Ufunuo usiosemwa: Je, Lilith ndio nyoka wa Eden? Je, ni mke wa kwanza wa Adam?

Ufunuo usiosemwa: Je, Lilith ndio nyoka wa Eden? Je, ni mke wa kwanza wa Adam?

Mshana na Zitto hii hoja ya Adam na lilith zen hawa ukitumia biblia kama source huipati tuanzie pale mwanzo 1:26 Mungu akasema na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; (hapa wanazungumzia mtu wakwanza) wakatawale samaki wa baharini na ......(hapa wanazunguzia couple nyingine/ama more than one peron ambayo itukiijumlisha na yule wa kwanza tunapata pengine watu wa 3 ama zaidi)

mwanzo 1:27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, (hapa mtu wa kwanza anaumbwa) kwa mfano wa Mungu alimuumba, (bado tunamzunguzia yule wa kwanza) mwanaume na mwanamke aliwaumba. (couple inaumbwa)

mpaka hapo tuna watu wa3 tofauti mwanaume peke yake zen mwanaume na mwanamke kuanzia mwanzo 1:28 Mungu anawamilikisha wale watu watatu/wote dunia anawapa utawala.

Mwanzo 2:7 Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya aridhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.(namna yule wakwanza alivyoumbwa ama huyu ni mwanaume wa 3, japo sitaki kuamini hivyo)

Mwanzo 2:15 Bwana Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya edeni, ailime na kuitunza. 2:16 Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu akisema "matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, 17 Lakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, (yule mtu wa kwanza ndie tunamzungumzia hapa achana na ile couple kumbuka mpaka hapo yuko peke yake hajapata kampani/mwenzi)

Mwanzo 2.18 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye(wazo au mpango wa kumtengenezea mke/mwanamke wawe couple pia linazaliwa)

Mwanzo 2: 21 Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake , 22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. (mwanamke wa pili anaumbwa now we have 2 women with 2 or 3 men)

Baada ya hayo yote nashawishika kuamini kua hakuna mwanamke alie muacha walieumbwa nae, na yale maelezo yote ni ufafanuzi tu wa namna hawa wawili walivyopatikana, pengine sasa tuseme ile couple ya kwanza ndio iliyokuja kudanganya hii couple ya pili ambayo hii nayo inakuja kuwa hoja tofauti kabisa na hii yako ya lilith. na ikiwa lilith ni mmoja kati ya ile couple ya kwanza je mumewe yuko wapi au alienda wapi? usiniambie ni huyu shetani/lusifa sababu yeye tunaambiwa aliumbwa kwa moto tena kabla ya dunia kuuumbwa
Mkuu walioanzisha nadharia hii wanatumia mstari huu

Mwanzo 2:23
23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume

Hapa ndio wakahoji why Adam aseme SASA HUYU.... Ikimaanisha alikuwepo mwingine so anafanya ulinganisho
 
Haya ndo matatizo ya kuzungumzia masuala ya imani kwa kutegemea waganga wa kienyeji, wachawi, wazimu, wapiga ramli n.k
 
Neno la Mungu halikosolewi au halisahihishwi kwa kuweka mapenzi yako liwe utakavyo wewe, huko ni kukengeuka ndg yangu mshana jr
 
Mkuu walioanzisha nadharia hii wanatumia mstari huu

Mwanzo 2:23
23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume

Hapa ndio wakahoji why Adam aseme SASA HUYU.... Ikimaanisha alikuwepo mwingine so anafanya ulinganisho
kabla ya huo mstari rudi nyuma kidogo Adamu analetewa wanyama wote anawapa majina lkn mwisho haoni wa kufanana nae kwa hali ya kawaida baada ya kumuona mwanamke lzm angetamka maneno hayo hiyo sio hoja labda kama kuna source nyingine zaidi ya biblia tujenge hoja yetu hapo.
 
Tunaterejea tena kutazama yale mambo yaliyoacha utata na pengine hayajawahi kujadiliwa na wengi.

