Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Zinazotengenezwa tanzania na zinazotoka nje. Zakuanzia mayai 100 mpaka 500. Bei zikoje?
 
Napenda kufahanu bei ya incubator zinazotengenezwa tanzania na zinazotoka china bei yake kuanzia ya mayai 100 mpaka 500.
Well said, ni sawa kabisa, kujifunzia unaweza anza na cha kununua, ila faida hamna, tengeneza chakula mwenyewe, hakikisha usafi wa vyombo na banda, zuia ubichi bandani, hakikisha wakiumwa tu, watenge ukianza kusitasita ndo anavyosema huyo banda zima linakwisha.

Unaweza fuga kiasi chochote ila as a precaution nakushauri weka 200 banda moja kwa kuanzia ila pata ushauri wa vipimo per sq mita.
 
Mimi naona unisaidie ushauri nina kuku wangu chotara mwanzon walikuwa wanataga vizur lakini kwa sasa ni kama hawatagi maana wanaweza taga mayai 10 au pungufu na nina kuku kama 80 hv. Halafu ikifikia kulalia hawa kuku wanalalia kweli maana nina wawili walilalia wakaangua vzur ila kama kuku wa5 hv waliharibu mayai wiki ya 2, tatizo ni nini?

Natanguliza shukrani
 
Mimi naona unisaidie ushauri nina kuku wangu chotara mwanzon walikuwa wanataga vizur lakin kwa sasa ni kama hawatagi maana wanaweza taga mayai 10 au pungufu na nina kuku kama 80 hv. Halafu ikifikia kulalia hawa kuku wanalalia kweli maana nina wawili walilalia wakaangua vzur ila kama kuku wa5 hv waliharibu mayai wiki ya 2, tatizo ni nini? Natanguliza shukrani
Kuhusu utagaji kuna dawa maalam za kuwapa ili kuwabust na kuwafanya waongoze kutaga, zaidi tunaweza kuwasiliana kwa msaada zaidi.Kuhusu kuharibu mayai, ni kutokana na kutotibiwa.Ni muhimu mayai kutibiwa kabla kuku hajaanza kuyaatamia.
 
Ina maana hayo mayai yakitibiwa kama unavyosema kuku hawa wanao uwezo wa kuangua vifaranga kama ilivyo kwa kuku wa kienyeji kabisa? Na je hizo dawa za kuwa boost ili watage hazina madhara maana nakwepa kufuga kuku wa kisasa kwa sababu ya madawa.
 
Ina maana hayo mayai yakitibiwa kama unavyosema kuku hawa wanao uwezo wa kuangua vifaranga kama ilivyo kwa kuku wa kienyeji kabisa? Na je hizo dawa za kuwa boost ili watage hazina madhara maana nakwepa kufuga kuku wa kisasa kwa sababu ya madawa.

Moureen,

Kuku wa kisasa hana uwezo wa kuangua mayai mwenyewe kama ilivyo kwa kuku wa kienyeji,isipokuwa mayai ya kuku wa kisasa (kuku wazazi) hutotolewa vifaranga kwa kutumia Incubators.

Busta hazina madhara,ni kama zilivyo dawa zingine. Dawa maalum ambazo huwachochea kuku kudaga zaidi.Busta mara nyingi hutumika kutokana na mfugaji kuwa na formula isiyofa isiyokidhi mahitaji kuwafanya kuku waweze kutaga zaidi, lakini kama mfugaji atakapata formula nzuri ya uchanganyaji wa chakula kuku wake watataga tu vizuri.
 
Hi! kichwa mbovu nilitaka kujua kama biashara ya mayai ya kuku wa kienyeji inalipa kwa hapa Tanzania. Nina plan za kufanya hii biashara on commercial basis. Na je unaposema kuku chotara inamaanisha bado mayai yake yatakuwa ni kama ya kuku wa kienyeji? Kuna aina ya kuku inaitwa Longhorn inasemekana ni aina ya kuku wanaotaga mayai mengi zaidi duniani je hii ni aina ya kuku wa kienyeji kama sio ni aina gani ya kuku wa kienyeji wanaotaga mayai mengi zaidi nijuze tu hata kama wanapatikana nje ya Tanzania ilimradi tu wawe wa kienyeji maana ndio biashara ninayotaka kufanya kwa sasa.
 
