Ufunuo usiosemwa: Je, Lilith ndio nyoka wa Eden? Je, ni mke wa kwanza wa Adam?

Ufunuo usiosemwa: Je, Lilith ndio nyoka wa Eden? Je, ni mke wa kwanza wa Adam?

Mshana bana; sijui anapataga wapi haya mambo? Anyway, binafsi nina mashaka sana na ukweli wa huyo mwanamke mgeni, sidhani kama ina ukweli wowote cause imenibidi nirudie kuisoma tena Biblia hasa pale kwenye uumbaji. The way Adam alivyo umbwa na the way ilivyo elezewa, sidhani kama kuna kiumbe chenye mfano wa binadamu kilikuwepo zaidi yake na Hawa baadae.
Hata hiyo habari ya Adam na Hawa nayo ni tungo ya watu tu. Si ya ukweli.
 
Nakuelewa mkuu, hebu mlengo wako huo huo wa kidini kufikiri:

Mosi,
Lucifer naye ni roho, sasa ataingiwaje na roho tena ?? roho haitawali roho hata siku moja. Nimesoma Biblia yote lakini sijaona sehemu ambapo roho mchafu imeingia roho nyingine mchafu, hata walipomwambia Yesu anaongozwa na Beelzebub alisema kwamba Ufalme ukijifitinisha hauwezi kusimama hata kidogo.

Pili, Lucifer alianguka hata kabla Adam hajaumbwa, alidanganya hadi malaika watakatifu wa mbinguni unahisi mwanadamu (Lilith) angeweza kumdanganya Lucifer kweli ?? Maana ukisoma kitabu cha Nabii Ezekiel anasema kwamba "Alikuwa amejawa na hekima au Full of Wisdom". Sasa kama kiumbe huyu alikaa jirani kabisa na Mungu na alitaka kabisa kumpindua, unahisi huyo Lilith angakuwa na uwezo wa kumshawishi Lucifer ???

Tatu, hoja yako ni tata kwasababu yule Nyoka (The Serpent) alikuwa ni mnyama kama wanyama wengine walioiumbwa pale bustanini na Biblia inasema "Naye nyoka alikuwa ni mwerevu kuliko wanyama wote wa mwituni". Lucifer hakuwahi kuwa mnyama wa mwituni.
Asante naomba nijibu hoja ya tatu....kwanza umeona kabisa nyoka akitambulishwa kwa uwerevu,...vilevile bado ishu yao inabaki kuwa ya kiroho zaidi kuliko kimwili...
Mwili wa nyama una limitatations nyingi lakini mwili wa roho ni powerful vast n very deep
 
Mwanzo 1:27
Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimuumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba..

Mwanzo 2:18
Bwana Mungu akasema, si vema huyo mtu awe peke yake, Nitamfanyia msaidizi wa kufanana nae.
Ndipo Bwana alipomletea Adamu usingizi mzito na kumuondolea ubavu mmoja na kumfanyia msaidizi nae alikuwa ni mwanamke (Eve).
Hii ilikuwa ni baada ya Adamu kupewa mamlaka ya kuitunza bustani ya Edeni..

Je, kuna uwezekano mkubwa huyu Lilith anayetajwa kuwa mke wa kwanza wa Adamu akawa ndiye?

Ukisoma maandiko matakatifu Mwanzo 1:27
Inazungumzia uumbaji wa mwanadamu, maandiko yanasema Mungu alimuumba mwanamume na mwanamke kwa mfano wake....hii ni kabla ya uwepo wa Adamu katika bustani ya Edeni...Na baada ya hapo ndipo Mungu alipo mfanyia Adamu msaidizi wa kufanana nae. Alimuumba Eva kutoka katika ubavu wa Adamu.

Je, huyu mwanamke aliye umbwa pamoja na Adamu (Mwanzo 1:27) kuna uwezekano mkubwa ndiye akawa Lilith???

Maandiko matakatifu hayajaeleza habari za Lilith wala habari za Adamu kuwa na mke kabla ya Eva.. Lakini tukienda nje ya biblia inasemekana Mungu alimuumba Lilith pamoja na Adamu kwa wakati mmoja.

Lilith alikuwa ni mwanamke mwenye akili na nguvu nyingi hivyo kupelekea kushindwa kumtii Adamu na mwisho wa siku aliamua kulikufuru jina la Mungu nae Mungu akamuadhibu na kumlaani yeye pamoja na uzao wake..
 
