Ugonjwa wa kifafa usikilizeni redioni. Simulizi yake ni ya kutishaa!

Ugonjwa wa kifafa usikilizeni redioni. Simulizi yake ni ya kutishaa!

Huu ugonjwa usikie tu, unanisumbua almost miaka miwili Sasa. Ikinitokea mkono wa kulia ndo naumia sana na kujing'ata.
Kitu kingine nilichonotice hivi karibuni ni kuwa ikinitokea huwa nakaa kama wiki hivi nakuwa sina kumbukumbu vizuri.
Ee Mungu naomba uniponye!!

Pole sana Mungu ni mwema [emoji1545]
 
Nakumbuka ilikuwa mwaka 1986 nikiwa na ufahamu na akili timamu, sikuwa naelewa kifafa ninini ila nilikuwa na maswali mengi sana Kila nikimtazama mama yangu mzazi ambaye asilimia kubwa mwili wake ulitawaliwa na vidonda. Nakumbuka Kuna wakati tukiwa kisimani mama alitumbukia kisimani si mara Moja na kupata vidonda na siku nyingine anadondoka kwenye moto na kupata majeraha makubwa sana. Kutoka kisimani au Mahali alipoanguka ilikuwa ni mpaka wasamaria wamtoe!! Nilikuwa najiuliza Sana kwamba ni nini kinamdondosha mama yangu niliyekuwa nampenda sana.

Kuna wakati niliona waganga wa asili wanapishana nyumbani kumtibia! Kwa kuwa nilikuwa mdogo sikuweza kufuatilia hasaa ni nini kinamsibu mama! Siku nyingine alidondoka sokoni katikati ya umati wa watu! Watu wakajaa kushangaa na wasamaria wema wakasaidia kutoa huduma ya kwanza ilikuwa ni hatari angeweza kudondoka kwa siku hata mara tatu! Wakati huo nilikuwa darasa la tatu!

Alipata ujauzito akafanikiwa kujifungua mapacha WAWILI lakini haikupita miezi mitatu alitumbukia nao kisimani hii ni kutokana na baba hakuwa mtu wa kukaa nyumbani muda mwingi alikuwa minadani, nakumbuka siku Ile mvua kubwa ilikuwa Ina nyesha!! Mama aliokolewa akiwa hai lakini watoto wale wote walipoteza maisha!! Ilimlazimu mama kuhamishiwa kijijini Kwa Babu mzaa mama na mimi pia nikatakiwa nikakae nae! Kwa kuwa ilikuwa kumtazamia Hali yake Kwa muda mfupi, niliombewa kusoma shule mojawapo hapo kijijini Kwa muda huku tukiendelea kumuuguza!

Babu na bibi walikuwa ni wanywaji wazuri wa pombe hivyo ikifika jioni tu huwezi kuwakuta nyumbani ,,bibi pia alikuwa mkorogaji mzuri sana wa pombe ,hivyo pale nyumbani muda mwingi mizigo ya Kuni ilikuwa haipungii!! Sasa siku Moja niliamka asubuhi mapema kuwahi shule ulipofika muda wa mapumziko nilitoloka shule kurudi nyumbani , Kiukweli siku Ile sikuwa na hamu ya kukaa darasani kabisa. Nilipofika nyumbani nikakuta bibi ametenga mapipa makubwa pombe na moto mkali wa makuti akiipika pombe kama kawaida yake .alipiniona tu kaniwakia sana kwa nini nimetoroka shule?

Akanikatia mahindi shambani nikachoma fasta na kuniamuru haraka nirudi shule!! Japo sikutaka kurudi shule lakini kishingo upande nilirejea tena shuleni!! Siku hiyo kukawa na michezo tukachelewa kidogo kurudi nyumbani !! Nilifika nyumbani jioni kabisa ila nilishangaa kuona Moshi mzito sana ndani na hakukuwa na dalili ya kuwepo mtu !! Nilizowea kumkuta mama amekaa nje ,lakini hakuwepo .nikajaribu kumuita hakuitika kabisa ! Nilijitahidi kuiingia ndani nikaona Kuna Moshi usio wa kawaida na harufu nzito kama vile mtu amechoma ngozi ya ng'ombe, harufu mbaya mnoo na kulikuwa Giza!! Nikalisogelea dirisha Ile kulifungua tu la haula!! Nikaushuhudia mwili wa mama ukiwa umeteketea kabisa!! Kilichobaki ni miguu ambayo ilikuwa nje ya makaa ya ule moto mkali sana.

