!!!!!!!

Ahsante, Ubarikiwe nawe pia lakini nakuomba ufuatilie vizuri huo mwongozo ambao kwa bahati mbaya sikuuleta mapema kule juu pale penye tatizo wasiliana na wataalamu wa mifugo. Nilishawahi kuwa mfugaji na nilihudhuria semina za ufugaji wa kuku wa kienyeji.
 
Dah! Asante sana gazeti. Hii inasisimua, inavutia kisha iko more practical than theory. Huu ni moyo wa kipekee Mungu azidi kukuongoza.
 
Reactions: 3D.
Ningependa kuuliza juu ya chakula, je, hawa nao wanalishwa chakula sawa na kile cha kuku wa kizungu?
 
Ningependa kuuliza juu ya chakula, je, hawa nao wanalishwa chakula sawa na kile cha kuku wa kizungu?

Ili kuku wawe na afya nzuri, ukuaji nzuri na kutoa mazao mengi na bora wanahitaji vyakula aina ya Wanga, protini, madini, vitamin na maji.

KUMBUKA
-Ukosefu wa vitamini A hujitokeza baada ya kiangazi kirefu
-Macho ya kuku huharibika
-Ugonjwa unakuwa mgumu kutibika dalili za wazi zikionekana
-Husababisha vifo hasa kwa kuku wanaokua.
-WAPE MAJANI MABICHI WAKATI WA KIANGAZI
-VITAMINI ZA KUKU ZA MADUKANI HUFAA KWA KINGA YA KUKU WENGI

MCHANGANYIKO WA VYAKULA WENYE ASILI ZIFUATAZO UNAFAA KWA KULISHA KUKU.
1.Mizizi - Mihogo, viazi vitamu, mbatata, magimbi n.k
2.Nafaka- Mahindi, mtama, mpunga, ulezi, pumba za nafaka n.k
3.Mboga- Jamii mbali mbali ya majani kama vile kunde,mboga za majani, nyanya, kisamvu n.k
4.Matunda- mapapai, maembe n.k
5.Mbegu za mafuta- karanga , ufuta, mashudu ya pamba, alizeti, machicha ya nazi n.k
6.Wadudu mbalimbali.
7.Maji

Vyakula nilivyotaja hapo juu hupatikana kwa wingi zaidi wakati wa mvua na mavuno, mara baada ya kipindi hicho kunakuwepo na upungufu mkubwa sana ambao unachangia ukuaji taratibu na utagaji hafifu.

Utafiti unaonyesha kuwa kiasi cha chakula wanachojitafutia wenyewe huwa hakiwatoshi. Inakadiriwa kuwa wakati wa mavuno kuku anaweza kuku anaweza kujitafutia asilimia 50 - 70 ya chakula na wakati wa kiangazi asilimia 30- 50 tu ya mahitaji yake ya chakula. Kwa kawaida kuku wa kienyeji hutumia zaidi ya 90% ya masaa ya siku katika umbali wa mita 110 hadi 175 ili kujitafutia chakula, kuku aliyepevuka anayefugwa huria anahitaji gramu 80 za chakula cha ziada kwa siku.

Hivyo ili kuku waweze kuzalisha wafikie uwezo wao ni muhimu wapewe chakula cha ziada. Chakula cha ziada mara nyingi hutokana na vyakula vinavyopatikana kwa urahisi katika mazingira aliyopo mfugaji. Nakuomba ufuatilie zaidi kwa mtaalamu wa mifugo aliye karibu nawe ili upate mbinu zaidi za namna ya kuandaa chakula cha kuku.

Kuhusu kuku wa kisasa sina uzoefu nao.
 
Reactions: 3D.
Gazeti. Nashukuru sana kwa msaada wako.

Umefanya vema, lkn kweli je gharama za banda?, kiwanja kama huna!?
Ila ni kweli huo ni mradi halisi zaidi ya DVDs na vitabu lukuki wanavyosoma watu siku hizi.....kama: how to get money, money trap, get rich n.k wanauza tu vitabu. Kwani kina sanga njombe na Ludewa wanatajirikaje ilhali hawajui hata kusoma! wao ni kuhesabu noti tu!
 
Mkuu Gazeti mimi naomba muongozo juu ya ufugaji wa bata. Nitashukuru kama utanisaidia kwa hilo kwani natamani kuchanganya hii mifugo.
 
Mkuu Gazeti mimi naomba muongozo juu ya ufugaji wa bata. Nitashukuru kama utanisaidia kwa hilo kwani natamani kuchanganya hii mifugo.

Kuhusu bata itakuwa ni ngumu kwa sababu nina nadharia zaidi kuliko vitendo kwa hiyo siko tayari kuelezea kitu ambacho utendaji wake siufahamu zaidi ya kuusoma tu!
 
Reactions: 3D.
naona umeignore gharama za kutengeneza banda la hao kuku (250,000 haitoshi)

Yap! Pia amesahau gharama ya chakula cha hao kuku na dawa manake hapa anazungumzia kuku wa kienyeji akasahau kuna gonjwa linaitwa "mdondo". Nilishawahi kuwa na kuku 120 nikajikuta nimebakiwa na kuku 8 kwa siku moja!!!
 
Yap! Pia amesahau gharama ya chakula cha hao kuku na dawa manake hapa anazungumzia kuku wa kienyeji akasahau kuna gonjwa linaitwa "mdondo". Nilishawahi kuwa na kuku 120 nikajikuta nimebakiwa na kuku 8 kwa siku moja!!!
Huo ulikuwa kama uamsho tu, nafikiri ukifuatilia hapo page 2 kuna majibu mengi na ya kina.
 
Reactions: 3D.
Huo ulikuwa kama uamsho tu, nafikiri ukifuatilia hapo page 2 kuna majibu mengi na ya kina.

Kweli mkuu, naona nilidandia treni kwa nyuma. Ngoja nilifuatilie hili sred kwa kina.
 
Reactions: 3D.
Asante sana Gazeti kwa mchanganuo wako, na Mungu akubariki sana. hakika itasaidia wengi jamvini na nje ya hapo, keep it up!
 
Mkuu Gazeti nashukuru sana nimejaribu hawa kuku umesema wanaitwa Chingwekwe, nimekubali maneno yako, aah wana balaa hawa kuku kwa kutaga.
 
Kwanza ngoja niiprint, Mazungumzo baadaye. Acha niseme kidogo. Mkuu Gazeti haya ndiyo mambo tunayotaka kuyasikia. Safi sana. Kwa kweli naamini atakayekuwa serious na kufuata ushauri ulioutoa ni lazima atafanikiwa. Kazi yako umeshamaliza, bado sisi kutekelza tu.

Thanks a lot Mkuu.
Thanks again.
 
thanx mkuu umetupa mambo sahihi kwa wakati sahihi ajuaye kuhusu dawa za hao mifugo atujuze
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…