Ufunuo usiosemwa: Je, Lilith ndio nyoka wa Eden? Je, ni mke wa kwanza wa Adam?

Ufunuo usiosemwa: Je, Lilith ndio nyoka wa Eden? Je, ni mke wa kwanza wa Adam?

Lilith anayesemekana ni mke wa kwanza wa Adam. Hatajwi popote kwenye Biblia takatifu zaidi ya kwenye kitabu cha Isaya 34 : 14, na ambapo hata hivyo kutajwa kwake hakuna mahusiano kabisa na Adam.

Kuna simulizi nyingi nje ya Biblia zinazokinzana na nyingine kushabihiana kumhusu mwanamama huyu Lakini zote zinakubaliana katika jambo moja kuwa Lilith alimwacha Adam kwakuwa hakutaka kuwa chini ya amri za mwanaume. Hakutaka kuongozwa wala kutawaliwa na mwanaume kwa utetezi kwamba, wote waliumbwa siku moja na kwa malighafi zinazofanana. Hivyo hakuna mkubwa kuliko mwingine.

Sasa asili ya Lilith ni nini!? ni wapi?

Lilith anaonekana mara nyingi kwenye Biblia ya Kiebrania na huko anajulikana kama malkia wa usiku, pepo katili la usiku lenye tamaa kubwa ya ngono... Huku kazi yake kubwa ikiwa ni kuiba watoto gizani usiku. Lilith sio jina jema popote zaidi ya kwenye imani za kipagani na kishetani.

Asili ya Lilith inatajwa sana kwenye simulizi za Wayahudi (c 700-1000). Hapa anatajwa kama mke wa kwanza wa Adam waliyeumbwa pamoja (mwanzo 1:27, kisha akafuatia mke wa pili wa Adam baada ya Lilith kuondoka (mwanzo 2:22). Hapa inasemekana Lilith alimuacha Adam kwenye bustani ya Eden na hakutaka kurudi huko na kwenda kugawa kipochi manyoya kwa malaika muasi aliyeitwa Samael. Lakini pia simulizi nyingine zinasema aliondoka na kwenda kungonoka na shetani ili kuendeleza kizazi na uzao wa shetani.

Hii inaweza kuleta uhalisia kidogo kutokana na vile satanism wanavyomchukulia Lilith, kumuamini na kumwabudu kama mungu mwanamke, mke wa baba yao shetani.

Hizi zote ni simulizi nje ya Biblia takatifu lakini kitu kimoja kilicho wazi ni kwamba kuna hicho kiumbe chenye jinsia ya kike kiitwacho Lilith ambacho hakuna popote kinatajwa kwa wema. Kuna mahali anaelezewa kama mchawi, pepo aliyengonoka na shetani kwa makusudi mazima ya kuendeleza kizazi chao kama tulivyoona hapo juu.


Ibada za kutoa kafara katika satanism

Tunaterejea tena kutazama yale mambo yaliyoacha utata na pengine hayajawahi kujadiliwa na wengi.

Tumeshajadiliana sana kuhudu Eden, Hawa, tunda la mti wa kati(mti wa ujuzi wa mema na mabaya), nyoka na Adam. Katika vyote hivi kuna mtu pia tumemjadili kwa kiasi, mtu huyu hata maandiko hayamtaji wala kumjadili sana. Mtu huyo ni Lilith, mwanamke anayesemekana kuwa mke wa kwanza wa Adam.

Jambo hili la Adam kuwa na mke aliyeitwa Lilith halitajwi kwenye misahafu yetu hii tunayoijua bali kwenye maandiko mengine lakini ya kiimani pia.

Lilith anayetajwa kwenye maandiko hayo kama mwanamke kiburi na mwenye nguvu, na ambaye pia inasemekana alizaliwa sawa na Adam, aliasi na kutengana na Adam baada ya kushindana tabia. Lilith alitaka kuwa na mamlaka makubwa kwa Adam.

Habari za Lilith zinaishia pale alipoachana na Adam, kisha Adam alirejea Eden kuanza maisha ya upweke akiwa kama mtalikiwa na tunaambiwa Lilith alikuja kugeuka kuwa kiumbe cha kuzimu.

Maisha ya upweke Eden yanamfanya Mungu kumtengenezea Adam msaidizi wa kufanana naye
ndipo Adam sasa anamshukuru Mungu kwa kusema. Sasa huyu ni nyama katika nyama zangu na mfupa katika mifupa yangu? (Wanazuoni wanatafsiri kauli hii kama kwamba mwanzoni alikuwepo mwingine ambaye hakutokana na Adam! ) Je, mtu huyo ni Lilith?