Nilitoka mbio kuelekea kilabuni huku nikiwa nimechanganyikiwa hata kuongea siwezi ,nilishindwa kumueleza Babu kilichotokea nyumbani zaidi ya kumshika mkono na kuanza kumvuta Kwa ishara ya kukimbia kuelekea nyumbani Kila mtu pale kilabuni aliduwaa. Mama ameungua:: hilo ndio neno pekee nililoweza kulitamka hakuna aliyebaki pale kilabuni. Kufika nyumbani Kila aliekuwa anaingia ndani alitoka meangua kilio huzuni kubwa ilitanda pale nyumbani. Kwa nini mliacha moto bila kuuzima?

Watu wengi walikuwa wanahoji swali hilo huku wazee wakianza kuutoa mwili motoni, lakini tayari yalishakuwa majivu !! Nakumbuka wazee wakiwa wanakusanya majivu na kuyatia kwenye kiroba kikubwa hivi!! Lawama zote wakizielekeza Kwa bibi na Babu. Kwamba Kwa nini hawakuuzima moto baada kumaliza kupika pombe? Hakuna tulichookoa !! Tulimzika mama akiwa kwenye kiroba ! Tulizika majivu.

Naweza kusema nauchukia sana ugonjwa huu. Na usimpuuze mtu yeyote mwenye ugonjwa huu! Popote pale iwe nje au ndani ya familia yenu!! Ugonjwa huu Hauna tiba ya Moja Kwa Moja! Lakini wagonjwa wake wanahitaji sana uangalizi maalumu!! Katika miaka yangu nimejitahidi Sana kufanya utafiti kuhusu ugonjwa huu.

Nimejifunza mengi na sasa naweza kusema nipo karibu sana na wagonjwa wa kifafa kuwapa elimu na namna ya kuishi Kwa tahadhari na kuepuka hatari zinazowahusu watu Hawa. Iwe una ndugu, rafiki au jirani wa karibu ambae anateseka na ugonjwa huu tafadhali njoo dm yangu nitakupa elimu ya jinsi ya kumsaidia na jinsi anavyoweza kupona kabisa!! Usiupuuze ugonjwa huu ni hatari kupita kiasi!
Pole kwa uliyopitia! Hongera kwa kujitolea na kujituma kutoa elimu kwa ugonjwa wa kifafa!
 
Pole sana kaka
Huu ugonjwa
Ulimuondoa baba yangu mzazi

Moja ya vitu huwa sipendi kusikia ni pamoja na huu ugonjwa

Baba alifariki mwaka 2004 aliangukia mahala ambapo watu wa kumsaidia hawakujua wafanyaje, walijua amezimia tu wakamwagia maji mengi sana
Mshua alikufa moja kwa moja bibi anakuja kupata taarifa wameshakosea,

Ile huwa sitamani hata kukumbuka
Anyway kwa kuwa maisha Mungu ndo mpangaji basi hatuna budi kumshukuru kwa yote
 
Nakumbuka ilikuwa mwaka 1986 nikiwa na ufahamu na akili timamu, sikuwa naelewa kifafa ninini ila nilikuwa na maswali mengi sana Kila nikimtazama mama yangu mzazi ambaye asilimia kubwa mwili wake ulitawaliwa na vidonda. Nakumbuka Kuna wakati tukiwa kisimani mama alitumbukia kisimani si mara Moja na kupata vidonda na siku nyingine anadondoka kwenye moto na kupata majeraha makubwa sana. Kutoka kisimani au Mahali alipoanguka ilikuwa ni mpaka wasamaria wamtoe!! Nilikuwa najiuliza Sana kwamba ni nini kinamdondosha mama yangu niliyekuwa nampenda sana.

Kuna wakati niliona waganga wa asili wanapishana nyumbani kumtibia! Kwa kuwa nilikuwa mdogo sikuweza kufuatilia hasaa ni nini kinamsibu mama! Siku nyingine alidondoka sokoni katikati ya umati wa watu! Watu wakajaa kushangaa na wasamaria wema wakasaidia kutoa huduma ya kwanza ilikuwa ni hatari angeweza kudondoka kwa siku hata mara tatu! Wakati huo nilikuwa darasa la tatu!

