Habari wakuu:
Bila shaka kuna watu ambao wanafuga kuku au walishawahi kufuga kuku. Naomba watu wenye uzoefu na maarifa kuhusu kufuga kuku wanipe mawazo, maana nataka kuanza kufuga kuku na sijawahi kufanya hivyo, hivyo nahitaji mawazo yenu wakuu.
Natanguliza shukrani zangu wakuu:
Mimi nilishawahi kufuga kuku na kwa kiasi fulani zimechangia kuniendeleza ki eleimu na kuwasaidia baadhi ya wategemezi - kuku nawakubali.
Ufugaji wa kuku inategemeana unataka wa aina gani (kisasa au Kienyeji) kwa kuku wa kisasa kidogo wanahitaji nguvu ya ziada na umakini wa hali ya juu wakati wakiwa wadogo na wanapokuwa kwa mazao bora. Vile vile kwa kuku wa kienyeji.
Kwa hapa nitatoa ushauri wa ju juu tu kwa kuwa taratibu zote za ufugaji ni nyingi kiasi kwamba kuandika hapa haitatosha, pia inategemeana unaishi wapi yaani maeneo ya baridi sana au joto.
Kwa kifupi, Ukitaka kufuga hasa wa kisasa wa mayai, chukua vifaranga vilivyozaliwa siku hiyo hiyo uanze kuvifuga wewe na si vile vilivyokaa juani kama pale buguruni kwa zaidi ya wiki1 au zaidi. Pia hakikisha unachukua vifaranga kwa mzalishaji ambaye anajali na si mchakachuaji kwa kuwa kama mazlishaji hakuwapa dawa fulani wakati wanataga mayai kuku wa kuzalisha vifaranga, vifaranga vinapozaliwa vinakuwa na ugonjwa wa kuzaliwa nao na vikifikisha miezi 3 vinakufa vyote kwa hiyo ni kuwa makini na utakaponunua vifaranga hivyo.
Ukifikisha vifaranga kutoka kwa aliyekuuzia unatakiwa uvipatie glucose ya kuku (Ya mifugo) na maji ya uvuguvugu kama unaishi mikoa ya baridi kama iringa au mbeya lakini kama dar hayahitajiki ya uvuguvugu. baada ya saa 2 unavipatia vitamini, vitamini hizo zipo za aina nyingi sana madukani kutokana na wazalishaji wengi na zingine inasemekana huwa ni feki inapaswa kuwa makini unaponunua, ila mimi napendelea Bidhaa za kutoka UFARANSA huwa ni nzuri zaidi.
Kwa maelezo zaidi ya ufugaji waweza kumtembelea mfugaji aliye karibu na wewe au hata daktari wa mifugo. Au MTAFUTE mwakilishi wa madawa ya kuku kutoka kampuni inayosambaza dawa za mifugo za LAPROVET, just I google tu, utamjua mwakilishi wa tanzania, ukimpigia simu hana kinyongo atakupa maelekezo ya kutosha.
Hata hivyo ufugaji wa kuku una tesa sana, kama hutafanya mwenyewe ukaajili msimamizi ambaye hayuko makin banda lote litateketea, halafu ukizembea kuwalisha watakonda na mazao hayakuwa mazuri na ndo mwanzo wa kuugua. Ukweli ni kwamba kuku wa kisasa wanakula balaa, yaani kama huna source nzuri ya pesa ya kununulia chakula cha kuku, bora usifuge, watakufilisi na mradi hautakuwa na matunda mazuri, kuku wanakula massaa 24, ila kuna rafiki yangu aliniambia wao kuku wao waliwazoesha kula mchana tu, na usiku walikuwa wakiwazimia taa. ukifanya hivyo utapata afueni, wanakula balaa.
Kwa kuku wa kienyeji ni rahisi zaidi, ukiwapa chakula cha kutosha na chanjo za kueleweka hawatakufa, kamwe na utapata faida nzuri zaidi.
Cha msingi katika ufugaji usizembee kuhakikisha unafuta taratibu zote za kutunza viumbe hawa, usikubali kumwachia mtu usiyemuamini kuwa atafanya unavyotaka na hata kama ni wa kisasa kienyeji jaribu kuwa na utaratibu wa kuwapa chakuala kwa muda fulani fulani na usipitilize hadi wazoee.
Pia usichelewe mpaka waanze kupiga makelele. La kuzongatia kabisa katika ufugaji wa kuku na mazao bora ni CHAKULA CHA KUTOSHA< UKIWEZA HILO HATA MAGONJWA HAYATAKUWA MENGI NA UTAFAIDI UFUGAJI WAKO.
Nawasilisha kama kuna sehemu nimekosea, hayo ni wawazo yangu naomba sahihisho tafadhali.