Ugomvi wa nyama ya kenge wasababisha mauaji mkoani Mtwara

Ugomvi wa nyama ya kenge wasababisha mauaji mkoani Mtwara

Tajiri wa kusini

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2022
Posts
1,079
Reaction score
2,947
UGOMVI WA NYAMA YA KENGE WASABABISHA MAUAJI MASASI MTWARA

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara limefanikiwa kuzuiya na kutanzua uhalifu kupitia operesheni na misako iliyoendeshwa kati ya tarehe 1 Desemba 2024 hadi 31 Desemba 2024. Katika operesheni hiyo, walikamata wahalifu wakiwemo watuhumiwa wa mauaji, kulawiti, wizi, na uhalifu mwingine, pamoja na kupata pombe haramu na dawa za kulevya.

Miongoni mwa matukio makubwa, watuhumiwa wawili, Danford Steven Seif na Daniel Steven Seif, mapacha wa umri wa miaka 24, walikamatwa kwa tuhuma za kumuua mama yao, Upendo Methew Mayaya, kwa kumshambulia kwa jembe na mwichi. Chanzo cha mauaji hayo kilikuwa ni imani za kishirikina.

Aidha, Renard Godfrey Ndonjima (62) alikamatwa kwa kumua Mohamed Kapile (52) baada ya kutokea ugomvi kuhusu nyama ya kenge, tukio lililotokea tarehe 22 Desemba 2024.

Katika operesheni hiyo, polisi walikamata watuhumiwa saba wakiwa na kete 61 za dawa za kulevya aina ya bhangi, lita 20 za pombe haramu (gongo), na mitambo ya kutengeneza pombe hiyo. Watuhumiwa walifikishwa mahakamani na kesi zao zipo katika hatua mbalimbali.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara alishukuru wananchi kwa ushirikiano wao na kuwataka kuendelea kutoa taarifa za uhalifu ili kudumisha usalama katika jamii.
 
Duh hali ngumu ya maisha ,nyama bei kubwa watu wanashindwa kumudu kununua
 
Habar imekaa kiutata au ndugu mwandishi kaamua kuuza headline
Ni kwamba watu waliuana wakigombea nyama ya kenge? Au waliuana baada ya kugundua wamelishwa kenge bila kujua
 
UGOMVI WA NYAMA YA KENGE WASABABISHA MAUAJI MASASI MTWARA

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara limefanikiwa kuzuiya na kutanzua uhalifu kupitia operesheni na misako iliyoendeshwa kati ya tarehe 1 Desemba 2024 hadi 31 Desemba 2024. Katika operesheni hiyo, walikamata wahalifu wakiwemo watuhumiwa wa mauaji, kulawiti, wizi, na uhalifu mwingine, pamoja na kupata pombe haramu na dawa za kulevya.

Miongoni mwa matukio makubwa, watuhumiwa wawili, Danford Steven Seif na Daniel Steven Seif, mapacha wa umri wa miaka 24, walikamatwa kwa tuhuma za kumuua mama yao, Upendo Methew Mayaya, kwa kumshambulia kwa jembe na mwichi. Chanzo cha mauaji hayo kilikuwa ni imani za kishirikina.

Aidha, Renard Godfrey Ndonjima (62) alikamatwa kwa kumua Mohamed Kapile (52) baada ya kutokea ugomvi kuhusu nyama ya kenge, tukio lililotokea tarehe 22 Desemba 2024.

Katika operesheni hiyo, polisi walikamata watuhumiwa saba wakiwa na kete 61 za dawa za kulevya aina ya bhangi, lita 20 za pombe haramu (gongo), na mitambo ya kutengeneza pombe hiyo. Watuhumiwa walifikishwa mahakamani na kesi zao zipo katika hatua mbalimbali.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara alishukuru wananchi kwa ushirikiano wao na kuwataka kuendelea kutoa taarifa za uhalifu ili kudumisha usalama katika jamii.
kenge mtamu bhana usisikie,,,mimi nilimla bila kujua,,,,pale RUVU mzee mmoja anaitwa mwakyusa,akaagiza nyama inaitwa MAKASI YA MUNGU!!! ilipoletwa nikaonja tamu balaa!!!,,,,,,,na mimi nikaagiza nusu kilo ya MAKASI YA MUNGU,,,,weee acha nijilambe,,,,,baada ya kumaliza kula nikamuuliza dogo mchomaji,,,,MAKASI YA MUNGU ni nya ya nini??? akaniambia ni nyama ya kenge,,,mpaka leo nawinda kenge,,,ni nyama laini sana!!
 
Hivi Leo nimelewa Kila nikiingia huku sielew Habari, kichwa na content ni mbingu na ardhi
 
Back
Top Bottom