Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Mimi niliingiza vifaranga wa mayai 2000, wana wiki ya tano sasa. Fasta tumia OTC plus - inatibu magonjwa mengi yanayotokana na Bacteria.
Fanya fasta utapoteza wengi.

Asante Mkuu; nitawapa OTC Plus kuanzia leo na nitaleta feedback hapa.
 
Mkuu FUSO; natumaini tutajifunza mengi kutoka kwako kwani inaonekana tayari una uzoefu wa kutosha hata kufikia kuwa na batch ya kuku 2000. Vipi vifaranga unaangua mwenyewe kwa maana una incubator au unategemea kununua. Kama unanunua unatumia kampuni gani?
 
Nami nakubaliana nanyi kuwa thread hii itatusaidia wengi. Mimi nataka nianze kufuga kuku from scrach. Je, ninatakiwa niandae vitu gani kabla sijafikia hatua ya kuanza kununua vifaranga?
 
Nami nakubaliana nanyi kuwa thread hii itatusaidia wengi. Mimi nataka nianze kufuga kuku from scrach. Je ninatakiwa niandae vitu gani kabla sijafikia hatua ya kuanza kununua vifaranga?
  1. Unatakiwa kujenga banda la kuku, kumbuka 1 square feet kwa kuku mmoja; hivyo basi kama unataka kuwa na banda la kuku 200 unahitaji kujenga banda la 200 square feet. Mimi nimejenga mabanda yenye uwezo wa kuchukua kuku 300 hivyo basi nilijenga mabanda yenye 300 square feet kila moja.

Naamini wadau wengine wanaweza kutoa maelezo ya ziada katika eneo hili kutokana na uzoefu au utaalamu.
 
Asante Mkuu; nitawapa OTC Plus kuanzia leo na nitaleta feedback hapa.

OTC ina antibiotic na Vitamini so its very good kwa vifaranga. kama una simu mpigie shamba boy abadilishe maji aweke yenye hii dawa.
 
OTC ina antibiotic na Vitamini so its very good kwa vifaranga. kama una simu mpigie shamba boy abadilishe maji aweke yenye hii dawa.

Mkuu FUSO; asante sana, sasa hivi nakwenda kununua hiyo dawa na kubadilisha maji. Kwa sasa nimejenga mabanda ninapoishi hivyo basi nahudumia mwenyewe kwa kushirikiana na mke wangu ili tupate uzoefu. Hivyo basi asubuhi naanza kuhudumia kuku kabla ya kwenda kazini; kwa hiyo naacha nimeweka maji na chakula cha kutosha. Nashukuru huku niliko hakuna shida ya foleni kama hapo DAR naweza ku-rash home for only 10 minutes.
 
Ni vema mkuu umeanzisha thread hii, itatusaidia sana. na mimi nimejitosa kwenye biashara hii lkn inaelekea sikuplan vem. tatizo langun kubwa ni masoko, kwa hiyo naomba msaada katika hilo kwa mwenye ufahamu
 
Ni vema mkuu umeanzisha thread hii, itatusaidia sana. na mimi nimejitosa kwenye biashara hii lkn inaelekea sikuplan vem. tatizo langun kubwa ni masoko, kwa hiyo naomba msaada katika hilo kwa mwenye ufahamu
Soko la kuku mbona lipo la kutosha!!
 
Ni vema mkuu umeanzisha thread hii, itatusaidia sana. na mimi nimejitosa kwenye biashara hii lkn inaelekea sikuplan vem. tatizo langun kubwa ni masoko, kwa hiyo naomba msaada katika hilo kwa mwenye ufahamu

Kwa sasa mimi natumia soko la kawaida; kuna mtu namtumia sokoni ambapo kila kuku wakiwa tayari huja kuchukua. Naona soko siyo changamoto kubwa sana, bali inategemea na eneo husika. Kama umeshakaa vizuri katika uzalishaji unaweza kuwaacha wapate uzito wa kutosha ili usiwe na ushindani mkubwa sokoni.

Kama utafanikiwa kuwaacha mpaka wakafikia 2 kg naamini unaweza kupata soko la uhakika kwa supply wa hotels, supermarkets etc. Malengo yangu ya baadae; baada ya kukaa vizuri katika uzalishaji ni kuwaacha kuku wafike 2 kg and above halafu nina wa-process mwenyewe na ku-pack ili soko langu liwe ni kwa supply wa hotels.
 