Tumeshajadiliana sana kuhudu Eden, Hawa, tunda la mti wa kati(mti wa ujuzi wa mema na mabaya), nyoka na Adam. Katika vyote hivi kuna mtu pia tumemjadili kwa kiasi, mtu huyu hata maandiko hayamtaji wala kumjadili sana. Mtu huyo ni Lilith, mwanamke anayesemekana kuwa mke wa kwanza wa Adam.

Jambo hili la Adam kuwa na mke aliyeitwa Lilith halitajwi kwenye misahafu yetu hii tunayoijua bali kwenye maandiko mengine lakini ya kiimani pia.
Lilith anayetajwa kwenye maandiko hayo kama mwanamke kiburi na mwenye nguvu, na ambaye pia inasemekana alizaliwa sawa na Adam, aliasi na kutengana na Adam baada ya kushindana tabia. Lilith alitaka kuwa na mamlaka makubwa kwa Adam.

Habari za Lilith zinaishia pale alipoachana na Adam, kisha Adam alirejea Eden kuanza maisha ya upweke akiwa kama mtalikiwa na tunaambiwa Lilith alikuja kugeuka kuwa kiumbe cha kuzimu.

Maisha ya upweke Eden yanamfanya Mungu kumtengenezea Adam msaidizi wa kufanana naye
ndipo Adam sasa anamshukuru Mungu kwa kusema. Sasa huyu ni nyama katika nyama zangu na mfupa katika mifupa yangu ....?(wanazuoni wanatafsiri kauli hii kama kwamba mwanzoni alikuwepo mwingine ambaye hakutokana na Adam! )Je mtu huyo ni Lilith?

Maisha mapya ya furaha upendo na mapatano ndani ya Eden kati ya Adam na Eva/Hawa yanamvuta nyoka anayetajwa kama ibilisi akijulikana kama malaika aliyeasi mbinguni (Lilith?) Huyu ndio pekee aliyejua siri ya uumbaji (ukiacha Mungu) na siri ya tunda la mti wa kati; mti wa ujuzi wa mema na mabaya!

Kwa hakika Lilith hakupenda kabisa kuona Adam akiwa na mwanamke mwingine na hilo liko wazi hata kwa kizazi cha leo. Ule usemi wa wanawake hawapendani asili yake ni huku. Lilith kwa uwezo alionao anavaa umbo la nyoka na kumlaghai Eva/Hawa ale tunda la mti wa kati; mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Mti ambao Adam alizuiwa kula matunda yake.

Bibie Eve/Hawa bila kujua nia ovu ya nyoka anakubali kula tunda la mti wa kati ambalo aliliona ni TAMU na linapendeza kwa macho! Kilichofuatia baada ya hapo kinajulikana wazi. Nyoka akawafitinisha Adam na mkewe Hawa kwa Mungu. Wakafumbuliwa macho yaonayo na kujiona wako uchi.

Nyoka akalaaniwa kuwa atatembea kwa tumbo
Eva akalaaniwa kuwa atazaa kwa uchungu
Adam akalaaniwa kuwa atakula kwa jasho na wote wakafukuzwa Eden palipokuwa na kila kitu cha bure.

Lengo la Lilith la kulipa kisasi likawa limetimia na kwa mtazamo huo inawezekana kabisa Lilith ndio ibilisi....!!!
Fiction tu hamna kitu cha hivyo..!

Ata uandishi wako ni wa kuungaunga tu.
 
Neno la Mungu halikosolewi au halisahihishwi kwa kuweka mapenzi yako liwe utakavyo wewe, huko ni kukengeuka ndg yangu mshana jr
Mkuu nadhani mshana hajakosoa neno la Mungu ila ameanzisha tu mjadala ili kuendelea kujadili kwa uelewa mpana!

Kama tungekuwa kwenye mdahalo Basi tungesema @Mshanar Jr amechokoza mada tu!
 