Maisha mapya ya furaha upendo na mapatano ndani ya Eden kati ya Adam na Eva/Hawa yanamvuta nyoka anayetajwa kama ibilisi akijulikana kama malaika aliyeasi mbinguni (Lilith?) Huyu ndio pekee aliyejua siri ya uumbaji (ukiacha Mungu) na siri ya tunda la mti wa kati; mti wa ujuzi wa mema na mabaya!

Kwa hakika Lilith hakupenda kabisa kuona Adam akiwa na mwanamke mwingine na hilo liko wazi hata kwa kizazi cha leo. Ule usemi wa wanawake hawapendani asili yake ni huku. Lilith kwa uwezo alionao anavaa umbo la nyoka na kumlaghai Eva/Hawa ale tunda la mti wa kati; mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Mti ambao Adam alizuiwa kula matunda yake.

Bibie Eve/Hawa bila kujua nia ovu ya nyoka anakubali kula tunda la mti wa kati ambalo aliliona ni TAMU na linapendeza kwa macho! Kilichofuatia baada ya hapo kinajulikana wazi. Nyoka akawafitinisha Adam na mkewe Hawa kwa Mungu. Wakafumbuliwa macho yaonayo na kujiona wako uchi.

Nyoka akalaaniwa kuwa atatembea kwa tumbo. Eva akalaaniwa kuwa atazaa kwa uchungu.

Adam akalaaniwa kuwa atakula kwa jasho na wote wakafukuzwa Eden palipokuwa na kila kitu cha bure.

Lengo la Lilith la kulipa kisasi likawa limetimia na kwa mtazamo huo inawezekana kabisa Lilith ndio ibilisi!
sasa issue imetoka nje ya Biblia takatifu wewe umeitoa wapi? nina mashaka kama hii mada si kutungwa
 
JE KABLA YA KUMUUMBA HAWA MUNGU ALIMUUMBA MWANAMKE MWINGINE?

Wapendwa naomba mnisaidie ukisoma mwa 1:26 - 27 hapo Mungu alimuumba mtu mwanamke na mtu mwanaume je huyu mwanamke aliyeumbwa hapa ni nani? Wakati huo huo Hawa aliumbwa baada ya Adam kulazwa usingizi na kuchomolewa ubavu? Mwa 2:18 - 19.
Karibuni na mje na hoja hai
 
JE KABLA YA KUMUUMBA HAWA MUNGU ALIMUUMBA MWANAMKE MWINGINE?

Wapendwa naomba mnisaidie ukisoma mwa 1:26 - 27 hapo Mungu alimuumba mtu mwanamke na mtu mwanaume je huyu mwanamke aliyeumbwa hapa ni nani? Wakati huo huo Hawa aliumbwa baada ya Adam kulazwa usingizi na kuchomolewa ubavu? Mwa 2:18 - 19.
Karibuni na mje na hoja hai
Wataalamu wa maandiko wanasema ni Hawa au Eva ndiye mwanamke wa kwanza kuumbwa na Mwenyezi Mungu kadiri ya maandiko uliyoyanukuu, andiko la kwanza linatoa habari ama taarifa ya kilichotokea hapo mwanzo kwamba mtu mume na mtu mke wote waliumbwa na Mwenyezi Mungu, andiko la pili linafafanua na kueleza mchakato wa uumbaji huo uliotajwa namna na jinsi ulivyofanyika....mtu mume aliumbwa vip na mke pia alipatikanaje... nadhan umeelewa ndugu yetu na hakuna haja ya Uzi kuendelea labda kama malengo yake sio kutaka kufahamu tafsiri ya maandiko hayo.
 
Itakuwa unamuulizia bi mkubwa wa Adam tulihadhithiwa tu aliitwa Lilith, unajua haya mambo ya mitala alianza Adam!
 
JE KABLA YA KUMUUMBA HAWA MUNGU ALIMUUMBA MWANAMKE MWINGINE?

Wapendwa naomba mnisaidie ukisoma mwa 1:26 - 27 hapo Mungu alimuumba mtu mwanamke na mtu mwanaume je huyu mwanamke aliyeumbwa hapa ni nani? Wakati huo huo Hawa aliumbwa baada ya Adam kulazwa usingizi na kuchomolewa ubavu? Mwa 2:18 - 19.
Karibuni na mje na hoja hai
Mimi sio msomi wa bibilia lakini aya iko wazi kabisa kwamba inaeleza Tu kwqmba Mungu alimuumba m2wnamke na mwanaume.

Ni sawa na kusema mwaka 2022 masudi kipanya aliunda gari.