Alipata ujauzito akafanikiwa kujifungua mapacha WAWILI lakini haikupita miezi mitatu alitumbukia nao kisimani hii ni kutokana na baba hakuwa mtu wa kukaa nyumbani muda mwingi alikuwa minadani, nakumbuka siku Ile mvua kubwa ilikuwa Ina nyesha!! Mama aliokolewa akiwa hai lakini watoto wale wote walipoteza maisha!! Ilimlazimu mama kuhamishiwa kijijini Kwa Babu mzaa mama na mimi pia nikatakiwa nikakae nae! Kwa kuwa ilikuwa kumtazamia Hali yake Kwa muda mfupi, niliombewa kusoma shule mojawapo hapo kijijini Kwa muda huku tukiendelea kumuuguza!

Babu na bibi walikuwa ni wanywaji wazuri wa pombe hivyo ikifika jioni tu huwezi kuwakuta nyumbani ,,bibi pia alikuwa mkorogaji mzuri sana wa pombe ,hivyo pale nyumbani muda mwingi mizigo ya Kuni ilikuwa haipungii!! Sasa siku Moja niliamka asubuhi mapema kuwahi shule ulipofika muda wa mapumziko nilitoloka shule kurudi nyumbani , Kiukweli siku Ile sikuwa na hamu ya kukaa darasani kabisa. Nilipofika nyumbani nikakuta bibi ametenga mapipa makubwa pombe na moto mkali wa makuti akiipika pombe kama kawaida yake .alipiniona tu kaniwakia sana kwa nini nimetoroka shule?

Akanikatia mahindi shambani nikachoma fasta na kuniamuru haraka nirudi shule!! Japo sikutaka kurudi shule lakini kishingo upande nilirejea tena shuleni!! Siku hiyo kukawa na michezo tukachelewa kidogo kurudi nyumbani !! Nilifika nyumbani jioni kabisa ila nilishangaa kuona Moshi mzito sana ndani na hakukuwa na dalili ya kuwepo mtu !! Nilizowea kumkuta mama amekaa nje ,lakini hakuwepo .nikajaribu kumuita hakuitika kabisa ! Nilijitahidi kuiingia ndani nikaona Kuna Moshi usio wa kawaida na harufu nzito kama vile mtu amechoma ngozi ya ng'ombe, harufu mbaya mnoo na kulikuwa Giza!! Nikalisogelea dirisha Ile kulifungua tu la haula!! Nikaushuhudia mwili wa mama ukiwa umeteketea kabisa!! Kilichobaki ni miguu ambayo ilikuwa nje ya makaa ya ule moto mkali sana.

Nilitoka mbio kuelekea kilabuni huku nikiwa nimechanganyikiwa hata kuongea siwezi ,nilishindwa kumueleza Babu kilichotokea nyumbani zaidi ya kumshika mkono na kuanza kumvuta Kwa ishara ya kukimbia kuelekea nyumbani Kila mtu pale kilabuni aliduwaa. Mama ameungua:: hilo ndio neno pekee nililoweza kulitamka hakuna aliyebaki pale kilabuni. Kufika nyumbani Kila aliekuwa anaingia ndani alitoka meangua kilio huzuni kubwa ilitanda pale nyumbani. Kwa nini mliacha moto bila kuuzima?

Watu wengi walikuwa wanahoji swali hilo huku wazee wakianza kuutoa mwili motoni, lakini tayari yalishakuwa majivu !! Nakumbuka wazee wakiwa wanakusanya majivu na kuyatia kwenye kiroba kikubwa hivi!! Lawama zote wakizielekeza Kwa bibi na Babu. Kwamba Kwa nini hawakuuzima moto baada kumaliza kupika pombe? Hakuna tulichookoa !! Tulimzika mama akiwa kwenye kiroba ! Tulizika majivu.

Naweza kusema nauchukia sana ugonjwa huu. Na usimpuuze mtu yeyote mwenye ugonjwa huu! Popote pale iwe nje au ndani ya familia yenu!! Ugonjwa huu Hauna tiba ya Moja Kwa Moja! Lakini wagonjwa wake wanahitaji sana uangalizi maalumu!! Katika miaka yangu nimejitahidi Sana kufanya utafiti kuhusu ugonjwa huu.

Nimejifunza mengi na sasa naweza kusema nipo karibu sana na wagonjwa wa kifafa kuwapa elimu na namna ya kuishi Kwa tahadhari na kuepuka hatari zinazowahusu watu Hawa. Iwe una ndugu, rafiki au jirani wa karibu ambae anateseka na ugonjwa huu tafadhali njoo dm yangu nitakupa elimu ya jinsi ya kumsaidia na jinsi anavyoweza kupona kabisa!! Usiupuuze ugonjwa huu ni hatari kupita kiasi!
Pole sana
 
Dah pole sana, inasikitisha sana.

katika tembea yangu katika pilika za kutafuta maisha nimewai fanya kazi na mjerumani mmoja mgonjwa wa kifafa, nilichoona jamaa alikuwa anavuta bangi, na alivyosema yeye inamsaidia sana, akivuta anakuwa sawa na anafanya kazi.

