Ugonjwa wa Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers Disease): Kinga, tiba na ushauri

Ugonjwa wa Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers Disease): Kinga, tiba na ushauri

Nini Dawa ya vidonda vya tumbo japo ya kupooza


aluminium hydroxide+magnesium hydroxide, cemetidine ,omeprazole , kwa ushauri muone dactari akufanyie diagnosis kujua nini kimesababisha vidonda vya tumbo (peptic ulcer)
 
Kama umepimwa na kuthibitishiwa kuwa ni vidonda vya tumbo, jaribu kufanya yafuatayo:-
pima kijiko kimoja cha unga wa habbat soda + kikombe kimoja cha maziwa fresh ya ngombe + kikombe kimoja cha asali
mbichi + kiini cha yai la kuku wa kienyeji koroga uchanganye vizuri.
Dozi kijiko cha chakula vitatu asb, vitatu mchana na vitatu usiku kwa siku 21.
Mchanganyiko huu umewasaidia wengi, jaribu kisha urudi kutueleza matokeo yake huna haja ya ku-pm.
 
Ndugu zangu naomba mnisaidie dawa ya vidonda vya tumbo nateseka sana
asants

Vidonda vya tumbo mara nyingi husababishwa na infection ya bacteria iitwayo H-Pylori, zinatibika kwa dawa za kawaida aina ya antibiotics, nenda hospitali wakupime kuhakikisha chanzo cha tatizo kisha utapewa dawa. Jihadhari sana unaweza kuishia kutibu dalili kumbe tatizo lako ni jingine kabisa!
 
Dawa ya vidonda vya tumbo Nakushauri Utumie Dawa ya Hii ya Kienyeji Akiamka Asubuhi kabla ya kula kitu akojowe mkojo wako mwenyewe kwa kipimo cha Glasi moja uwe unakunywa mkojo wako kila siku Asubuhi kabla ya kula kitu kwa muda wa Siku Saba kisha Uende kupima hivyo Vidonda vya Tumbo Vitapona na kukauka kabisa ajaribu kutumia hiyo Dawa itakusaidia Sana.

Chanzo.
https://www.jamiiforums.com/jamii-p...ako-mwenyewe-kama-huyu-nyani-anavyofanya.html

https://www.jamiiforums.com/jf-doctor/203168-umetenda-maajabu-siwezi-kueleza-2.html
 
Ugonjwa wa Vidonda Vya Tumbo (Peptic Ulcer Disease)

Stomach-Ulcers-300x234.jpg
Ugonjwa wa vidonda vya tumbo hutokea iwapo kidonda cha ukubwa wa angalau wa nusu sentimita kitatokea kwenye sehemu yeyote ya ukuta wa tumbo au utumbo wa binadamu.

Kwa kawaida tatizo hili huleta maumivu makali sana ya tumbo ingawa si lazima kila maumivu ayapatayo mgonjwa husababishwa na vidonda vya tumbo.
Tafiti zimeonesha kwamba karibu asilimia 70 mpaka 90 ya vidonda vya tumbo husababishwa na aina ya vimelea vya bakteria wajulikanao kama Helicobacter pylori. Aidha matumizi ya baadhi ya dawa za kutuliza maumivu za jamii ya Non Steroid Anti-inflamatory Drugs kama Aspirin au Diclofenac huweza kusababisha au kuongeza uwezekano wa kupata ugonjwa huu.
Kuna dhana iliyozoeleka kuwa vidonda vya tumbo huathiri zaidi mfuko wa kuhifadhia chakula yaani tumbo (stomach). Dhana hii si kweli kwani sehemu inayoadhiriwa zaidi na tatizo hili ni sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo ijulikanayo kama duodenum.
Makundi ya PUD
Kuna makundi makuu yafuatayo ya ugonjwa huu
1. Vidonda vinavyotokea kwenye mfuko wa kuhifadhia chakula yaani tumbo (Gastric ulcers)
2. Vidonda vinavyotokea kwenye sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (Duodenal Ulcers)
3. Vidonda vinavyotokea kwenye koo (Oesophageal ulcers)
4. Vidonda vijulikanavyo kama Merckel's Diverticulum ulcers.