hi! kichwa mbovu nilitaka kujua kama biashara ya mayai ya kuku wa kienyeji inalipa kwa hapa Tanzania.Nina plan za kufanya hii biashara on commercial basis.Na je unaposema kuku chotara inamaanisha bado mayai yake yatakuwa ni kama ya kuku wa kienyeji? kuna aina ya kuku inaitwa Longhorn inasemekana ni aina ya kuku wanaotaga mayai mengi zaidi duniani je hii ni aina ya kuku wa kienyeji kama sio ni aina gani ya kuku wa kienyeji wanaotaga mayai mengi zaidi nijuze tu hata kama wanapatikana nje ya Tanzania ilimradi tu wawe wa kienyeji maana ndio biashara ninayotaka kufanya kwa sasa.
Salari,

Kiasili kuku wa kienyeji si watagaji sana,kama ilivyo kwa kuku wa kisasa wa mayai.Ndio maana ili kuboresha kosaafu ya kuku wa kienyeji tuna wacross na kuku wa kisasa wenye wenye uwezo mkubwa wa kutaga mayai.Na kwa kufanya hivyo,tunakuwa tumewaongezea uwezo wa utagaji wa hawa kuku wa kienyeji. Mayai yanayotagwa na kuku chotara hayana tofauti na kuku wa kienyeji.

Na kwa upande wa longhorn, hao ni kuku wa kisasa,kama walivyo kuku wengine wa kisasa.Mara nyingi kuku wa kienyeji wanapatikana zaidi kwenye nchi zetu za afrika,kwa nchi za wanzetu nje ya Afrika hii kosaafu ya kuku wa kienyeji imetoweka na waliobaki nao ni kuku wa kisasa ambao wamepitia kwenye mlolongo mwigi wa mabadiliko yao.Kuku wa kienyeji aina ya kuchi ukimcross na kuku wa kisasa aina rhode island red au Barred polymouth rock wale wachotara watakaozaliwa huwa wana uwezo mkubwa wa kutaga mayai.

Soko la mayai hapa nchini ni kubwa sana kuazia kwenye supermakerts hadi mitaani kwa wachoma chips.
 
Mkuu Kichwa, si kweli kwamba Kuku wa kienyeji wako Africa pekee, Bado hata baadhi ya Nchi za Ulaya wako wengi tu, Asia ndo usiseme, na Kuna Mbegu fulani ya kuku wa Kienyeji kutoka Israeli naifuatalia Kenya make niliambiwa wanapatikana huko so niko kwenye process za kuwanunua baadhi nione wako vipi
 
Mkuu Kichwa, si kweli kwamba Kuku wa kienyeji wako Africa pekee, Bado hata baadhi ya Nchi za Ulaya wako wengi tu, Asia ndo usiseme, na Kuna Mbegu fulani ya kuku wa Kienyeji kutoka Israeli naifuatalia Kenya make niliambiwa wanapatikana huko so niko kwenye process za kuwanunua baadhi nione wako vipi

Chasha,

Nashukrani kwa kunifahamisha hilo,nilikuwa sijui maana siku zote huwa naagiza kuku wazazi kutoka nje ila sijapata kusikia uwepo wa kuku wa kienyeji huko. Nimepata somo jipya leo nitafuatilia zaidi ili nipate kuwajua zaidi tena ikibidi majina yao kama ilivyo kwetu mfano kuchi nk.
 
Nimekupata mtaalam. Nipi hizo contact zako tuwasiliane.

NAFASI INAYOHITAJIKA KWA KUKU 1000 WENYE RIKA TOFAUTI (MABANDA YA KUKU)

[TABLE="class: grid, width: 500, align: center"]
[TR]
[TD]RIKA[/TD]
[TD]CHICKS

VIFARANGA[/TD]
[TD]GROWERS

KUKU
WANAOKUWA[/TD]
[TD]LAYERS

KUKU
WANAOTAGA[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]UMRI
KTK
WIKI[/TD]
[TD]0-6[/TD]
[TD]7-20[/TD]
[TD]20-80[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]KUKU/ENEO LA
M[SUP]2 [/SUP]MOJA ZA MRABA[/TD]
[TD]12[/TD]
[TD]9[/TD]
[TD]6[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]M[SUP]2 [/SUP]ZINAZOHITAJIKA
/KUKU 1000
[/TD]
[TD]83.7M[SUP]2[/SUP][/TD]
[TD]111.2M[SUP]2[/SUP][/TD]
[TD]166.6M[SUP]2[/SUP][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]


