Habari wandugu:
Nimejaribu kufuatilia mjadala toka mwanzo, lakini nikiri kwamba kuna uwezekano mkubwa kuna pages sijasoma.
Nimekuwa na hamu ya kuanza hii shughuli ya ufugaji wa kuku wa kisasa. Na kwa msaada wenu nimeweza kuchanganua kwa kadri niliyoweza na data nilizozipata humu na kwingineko kupata business plan. Huu chini ni mchanganuo wangu, kwa kifupi nimepiga hesabu ya kuku/vifaranga 200, halafu nikajaribu kuangalia kama unaongeza hadi 2000. Na pia nimejichukulia mimi kama muwekezaji kwa maana kwamba mimi nitaweka mtaji na kusimamia pesa lakini mtendaji/mtaalamu ni mwingine.
Kwa Ufupi:
Mahitaji:
[TABLE="width: 255"]
[TR]
[TD="colspan: 2"]Kuku (Vifaranga) 200[/TD]
[TD]TZS 260,000[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 2"]Madawa na Chanjo[/TD]
[TD]TZS 30,000[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 2"]Chakula jumla gunia 12[/TD]
[TD]TZS 456,000[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 2"]Uendeshaji[/TD]
[TD]TZS 219,000[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD] [/TD]
[TD][/TD]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 2"]Total[/TD]
[TD]TZS 965,000[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
1. Gharama za kuwafuga/kuwatunza vifaranga 200 hadi unauza ni TZS 965,000
2. Ukiwauza tuseme kuku 200 kwa bei ya 5000 kwa kuku mmoja jumla unapata TZS 1,000,000.
3. Faida ni kiasi cha TZS 35,000.
4.Tuseme basi utafuga/watunza vifaranga 2000 hadi unauza basi gharama itakuwa TZS 905,000 x 10 + 200,000(mshahara) = 9,250,000
5. Faida ya kuku 2000 ni 2000x5000-9,250,000 = 750,000.
Hitimisho:
Maswali niliyonayo:
1. Gharama za madawa na chanjo kwa kuku 200 zinaweza kuzidishwa mara 10 ili kupata gharama ya kuku 2000?
2. Nimeona mshahara kwenye hii thread wa shilingi 100 kwa kuku mmoja kwa mwezi ina maana kuku 2000 kwa mwezi mshahara ni 200,000. je huu mshahara ina maana mfanyakazi anakaa kwake au anakaa na kula kwako? Je ratio ya mshahara na kazi ya kuku 2000 ipo sawa?
3. Kama unaajiri mfanyakazi kwa mwezi je ni kuku kiasi gani mfanyakazi mmoja anaweza kuwaudumia?
4.Kuhusu gaharama za banda au kupangisha banda: Nimeona kwenye hii thread kwamba banda la kuku 1000 kwa vipimo vya 15 x8 m linagharimu kama million 12 huko dodoma. Hizi gharama zipo sahii kweli?
5. Kama unapangisha ardhi ya mtu kujenga banda la size hilo la kuku 2000 inaweza kugharimu kiasi gani?
6. Kama unapangisha banda la size hiyo hapo juu linaweza kugharimu kiasi gani kwa mwezi?
7. Kuna maeneo gani mengine kwenye biashara ya kuku unaweza kupunguza gharama kama unafuga kuku wengi kama 2000 au zaidi?
Nitashukuru kwa msaada wa majibu yenu. Mchanganuo wangu wa hesabu ya kuku 200 upo hapa chini.
View attachment 180842
Mchanganuo wako ni wa kuku gani? Layers,Broiler Or Chotara?