Visababishi vya PUD
Vidonda vya tumbo husababishwa na
imagesCAW9HZZ6.jpg
Maambukizi ya bakteria aina ya Helicobacter pylori: Imeonekana kuwa zaidi ya asilimia 50 ya watu duniani wana vimelea hivi katika utumbo. Aidha, miongoni mwao, karibu asilimia 80 huwa hawaoneshi dalili yeyote ya kuugua ugonjwa wa vidonda vya tumbo.

Aina hii ya vimelea vya bacteria husababisha karibu asilimia 60 ya vidonda vinavyotokea kwenye tumbo (gastric ulcers) na zaidi ya asilimia 90 yaduodenal ulcers.
Hali hii husababishwa zaidi na kushindwa kwa mfumo wa kinga mwilini kuwaua na kuwaondoa kabisa vimelea hawa ndani ya mwili. Matokeo ya kushindwa huku husababisha kuwepo kwa uambukizi wa kudumu katika kuta za tumbo (chronic active gastritis), uambukizi ambao huharibu mfumo na uwezo wa kuta za tumbo kutunza homoni ya Gastrin, ambayo ni muhimu katika kuhakikisha mazingira ya tumbo yanakuwa na kiwango salama cha tindikali.
Kwa kawaida, kazi ya gastrin ni kuchochea utolewaji wa tindikali (gastric acid) kutoka kwenye seli za ukuta wa tumbo zijulikanazo kama Parietal cells. Iwapo bacteria hawa watashambulia na kuharibu ukuta wa tumbo, mfumo wa gastrin pia uharibika, na hivyo kusababisha gastrin kuzalishwa kwa wingi hali ambayo pia huchochea uzalishaji wa gastric acid kwa wingi. Matokeo ya kuzalishwa kwa wingi kwa tindikali hii hupelekea kuchubuka kwa ukuta wa tumbo na hivyo kusababisha vidonda vya tumbo.
Matumizi ya muda mrefu ya dawa za kuondoa maumivu za kundi la NSAIDs: Ukuta wa utumbo hujilinda na madhara yatokanayo na tindikali ya utumbo (gastric acid) kwa kuwa na utando laini (mucus) ambao hutolewa na vichocheo vijulikavyo kama Prostaglandins. Dawa hizi za kundi la NSAIDs huharibu mfumo wa kutengeza vichocheo hivi yaani prostaglandins na hivyo kufanya kuta za tumbo kukosa utando wa kuzilinda na mashambulizi ya tindikali hali ambayo hupelekea kutokea kwa vidonda vya tumbo.
Uvutaji wa sigara: Uvutaji sigara sambamba na maambukizi ya bakteria aina ya Helicobacter pylori huongeza madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo. Ifahamike tu kuwa uvutaji sigara pekee hausababishi vidonda vya tumbo.
Vyakula au viungo vya chakula vyenye uchachu: Kinyume na dhana iliyozoeleka miongoni mwa watu wengi, baadhi ya vyakula vyenye uchachu na upilipili kama vile pilipili, ndimu, limao na masala havina uhusiano na uwezekano wa kupata vidonda vya tumbo.
Watu walio katika kundi la damu la O: Imeonekana pia kwamba kundi la damu lijulikanalo kama blood group O, halina uhusiano wa kusababisha vidonda vya tumbo.
Unywaji wa pombe: Unywaji wa pombe pekee hausababishi vidonda vya tumbo. Hata hivyo, unywaji wa pombe sambamba na maambukizi ya vimelea vya Helicobacter pylori huongeza madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo.
Vitu vingine: Vitu vinavyohusishwa na uongezaji wa madhara ya vidonda vya tumbo ni pamoja na upasuaji wa tumbo (major abdominal surgeries), kuungua kwa moto (burns), ugonjwa wa figo; na kubadilishwa kwa viungo vya mwili kama figo au ini.
Dalili au viashiria vya PUD