Eneo watakaloshinda kuku 1000 wakati wa mchana, ambao hufugwa ktk mfumo wa nusu huria ni mita za mraba 10,000 .Hii inamaana kwamba ,kuku mmoja anahitaji eneo lenye mita za mraba 10.Kuhusu utagaji kuku wa kienji hana sifa ya utagaji wa mayai mengi.Kuku wa kienyeji hutaga kwa mzunguko.Kila mzunguko mmoja hutaga hutaga wastani wa mayai 15 na kuanza kuatamia,kutotoa na kulea vifaranga.Mzunguko huo huchukua wastani wa kipindi cha miezi 4 hadi 6 .Hali hiyo hiyo humfanya atage mayai machache kati ya mayai 30 hadi 60 kwa mwaka ukilinganisha na kuku wa kisasa ambao hutaga mayai 270 hadi 300.

Kuku wa kienyeji ukitaka watage mayai mengi wasiruhusiwa kuatamia,kila mayai yanayotagwa yaokotwe na kuhifadhiwa na kama mfugaji atahitaji kutotoresha, kama kuna kuku wengi ,ni vyema ikatumika machine ili kuzalisha vifaranga wengi zaidi.Kuku wa kienyeji anapokuwa kwenye mzunguko wa utagaji,kila siku hutaga yai moja.

Mawasiliano yangu nimekutumia kwenye private message yako ya jf,nenda kwenye notification yako fungua utaona.
 
Kwa wanaohitaji kuku mcahotara kwa ajili ya mbegu,wanapatikana, wako 1600,wana umri wa miezi 5,wote wako rika moja.Kama utawachukua utakaa nao mwezi mmoja tu kisha wataanza kutaga.Utakuwa na uwezo wa kupata mayai mengi,bora na salama ambayo utayatumia kuzalisha vifaranga kwa njia ya mashine.Pia wana uwezo wa kuatamia wenyewe.

Bei yake ni tsh 9000.Kwa anayehitaji anipm.

Ok nitawahitaji hao mwezi uao, wasiwasi yangu ni moja tu. Nayo ni kuwa hawataathirika na mabadiliko ya ghafla ya mizingira? Kuna uwezekano mkubwa wa kuwepo na tofauti kubwa ya mazingira yako na yangu na pia hata chakula kwani unajua kuna mavyakula mengi tu sokoni yeynye ubora tofauti tofauti. hebu saidia katika hili mkuu wetu.
 
Kwa wanaohitaji kuku mcahotara kwa ajili ya mbegu,wanapatikana, wako 1600,wana umri wa miezi 5,wote wako rika moja.Kama utawachukua utakaa nao mwezi mmoja tu kisha wataanza kutaga.Utakuwa na uwezo wa kupata mayai mengi,bora na salama ambayo utayatumia kuzalisha vifaranga kwa njia ya mashine.Pia wana uwezo wa kuatamia wenyewe.

Bei yake ni tsh 9000.Kwa anayehitaji anipm.

Asante sana kwa yote kichwa mbovu. Mimi pia nitawahitaji labda mwezi ujao kwani sasa hivi kwenye Mpango Kazi wa ukarabati wa mabanda. Wasiwasi au hofu yangu ni moja tu. Hawa hawataathirika na mabadiliko ya ghafla ya mazingira. Kwani mazingira ya huko kwako yanaweza kuwa tafauti na ya kwangu.

Hata chakula pia, kuna uwezekano wa kuwa na tofauti za vyakula kwani siku hizi mavyakula ya kuku yako ya aina nyingi sana na yaliyo chakachuliwa ni mengi sana. Tusaidie katika hili. By the way nilielezwa kuwa asali pia ni good appetizer kwa kuku, hili lina ukweli gani kitaalam mkuu?
 
