Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Wazo nzuri sana ila kazi ipo apo kwenye kushirikiana inabidi kumtafuta mtu ulie nae karibu na ufahamu tabia zake kwa undani nae awe nakupata kwa ndani
 
Nimevutiwa na huduma zenu mnazotoa kwani mimi pia ni mdau wa muda mrefu katika masuala ya ufugaji.
Niko Tarime Mkoa wa Mara.Mnatufikiaje watu wa maeneo haya.
Namba yangu ya simu ni 0717400751.
E-mail: gillystrongest@gmail.com
 
Huu Uzi, ndo nauona Leo, nilipoangalia vizuri nikagundua ni wa tangu 2012. Nikawa na hofu, mleta Uzi tangu wakati huo atakuwa bado anatoa ushauri huu alioahidi hadi sasa?

Hivyo ikanilazimu kufuatilia hadi mwisho kujua aliishia mwaka gani? Nimefarijika kukuta kuna post hadi za sasa mleta Uzi bado anajibu changamoto za wafugaji na kutoa ushauri na Huduma mbalimbali.

Aman, hongera sana kwa Uzi huu! Nimejifunza mengi, lakini pia nakukumbuka kwa wema wako, niliwahi kukupigia simu juu ya Ufugaji wa mbuzi, kama miaka 3 hivi iliyopita, ulinishauri vizuri na kwa wema kabisa. Nina imani wewe bado ni MTU wa msaada.
Nitakutafuta kuhusiana na Ufugaji wa Kuku, maana nishaanza hatua za awali za kutafuta eneo nje ya mji, kwani nataka Ufugaji huria, mabanda na nyumba ya mfanyakazi, na kisima cha maji. Maana nimejipanga kufanya Ufugaji mkubwa wa kibiashara,

Nitakutafuta kwa simu/,email.

Asubuhi njema.
 
Msaada pliiiz kwa hawa Chotara.........................
Je ni vyema kuwalisha ndani au niwe nawatoa nje mkuu ili wajitaftie msoci
 
Huu Uzi, ndo nauona Leo, nilipoangalia vizuri nikagundua ni wa tangu 2012. Nikawa na hofu, mleta Uzi tangu wakati huo atakuwa bado anatoa ushauri huu alioahidi hadi sasa?

Hivyo ikanilazimu kufuatilia hadi mwisho kujua aliishia mwaka gani? Nimefarijika kukuta kuna post hadi za sasa mleta Uzi bado anajibu changamoto za wafugaji na kutoa ushauri na Huduma mbalimbali.

Aman, hongera sana kwa Uzi huu! Nimejifunza mengi, lakini pia nakukumbuka kwa wema wako, niliwahi kukupigia simu juu ya Ufugaji wa mbuzi, kama miaka 3 hivi iliyopita, ulinishauri vizuri na kwa wema kabisa. Nina imani wewe bado ni MTU wa msaada.
Nitakutafuta kuhusiana na Ufugaji wa Kuku, maana nishaanza hatua za awali za kutafuta eneo nje ya mji, kwani nataka Ufugaji huria, mabanda na nyumba ya mfanyakazi, na kisima cha maji. Maana nimejipanga kufanya Ufugaji mkubwa wa kibiashara,

Nitakutafuta kwa simu/,email.

Asubuhi njema.
Karibu Honda XP, ushauri wa miradaji ya ufugaji ndiyo kazi yangu siwezi kuiacha, still niko hewani sema nimesimama kidogo kuendelea kuandika since naona karibu mambo mengi tumeyakava.
 
Nategemea kuanza kufuga kuku kama 300 aina ya kuroiler ili niwauze pasaka mwakani.maana maisha ya kutegemea mshahara yanaumiza sana kwakuwa nitakuwa mgeni katika ufugaji nitakuwa nawasumbua sana kwa maswahili kuhusiana na ufugaji wa kuku
 
Slim5,
Ni matumaini yangu kuwa mzima. Nashukuru kwa maswali yako lkn naomba uniwie radhi kwa kuchelewa kukujibu. Banda lenye Square meta 140 kama ni kuku wa kienyeji unataka kufuga kwa ajili ya kuwafanya watagaji basi eneo hili litawatosha kuku 1120 maximum na Minimum Kuku 700. Lakini pia eneo hilo kama utamua kufuga kuku hao kwa ajili ya nyama kwa maana baada ya wiki miezi 3 au 4 unawauza basi utakuwa na uwezo wa kufuga kuku hadi 2100.

