Elections 2010 Ufunguzi wa Kampeni ya Chadema Jangwani 2010

Elections 2010 Ufunguzi wa Kampeni ya Chadema Jangwani 2010

RedDevil

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2009
Posts
2,367
Reaction score
1,523
Leo kama tunavyojua wengi wetu kuwa Chadema inafanya ufunguzi wake wa kampeni hapo jangwani jijini Dar. Naomba wadau tupeane taarifa (Breaking News) za kuhusu huo mkutano pamoja na JWTZ, vipi wanarusha midege yao.

Ahsanteni.:violin::violin::juggle:

PICHA:

10pbo5s.jpg

5drouh.jpg

ilf4aa.jpg

 
Ingalikuwa vyema iwapo Chadema itakuwa imenunua muda kwa hivi vituo vyetu vya TV kwa ajili ya sisi tuliokuwa mbali kushuhudia tukio hilo muhimu. Ila sidhani kama kuna Kituo cha TV kitadiriki kurusha matangazo hayo jinsi walivyo waoga!
 
Hivi mkutano unaanza saa ngapi?
Nimepita jangwani nimeona pamepooza sana
 
TBC1 wataonyesha live kuanzia saa 9 mchana mpaka saa 12 jioni. Kwahiyo kwa wale wasioweza kwenda jangwani wanaweza kuangalia kupitia luninga zao.

CHADEMA hawajanunua air time lakini ni sheria kwa TBC1 as a public TV to air, kama ambavyo walifanya kwa CCM jumamosi iliyopita, CUF jana, leo watafanya vivyo hivyo kwa CHADEMA.
 
Nimeisoma ilani ya Chadema na mwanzoni kabisa nimeanza kuona tatizo lile lile ambalo Chadema wanasema wanapingana nalo.Longolongo na kutoweka jambo wazi kwa mapana yake.Sehemu iliyoanza kunipa mashaka kabla hata sijafika mbali ni hii:

Ufisadi ni nini?

Tunapozungumzia Ufisadi tunazungumzia mfumo na muundo wa utawala ambao umetengeneza utamaduni wa kuishi kiujanja ujanja, matumizi mabaya ya madaraka na vyeo, ufujaji wa mali ya umma, wizi wa fedha za umma, utaratibu wa kubebana na ajira zinazotegemea kujuana, na mahusiano ya watawala na watawaliwa ambayo msingi wake ni woga, vitisho, na kujiona watu wanastahili zaidi kuliko wengine. Ni mfumo uliodidimiza tawala mbalimbali duniani na ambao pasipo kuushughulikia kwa makusudi unasimama kama tishio lilopo na la hatari kwa Tanzania kuliko vita. Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alisema kuwa "ufisadi na rushwa ni adui mkubwa zaidi wa maslahi ya wananchi wakati wa amani kuliko vita" (Bungeni, Mei 17, 1960, kikao cha 35 cha bajeti).

Ufisadi ndio kizuizi kikubwa cha kuboresha maisha ya watu wetu; ni kikwazo kikubwa katika kujenga na kuimarisha utawala bora, utawala wa sheria na haki za raia. Ufisadi ndio kikwazo kikubwa kabisa cha maendeleo ya nchi. Ndio kusema, juhudi zetu za kujiletea maendeleo kama nchi haziwezi kufanikiwa bila kwanza kukomesha ufisadi.

Tumekuwa na miaka takribani 50 ya CCM. Wameahidi kila aina ya ahadi na wamefanya kila makosa, lakini tukawavumilia na tukawapa nafasi nyingine tukiamini kwamba mambo yatabadilika. Kila tulipowapa nafasi, hali ilizidi kuwa mbaya, tukasogea kutoka kubaya kwenda kubaya zaidi. Lengo lao kubwa limekuwa ni kushinda uchaguzi, ili waendelee kutumia madaraka tunayowapa kwa ajili ya kujinufaisha kwa njia ya ufisadi.

Ni wakati wa mabadiliko, na fursa ya kufanya mabadiliko ni huu uchaguzi wa 2010 na siyo 2015. Tukisubiri wakati mwingine tutakuwa tumechelewa sana. Na tukiwapa nafasi nyingine moja CCM ya kututawala tena tutakuwa tumewapa leseni ya kuendelea kutawala wapendavyo na tutakuwa tumejihukumu sisi wenyewe na uzao wetu katika maisha ya umaskini wa kudumu.
Katika sehemu hiyo ni wazi kuwa Chadema wanataka umma uamini kwamba matatizo yote tuliyo nayo yanatoka na utawala!

Wanataka tuamini hata wale watu wanaotumia vyandarua kufugia kuku badala ya kujikinga na malaria kuwa ni tatizo la watawala.

Wanataka tuamini kuwa serikali inawafuatilia wakwepa kodi sugu kuwa ni unyanyasaji simply kwa sababu JK kapita mahali basi hata kama TRA walitaka kudai kodi basi wasidai tena.

Wanataka tuamini hata kushindwa kwetu kuweka akiba na kujaa kwenye sehemu za starehe siku za kazi,kuchangia mambo ya burudani zaidi kuliko elimu na maendeleo yote hayo kuwa ni tatizo la serikali!!!!!