Wakuu nafurai kwa kuanzishwa hii topic hapa mm mama yangu ndio mzoefu sana kwani ni wafugaji wale wa mwanzoni kabisa ushauri wangu ni huu hapa tupeane ushauri na mawazo ila matatizo yanatofautiana sana asa kwa vifaranga wa sasa hivi maana wanatoka sehemu mbali mbali hivyo basi vizuri kupendelea sana unapoona tatizo ukijaribu dawa hii ukiona aina afadhali bora kupeleka kifaranga au kuku kufanyiwa uchunguzi kisha wanajua dawa gani yakutibia aswa. kwanini nasema hivi jirani yangu alipoteza kuku 500 layers ndo walikuwa wanaanza kutaga akawa anapewa ushauri na kila mfugaji huu ni ugonjwa fulani tumia dawa hii, huyu nae anamwambia tumia hii mwisho wa siku kukuwanaendelea kufa alipokuja kwenda vetenary kufanyiwa uchunguzi ulikuwa ni ugonjwa mpya tofauti kidogo na walivyokuwa wanafananisha wafugaji wenzake alikuja kunusuru kuku 100.
 
Asante mkuu kwa kuweka hii thread hapa jamvini. Naona unaendela kupata ushauri mzuri tu. Ila ingependeza sana mkuu kama ungejitahidi kuangalia dalili zote zinazoonekana. Kubandika tu picha haitoshi maana magonjwa yanayowafanya vifaranga wajikunyate yako mengi tu. Pengine ungetueleza kuhusu kinyesi chao (kina rangi gani?), kwenye pua zao kukoje, vichwa vyao vikoje, manyoya yao yamekaaje, tabia yao kwenye chanzo cha joto zikoje n.k. Hii itawasaidia hata madaktari wa mifugo waliopo hapa jamvini kukushauri vizuri zaidi.

Habari ya kukimbilia tu Antibiotics bila kujua tatizo ni nini siyo vizuri, ingawa hii watu wengi wanaipenda lakini huwa ni zima moto, yaani unafanya kwa vile tu Antibiotics zinatibu magonjwa mengi. Madhara ya kutumia antibiotics bila uhakika ni kuwafanya wanyama wawe sugu kwa dawa zingine, hii inaweza kusababisha mifugo kufa kutokana na ugonjwa umekosa dawa maana walishakuwa sugu.

Sitaki kuamini kwamba eneo ulilopo hakuna kabisa mtaalam wa mifugo, lakini mara nyingi wafugaji mnaogopa gharama za kumwita Mtaalam na mnajifanyia wenyewe bila kujua madhara yanayoweza kutokea. Kwa leo naweza kukuacha ukatumia hiyo dawa uliyoshauriwa na huyo mwenzetu lakini siku nyingine hebu jitahidi umwone mtaalam wa mifugo. Kwa vile umeamua kuingia kwenye hii shughuli hebu kubali gharama zozote zinazokuja kwa ajili ya kuboresha ufugaji wako.
 
Asante sana kwa thread hii, kwani hata mimi ni mmoja wa watu ambao nipo njiani kuanza kufanya ufugaji wa kuku, kwa sasa nimejenga banda la ukubwa wa feet 36 kwa 12 natarajia kuingiza kuku wa kuanzia tarehe 13/3 na nilikuwa sijui ni kuku wangapi niweke kwa ukubwa wa banda hili, na pia natarajia kujenga lingine kubwa zaidi ya hili mwezi huu ila sina utaalamu wowote na ufugaji nashukuru sana kwa hilo. Nitawaomba msaada kila ninapokwama.
 
Asante mkuu kwa kuweka hii thread hapa jamvini. Naona unaendela kupata ushauri mzuri tu. Ila ingependeza sana mkuu kama ungejitahidi kuangalia dalili zote zinazoonekana. Kubandika tu picha haitoshi maana magonjwa yanayowafanya vifaranga wajikunyate yako mengi tu. Pengine ungetueleza kuhusu kinyesi chao (kina rangi gani?), kwenye pua zao kukoje, vichwa vyao vikoje, manyoya yao yamekaaje, tabia yao kwenye chanzo cha joto zikoje n.k. Hii itawasaidia hata madaktari wa mifugo waliopo hapa jamvini kukushauri vizuri zaidi.

Habari ya kukimbilia tu Antibiotics bila kujua tatizo ni nini siyo vizuri, ingawa hii watu wengi wanaipenda lakini huwa ni zima moto, yaani unafanya kwa vile tu Antibiotics zinatibu magonjwa mengi. Madhara ya kutumia antibiotics bila uhakika ni kuwafanya wanyama wawe sugu kwa dawa zingine, hii inaweza kusababisha mifugo kufa kutokana na ugonjwa umekosa dawa maana walishakuwa sugu.