Maumivu makali au kiungulia maeneo ya chembe moyo (epigastic pains): Maumivu juu kidogo ya tumbo mara nyingi huendana na muda wa kula chakula. Mtu mwenye vidonda kwenye tumbo (gastric ulcers) hupata maumivu makali sana kipindi anapokula au mara tu baada ya kumaliza kula wakati aliye na vidonda kwenye sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (duodenal ulcers) hupata maumivu makali anapokuwa na njaa na hupata nafuu pindi anapokula.
  • Kuvimbiwa au tumbo kujaa gesi. Hali hii pia yaweza kuendana na kubeua au kujamba mara kwa mara.
  • Kucheua na kuongezeka kwa mate yanayoshuka tumboni baada ya kucheua.
  • Kichefuchefu na kutapika
  • Kupoteza hamu ya kula na kupungua uzito
  • Kutapika damu
  • Kupata haja kubwa cha rangi nyeusi au kahawia chenye harufu mbaya sana. Hii humaanisha mgonjwa anapata haja kubwa au choo kilichochanganyika na damu kwa mbali
Uwepo wa dalili kama kiungulia cha muda mrefu, kucheua na kutapika baada ya kula na historia ya kutumia dawa za kupunguza maumivu (NSAIDs) kwa muda muda mrefu bila kufuata ushauri wa daktari ni ishara tosha ya kumfanya mgonjwa kumuona daktari kumpima na kumfanyia uchunguzi ili kujiridhisha kuwa hana tatizo la vidonda vya tumbo.
Vipimo vya kutambua Ugonjwa wa vidonda vya tumbo
Vipimo vinavyotumika katika kutambua tatizo la vidonda vya tumbo ni pamoja na
1. Vipimo vya kuangalia ndani ya utumbo ambavyo ni pamoja na
  • Kipimo cha oesophagogastroduodenoscopy (EGD) au Upper GI endoscopy au gastroscopy. Kwa kutumia kipimo hiki, daktari huangalia moja kwa moja ndani ya utumbo wa mgonjwa kuona sehemu iliyo na vidonda pamoja na ukubwa wa tatizo lake. Aidha vipimo hivi humuwezesha daktari kuchukua sehemu ya utumbo iliyoathiriwa kwa ajili ya kuchunguza zaidi maabara ili kutambua uwepo wa vidonda au tatizo jingine linalomsumbua mgonjwa tofauti na vidonda vya tumbo.
  • Kipimo kingine kijulikanacho kama Barium meal kina uwezo pia wa kuthibitisha uwepo wa ugonjwa wa vidonda vya tumbo.
2. Vipimo vya kutambua uwepo wa uambukizi wa bakteria aina ya Helicobacter pylori kama
  • Kipimo kiitwacho Urea breath test
  • Kipimo cha kuotesha kinyama kilichochukuliwa kutoka katika kipimo cha OGD (culture from an OGD biopsy specimen).
  • Kipimo kinachoitwa Rapid Urease Test ambacho hufanywa kwa kutumia kinyama kilichochukuliwa kutoka kwenye utumbo wakati wa kufanya OGD. Kipimo hiki huangalia tabia ya vimelea hawa wa H. pylori.
  • Kipimo cha damu kwa ajili ya kutambua kiwango cha maambukizi ya vimelea wa H. pylori (antibody levels).
  • Kipimo cha haja kubwa kwa ajili ya kutambua kama bacteria wapo hai au wamekufa (stool antigen test). Kipimo hiki ni cha uhakika zaidi na nafuu kuliko kipimo cha Urea Breath Test.
  • Kipimo cha kimaabara cha kuchunguza kinyama kilichochukuliwa wakati wa kipimo cha OGD.
3. Vipimo vingine maalum vya kitaalamu zaidi kama
  • Kiwango cha homoni ya gastrin katika damu
  • Kipimo cha kuangalia uzalishaji wa homoni ya secretin ambayo uhusika katika uchocheaji wa homoni yagastrin
  • Kupima kiwango cha tindikali inayozalishwa katika tumbo.
Hata hivyo vipimo hivi ni vya gharama zaidi na ni aghalabu hutumika mara kwa mara.
Matibabu ya Ugonjwa wa vidonda vya tumbo
inti.jpg
Habari nzuri ni kuwa ugonjwa huu wa vidonda vya tumbo unatibika. Hata hivyo tabia ya baadhi ya wagonjwa wengi kuacha kumalizia dawa au kutumia dawa chini ya kiwango tofauti na walivyoshauriwa na madaktari husababisha kujirudia kwa tatizo au kufanya tatizo kuwa sugu zaidi.

