Hello wadau woote...Malila naomba niunganishe na huyo jamaa nipate majogo hayo..mimi nina chotara niliponunua wanasema ni cross ya astralop..pia ni wakubwa na wazuri but hao wa kuchi nahua watakua zaidi
habarini za mida, jaman mwenzenu mbona nashindwa kufungua private messages? yaan kwakweli mimi ni mgeni kabisa humu, so bado sijaelewa vizuri jinsi ya kuitumia hii jamiiforum. naona kabisa nina msg private, ila nahangaika jinsi ya kuifungua nashindwa, msinicheke jamani
Hivi ni kweli mayai ya kienyeji yana market sana.mimi sidhani kwani naona bei yake ni ghali ivo watu wengi hawanunui mayai hayo kwa sana sijui kwako unamarket ya wapi
Nashukuru kwa concern yako. Bahati nzuri hicho na mimi ninacho ili cha dawa asilia. Niliona kwenye u tube mama mmoja nchi za kiasia anashamba kubwa la kuku wa mayai na anatumia dawa za asili na kuepuka kuimport magonjwa
Nimeanza na kuku mmoja toka janury na ametotoa vifaranga saba nimejenga kibanda kidogo cha kuanzia nategemea natakuwatunza hawa vizuri natumaini mpaka mwakani mwezi kaa huu kupata kuku wasiopungua 40 kama watataga na kutotoana mama yao kutaga kwa mara 1 au 2 tena mpaka mwakani napenda kwenda mdogomdogo ili wasinipe stress na kupata muda wa kufanya mambo mengine pia.
Pata super gro kwa ajili ya kurutubisha kuku na kuondoa maradhi,soma Uzi wa Wafugaji na wakulima wote soma hii kupata data kamili za matumizi ya super gro View attachment 149518
wakuu, nawashukuruni sana kwa thread hii na contents zote pamoja na wadau wote walioshiriki katika kuchangia mawazo yao. kiukweli nimeelimika sana katika suala zima la ufugaji bora kwa kuku wa kienyeji...