Alafu baadae ukaja kutaja process kwwmba alifanya hivi akafanya vile kisha likazuka gari,huwezi kudai kwamba masudi aliunda gari mbili itakuwa ni ufinyu wa uelewa.
 
Siye twamtambua hawa...huyo mwingine ndo tunakusikia wewe
 
JE KABLA YA KUMUUMBA HAWA MUNGU ALIMUUMBA MWANAMKE MWINGINE?

Wapendwa naomba mnisaidie ukisoma mwa 1:26 - 27 hapo Mungu alimuumba mtu mwanamke na mtu mwanaume je huyu mwanamke aliyeumbwa hapa ni nani? Wakati huo huo Hawa aliumbwa baada ya Adam kulazwa usingizi na kuchomolewa ubavu? Mwa 2:18 - 19.
Karibuni na mje na hoja hai
Kulikuwa na uumbaji wa mwanamke mwingine kabla ya Hawa.. Kumbuka Hawa hakuumbwa...!
 
Itakuwa unamuulizia bi mkubwa wa Adam tulihadhithiwa tu aliitwa Lilith, unajua haya mambo ya mitala alianza Adam!
Sasa huyo aliyekuhadithia aliyatoa wapi! Ndiyo unapaswa kumuuliza hiyo hadithi hadithi aliipata wapi kama wote tunatumia Bible moja labda aseme kuna Bible nyingine na iko wapi tuisome sote, [kusadiki kwa Toma mpaka ujionee]
 
Sasa huyo aliyekuhadithia aliyatoa wapi! Ndiyo unapaswa kumuuliza hiyo hadithi hadithi aliipata wapi kama wote tunatumia Bible moja labda aseme kuna Bible nyingine na iko wapi tuisome sote, [kusadiki kwa Toma mpaka ujionee]
Kama una uelewa wa kawaida unajua bible kina ngano kama kitabu Cha hadithi kingine unacho unakijua ukirejea huko Kuna mwanamke aliyeumbwa "Lilith" na aliyetolewa kwenye ubavu "Eva".


Sijui nilitaka kukuambia Nini nimesahau kidogo Ila nikutakie sikukuu njema ya kushangilia malaika kuua wanadam huko wamisri hapo siku chache zijazo!
 
ni mwanamke wa kwanza kabla ya hawa/eve ambae alikuwa anaishi na lucifer/shetani pangoni na ndie aliyempa tunda bwana adam pale eden....
 
ni mtu mwenye utata sana katika ngano za Kiyahudi. Jina la Lilith halijajumuishwa katika hadithi ya uumbaji wa Torati lakini anaonekana katika maandishi kadhaa ya midrashic. Ishara, historia na fasihi yake vinajadiliwa kati ya wasomi wa Kiyahudi, wanafeministi na wasomi wengine. Kuna hadithi nyingi za asili za Lilith lakini historia maarufu zaidi ilisimulia maoni ya Lilith kama mke wa kwanza wa Adamu. Kulingana na hadithi ya "Hawa wa kwanza" Lilith aliumbwa na Mungu kutoka kwa udongo na kuwekwa kwenye bustani na Adamu mpaka matatizo yalipotokea kati ya Adamu na Lilith wakati Adamu alijaribu kutumia utawala juu ya Lilith. Hadithi moja inasema kwamba Lilith alikataa kulala chini ya Adamu wakati wa ngono. Aliamini kuwa waliumbwa sawa, wote kutoka kwa mavumbi ya ardhi, kwa hivyo hakupaswa kulala chini yake. Baada ya Adam kutokubaliana, Lilith alikimbia Bustani ya Edeni ili kupata uhuru wake. Adamu alimwambia Mungu kwamba Lilith ameondoka na Mungu akatuma malaika watatu, Senoi, Sansenoi, na Sammangelof, kumchukua. Malaika watatu walimkuta Lilith kwenye pango la kuzaa watoto lakini Lilith alikataa kurudi kwenye bustani. Malaika walimwambia wangewaua watoto wake 100 kila siku kwa sababu ya kutotii kwake. Katika kulipiza kisasi, anasemekana kuwaibia watoto maisha na anahusika na vifo vya watoto wachanga waliozaliwa bado na vifo vya crib (SIDS). Watoto wa kiume wako katika hatari ya kukasirika kwa Lilith kwa siku 8 baada ya kuzaliwa (hadi tohara) na wasichana wako hatarini kwa siku 20. Ingawa Lilith aliiba maisha ya watoto usiku, alikubali kutoua watoto ambao walikuwa na hirizi za malaika watatu. Baada ya malaika kuondoka, Lilith alijaribu kurudi kwenye bustani lakini alipofika aligundua kuwa Adamu tayari alikuwa na mwenzi mwingine, Hawa. Kwa kulipiza kisasi, Lilith alifanya ngono na Adamu alipokuwa amelala na "aliiba mbegu yake." Pamoja na uzao wake yeye huzaa ‘lilium,’ roho waovu wanaosafirishwa duniani kuchukua mahali pa watoto wake waliouawa na malaika. Lilith pia anasemekana kuwajibika kwa ndoto za wanaume na utoaji wa hewa chafu usiku. Nadharia nyingine inasema kwamba Lilith amepachikwa mimba, hivyo basi kuunda pepo zaidi kwa kupiga punyeto na ndoto za mapenzi.