Ilani haisemi kwamba hakuna chama kinachoweza kuwaondolea watu umasikini kwa asilimia mia. Natumaini Chadema watajipanga zaidi miaka ijayo kuelezea wananchi kwamba elimu ya kujitambua binafsi ni muhimu sana kabla ya lolote.On top of that Chadema inasema kwamba 2010 ndo wakati muafaka!!!

What are the justifications kwa hili??U mean 2010 ndo Chadema imeona nchi inaporomoka au ni ile "I wana be the boss too"!!!

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
I will be there, the first one to attend since the old school days when it was compulsory. Sitalipwa na mtu ili kuhudhuria, sitahitaji usafiri wa mtu ili kuhudhuria, nikikuta posters nitanunua , nikikuta fulana nitanunua, kama ilani inauzwa nitanunua ili kuchangia chama changu.

Dr. SLAA - The Presdent of The United Republic of Tanzania (2010-2015)
 
Mkuu kati ya vitu ambavyo Chadema wasingependa kusikia, ni kujaribu kuwakosoa; hapa si ajabu ukabatizwa 'kibaraka wa mafisadi'
 
Ntemi: Longolongo wagon, hawana jipya hawa jamaa. Ilani yao ni kama proposal moja ndefu sana. Isome kwa makini.

Kakalende: Siku hizi nasikia mtu ukiongea wanasema umetumwa, sasa sijui mimi nimetumwa na CCM au mzimu wa Nyerere!

Teh teh
 
Hawa hawajajipanga katika kuchukua madaraka.Hawakujitayarisha na hawana strategy na joto hasa la opposition kwa sababu hawakuja na sera za maana.Kila kitu wanalaumu serikali.Hat akiwa na na suruali ilijoyajaa viraka atalaumu serikali.Ajabu hawa watu!!
 
Kwa hiyo unasemaje?

Sasa Ntemi hapo una maana gani?Jamaa ndiyo kasema.Chadema kwa mfano wanalaumu miaka takriban 50 ya utawala wa CCM na papo hapo wana quote maneno ya Mwalimu ambaye alikuwa Rais na Mwenyekiti wa CCM kwa takriban miaka 23 kati ya hiyo 50.

Wapinzani wa kweli wanatakiwa kuja na kauli zao mbadala siyo kuchukua mawazo ya Mwenyeketi wa CCM wa zamani.
Unadhani angekuwa hai ange suport Chadema?? What a miscalculation!
 
Hawa hawajajipanga katika kuchukua madaraka.Hawakujitayarisha na hawana strategy na joto hasa la opposition kwa sababu hawakuja na sera za maana.Kila kitu wanalaumu serikali.Hat akiwa na na suruali ilijoyajaa viraka atalaumu serikali.Ajabu hawa watu!!
Alnadaby na Nostradamus mna-share kitu kimoja: mawazo yenu hayaoni mbali ya pua zenu!!! CCM yenye sera na ''ilani ya maana na iliyokamilika'' imeipeleka wapi Tanzania na Watanzania? Mkiweza kujibu then kosoeni ilani za vyama vingine!
 
Very contradictory!!!Naamini watanzania wana macho na masikio.Kama wapinzani ni wa dizaini hii,CCM itakuwepo for lots of years to come.
 