Iwapo itagundulika uwepo wa H. pylori tiba inayotumika ni kuchanganya dawa za antibayotic (antibiotic) za aina tofauti kama Amoxicillin, Tetracycline, Clarithromycin au Metronidazole na dawa zenye uwezo wa kupunguza uzalishaji wa tindikali kwa wingi au kwa kitaalamu Proton Pump Inhibitors (PPI). Wakati mwingine daktari anaweza pia kuongeza dawa ya Bismuth Compound.
1. Kwa wagonjwa sugu, dawa za antibioc za aina tatu tofauti zinaweza kutumika. Dawa hizi ni pamoja naAmoxicillin + Clarithromycin + Metronidazole ambazo hutumika sambamba na dawa yeyote moja kutoka kundi la PPI kama vile Omeprazole au Pantoprazole pamoja na Bismuth Compound.
2. Kwa mgonjwa wa kawaida ambaye si sugu tiba bora inayoshauriwa ni kuchanganya dawa za antibiotic za aina mbili kama Amoxycillin + Metronidazole sambamba na dawa yeyote moja ya jamii ya PPI kama Pantoprazole.
3. Iwapo hakuna ushahidi wa kuwepo kwa uambukizi wa bacteria, dawa yeyote moja ya jamii ya PPI yaweza kutumika kwa muda mrefu zaidi bila kuchanganya na antibiotic yeyote.
Kwa kawaida kitendo cha kutibu na kuwaondoa Helicobacter Pylori humaliza na kuponyesha kabisa vidonda vya tumbo.
Hata hivyo, inawezekana kabisa ugonjwa huu kujirudia tena, hali ambayo hulazimisha kurudiwa tena kwa matibabu kwa kutumia aina nyingine ya antibiotics.
Aidha msomaji, inashauriwa si vyema kwa mgonjwa kujitibu mwenyewe bila kufuata ushauri wa daktari ili kuepuka madhara yanayoweza kutokea iwapo dawa hazitatumiwa inavyopaswa.
Ni kweli Maziwa ya ng'ombe yanaponyesha vidonda vya tumbo?
Kinyume na dhana iliyozoeleka ndani ya jamii, maziwa ya ng'ombe hayaponyeshi vidonda vya tumbo, bali huongeza madhara yatokanayo na ugonjwa huu. Hii ni kwa sababu, maziwa huwa na tabia ya kutengeneza aina fulani ya kinga au ukuta (protective coat) kwa vimelea vya Helicobacter Pylori ambayo huvikinga vimelea hivi dhidi ya mashambulizi ya dawa na hivyo kufanya dawa kushindwa kuwaua na kuwaondoa kabisa vimelea hivi.
Kinachotokea ni kuwa, maziwa huondoa tu kwa muda maumivu ya tumbo kwa kupunguza makali ya tindikali iliyopo tumboni. Pindi maziwa haya yanapoisha, maumivu hurejea tena na kuwa makali kama hapo awali.
Matibabu ya vidonda vya tumbo kwa njia ya upasuaji
Zipo aina nyingi ya upasuaji unaofanywa ili kutibu ugonjwa huu. Kuvuja damu ndani ya mwili kupitia vidonda vya tumbo ni sababu mojawapo ya kufanyiwa upasuaji kwa vile ni hatari sana hata kupelekea kifo iwapo mgonjwa hatapata tiba haraka.
  1. Endoscopy: ni njia inayotumika kutibu uvujaji wa damu unaotokana na vidonda vya tumbo. Aina hii ya tiba hutegemea sana aina na sehemu vilipo vidonda vya tumbo. Tiba hii yaweza kufanyika kwa kuchoma sehemu inayovuja damu ndani ya tumbo au utumbo kwa lengo la kusitisha uvujaji wa damu (cautery) au kwa kuvifunga vidonda kwa kutumia vifaa maalum (clippings). Aidha tiba hii ni nzuri na haina madhara yeyote yale.
  2. Madaktari wengi hupendelea upasuaji ujulikanao kitaalamu kama simple oversewing sambamba na tiba ya kuondoa bakteria. Aidha, mgonjwa pia hushauriwa kuacha matumizi ya dawa za NSAIDs kwa ajili ya kuondoa uwezekano wa damu kuendelea kutoka kwa vile kama ilivyoonekana hapo awali, matumizi ya dawa hizi huweza kusababisha uvujaji wa ndani kwa ndani ya mwili.
  3. Wagonjwa sugu, hufanyiwa baadhi ya upasuaji ambao huitaji utaalamu wa hali ya juu katika kuondoa neva na mishipa ya fahamu yenye kuhusika na uzalishaji wa tindikali katika tumbo.
Madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo
  1. Uvujaji wa damu ndani ya utumbo: Hali hii yaweza kusababishwa na vidonda kuenea hadi kwenye mishipa ya damu na hivyo kufanya damu kuanza kuvuja. Hali hii ni hatari sana na inahitaji tiba ya dharura.
  2. pen.jpg
    Vidonda vya tumbo huweza kusababisha tundu (kutoboka kwa ukuta wa tumbo) na kufanya vitu vilivyo ndani ya utumbo kutapakaa katika tumbo (abdomen) Hali hii huitwa peritonitis na ni hatari sana na inahitaji matibabu ya dharura. Aidha, kuenea huko kunaweza pia kuathiri tezi kongosho na kusababisha madhara katika tezi hiyo, ugonjwa unaojulikana kama pancreatitis.
  3. Vidonda vya tumbo vinaweza pia kuenea na kuathiri pia viungo vya jirani kama vile ini au kongosho (pancrease)
  4. Kuvimba kwa kuta za tumbo pamoja na makovu yasababishwayo na vidonda hivi huweza kusababisha kuziba kwa njia ya kupitishia chakula kutoka kwenye tumbo (stomach) kwenda sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (duodenum) hali ambayo kitaalamu huitwa gastric outlet obstruction.
  5. Iwapo vidonda vya tumbo vimesababishwa na H. pylori, kuna uwezekano wa kati ya mara tatu hadi ya sita ya mgonjwa kupata kansa ya tumbo (stomach cancer).
chanzo. Ugonjwa wa Vidonda Vya Tumbo (Peptic Ulcer Disease)
 