Sitaki kuamini kwamba eneo ulilopo hakuna kabisa mtaalam wa mifugo, lakini mara nyingi wafugaji mnaogopa gharama za kumwita Mtaalam na mnajifanyia wenyewe bila kujua madhara yanayoweza kutokea. Kwa leo naweza kukuacha ukatumia hiyo dawa uliyoshauriwa na huyo mwenzetu lakini siku nyingine hebu jitahidi umwone mtaalam wa mifugo. Kwa vile umeamua kuingia kwenye hii shughuli hebu kubali gharama zozote zinazokuja kwa ajili ya kuboresha ufugaji wako.

Mkuu Job K; nashukuru sana kwa mchango wako na ushauri kwa ujumla. Kwa kweli nilifikiri kuweka picha ingeweza kutoa maelezo zaidi juu ya ugonjwa; lakini nilivyowachunguza hawa vifaranga huku nyuma kunakuwa kumelowa (inaonekana kama wanaharisha lakini majimaji yakiwa na rangi ya kijivu). Nafikiri wataalamu wataweza kubainisha kwamba huu ni ugonjwa gani, chanzo chake na tiba sahihi.

Nafikiri idadi ya wataalamu bado ni ndogo ukilinganisha na idadi ya huduma wanazotakiwa kutoa; hivyo basi ninaendelea kushirikiana na wataalamu wa mifugo, lakini ninaamini kupitia jukwaa hili tutaweza kujifunza zaidi kwa kutumia uzoefu na wataalamu.
 
Asante sana kwa thread hii, kwani hata mimi ni mmoja wa watu ambao nipo njiani kuanza kufanya ufugaji wa kuku, kwa sasa nimejenga banda la ukubwa wa feet 36 kwa 12 natarajia kuingiza kuku wa kuanzia tarehe 13/3 na nilikuwa sijui ni kuku wangapi niweke kwa ukubwa wa banda hili, na pia natarajia kujenga lingine kubwa zaidi ya hili mwezi huu ila sina utaalamu wowote na ufugaji nashukuru sana kwa hilo. nitawaomba msaada kila ninapokwama.

Mkuu Nicazius; nakupongeza kwa hatua uliyofikia na ninakukaribisha katika ufugaji wa kuku. Kwa ukubwa wa banda lako nafikiri unaweza kuweka vifaranga 400 kwani utakuwa na square feet 432. Itakubidi kutenga sehemu ya banda (nusu ya nafasi iliyopo) ndiyo utakayoweza kuitumia katika siku za mwanzo na kadri kuku wanapoongezeka ukubwa nawe unaendelea kutumia sehemu ya banda iliyobaki.
 
wakuu nafurai kwa kuanzishwa hii topic hapa mm mama yangu ndio mzoefu sana kwani ni wafugaji wale wa mwanzoni kabisa ushauri wangu ni huu hapa tupeane ushauri na mawazo ila matatizo yanatofautiana sana asa kwa vifaranga wa sasa hivi maana wanatoka sehemu mbali mbali hivyo basi vizuri kupendelea sana unapoona tatizo ukijaribu dawa hii ukiona aina afadhali bora kupeleka kifaranga au kuku kufanyiwa uchunguzi kisha wanajua dawa gani yakutibia aswa. kwanini nasema hivi jirani yangu alipoteza kuku 500 layers ndowalikuwa wanaanza kutaga akawa anapewa ushauri na kila mfugaji huu ni ugonjwa fulani tumia dawa hii, huyu nae anamwambia tumia hii mwisho wa siku kukuwanaendelea kufa alipokuja kwenda vetenary kufanyiwa uchunguzi ulikuwa ni ugonjwa mpya tofauti kidogo na walivyokuwa wanafananisha wafugaji wenzake alikuja kunusuru kuku 100

Mkuu drphone, unanikumbusha wakati fulani niliweka vifaranga 600 bandani na baada ya siku mbili nilianza kuokota vifaranga zaidi ya 50 kila siku vilivyokufa na hatimaye kubakiwa na kuku wasiozidi 50. Kweli nilijaribu dawa nyingi, lakini baada ya kumwomba mtaalamu bingwa kufanya uchunguzi wa kina ndipo tulipobaini kwamba wote tuliyochukua vifaranga vya batch ile tulikuwa na tatizo moja na kwamba vifaranga walipata ugonjwa wakati wa uzalishaji.

Supply kwa kushirikiana na wazalishaji walikubali kutulipa. Lakini kutumia jukwaa hili naamini tutapeana uzoefu zaidi na kusaidia kupunguza hasara katika ufugaji kwani wataalamu bigwa ambao wanaweza kufanya tafiti za kutosha bado ni wachache.
 