Historia ya Lilith

Ingawa sura ya Lilith hupatikana kwa kawaida katika ngano za Kiyahudi na midrash, asili ya Lilith ni kama sucubus wa Sumeri. Hadithi ya kwanza ya Kiyahudi ya Lilith ilisimuliwa katika Alfabeti ya ben sirah. Kabla ya kuanzishwa kwa Alfabeti ya ben sirah, Lilith alionekana zaidi kama pepo badala ya "Hawa wa kwanza". Kwa sababu ya utata wa Lilith, amewakilishwa kwa njia nyingi katika fasihi na sanaa. Baadhi ya wasomi wa theolojia wanamkubali Lilith kama "Hawa wa kwanza" ilhali wengine bado wanamwona kama pepo. Kihistoria katika sanaa, Lilith ameonyeshwa kwa njia mbalimbali kuanzia matoleo ya risqué hadi Lilith kwenye bustani. Kutazama baadhi ya maonyesho haya bofya kwenye picha kwenye tovuti ya UPenn kwenye Lilith.


Lilith: ishara ya nguvu?

Asili ya wazi ya ishara ya Lilith imeruhusu vikundi tofauti kumtumia kama ishara ya uharibifu wa kike au ishara ya nguvu za kike. Wanafeministi wengi wanaona Lilith sio tu mwanamke wa kwanza bali mwanamke wa kwanza wa kujitegemea aliyeumbwa. Katika hadithi ya uumbaji anakataa kuruhusu Adamu kumtawala na kukimbia bustani licha ya matokeo. Ili kuhifadhi uhuru wake lazima awape watoto wake na kwa kulipiza kisasi anaiba uzao wa Adamu. Katika akaunti moja ya hadithi hii, Lilith inasemekana "mlima Adamu" (bofya hapa kwa toleo hili). Toleo hili la hadithi ina maana kwamba Lilith alikiuka kijinsia Adamu; hata hivyo, hadithi nyingine zinaonyesha Lilith kama pepo anayeua watoto na kuchukua fursa ya wanaume wakati wamelala. Sheria ya Kiyahudi ya halakhic inakataza kumwagika kwa mbegu ya mtu na Lilith anachukua fursa hii, wakati wa kupiga punyeto na ndoto za ngono, na kuitumia kujaza watoto wake mwenyewe. Ingawa Lilith ana utata baadhi ya wanafeministi wamemtumia kama ishara ya uwezeshaji. Kwa mfano, jarida moja la kifeministi la Kiyahudi linaitwa Lilith linajiandikisha kama "Jarida Huru la Mwanamke wa Kiyahudi." Wachapishaji wanatumia Lilith kama cheo kwa sababu wanaamini kuwa yeye ni ishara ya uhuru. Hata hivyo, wale ambao bado wanamfikiria kama kijini wanaweza kugeuza na kwa mara nyingine tena kuwataja watetezi wa haki za wanawake kama waharibifu wa kiume au wanaochukia wanaume. Wanamwona Lilith kuwa mwovu na mwenye kulipiza kisasi kwa wanaume na watoto. Kwa ishara au icon yoyote inayotumiwa na watetezi wa haki za wanawake, hasa ndani ya mazingira ya kidini, kutakuwa na mabishano na upinzani. Ikiwa hadithi ya Lilith ni sahihi au la sio suala kuu. Toleo la hadithi ya "Hawa wa kwanza" la hadithi inampa Lilith jukumu ambalo wanawake wengi wanaweza kutambua ndani ya Uyahudi na mila zingine za kidini. Ni mwanamke huru anayepinga mfumo dhalimu aliowekwa. Kuiba maisha ya watoto huwakilisha wazimu fulani unaoambatana na upweke na kutengwa kwake. Licha ya mapungufu ya Lilith, bado anabaki ishara ya nguvu kwa kuishi kwake na kushangaza kwake. Yeye yuko wazi kwa tafsiri na kwa hivyo huwaruhusu wanawake kutafsiri tena ishara na nguvu yake ndani ya mila.
 
Back
Top Bottom