Kwa wenye ndugu wenye kifafa labda mujaribu, siyo kuvuta msokoto mzima kwa mara moja, msokoto mmoja anauvuta mara tatu hivi kwa siku, Maybe inaweza ikasaidia.

Kaka naomba unijibu pm
 
Kifafa ni hatari mkuu pole sana, kuna dada mmoja alianguka akipika mkono ukawa kwenye moto, msaada aliupata kwa majirani baada ya kuhisi harufu.
Samahani naomba kuuliza,inamaana anapokuwa karibu na moto hisia za kusema mkono ama mguu kuungua anakuwa hana,nauliza sio kwa kejeri ni katika kujua tu
 
Pole sana kwa yaliyokukuta

Kuhusu njia za kumsaidia mtu mwenye huo ugonjwa kwanini usiweke hapa kwa faida ya wasomaji wa sasa na wa baadae(miaka ijayo)

Naamini sio siku zote utapatikana PM lakini nyuzi za JF huwa zinaishi
Kati ya vitu ambavyo babu yetu alikuwa anaweza kutibu ni ugonjwa huu wa kifafa. Babu amefariki mwaka 1996 mungu saidia kuna baba yetu mdogo na binamu yetu wao w alikuwa karibu na babu wanaweza kutibu ugonjwa huu. Sharti kubwa asiwe ameshaanguka kwenye moto. Akiwa mgonjwa hajaanguka kwenye moto anapona. Nimeshuhudia wagonjwa wanne. Kama kuna mgonjwa DM nikuunganishe na huyu jamaa inshallah kama bahati unaweza kupona maana kila kitu ki nategemea na bahati ya mtu mwenzio anapona mwingine ikadunda naomba hili lizingatiwe. Kingine sikuhizi hata hosp kuna dawa hospitali inatuliza huu ugonjwa
 
Nakumbuka ilikuwa mwaka 1986 nikiwa na ufahamu na akili timamu, sikuwa naelewa kifafa ninini ila nilikuwa na maswali mengi sana Kila nikimtazama mama yangu mzazi ambaye asilimia kubwa mwili wake ulitawaliwa na vidonda. Nakumbuka Kuna wakati tukiwa kisimani mama alitumbukia kisimani si mara Moja na kupata vidonda na siku nyingine anadondoka kwenye moto na kupata majeraha makubwa sana. Kutoka kisimani au Mahali alipoanguka ilikuwa ni mpaka wasamaria wamtoe!! Nilikuwa najiuliza Sana kwamba ni nini kinamdondosha mama yangu niliyekuwa nampenda sana.

Kuna wakati niliona waganga wa asili wanapishana nyumbani kumtibia! Kwa kuwa nilikuwa mdogo sikuweza kufuatilia hasaa ni nini kinamsibu mama! Siku nyingine alidondoka sokoni katikati ya umati wa watu! Watu wakajaa kushangaa na wasamaria wema wakasaidia kutoa huduma ya kwanza ilikuwa ni hatari angeweza kudondoka kwa siku hata mara tatu! Wakati huo nilikuwa darasa la tatu!

Alipata ujauzito akafanikiwa kujifungua mapacha WAWILI lakini haikupita miezi mitatu alitumbukia nao kisimani hii ni kutokana na baba hakuwa mtu wa kukaa nyumbani muda mwingi alikuwa minadani, nakumbuka siku Ile mvua kubwa ilikuwa Ina nyesha!! Mama aliokolewa akiwa hai lakini watoto wale wote walipoteza maisha!! Ilimlazimu mama kuhamishiwa kijijini Kwa Babu mzaa mama na mimi pia nikatakiwa nikakae nae! Kwa kuwa ilikuwa kumtazamia Hali yake Kwa muda mfupi, niliombewa kusoma shule mojawapo hapo kijijini Kwa muda huku tukiendelea kumuuguza!

