Wana Great Thinker Nafikiri soote humu tunaujua ugonjwa wa Kifafa, Ama kuugua binafsi au kuuguliwa na ndugu na Jamaa zetu Au hata kuuona au kumuona binadamu mwenzetu akianguka kifafa,Twende sote japo Dawa hii ni ngumu na inataka Ujasiri, Usiri, Wepesi na Uharaka Pia.
Kama Una mgonjwa wa Kifafa Unachotakiwa kukifanya ili apone,Tegea siku kuna msiba uwe unakuhusu au Haukuhusu, Chamsingi huo Msiba uwe ni siku ya Mazishi yaani siku Marehemu anazikwa.Kabla ya mazishi si kuna suala la kuchimbwa kwa kaburi,sasa unachotakiwa kufanya unatakiwa uwe miongoni mwa wa wanaolichimba kaburi hilo yaani uwe mmoja wapo wa wachimba kaburi.
Unachotakiwa kufanya mnapoendelea kulichimba kaburi hilo kwa vyovyote ni lazima mkutane na mizizi ndani ya Kaburi hilo so unachotakiwa kufanya ni kuichukua mizizi inayotoka ndani ya kaburi kwa usiri mkubwa sana bila ya wachimbaji wenzio kukuona.
Unachukua kiasi tu hakikisha usionekane baada ya kufanikiwa kuichukua mizizi hiyo kwa siri bila ya kuonekana ondoka nayo mpaka alipo mgonjwa wako ichemshe ile mizizi ena kwa siri bila Mgonjwa wako kujua, ikishachemka chuja mpe kwenye kikombe kiasi tu na akishakunywa unachotakiwa kufanya chukua ile mizizi tena kwa siri kubwa urudi nayo makaburini kule ulikowaacha wenzio wanachimba kaburi baada ya kufika huko unatakiwa uirudishe ile mizizi ndani ya kaburi kwa siri bila ya kuonekana na yoyote miongoni mwa wanaochimba, ukionekana tu Dawa haitofanya kazi.
Na unatakiwa uiweke kaburini kabla mwili haujaletwa kuzikwa. ukifanikiwa marehemu atakapokuja kuzikwa hapo hapo KIFAFA kitakuwa kimezikwa na mgonjwa kapona kabisa.
NAWASILISHA.