Kwa eneo la square mita 90 utafuga kuku 750 maximum na Minimum 500 kama utawafuga kwa ajili kuwafanya watagaji.

Ushauri wangu ni kuwa kama unataka kufanya Ufugaji wa Kibiashara fuga kuku chotara. unaweza kupata wale cross breed ya Pure line ya Rhode Island Red na Local wakwetu, au wale kuku weusi wa malawi nk, au Ukapata ile breed ya kenya na Uganda Kuroiler ukafuga hao utaiona faida ya ufugaji. Lakini kama utasema ufuge kuku pure wa kienyeji hawatakulipa kwakuwa ukuwaji wao pamoja uzalishaji wao ni mdogo ukilinganisha na gharama za uzalishaji.
Asante


Nategemea kufugakufugakama 300 aina yainaroilkuroileriilizniwauzeapasakani.maana maishamaishategekutegemeaamshaharamyanaumizakwakuwkwakuwaunitakuwa mgeniakatikajufugajiunitakuwaumbua sana kwa kuanzamaswali akuhusianagajiufugajiu
 
Ndugu wana JF habari za majukumu ya kulijenga Taifa letu , mi ni mmoja wa wadau amabaye nilijikita sana kwenye kilimo cha umwagiliaji mpunga pale Dakawa kwa sasa nataka kupunzika na kuku wa kienyeji na Kisasa ...
ishu ipo kwenye kudizaini Banda lao ..
1. Naomba kuuliza Je naweza niakawachanganya kwa pamoja? au ni vizri nikawawekea partition?

2. Vipi nawezaje Kukamata soko,

3. Sokoni kuku wa kisasa shingapi na wa Kienyeji shingapi?

4 Ni mbegu gani ipo kwenye Trend?

5. Changamoto zake

Asanteni
 
Ndugu wana JF habari za majukumu ya kulijenga Taifa letu , mi ni mmoja wa wadau amabaye nilijikita sana kwenye kilimo cha umwagiliaji mpunga pale Dakawa kwa sasa nataka kupunzika na kuku wa kienyeji na Kisasa ...
ishu ipo kwenye kudizaini Banda lao ..
1. Naomba kuuliza Je naweza niakawachanganya kwa pamoja? au ni vizri nikawawekea partition?

2. Vipi nawezaje Kukamata soko,

3. Sokoni kuku wa kisasa shingapi na wa Kienyeji shingapi?

4 Ni mbegu gani ipo kwenye Trend?

5. Changamoto zake

Asanteni
Upo Mkoa gani?
 
VISUMBUFU KATIKA UFUGAJI WA KUKU ( VIROBOTO, CHAWA NA UTITIRI)

Mara nyingi wafugaji wanakabiliwa na changamoto kadhaa katika ufugaji wao wa kuku. Changamoto hizo ni pamoja na Visumbufu mbalimbali mfano, Viroboto, Utitiri na chawa. Visumbufu hivi vimekuwa tishio kubwa katika kufanya ufugaji wa kuku uwe wenye tija kutokana na kusababisha vifo vingi.

Katika banda lako la kuku ukivamiwa na wadudu hawa kwa hakika afya ya kuku wako itaanza kuzorota kwa haraka na kuwafanya kuku wako waonekane kama wanaumwa vile. Ni wadudu wanaonyonya damu kwa kiasi kikubwa sana na hivyo kusababisha kuku kufa kwa ugonjwa wa kuishiwa damu mwilini. Lakini vilevile kwa kuku wanaotaga huwafanya washushe utagaji wao ghafla. Ukiwatazama unaweza kuona kama wanaumwa kwa maana wanakonda, kuzubaa na kupoteza hamu ya kula. Muda mwingi wanakuwa wanajisokonyosokonyoa katika manyoya yao kwa kutumia midomo yao. Hii ni kutokana na adha wanayopata hasa kuwashwa na maumivu wanayosababishiwa.

