Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Kuku wa kienyeji kama wanafugwa huria wanatumia gharama ndogo sana. Cha msingi anapototoa unamnyang'anya vifaranga ndani ya wiki mbili ili aanze kutaga tena. Kuku wa kisasa wana gharama kubwa.
 
Mtaalamu wa huduma za mifugo (veterinary services) anapatikana hapa. Huduma nitoazoni ushauri wa ufugaji bora, kutibu mifugo inayoumwa, kuchanja mifugo ili kuzuia magonjwa, kuchunguza na kugundua ugonjwa uliomuua mfugo wako kama wewe hufahamu ili utibu waliobaki, kupandisha kwa chupa (A.I) kwa wale wafugaji wa ng'ombe, kuhasi vidume vya mifugo kama vile nguruwe, ng'ombe, mbuzi, kondoo pamoja na huduma nyingine nyingi. Kama umegundua unahitaji huduma yangu usisite kunitafuta kwa namba 0786909993, makazi yangu ni morogoro na Dodoma. Kauli mbiu yangu ni "Uliza, Utajibiwa, Utahudumiwa" Karibuni sana.
 
Msaada wadau mm Nina kuku wa kienyeji lkn kuna kuku anataga anakula mayai tatizo ni nn?na nimpatie nn.
 
mi naomba kujua matumiz ya super grow kwn nafuga kuku wa nyama nipo arusha..nahitaj kuitumia
 
: Je unafaham kuhusu wa mayai kutoka manyoya
Hao ninao 250 na wana miezi 3 sasa
 
Wanabodi, nauza mayai ya kuku wa kisasa tray moja ni Tshs elfu sita tu kwa bei ya jumla na reja reja ni elfu saba kwa tray, kwa anaehitaji ni PM namba yako tuwasiliane. Angalizo mi nipo Dar es salaam
 
Je viranga hawa wana wiki ngapi? Na husaidia nini kuwaweka hao kuku katika chanja au kuwaeka chini tu na kuwawekea maranda ya mbao katika kipindi cha udogo.
 
Je viranga hawa wana wiki ngapi? Na husaidia nini kuwaweka hao kuku katika chanja au kuwaeka chini tu na kuwawekea maranda ya mbao katika kipindi cha udogo.

: Je unafaham kuhusu wa mayai kutoka manyoya
Hao ninao 250 na wana miezi 3 sasa
 
Mkuu naona shule hapo imetulia........!

Lakini mbona mnazungumzia haya makuku ya kisasa tu? Je, ufuguja wa kitaalam wa kuku wa KIENYEJI unakuwaje? Kumbuka hawa nao wana soko zuri sana..........!

Mkuu kuna thread moja humu ndani ilirushwa mwaka jana ina nondo za kufa mtu kuhusiana na ufugaji wa kuku wa kienyeji, mimi nilikopi hizo nondo nilizi-save kwenye pc yangu nazitumia kama msahafu kwenye shamba langu la kuku wa kienyeji, nikiipata hiyo thread nakupa link
 
wafugaji wenzangu, kwa wale wanaohitaji vifaranga vya kuku wa kisasa wa nyama Broilers wasiliana nami kwa kutuma private message (inbox me)
Karibu

Mkuu hizo bei za vifaranga zikoje kwa sasa? ?
 

naomba contacts zenu
 
Ufugaji wa kuku wa mayai unachangamoto kidogo hasa kama utawalisha chakula chenye upungufu wa virutubisho. Mara nyingi kuku wa mayai wakika chakula chenye upungufu wa virutubisho hisababisha utagaji kushuka au ambao hawajaanza kutaga huwafanya wachelewwe kutaga, huwafanya wadonoane, lakini wakati mwingine kuku hufa wakati wa utagaji kutokana na kupasukia mayai tumboni.

Mayai hupasukia tumboni kutokana na kuku kula chakula vhenye upungu wa madini ya calcium na hivyo kulifanya yai liwe tepetepe na wakati wa kutaga yai hilo hupasuka kabla ya kutoka nje.

JE UNACHANGAMOTO YOYOTE INAKUKABILI, HEBU ILETE TUIJADILIBKWA PAMOJA
 
Sababu zinazowafanya kuku ashushe utagaji ni pamoja na zifuatazo
Kwanza ugojwa. Kuku akiwa mgonjwa dalili ya kwanza kushusha utagaji mfano wa wagonjwa yanayosababisha ushukaji wa utagaji ni pamoja na Typhoid, minyoo, Utitiri, Chawa, Mafua nk.

Pili Chakula. Chakula kina mchango mkubwa katika utagaji wa kuku. Kuku wakilishwa chakula kizuri husaidia kuongeza utagaji.

Mndikano wa kuku. Kuku wanatakiwa wakae kulingana na ukubwa wabanda. Kuku wakiwa wengi kuliko nafasi inayotakiwa. Kwa kuku wa mayai mita square 1 ni kwa kuku 5-6.

Kumlisha kuku bila kumpimia chakula. Kuku wa mayai anatakiwa apimiwe chakula ili asiwe mnene kupita kiasi. Kuku mnene sana si mtagaji kwakuwa anakuwa amejaza mafuta mengi mwilini kwake na hata sehemu utagaji wake.
 

Yai likichafuliwa na kinyesi litafaa kutotolewa?na km ni chafu kuna njia mbadala ya kulisafisha likatotolewa?
 
Yai likichafuliwa na kinyesi litafaa kutotolewa?na km ni chafu kuna njia mbadala ya kulisafisha likatotolewa?

Kuku wa Kabanga, yali likichafuliwa kwa kinyesi wakati wa utagaji ili liweze kutotolewa vyema kwanza linahitaji lisafishwa kwa kitambaa kisafi na kikavu kama litakuwa limelowa kenyesi na kama kenyesi ni kikavu kimegandamana kwenye yai itabidi utafutwe mti uchongwe kisha yai liparazwe kuondoa kenyesi kisha liatamishwe.

Unyevunyevu husababisha yai livamiwe na wadudu.

Hakikisha yai la kutotolewa halikutani na maji.

Ni muhimu mayai kutibiwa kabla ya kuingizwa katika mashine kwa ajili ya kuua wadudu.
 

nielezee kuhusu battery farming system
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…