Mkuu FUSO; natumaini tutajifunza mengi kutoka kwako kwani inaonekana tayari una uzoefu wa kutosha hata kufikia kuwa na batch ya kuku 2000. Vipi vifaranga unaangua mwenyewe kwa maana una incubator au unategemea kununua. Kama unanunua unatumia kampuni gani?

Kwa hawa wa kisasa nimenunua toka Arusha Poutry farms wanauza 2,100 kila kimoja. sijafikia level ya kuanza kuangua vifaranga vya mayai mwenyewe.
 
Mgombezi uwe makini sana unapopata ushauri jamvini hasa kwenye suala la magonjwa ya kuku, navyojua mimi karibia 90% ya magonjwa ya kuku ni Typhoid, mafua, minyoo, utitiri, kuharisha maji maji ambayo yote haya yanatibika kwa urahisi sana ni kuwa makini tu kugundua dalili zake.

Pia lazima uwe makini sana kwenye chanjo. kwa vifaranga vidogo kama hivyo vyako ni vizuri kama nilivyokushauri kutumia OCT Plus sababu haina madhara na ina vitamini ndani yake. hiyo inataidia kuua bacteria unless hao vifaranga waka wamekuja na magonjwa mengine ambayo wametoka nayo huku huko kwenye parents stock.

Unashauriwa pia ukiona vifo vinafika 4 -10 kwa siku nakushauri kupeleka vifaranga wako (waliokufa) kwenye maabala kwa ajiri ya uchunguzi zaidi.
 
Mgombezi uwe makini sana unapopata ushauri jamvini hasa kwenye suala la magonjwa ya kuku, navyojua mimi karibia 90% ya magonjwa ya kuku ni Typhoid, mafua, minyoo, utitiri, kuharisha maji maji ambayo yote haya yanatibika kwa urahisi sana ni kuwa makini tu kugundua dalili zake.

Pia lazima uwe makini sana kwenye chanjo. kwa vifaranga vidogo kama hivyo vyako ni vizuri kama nilivyokushauri kutumia OCT Plus sababu haina madhara na ina vitamini ndani yake. hiyo inataidia kuua bacteria unless hao vifaranga waka wamekuja na magonjwa mengine ambayo wametoka nayo huku huko kwenye parents stock.

Unashauriwa pia ukiona vifo vinafika 4 -10 kwa siku nakushauri kupeleka vifaranga wako (waliokufa) kwenye maabala kwa ajiri ya uchunguzi zaidi.

Asante Mkuu; lakini naamini hapa tutakuwa tunaendelea kushirikishana uzoefu.
 
Mkuu drphone, unanikumbusha wakati fulani niliweka vifaranga 600 bandani na baada ya siku mbili nilianza kuokota vifaranga zaidi ya 50 kila siku vilivyokufa na hatimaye kubakiwa na kuku wasiozidi 50. Kweli nilijaribu dawa nyingi, lakini baada ya kumwomba mtaalamu bingwa kufanya uchunguzi wa kina ndipo tulipobaini kwamba wote tuliyochukua vifaranga vya batch ile tulikuwa na tatizo moja na kwamba vifaranga walipata ugonjwa wakati wa uzalishaji. Supply kwa kushirikiana na wazalishaji walikubali kutulipa. Lakini kutumia jukwaa hili naamini tutapeana uzoefu zaidi na kusaidia kupunguza hasara katika ufugaji kwani wataalamu bigwa ambao wanaweza kufanya tafiti za kutosha bado ni wachache.

Mkuu nimefuraia kwa kuelewa dhumuni langu nilichotaka kueleza ni kweli hapa tutabadilishana mawazo na uzoefu mzuri sana nina uhakika na hilo mkuu hapa ni mwisho wa reli.
 
Mkuu Nicazius; nakupongeza kwa hatua uliyofikia na ninakukaribisha katika ufugaji wa kuku. Kwa ukubwa wa banda lako nafikiri unaweza kuweka vifaranga 400 kwani utakuwa na square feet 432. Itakubidi kutenga sehemu ya banda (nusu ya nafasi iliyopo) ndiyo utakayoweza kuitumia katika siku za mwanzo na kadri kuku wanapoongezeka ukubwa nawe unaendelea kutumia sehemu ya banda iliyobaki.

Asante sana Mgombezi. Nitakupa taarifa na maendeleo yangu kadri siku zinavyokwenda mbele.
 
Back
Top Bottom