Inategemea unataka incubator za kutoka wapi,hapa hapa nchini au nje ya nchi

Kwa ajili ya incubator za nje, jaribuni pia kupitia website ya Egg incubators | Poultry incubator | Egg incubation | Chicken incubation | Incubation eggs pia deliveriestheincubatorshop.co.uk.Wana incubators nyingi na vitu vingine vingi kwa ajili ya ufugaji wa kuku na hata hao parent stock wanoa. Ebu wapitieni ila tatizo lao ni kuwa sheria za EU haziwaruhusu kuuza moja kwa moja nje ya EU lakini
ukiwa na mtu au ndugu yako huko Ulaya, anaweza kukununulia na kukutumia. Hii haizuiliwi. Asanteni kwa leo.
 
Kimsingi kuku wote wanalipa katika ufugaji,mfano kuku wa nyama broilers,kila wiki ukaingiza let say vifaranga 300 ,ukawafuga kwa kufuata kanuni,ukawafuga kwa wiki 8 ili uwauze kwa tshs. 6000/=.Kama kila wiki utaingiza vifaranga ina maana bechi ya kwanza watakapofikia wiki 8,tayari utakuwa na bechi nyingine 7 zinafuata.Chukulia vifo ni 50 katika kuku 300 ingawa inaweza ikawa chini ya hapo.Kwa hiyo katika kila bechi kila wiki utakuwa na kuku 250.

Kimahesababu kuku 250 ukizidisha mara tshs.6000/=,utapata tshs. 1500,000/= kwa wiki na kwa mwezi utapata tshs 6000,000/=.Mapato ya broilers yanaanza baada ya miezi 2 yaani wk 8 ingawa unaweza ukawauza chini ya hapo lkn kwa uzito wa chini kidogo ndio maana inashauriwa wauzwe wk ya nane.

Kuku wa mayai pia nao wanalipa sana tatizo inatakiwa uwe na mtaji mkubwa kwa ajili ya gharama ya kuwanunua na chakula ,mathalani kwa sasa baadhi ya makampuni ya kutotoresha vifaranga wanauza kila kifaranga tshs.2500.Kila kifaranga mpaka atakapoanza kutaga atahitaji kilo 8 za chakula,ukiongeza na madawa,mfanyakazi nk utajikuta unatakiwa uwe na mtaji mkubwa kweli.Mapato ya kuku wa mayai utaanza kupata kwa wastani kuanzia mwezi wa 5 katikati .Baada ya hapo utakuwa na kazi kuuza mayai tu mpaka watakapo choka wiki ya 80 kama umewatunza kwa kufuata misingi na kanuni boro za ufugaji.

Kama ni kuku wa mayai,wakisasa ni wazuri zaidi kwa kuwa wanataga kwa wingi. Kama ni wa nyama ukiweza kufaga machotara ni wazuri zaidi kutokana na kuwa na soko la uhakika.Watu wengi sasa hivi wanapenda kuku wa kienyeji hivyo machota, nyama yake haina tofauti na kuku wa kienyeji,pia ukiweza kuwafuga kwa miezi 6 utaweza kuwauza kila kuku kwa tsh.10000/= bila mteja anayenunua kulalamika.Kuku pure wa kienyeji wana ukuaji hafifu.

Nimehamasika kwa kiasi kikubwa na ufugaji wa kuku wa kizungu na kienyeji, shida yangu kubwa ni kupata soko la uhakika, je unaweza kunisaisia kupata masoko ya aina tajwa ya kuku hao ili kupunguza usumbufu wa kupata masoko ya uhakika? Usisite kuwasiliana nami. Regards
 
Jamani msione kimya kwa muda mrefu,nilikuwa kwenye mitihani kwa muda wa wiki tatu mfululizo,na baada ya kumaliza mitihani nikawa nimeondoka kuelekea Songea na mpaka hivi sasa nipo huku Songea.Nimefika huku Songea moderm yangu ya tigo inasumbua kidogo,nashindwa kujibu kwa wakati na kuendelea na darasa letu.Ila kwa wale wanaohitaji miongozo mbalimbali ya ufugaji bora wa kuku wa kisasa na kienyeji naomba tuwasiliane kwa namba 0767989713 au 0715989713.

Hata kama una mambo yanakutatatiza kwenye ufugaji wako pia usisite kuwasiliana nami,tutasaidiana.

Pia kwa wale ambao wanafuga kuku wa mayai,wamejitahidi kuwahudumia kwa kila namna lakini kuku wakawa hawatagi katika kiwango cha kukuwezesha kupata faida,nina ufumbuzi wa tatizo hilo.
 
Back
Top Bottom