Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

kwa uzoefu wangu w miaka3 ktk kufuga kuku wa nyama n mayai,vifaranga wa interchick ndio mimi nawanunua n kuwakuuza.pia natumia chakula cha interchick vilevile.kuku 100(yaan box1) hula mifuko 4 y chakula mpaka unawauza.na muda wa kukaa bandani wakapata maji na chakula cha kutosha na kwa wakati,mimi uwa nawauza ktk umri wa siku 25 mpaka 28. hvyo kwa kuku hao 300 jiandae kwa mifuko 12.na kila mfuko kwa starter ni 50000 na finisher ni 48000.ni biashara nzr sn,inalipa na naipenda sn ikiwa utaifanya kwa umakini mkubwa.ufugaji mwema mkuu.
 
Ndugu mkwawa, mimi pia nafuga broilers wa interchick na natumia chakula cha interchick lakini kwa kuku 400 natumia 22 bags badala 16 wanazoshauri, je wewe kwa hizo siku 28 wabakuwa na uzito wa gms ngapi? Mimi wanakaa 5 weeks kufikisha 1.2to 1.3 kgs.
 
Nina dawa nzuri ya kuua bakiteria,virus kuzuia kuharisha.PM me
 
Fuga kuku wa kienyeji hawa wq kisasa pasua si umesema unaeneo kubwa basi fanya hivyo.
 
Niko Morogoro mjini mkuu..karibu sana...my no 0659300000 waeza nitext
 
huu uzi umeni inspire sana, nimekuwa nikiufuatilia toka mwanzo mpaka na mimi nimeanza kufuga. nitaanzisha uzi ambao nitashare my experience ktk ufugaji wa Layers ili wengine pia wazidi kujifunza
 
Mimi nina 1000000 je naweza fuga kuku wangapi wa kienyeji. Mabanda yapo
 
Nimependa sana hii biashara lazima niingie kazini nahisi inaweza kunitoa


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
nimependa hii thread, nilitaka kujua ni nini unatakiwa kuwa nacho kabla hujaanza kufuga kuku, sasa nimejua..napendelea zaidi kuku wa kienyeji. asante
 
Habarini wadau,

Still niko humu jamvini.

Leo nina habari njema kwa wakazi wa Dar es salaam. Kuna semina kabambe inaratibiwa, soon nitawapa habari kamili. Mimi pia nitakuwa mjengoni siku hiyo. Nitakuwepo katika wale watakao wasilisha mada. Kaeni mkao wa kula ni semina ya siku moja kiingilio ni tsh 20000/=

Kama kweli wewe ni mfugaji ama unakusudia kuanza ufugaji basi tafadhali usikose siku hiyo. Ukikosa utakuwa umepitwa na mengi.

Wadau mbalimbali wa kuku watakuwepo siku hiyo, mabenki yanayotoa mikopo kwa wafugaji, wafugaji wakuliofanikiwa katika ufugaji watatoa ushuhuda wao siku hiyo, wanunuzi wa mazao ya kuku, watu wa mahoteli mbalimbali, supermarkets,nk madaktari na watu mbailmbali waliobobea katika tasnia ya kuku nk. Watakuwepo pia wazalishaji wa vifaranga, watengenezaji wa vyakula mbalimbali vya kuku, watengenezaji wa Incubator wa ndani ya nchi na wawakilishi wa watengenezaji wa mashine za nje.

Kila kitu utakachohitaji kukifahamu siku hiyo utafahamu. Je wajua ukitaka kuanzisha hatchery hatua gani muhimu za kufuata, nini kinahitajika na wapi uanzie, siku hiyo ni siku muafaka. Je wajua watawezaje kupunguza gharama katika ufugaji wa kuku?

Mambo yakikaa sawa tutawajulisha, lini na ukumbi gani semina hiyo itafanyika. Kwa wale watakaohitaji basi tuwasiliane kupitia namba zangu 0767989713, 0715989713 na 0786989713

Kwa pamoja tunaweza kuutokomeza umasikini.
 
Nina mtaji wa milioni 5 nianze ma.kuku wangapi na wa aina gani wa umri gani na nina uwezo wa kupata sh ngapi kama faida?
 
Nina mtaji wa milioni 5 nianze ma.kuku wangapi na wa aina gani wa umri gani na nina uwezo wa kupata sh ngapi kama faida?
Ndugu yangu Sunshine,
Tafadhali ebu rudi nyuma page ya tatu kutoka hii tuliyokuwepo utapata majibu ya swali lako na kwa kuku wa nyama itabidi urudi nyuma sana.

Asante
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…