Babu na bibi walikuwa ni wanywaji wazuri wa pombe hivyo ikifika jioni tu huwezi kuwakuta nyumbani ,,bibi pia alikuwa mkorogaji mzuri sana wa pombe ,hivyo pale nyumbani muda mwingi mizigo ya Kuni ilikuwa haipungii!! Sasa siku Moja niliamka asubuhi mapema kuwahi shule ulipofika muda wa mapumziko nilitoloka shule kurudi nyumbani , Kiukweli siku Ile sikuwa na hamu ya kukaa darasani kabisa. Nilipofika nyumbani nikakuta bibi ametenga mapipa makubwa pombe na moto mkali wa makuti akiipika pombe kama kawaida yake .alipiniona tu kaniwakia sana kwa nini nimetoroka shule?

Akanikatia mahindi shambani nikachoma fasta na kuniamuru haraka nirudi shule!! Japo sikutaka kurudi shule lakini kishingo upande nilirejea tena shuleni!! Siku hiyo kukawa na michezo tukachelewa kidogo kurudi nyumbani !! Nilifika nyumbani jioni kabisa ila nilishangaa kuona Moshi mzito sana ndani na hakukuwa na dalili ya kuwepo mtu !! Nilizowea kumkuta mama amekaa nje ,lakini hakuwepo .nikajaribu kumuita hakuitika kabisa ! Nilijitahidi kuiingia ndani nikaona Kuna Moshi usio wa kawaida na harufu nzito kama vile mtu amechoma ngozi ya ng'ombe, harufu mbaya mnoo na kulikuwa Giza!! Nikalisogelea dirisha Ile kulifungua tu la haula!! Nikaushuhudia mwili wa mama ukiwa umeteketea kabisa!! Kilichobaki ni miguu ambayo ilikuwa nje ya makaa ya ule moto mkali sana.

Nilitoka mbio kuelekea kilabuni huku nikiwa nimechanganyikiwa hata kuongea siwezi ,nilishindwa kumueleza Babu kilichotokea nyumbani zaidi ya kumshika mkono na kuanza kumvuta Kwa ishara ya kukimbia kuelekea nyumbani Kila mtu pale kilabuni aliduwaa. Mama ameungua:: hilo ndio neno pekee nililoweza kulitamka hakuna aliyebaki pale kilabuni. Kufika nyumbani Kila aliekuwa anaingia ndani alitoka meangua kilio huzuni kubwa ilitanda pale nyumbani. Kwa nini mliacha moto bila kuuzima?

Watu wengi walikuwa wanahoji swali hilo huku wazee wakianza kuutoa mwili motoni, lakini tayari yalishakuwa majivu !! Nakumbuka wazee wakiwa wanakusanya majivu na kuyatia kwenye kiroba kikubwa hivi!! Lawama zote wakizielekeza Kwa bibi na Babu. Kwamba Kwa nini hawakuuzima moto baada kumaliza kupika pombe? Hakuna tulichookoa !! Tulimzika mama akiwa kwenye kiroba ! Tulizika majivu.

Naweza kusema nauchukia sana ugonjwa huu. Na usimpuuze mtu yeyote mwenye ugonjwa huu! Popote pale iwe nje au ndani ya familia yenu!! Ugonjwa huu Hauna tiba ya Moja Kwa Moja! Lakini wagonjwa wake wanahitaji sana uangalizi maalumu!! Katika miaka yangu nimejitahidi Sana kufanya utafiti kuhusu ugonjwa huu.

Nimejifunza mengi na sasa naweza kusema nipo karibu sana na wagonjwa wa kifafa kuwapa elimu na namna ya kuishi Kwa tahadhari na kuepuka hatari zinazowahusu watu Hawa. Iwe una ndugu, rafiki au jirani wa karibu ambae anateseka na ugonjwa huu tafadhali njoo dm yangu nitakupa elimu ya jinsi ya kumsaidia na jinsi anavyoweza kupona kabisa!! Usiupuuze ugonjwa huu ni hatari kupita kiasi!
pole sana ndugu yangu,lakini nakupa ukweli mmoja,sio kwamba nakupa moyo,hapana,ni uhalisia" amini usiamini,mama yako yupo sehemu sahihi huko alipo na ninakuhakikishia,siku ya ufufua{ukitenda mema}utaungana na mama yako mbele ya uso wa MUNGU" nasema ivo kwa sababu mateso aliyopitia sidhani kwamba alikuwa na kiburi au jeuri ya kutenda dhambi,sidhani kwamba alikuwa mzinzi kwa nina uhakika wanaume wengi walimkwepa licha ya kwamba yeye pia alikuwa hataki kutokana na hofu ya MUNGU!!!!!,,,,,,,asante
 
Back
Top Bottom