Asante ndugu,nilipima wakakuta na Duodenal Ulcers,nikapewa dawa lakini bado tatizo lipo

Ugonjwa wa Vidonda Vya Tumbo (Peptic Ulcer Disease)

Stomach-Ulcers-300x234.jpg
Ugonjwa wa vidonda vya tumbo hutokea iwapo kidonda cha ukubwa wa angalau wa nusu sentimita kitatokea kwenye sehemu yeyote ya ukuta wa tumbo au utumbo wa binadamu.

Kwa kawaida tatizo hili huleta maumivu makali sana ya tumbo ingawa si lazima kila maumivu ayapatayo mgonjwa husababishwa na vidonda vya tumbo.
Tafiti zimeonesha kwamba karibu asilimia 70 mpaka 90 ya vidonda vya tumbo husababishwa na aina ya vimelea vya bakteria wajulikanao kama Helicobacter pylori. Aidha matumizi ya baadhi ya dawa za kutuliza maumivu za jamii ya Non Steroid Anti-inflamatory Drugs kama Aspirin au Diclofenac huweza kusababisha au kuongeza uwezekano wa kupata ugonjwa huu.
Kuna dhana iliyozoeleka kuwa vidonda vya tumbo huathiri zaidi mfuko wa kuhifadhia chakula yaani tumbo (stomach). Dhana hii si kweli kwani sehemu inayoadhiriwa zaidi na tatizo hili ni sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo ijulikanayo kama duodenum.
Makundi ya PUD
Kuna makundi makuu yafuatayo ya ugonjwa huu
1. Vidonda vinavyotokea kwenye mfuko wa kuhifadhia chakula yaani tumbo (Gastric ulcers)
2. Vidonda vinavyotokea kwenye sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (Duodenal Ulcers)
3. Vidonda vinavyotokea kwenye koo (Oesophageal ulcers)
4. Vidonda vijulikanavyo kama Merckel’s Diverticulum ulcers.