Hili nalifahamu vizuri kabisa,
Lakini hakuna sehemu kwenye Biblia kuna ushahidi wa kwamba pepo kamvamia pepo.
Yeah ulimwengu wa roho ni replica ya ulimwengu wa nyama ....chochote cha kiroho kina mfanano na tafsiri ya kimwili na kinyume chake
 
Mshana bana; sijui anapataga wapi haya mambo? Anyway, binafsi nina mashaka sana na ukweli wa huyo mwanamke mgeni, sidhani kama ina ukweli wowote cause imenibidi nirudie kuisoma tena Biblia hasa pale kwenye uumbaji. The way Adam alivyo umbwa na the way ilivyo elezewa, sidhani kama kuna kiumbe chenye mfano wa binadamu kilikuwepo zaidi yake na Hawa baadae.
Nimesema wazi habari za Lilith hazitajwi almost kabisa kwenye Bible
 
Asante naomba nijibu hoja ya tatu....kwanza umeona kabisa nyoka akitambulishwa kwa uwerevu,...vilevile bado ishu yao inabaki kuwa ya kiroho zaidi kuliko kimwili...
Mwili wa nyama una limitatations nyingi lakini mwili wa roho ni powerful vast n very deep
Mimi ambacho nataka hapa ni ushahidi wa roho kuingia roho,
Au kiingereza nisema "An evidence of a demon possessing a demon"
 
Ukijua habari za Mungu ni hekaya tu, hivi vibwagizo vya habari hiyo sijui Adam na Hawa na Lilith haviwezi kukusumbua.
[emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] missed you
 
Mkuu labda nimsaidie Mshana Jr kujibu hili..... Ni kweli Adam na Lilith walikuwa na nguvu sawa actually zaidi hata ya malaika ila Adam aliondolewa nguvu hizi za kiungu pale alipokula tunda ila unachosahau ni kwamba lilith aliondoka bila kula hilo tunda actually mambo ya tunda yalikuja baada ya Hawa kuletwa kuziba pengo la lilith.... Hivyo Lilith aliondoka na nguvu zake kama ambavyo shetani aliondoka na nguvu zake alipotolewa mbinguni... Ila Adam nguvu zake ziliisha siku anakula tunda hicho muhim tutambue


Lilith hakula tunda mkuu hivyo ile hukumu ya Adamu ya kwamba atakufa ni ya Adam na hawa pekee ndio maana shetani yeye mpka leo yupo hai na lilith pia sababu wao bado walibaki na nguvu zao za siku zote ila kama Mungu angetamka kuwa wote waliomfanya adam afanye dhambi wafe basi lilith na shetani wangeshakufa kitambo sana kma adam na hawa.

Kama hilo ni dogo kwanni usishangae Yesu aliyekuja kuleta wokovu aliishi miaka 33 pekee hapa duniani ila aliyepinga wokovu toka Yesu wa hapa duniani amekufa yeye bado anaishi milele na anazidi kupotosha watu?? Ukipata jibu la hapo ndio utaelewa kwanni Mungu hakumhukumu lucifer/ lilith kifo siku ile Adam ameasi kwa kula tunda.

Ni hayo tu
Daah kazi kweli kweli

I nashangaza sana yaan Lucifer aliyemuasi Mungu na akasababisha Kina Adam na Hawa kula tu hakuhukumiwa kufa ameachwa tu anadunda ila aliyepewa tunda akala akaondolewa nguvu zote na mamlaka plus kufa
 
[emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] missed you
Huo nao ni ushahidi Mungu hayupo.

Angekuwepo tungekuwa tuna uwezo wa kuwasiliana muda wote bila kutumia kifaa chochote na hakuna ambaye angem miss mwingine.
 
Mimi ambacho nataka hapa ni ushahidi wa roho kuingia roho,
Au kiingereza nisema "An evidence of a demon possessing a demon"
Sidhani kama utaweza kupata ushahidi kama huu kwakuwa roho sio visible sanasana nitakupa tu mifano ya haunted souls nk
 
Tunaterejea tena kutazama yale mambo yaliyoacha utata na pengine hayajawahi kujadiliwa na wengi.

Tumeshajadiliana sana kuhudu Eden, Hawa, tunda la mti wa kati(mti wa ujuzi wa mema na mabaya), nyoka na Adam. Katika vyote hivi kuna mtu pia tumemjadili kwa kiasi, mtu huyu hata maandiko hayamtaji wala kumjadili sana. Mtu huyo ni Lilith, mwanamke anayesemekana kuwa mke wa kwanza wa Adam.

Jambo hili la Adam kuwa na mke aliyeitwa Lilith halitajwi kwenye misahafu yetu hii tunayoijua bali kwenye maandiko mengine lakini ya kiimani pia.
Lilith anayetajwa kwenye maandiko hayo kama mwanamke kiburi na mwenye nguvu, na ambaye pia inasemekana alizaliwa sawa na Adam, aliasi na kutengana na Adam baada ya kushindana tabia. Lilith alitaka kuwa na mamlaka makubwa kwa Adam.

Habari za Lilith zinaishia pale alipoachana na Adam, kisha Adam alirejea Eden kuanza maisha ya upweke akiwa kama mtalikiwa na tunaambiwa Lilith alikuja kugeuka kuwa kiumbe cha kuzimu.

Maisha ya upweke Eden yanamfanya Mungu kumtengenezea Adam msaidizi wa kufanana naye
ndipo Adam sasa anamshukuru Mungu kwa kusema. Sasa huyu ni nyama katika nyama zangu na mfupa katika mifupa yangu ....?(wanazuoni wanatafsiri kauli hii kama kwamba mwanzoni alikuwepo mwingine ambaye hakutokana na Adam! )Je mtu huyo ni Lilith?