<p>
Nimeisoma ilani ya Chadema na mwanzoni kabisa nimeanza kuona tatizo lile lile ambalo Chadema wanasema wanapingana nalo.Longolongo na kutoweka jambo wazi kwa mapana yake.Sehemu iliyoanza kunipa mashaka kabla hata sijafika mbali ni hii:</p>
<blockquote><blockquote><p><font face="Georgia"><font size="3"><font color="navy"><b>Ufisadi ni nini?</b></font></font></font></p>
<p>&nbsp;</p>
<p><font face="Georgia"><font size="3"><font color="navy"> Tunapozungumzia Ufisadi tunazungumzia mfumo na muundo wa utawala ambao umetengeneza utamaduni wa kuishi kiujanja ujanja, matumizi mabaya ya madaraka na vyeo, ufujaji wa mali ya umma, wizi wa fedha za umma, utaratibu wa kubebana na ajira zinazotegemea kujuana, na mahusiano ya watawala na watawaliwa ambayo msingi wake ni woga, vitisho, na kujiona watu wanastahili zaidi kuliko wengine. Ni mfumo uliodidimiza tawala mbalimbali duniani na ambao pasipo kuushughulikia kwa makusudi unasimama kama tishio lilopo na la hatari kwa Tanzania kuliko vita. Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alisema kuwa &quot;ufisadi na rushwa ni adui mkubwa zaidi wa maslahi ya wananchi wakati wa amani kuliko vita&quot; (Bungeni, Mei 17, 1960, kikao cha 35 cha bajeti). </font></font></font></p>
<p>&nbsp;</p>
<p><font face="Georgia"><font size="3"><font color="navy"> Ufisadi ndio kizuizi kikubwa cha kuboresha maisha ya watu wetu; ni kikwazo kikubwa katika kujenga na kuimarisha utawala bora, utawala wa sheria na haki za raia. Ufisadi ndio kikwazo kikubwa kabisa cha maendeleo ya nchi. Ndio kusema, juhudi zetu za kujiletea maendeleo kama nchi haziwezi kufanikiwa bila kwanza kukomesha ufisadi.</font></font></font></p>
<p>&nbsp;</p>
<p><font face="Georgia"><font size="3"><font color="navy"> Tumekuwa na miaka takribani 50 ya CCM. Wameahidi kila aina ya ahadi na wamefanya kila makosa, lakini tukawavumilia na tukawapa nafasi nyingine tukiamini kwamba mambo yatabadilika. Kila tulipowapa nafasi, hali ilizidi kuwa mbaya, tukasogea kutoka kubaya kwenda kubaya zaidi. Lengo lao kubwa limekuwa ni kushinda uchaguzi, ili waendelee kutumia madaraka tunayowapa kwa ajili ya kujinufaisha kwa njia ya ufisadi. </font></font></font></p>
<p>&nbsp;</p>
<p><font face="Georgia"><font size="3"><font color="navy"> Ni wakati wa mabadiliko, na fursa ya kufanya mabadiliko ni huu uchaguzi wa 2010 na siyo 2015. Tukisubiri wakati mwingine tutakuwa tumechelewa sana. Na tukiwapa nafasi nyingine moja CCM ya kututawala tena tutakuwa tumewapa leseni ya kuendelea kutawala wapendavyo na tutakuwa tumejihukumu sisi wenyewe na uzao wetu katika maisha ya umaskini wa kudumu.</font></font></font></p>
</blockquote></blockquote><p>Katika sehemu hiyo ni wazi kuwa Chadema wanataka umma uamini kwamba matatizo yote tuliyo nayo yanatoka na utawala!</p>
<p>&nbsp;</p>
<p>Wanataka tuamini hata wale watu wanaotumia vyandarua kufugia kuku badala ya kujikinga na malaria kuwa ni tatizo la watawala.</p>
<p>&nbsp;</p>
<p>Wanataka tuamini kuwa serikali inawafuatilia wakwepa kodi sugu kuwa ni unyanyasaji simply kwa sababu JK kapita mahali basi hata kama TRA walitaka kudai kodi basi wasidai tena.</p>
<p>&nbsp;</p>
<p>Wanataka tuamini hata kushindwa kwetu kuweka akiba na kujaa kwenye sehemu za starehe siku za kazi,kuchangia mambo ya burudani zaidi kuliko elimu na maendeleo yote hayo kuwa ni tatizo la serikali!!!!!</p>
<p>&nbsp;</p>
<p>Ilani haisemi kwamba hakuna chama kinachoweza kuwaondolea watu umasikini kwa asilimia mia. Natumaini Chadema watajipanga zaidi miaka ijayo kuelezea wananchi kwamba elimu ya kujitambua binafsi ni muhimu sana kabla ya lolote.On top of that Chadema inasema kwamba 2010 ndo wakati muafaka!!!</p>
<p>&nbsp;</p>
<p>What are the justifications kwa hili??U mean 2010 ndo Chadema imeona nchi inaporomoka au ni ile &quot;I wana be the boss too&quot;!!!</p>
<p>&nbsp;</p>
<p>MUNGU IBARIKI TANZANIA.
</p>
<p>&nbsp;</p>
wakuu heshima kwenu, naheshimu sana mawazo na mitizamo yenu, ukiipitia vizuri ilani ya Chadema utakuta imeainisha mapungufu na juu ya nini chadema itakifanya, ukipitia na kuangalia negative tu mapungufu utayakutata hata katika uumbaji wa Mungu unaweza kukosoa, sijaona tatizo kama ni la tafsiri juu ya ufisadi maana waliotengeneza si mabingwa wa lugha, ni wataalam na mabingwa katika fani zao, tunayo,imani watanzania watapata muda wa kuwasikiliza wagombea wetu na kununua bidhaa hiyo ya ilani kwa maslahi ya nchi yetu

Natanguliza shukrani kwenu wana jamvi.
 
Kweli Macho Mdiliko!Kuna tofauti yoyote kimaisha unayoiona toka mwaka 2005 hadi 2010?A very fair question.
 
@Hamuyu:safi kabisa.Kwa hiyo unakubali ina makosa na unakubali tatizo na upinzani ni kushambulia tu mabaya ya serikali??Hii ni kazi ya civil society,si chama cha siasa!!Tuamke!!Wapinzani hawana jipya
 
I will be there, the first one to attend since the old school days when it was compulsory. Sitalipwa na mtu ili kuhudhuria, sitahitaji usafiri wa mtu ili kuhudhuria, nikikuta posters nitanunua , nikikuta fulana nitanunua, kama ilani inauzwa nitanunua ili kuchangia chama changu.

Dr. SLAA - The Presdent of The United Republic of Tanzania (2010-2015)
asante mkuu kwa uzalendo wako, nchi yetu tutaijenga wenyewe au kuibomoa wenyewe, inshaallah
 
Back
Top Bottom