Visababishi vya PUD
Vidonda vya tumbo husababishwa na
imagesCAW9HZZ6.jpg
Maambukizi ya bakteria aina ya Helicobacter pylori: Imeonekana kuwa zaidi ya asilimia 50 ya watu duniani wana vimelea hivi katika utumbo. Aidha, miongoni mwao, karibu asilimia 80 huwa hawaoneshi dalili yeyote ya kuugua ugonjwa wa vidonda vya tumbo.

Aina hii ya vimelea vya bacteria husababisha karibu asilimia 60 ya vidonda vinavyotokea kwenye tumbo (gastric ulcers) na zaidi ya asilimia 90 yaduodenal ulcers.
Hali hii husababishwa zaidi na kushindwa kwa mfumo wa kinga mwilini kuwaua na kuwaondoa kabisa vimelea hawa ndani ya mwili. Matokeo ya kushindwa huku husababisha kuwepo kwa uambukizi wa kudumu katika kuta za tumbo (chronic active gastritis), uambukizi ambao huharibu mfumo na uwezo wa kuta za tumbo kutunza homoni ya Gastrin, ambayo ni muhimu katika kuhakikisha mazingira ya tumbo yanakuwa na kiwango salama cha tindikali.
Kwa kawaida, kazi ya gastrin ni kuchochea utolewaji wa tindikali (gastric acid) kutoka kwenye seli za ukuta wa tumbo zijulikanazo kama Parietal cells. Iwapo bacteria hawa watashambulia na kuharibu ukuta wa tumbo, mfumo wa gastrin pia uharibika, na hivyo kusababisha gastrin kuzalishwa kwa wingi hali ambayo pia huchochea uzalishaji wa gastric acid kwa wingi. Matokeo ya kuzalishwa kwa wingi kwa tindikali hii hupelekea kuchubuka kwa ukuta wa tumbo na hivyo kusababisha vidonda vya tumbo.
Matumizi ya muda mrefu ya dawa za kuondoa maumivu za kundi la NSAIDs: Ukuta wa utumbo hujilinda na madhara yatokanayo na tindikali ya utumbo (gastric acid) kwa kuwa na utando laini (mucus) ambao hutolewa na vichocheo vijulikavyo kama Prostaglandins. Dawa hizi za kundi la NSAIDs huharibu mfumo wa kutengeza vichocheo hivi yaani prostaglandins na hivyo kufanya kuta za tumbo kukosa utando wa kuzilinda na mashambulizi ya tindikali hali ambayo hupelekea kutokea kwa vidonda vya tumbo.
Uvutaji wa sigara: Uvutaji sigara sambamba na maambukizi ya bakteria aina ya Helicobacter pylori huongeza madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo. Ifahamike tu kuwa uvutaji sigara pekee hausababishi vidonda vya tumbo.
Vyakula au viungo vya chakula vyenye uchachu: Kinyume na dhana iliyozoeleka miongoni mwa watu wengi, baadhi ya vyakula vyenye uchachu na upilipili kama vile pilipili, ndimu, limao na masala havina uhusiano na uwezekano wa kupata vidonda vya tumbo.
Watu walio katika kundi la damu la O: Imeonekana pia kwamba kundi la damu lijulikanalo kama blood group O, halina uhusiano wa kusababisha vidonda vya tumbo.
Unywaji wa pombe: Unywaji wa pombe pekee hausababishi vidonda vya tumbo. Hata hivyo, unywaji wa pombe sambamba na maambukizi ya vimelea vya Helicobacter pylori huongeza madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo.
Vitu vingine: Vitu vinavyohusishwa na uongezaji wa madhara ya vidonda vya tumbo ni pamoja na upasuaji wa tumbo (major abdominal surgeries), kuungua kwa moto (burns), ugonjwa wa figo; na kubadilishwa kwa viungo vya mwili kama figo au ini.
Dalili au viashiria vya PUD