Maisha mapya ya furaha upendo na mapatano ndani ya Eden kati ya Adam na Eva/Hawa yanamvuta nyoka anayetajwa kama ibilisi akijulikana kama malaika aliyeasi mbinguni (Lilith?) Huyu ndio pekee aliyejua siri ya uumbaji (ukiacha Mungu) na siri ya tunda la mti wa kati; mti wa ujuzi wa mema na mabaya!

Kwa hakika Lilith hakupenda kabisa kuona Adam akiwa na mwanamke mwingine na hilo liko wazi hata kwa kizazi cha leo. Ule usemi wa wanawake hawapendani asili yake ni huku. Lilith kwa uwezo alionao anavaa umbo la nyoka na kumlaghai Eva/Hawa ale tunda la mti wa kati; mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Mti ambao Adam alizuiwa kula matunda yake.

Bibie Eve/Hawa bila kujua nia ovu ya nyoka anakubali kula tunda la mti wa kati ambalo aliliona ni TAMU na linapendeza kwa macho! Kilichofuatia baada ya hapo kinajulikana wazi. Nyoka akawafitinisha Adam na mkewe Hawa kwa Mungu. Wakafumbuliwa macho yaonayo na kujiona wako uchi.

Nyoka akalaaniwa kuwa atatembea kwa tumbo
Eva akalaaniwa kuwa atazaa kwa uchungu
Adam akalaaniwa kuwa atakula kwa jasho na wote wakafukuzwa Eden palipokuwa na kila kitu cha bure.

Lengo la Lilith la kulipa kisasi likawa limetimia na kwa mtazamo huo inawezekana kabisa Lilith ndio ibilisi....!!!

Unaandika habari za biblia ila kwa vyanzo vya kufikirika,huna hata reference yoyote kwenye maandiko unakotoa title ya story yako,just tu unaandika "INASEMEKANA" inasemekana na nani?,umeona wapi ilipoandikwa kwenye maandiko hayo unayosema inasemekana? how tu uje na neno lilith umelitoa wapi?,na pia INASEMEKANA wewe ni muongo unajiandikia andikia tu kwakuwa una bundle ya kutosha!
Na pia INASEMEKANA unamatatizo kama TULIVYOONA kwenye post zako za nyuma ndio hayo matatizo yanakupelekea uwe unatamaa ya kupost post mara kwa mara hata kama huna hoja wala evidence za msingi
Ndugu mshana next time unapokuja na hoja kama hizi useme mapema kama ni swali unauliza unaomba ufafanuzi au ni habari ambayo umeireserch so unataka wenzio tujue au ni story tu ya kusadikika iliyosheheni habari za "inasemekana"
 
Huo nao ni ushahidi Mungu hayupo.

Angekuwepo tungekuwa tuna uwezobwa kuwasiliana muda wote bila kutumia kifaa chochote na hakuna ambaye angem miss mwingine.
[emoji15] [emoji3] [emoji3] huo ndio ushahidi sasa wa uwepo wake....mawasiliano yanakuwa yapo kama kuna nishati kisababishi kati ya pande mbili ambazo ziko controlled na main server
God as main server amesababisha nikumiss lakini kisabishi cha mawasiliano (JF) kilikuwa hakipo
 
Unaandika habari za biblia ila kwa vyanzo vya kufikirika,huna hata reference yoyote kwenye maandiko unakotoa title ya story yako,just tu unaandika "INASEMEKANA" inasemekana na nani?,umeona wapi ilipoandikwa kwenye maandiko hayo unayosema inasemekana? how tu uje na neno lilith umelitoa wapi?,na pia INASEMEKANA wewe ni muongo unajiandikia andikia tu kwakuwa una bundle ya kutosha!
Na pia INASEMEKANA unamatatizo kama TULIVYOONA kwenye post zako za nyuma ndio hayo matatizo yanakupelekea uwe unatamaa ya kupost post mara kwa mara hata kama huna hoja wala evidence za msingi
Ndugu mshana next time unapokuja na hoja kama hizi useme mapema kama ni swali unauliza unaomba ufafanuzi au ni habari ambayo umeireserch so unataka wenzio tujue au ni story tu ya kusadikika iliyosheheni habari za "inasemekana"
Asante sana kwa kushiriki na kuchangia mjadala....endelea kuufuatilia una mengi ya kujifunza...
Nami pia najifunza kama wengine wanavyojifunza....hii ndio aina yangu ya uandishi si kila mmoja anaweza kuipenda....cha muhimu ni kwamba tunapata wote maarifa hata tusipokiri
 
Isaiah 34:14 (NAB)
Wildcats shall meet with desert beasts,
satyrs shall call to one another;There shall the lilith repose, and find for herself a place to rest
.

Na kwenye footnotes za biblia inasema Lilith ni shetani anayeranda majangwani..... Ila bado unataka kubisha biblia haimtaji. Tupende kujifunza sio kukejeli kila kitu sasa unaposema mafundisho ya kishetani tukueleweje ilihali biblia inamtambua kuwa lilith ni shetani pia kama anavyodai Mshana Jr !!!

Kazi kwelikweli
kwa hiyo lilith ni shetani au mke wa Adam
 
Back
Top Bottom