kaka tembelea website hii Home utajifunza mengi!!!Hey JF Members.
Ee bwana kuna mtu anaweza kunipa msaada wa mchanganuo wa kufuga kuku. naona soko la kuku ni kubwa sana. hii ni biashara ambayo soko lake liko tayari. hotels, functions, vibanda vya chipss.... Yeyote mwenye idea naomba msaada please!!!!!
Mayu,Mkuu Zantsan naomba ufafanuzi kuhusu kuangulisha vifaranga kuku wa kienyeji marambili Nimeambiwa eti unaweza kuwa labda na kuku wa 5 na wakataga kwa pamoja, utakuwa unawaondolea mayai kila yanapozidi matatu na hii itawafanya watage mayai mengi zaidi kuliko uwezo wao wa kuatamaia Baada ya kuanza kuatamia utawarudishi maya let say 10 kwa kila kuku, na mengine utayabakisha Baada kuku kumaliza kuatamia eti unawanyanganya vifaranga na kuwawekea mayai yalio salia na wataanza kuayaatamia tena kwa siku zingine 21 huku wewe ukiendelea kulea vifaranga katika boksi lao maalamu lenye joto la kutosha Kuna ukweli wowote kuhusu hili mkuu?
Wanajf, Kwasasa niko mkoani Dodoma,kwa wale wafugaji wa dodoma mnaweza kunitafuta kwa msaada zaidi. Tuko pamoja kwenye ujenzi wa Taifa na kijikwamua binafsi.Ujasiriamali unalipa.
Nimekutumia kwenye private yako namba zangu nipigie ili nikuelekeze kwa huko Dar wapi utapa vifaranga chotara,ingawa hawa vifaranga wa kuchi upatikanaji wake si rahisi sana kama ilivyo kwa kuku wa weusi wa malawi,wanaopatikana ni wale chotara waliokrosiwa kwa kutumia majogoo ya Rhode Island Red wale wekundu.Nipo dar natafuta vifaranga chotara wa kuchi na wale wa malawi, tafadhali msaada.
Habari yako mkuu,
Tafadhali ninaomba uni-PM kitabu cha ufugaji wa kuku wa kienyeji maana mie nae ni mfugaji ila napata changamoto sana juu ya hili
Nashukuru sana na ubarikiwe...
Ndugu wana jamii forum, sasa ni wakati wa kuacha kulalamika, tunapaswa kujituma na kupiga kazi kwa bidii. Vijana graduates kutoka vyuo mbalimbali tuwaze zaidi kwenye kujiajiri kuliko kuajiriwa, kujiajiri kunatoa uhuru wa kufanya kazi na kutoa maamuzi binafsi tena kwa wakati. Kuajiriwa kimsingi hakuna tofauti na utumwa na kama utapiga hesabu vizuri utagundua kuwa kuajiriwa ni hasara na pia huzuia mtu kuitumia elimu yake ipasavyo hasa ukiajiriwa serikalini. Kwa wastaafu pia wana fursa ya kutumia mafao yao vyema kwenye miradi ya ufugaji.
Kwa kuanzia tu naruhusu kuulizwa maswali kutoka kwa wale wote wanaojihusisha na ufugaji wa kuku, kama kuna jambo lolote linasumbua na kutaka kupata ufafanuzi. Pia kwa wanaohitaji kuanzisha mradi wa ufugaji wa kuku,utotoreshaji wa vifaranga,biashara ya uchanganyaji na uuzaji wa vyakula vya kuku nk , kama watanzania tunaweza kusaidiana ili hatimae tuondokane na umasikini. Kila mtu awe msaada kwa watu wengine kwa fani aliyesomea.
Karibuni kwa mjadala.
Shukrani sana mkuu
Mchumba,
Mapungo ameweka link hapo juu.
Ukishaifungua, bofya BLOG utaona "Kuku (swahili)"
All the best.
Mkuu, kuhusu chakula hesabu zako si sahihi sana, kifaranga hakili msosi sawa na kuku mkubwa, hebu cheki mchanganuo huu,
Hebu tuone hesabu hii:
Kuwanunua 2000 @2400 = 4,800,000/=
Chakula:
Mwezi wa kwanza (Wiki 0- 4) average kilo 75 kwa siku ( Mfuko mmoja na nusu hii ni Stater) @ 34,000 = 51,000 X 30 days =1,530,000/=
Mwezi wa pili ( Wiki ya 5 - 8) average kilo 100 kwa siku ( Mifuko miwili finisher) @ 34,000 = 2,040,000/=
Glower (wiki ya 9 - 11) siku 14, kila siku mifuko 3 @28,000 = 1,176,000/=
Glower (wiki ya 12 - 18) siku 42, kila siku mifuko 5 @28,000 = 5,880,000/=
Layers (wiki ya 19 -23) siku 28, kila siku mifuko 5 @32,000 = 4,480,000/=
------------------------
15,070,000
add Manunuzi 4,800,000
------------------------
19,870,000
-------------------------
Wiki ya 19 wataanza kutaga kidogo kidogo mpaka wiki ya 24 utaanza sales ya 50% ikiongezeka kadri siku zinavyosonga. Kwa hiyo mtu anayetaka kuanza ufugaji kwa kuku 2000 anahitaji mil 20,000,000/=. Ukiweka na gharama za banda na uendeshaji hadi waanze kutaga ni lazima uwe na 27m- 30million.
shughuli pevu hii, nashauri anayeanza, ni vyema basi aanze na kuku 500 then aongeze taratibu taratibu huku akijifunza challenges.
Ungesema kwanza upo wapi..kwa kuwa gharama hutofautina toka eneo moja mpaka jingine....Naombeni msaada wa kujua gharama za chakula , madawa kwa kuku wa mayai 200 toka vifarnga hadi kutaga na wastani wa trei