Maumivu makali au kiungulia maeneo ya chembe moyo (epigastic pains): Maumivu juu kidogo ya tumbo mara nyingi huendana na muda wa kula chakula. Mtu mwenye vidonda kwenye tumbo (gastric ulcers) hupata maumivu makali sana kipindi anapokula au mara tu baada ya kumaliza kula wakati aliye na vidonda kwenye sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (duodenal ulcers) hupata maumivu makali anapokuwa na njaa na hupata nafuu pindi anapokula.
  • Kuvimbiwa au tumbo kujaa gesi. Hali hii pia yaweza kuendana na kubeua au kujamba mara kwa mara.
  • Kucheua na kuongezeka kwa mate yanayoshuka tumboni baada ya kucheua.
  • Kichefuchefu na kutapika
  • Kupoteza hamu ya kula na kupungua uzito
  • Kutapika damu
  • Kupata haja kubwa cha rangi nyeusi au kahawia chenye harufu mbaya sana. Hii humaanisha mgonjwa anapata haja kubwa au choo kilichochanganyika na damu kwa mbali
Uwepo wa dalili kama kiungulia cha muda mrefu, kucheua na kutapika baada ya kula na historia ya kutumia dawa za kupunguza maumivu (NSAIDs) kwa muda muda mrefu bila kufuata ushauri wa daktari ni ishara tosha ya kumfanya mgonjwa kumuona daktari kumpima na kumfanyia uchunguzi ili kujiridhisha kuwa hana tatizo la vidonda vya tumbo.
Vipimo vya kutambua Ugonjwa wa vidonda vya tumbo
Vipimo vinavyotumika katika kutambua tatizo la vidonda vya tumbo ni pamoja na
1. Vipimo vya kuangalia ndani ya utumbo ambavyo ni pamoja na
  • Kipimo cha oesophagogastroduodenoscopy (EGD) au Upper GI endoscopy au gastroscopy. Kwa kutumia kipimo hiki, daktari huangalia moja kwa moja ndani ya utumbo wa mgonjwa kuona sehemu iliyo na vidonda pamoja na ukubwa wa tatizo lake. Aidha vipimo hivi humuwezesha daktari kuchukua sehemu ya utumbo iliyoathiriwa kwa ajili ya kuchunguza zaidi maabara ili kutambua uwepo wa vidonda au tatizo jingine linalomsumbua mgonjwa tofauti na vidonda vya tumbo.
  • Kipimo kingine kijulikanacho kama Barium meal kina uwezo pia wa kuthibitisha uwepo wa ugonjwa wa vidonda vya tumbo.
2. Vipimo vya kutambua uwepo wa uambukizi wa bakteria aina ya Helicobacter pylori kama
  • Kipimo kiitwacho Urea breath test
  • Kipimo cha kuotesha kinyama kilichochukuliwa kutoka katika kipimo cha OGD (culture from an OGD biopsy specimen).
  • Kipimo kinachoitwa Rapid Urease Test ambacho hufanywa kwa kutumia kinyama kilichochukuliwa kutoka kwenye utumbo wakati wa kufanya OGD. Kipimo hiki huangalia tabia ya vimelea hawa wa H. pylori.
  • Kipimo cha damu kwa ajili ya kutambua kiwango cha maambukizi ya vimelea wa H. pylori (antibody levels).
  • Kipimo cha haja kubwa kwa ajili ya kutambua kama bacteria wapo hai au wamekufa (stool antigen test). Kipimo hiki ni cha uhakika zaidi na nafuu kuliko kipimo cha Urea Breath Test.
  • Kipimo cha kimaabara cha kuchunguza kinyama kilichochukuliwa wakati wa kipimo cha OGD.
3. Vipimo vingine maalum vya kitaalamu zaidi kama
  • Kiwango cha homoni ya gastrin katika damu
  • Kipimo cha kuangalia uzalishaji wa homoni ya secretin ambayo uhusika katika uchocheaji wa homoni yagastrin
  • Kupima kiwango cha tindikali inayozalishwa katika tumbo.
Hata hivyo vipimo hivi ni vya gharama zaidi na ni aghalabu hutumika mara kwa mara.
Matibabu ya Ugonjwa wa vidonda vya tumbo
inti.jpg
Habari nzuri ni kuwa ugonjwa huu wa vidonda vya tumbo unatibika. Hata hivyo tabia ya baadhi ya wagonjwa wengi kuacha kumalizia dawa au kutumia dawa chini ya kiwango tofauti na walivyoshauriwa na madaktari husababisha kujirudia kwa tatizo au kufanya tatizo kuwa sugu zaidi.