Kama sikosei, wewe ni wale wasio amini uwepo wa Mungu? right? if that is the case then nadhani hatuwezi kwenda pamoja cause mi nitakua nafanya reference kwenye vitabu ambavyo wewe huviamini and hence utakua ni upotezaji wa muda wa each other!
Kama vitabu vyako haviwezi kuthibitishwa kwamba ni vya ukweli na si hadithi tu, na wewe unavichukulia kama vya ukweli, hata usipojadiliana nami, ukaendelea kuvitumia hivyo vitabu kama vya ukweli na si hadithi tu, hata wewe mwenyewe utakuwa unajipotezea muda tu.
 
sawa twende kwenye Tafsiri yako,ya version ya kwanza ya kiebrania,ambao mstari huujui, uweke hapa tuangalie nani alikua anasema hayo maneno...na mimi nitaangalia...kupata earlier version sio ishu bro...
New jerusalem Translation
Genesis 4:1
........I have gotten a man from an angel of the LORD

Hii ndio moja ya translation kutoka biblia ya kiebrania..... Inakubali kuwa cain hakuwa mtoto wa Adam ila mtoto wa MALAIKA sasa naomba uje uikane biblia hapa
 
Kitabu gani kimeandika hii kitu ya lol lilith??.. Na sisi tukipitie.....

Nachofahamu Adam alikua first man, na alikua first man sababu alikua mmoja wa Malaika MBINGUNI aliyeongoza mapambano Kati ya lucifer na Mungu kule MBINGUNI tunaiita (Pre-mortal) life... Award yake akapewa aje Duniani aanzishe mankind...... Sasa huyu lilith hata kwenye Pre-mortal life hakuwepo.

Tunajua waliokua kwenye Maisha kabla Dunia haijaumbwa ambao walikua mashuhuri kule kwa kazi zao. Baadhi Yao ni

JESUS CHRIST - JEHOVAH
MICHAEL - ADAM
GABRIEL - NOAH
LUCIFER - SATAN/DEVIL

Na wengine wengi.

Jina la kushoto ni Pre-mortal name, jina la kulia ni Mortal (earth) name.. Mfano YESU KRISTO kwenye pre earth alikua anaitwa JEHOVAH.

Sasa huyu lilith hatujui alikua Nani kule na aliletwa kwa mission gani Dunian maana Adam, eve na wengine walioanzisha Dunia kama viumbe wa kwanza walikua wana kazi ya kufanya.
Samani mkuu ebu niongeze mahalifa kidogo hayo maelezo umenuku kwenye kitabu gani namie nikapitie maana kwangu mapya kabisa
 
kabla ya huo mstari rudi nyuma kidogo Adamu analetewa wanyama wote anawapa majina lkn mwisho haoni wa kufanana nae kwa hali ya kawaida baada ya kumuona mwanamke lzm angetamka maneno hayo hiyo sio hoja labda kama kuna source nyingine zaidi ya biblia tujenge hoja yetu hapo.
Wao wanaanzia hapa
mwanzo 1
27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba

Ndio wakasema huenda mwanzo 1 aliongelewa lilith maana aliumbwa muda mmoja na adam ila hapa mwanzo 2 adam anasema SASA HUYU akimaanisha kuwa eva alitoka kwenye ubavu wake tofauti na lilith aliyeumbwa na udongo kama adam na ndio maana hakumheshimu

Na kuna wanatheolojia wameandika machapisho kukubaliana na hili hivyo sio hoja ya wapagani tu bali hata waliokoka na wasomi wa dini kuliko sisi wanakubali hili
 
Mkuu walioanzisha nadharia hii wanatumia mstari huu

Mwanzo 2:23
23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume

Hapa ndio wakahoji why Adam aseme SASA HUYU.... Ikimaanisha alikuwepo mwingine so anafanya ulinganisho
Simple n very clear
 
Haya ndo matatizo ya kuzungumzia masuala ya imani kwa kutegemea waganga wa kienyeji, wachawi, wazimu, wapiga ramli n.k
Matokeo yake unapata wachangiaji aina yako waliofungwa kwenye box la nira za kiimani ambao hawako tayari kuona nje kuna nini
 
Neno la Mungu halikosolewi au halisahihishwi kwa kuweka mapenzi yako liwe utakavyo wewe, huko ni kukengeuka ndg yangu mshana jr
Naheshimu mno maandiko na imani yangu juu ya Mungu kwenye maandiko yake ni thabiti kuliko mwamba...tatizo hujaelewa kabisa muktadha wa mada
 
Back
Top Bottom