Viroboto ni rahisi kuonekana kwa kuwa wanakaa sehemu za wazi za kuku mfano kuzunguka maeneo ya macho, katika ndevu na mapanga yao nk. Tatizo ni kwa utitili na chawa wenyewe si rahisi kuonekana kama mfugaji siyo mfuatiliaji wa karibu wa kuku wake. Utitiri na chawa wenyewe wanakaa ndani ya manyoya ya kuku kwenye ngozi kabisa. Utitiri ni mdogo kuliko chawa. Chawa wanakuwa weupe hivi wanajishika katika ngozi. Utawaona endapo utapekenyua katika manyoya ya kuku. Wakati utitiri wenyewe unatakiwa uwe na macho mazuri kuweza kuwaona kwa kuwa ni wadudu wadogo zaidi lakini ukipekenyua kwenye manyoya na kufika ndani kabisa kwenye ngozi utawaona wakitembeatembea. Wanapenda kukaa kwenye kwapa ya kuku na kwenye ngozi ya mwili wake

Usipojua vizuri kuhusu visumbufu hivi unaweza ukadhani kuwa kuku wako wanaumwa ugonjwa mwingine kabisa katika magonjwa ya kuku. Na kwamba utahangaika kutumia gharama nyingi ya madawa huku kuku wako wakiendelea kuzorota bila kupata nafuu ya matibabu unayohatumia.

Ni muhimu kabla ya kutibu kuku wako ukawasiliana na mtaalamu wa mifugo aliyekaribu yako ili aweze kukusaidia kukukagulia na kubaini tatizo halisi la kuku wako. Kwa maana kuku hawahitaji mchezo wa kubahatisha. Unatakiwa ujue ni tatizo gani hasa linawakabili kuku wako ili waweze kupatiwa tiba ya uhakika.

Sasa nini kifanyike kama banda lako litakuwa limevamiwa na Visumbufu hivyo?

Kuna dawa nyingi za kutumia, unaweza kutumia Dawa za unga za kunyunyiza mfano Akheri powder au nyingine inaitwa Sevin (Dudu) Dust. Dawa hizi utanyunyiza kuku wako wote mmoja baada ya mwengine kwenye manyoya yao na sehemu zile ambazo zimevamiwa na wadudu hao mfano machoni na kwenye mapanga yao na vilevile utapaswa dawa hizo kunyunyiza kwenye malanda au vumbivumbi la ndani ya banda la kuku kwa sababu vumbi ni makazi mazuri ya Viroboto na Utitiri.

Lakini wakati mwingine unaweza kujitahidi kutumia dawa hizo za kunyunyiza kwenye mabanda na kuku wenyewe lakini zisifue dafu. Mara nyingi nimeliona hili kwenye mabanda mengi ya wafugaji. Sasa ukifikia katika hali hii ufumbuzi wa haraka ni kufanya usafi wa banda lako lote. Ondoa malanda na vumbi lote la samadi kisha deki kwa kutumia dawa ya V- RID Disinfectant. Pia utapaswa kupuliza dawa hiyo katika kuta za banda lako. Ukiona tabu kufanya hivyo basi baada ya kuondolewa samadi yote katika banda lako la kuku na kufuta vumbi kutani, deki kwa maji vuzuri bila dawa kisha baada ya banda kukauka vyema paka chokaa kote sakafuni kutani hadi dalini kama banda lako lina dali na kama halina basi utaishia tu katika kuta za banda na sakafuni.

Baada ya kukamilisha zoezi hilo ogesha kuku wako wote kwa kutumia dawa ya Paranex iliyochanganywa kwenye maji yaliyowekwa kwenye dishi kubwa la lita ishirini au arobaini au hata ndoo unaweza kitumia. Uogeshaji utafanyika kwa namna ya kumtumbukiza kuku mmoja mmoja katika lile dishi au ndoo kisha utamtoa. Ni tendo linalotumia chini ya nusu dakika. Unamtumbikiza unamtoa unamtumbikiza tena unamtoa ni kama mara mbili hivi lengo ni kuhakikisha kuwa dawa inapenya vizuri katika kila sehemu ya mwili wake.

Baada ya kukamilisha zoezi hilo basi kuku wako watarudi bandani wakiwa wako vizuri na visumbufu vyote vikiwa vimetokomezwa kabisa. Kutokea hapo utaanza kuona sasa afya ya kuku wako ikianza kuimarika na kama walikuwa walishaanza kutaga watarudi katika utagaji wao wa kawaida.

Angalizo. Unapotumia dawa ya kuogesha ni vizuri zoezi hili likafanyika mchana wakati jua linawaka ili kusudi kuku waweze kukingwa na athari ya baridi itakayowasababishia kupata nimonia. Vilevile ni vizuri ukawa na mtaalamu karibu atakayekusaidia kuchanganya dawa kwa uwiano sahihi na maji ili kuepusha madhara kama dawa haitachanganywa katika uwiano.

Aman Ng'oma
Mkurugenza Mtendaji
Kinasoru East Africa (T) Ltd
0767989713
Nduka street, Chamwino Bananza
Dodoma - Tanzania
 
kuku pure kienyeji wamebaki 8 baada ya jana kumalza kusambaza oda n wa miezi 5&6 nawafuga mwnyw chanjo mdondo gombolo na ndui wamepata wazuri sana kwa wafugaji bei elfu 15 kwa kila mmoja napatikana 0624078252 picha njoo whtspp utapata napatkana goba dsm
 
Kwa kuzingatia wajibu wetu kwa Jamii, siku zote Kinasoru East Africa (T) Ltd inajaribu kuja na mawazo mapya kila siku, mawazo yenye msaada kwa wakulima na wafugaji wetu. Kwasasa tumetanua wigo wetu wa kuwahudumia wateja wetu. Tumeandaa wawakilishi wetu nchi nzima kwa ajili ya kurahisisha upatikanaji wa huduma zetu.
Tumeimarisha zaidi kitengo chetu cha masoko kwa mazao ya kilimo na mifugo. Na toka kitengo hiki kianze rasmi kufanya kazi yake kimeonyesha mafanikio makubwa. Dodoma tumeweza kusaidia kuwatafutia masoko wafugaji 75 mpaka sasa kati yao 40 ni wafugaji wa kuku wa asili waliyoboreshwa, 20 ni wafugaji wa kuku wa mayai wa kisasa Layers na 15 ni wafugaji wa kuku wa nyama wa kisasa Broilers.
Morogoro tuna wafugaji 60 wa kuku wa asili waliyoboreshwa na wana uongozi wao madhubuti na wote tunawasaidia kwenye kuwapatia masoko ya uhakika kwa ajili ya mayai yao. Lengo letu ni kufanya ufugaji uonekane wenye tija kwa wateja wetu.
Ili kuboresha huduma zetu kampuni yetu ya Kinasoru East Africa (T) Ltd imeanza rasmi kusajili wanachama ambao watakuwa wakipata huduma kutoka Kwetu. Huduma tutakazo toa kwa wanachama wetu ni pamoja kuwasaidia kutafuta Masoko ya mifugo pamoja na mazao yake. Pia wanachama wetu wafugaji watanufaika kwa ushauri na tiba kwa haraka pale mifugo yao itakapokuwa inaumwa. Njia tutakazotumia ni simu pamoja kutembelea na kufika eneo la tukio kwa wakati inapolazimu. Wakati huo huo wakulima wa viazi vya lishe pamoja na mihogo wao watanufaika na soko letu la uhakika ambalo liko tayari kwa ajili ya kuuza mbegu za mazao hayo.
Siku za mbele tumezamilia kutoa huduma ya kuwakopesha wanachama wetu waaminifu Vifaranga na Vyakula vya mifugo ili kuwajengea uwezo wa kumudu ufugaji pale wanapokuwa wamekwama. Tutafanya hivyo kwa kutambua kuwa wakati mwingine unakuta mfugaji umejenga banda na hela yote ikawa imeishia huko na ukawa huna tena pesa ya kuendelea na mradi wako wa ufugaji. Lakini vilevile tunatambua kuwa si kila siku mtu unaweza ukawa na pesa kwa ajili ya kuwanunulia chakula mifugo yako. Tunaamini huduma hii itakapoanza itakuwa na manufaa makubwa kwa wanachama wetu.
Ili uweze kuwa mwanachama na kunufaika na huduma zetu unapaswa kulipa ada ya tsh 50,000/= kwa mwaka.
Huduma ya Vifaranga tunasupply nchi nzima na kwa aina yoyote utakayoihitaji.
Tumedhamiria kuwahudumia wakulima na wafugaji kwa uadilifu na uaminifu mkubwa.
Karibu tukuongoze katika miradi ya Kilimo na Ufugaji.
Aman Ng'oma
Mkurugenzi Mtendaji
Kinasoru East Africa (T) Ltd
0767989713, 0715989713, 0786989713
Dodoma - Tanzania.
 
Back
Top Bottom