Iwapo itagundulika uwepo wa H. pylori tiba inayotumika ni kuchanganya dawa za antibayotic (antibiotic) za aina tofauti kama Amoxicillin, Tetracycline, Clarithromycin au Metronidazole na dawa zenye uwezo wa kupunguza uzalishaji wa tindikali kwa wingi au kwa kitaalamu Proton Pump Inhibitors (PPI). Wakati mwingine daktari anaweza pia kuongeza dawa ya Bismuth Compound.
1. Kwa wagonjwa sugu, dawa za antibioc za aina tatu tofauti zinaweza kutumika. Dawa hizi ni pamoja naAmoxicillin + Clarithromycin + Metronidazole ambazo hutumika sambamba na dawa yeyote moja kutoka kundi la PPI kama vile Omeprazole au Pantoprazole pamoja na Bismuth Compound.
2. Kwa mgonjwa wa kawaida ambaye si sugu tiba bora inayoshauriwa ni kuchanganya dawa za antibiotic za aina mbili kama Amoxycillin + Metronidazole sambamba na dawa yeyote moja ya jamii ya PPI kama Pantoprazole.
3. Iwapo hakuna ushahidi wa kuwepo kwa uambukizi wa bacteria, dawa yeyote moja ya jamii ya PPI yaweza kutumika kwa muda mrefu zaidi bila kuchanganya na antibiotic yeyote.
Kwa kawaida kitendo cha kutibu na kuwaondoa Helicobacter Pylori humaliza na kuponyesha kabisa vidonda vya tumbo.
Hata hivyo, inawezekana kabisa ugonjwa huu kujirudia tena, hali ambayo hulazimisha kurudiwa tena kwa matibabu kwa kutumia aina nyingine ya antibiotics.
Aidha msomaji, inashauriwa si vyema kwa mgonjwa kujitibu mwenyewe bila kufuata ushauri wa daktari ili kuepuka madhara yanayoweza kutokea iwapo dawa hazitatumiwa inavyopaswa.
Ni kweli Maziwa ya ng’ombe yanaponyesha vidonda vya tumbo?
Kinyume na dhana iliyozoeleka ndani ya jamii, maziwa ya ng'ombe hayaponyeshi vidonda vya tumbo, bali huongeza madhara yatokanayo na ugonjwa huu. Hii ni kwa sababu, maziwa huwa na tabia ya kutengeneza aina fulani ya kinga au ukuta (protective coat) kwa vimelea vya Helicobacter Pylori ambayo huvikinga vimelea hivi dhidi ya mashambulizi ya dawa na hivyo kufanya dawa kushindwa kuwaua na kuwaondoa kabisa vimelea hivi.
Kinachotokea ni kuwa, maziwa huondoa tu kwa muda maumivu ya tumbo kwa kupunguza makali ya tindikali iliyopo tumboni. Pindi maziwa haya yanapoisha, maumivu hurejea tena na kuwa makali kama hapo awali.
Matibabu ya vidonda vya tumbo kwa njia ya upasuaji
Zipo aina nyingi ya upasuaji unaofanywa ili kutibu ugonjwa huu. Kuvuja damu ndani ya mwili kupitia vidonda vya tumbo ni sababu mojawapo ya kufanyiwa upasuaji kwa vile ni hatari sana hata kupelekea kifo iwapo mgonjwa hatapata tiba haraka.
  1. Endoscopy: ni njia inayotumika kutibu uvujaji wa damu unaotokana na vidonda vya tumbo. Aina hii ya tiba hutegemea sana aina na sehemu vilipo vidonda vya tumbo. Tiba hii yaweza kufanyika kwa kuchoma sehemu inayovuja damu ndani ya tumbo au utumbo kwa lengo la kusitisha uvujaji wa damu (cautery) au kwa kuvifunga vidonda kwa kutumia vifaa maalum (clippings). Aidha tiba hii ni nzuri na haina madhara yeyote yale.
  2. Madaktari wengi hupendelea upasuaji ujulikanao kitaalamu kama simple oversewing sambamba na tiba ya kuondoa bakteria. Aidha, mgonjwa pia hushauriwa kuacha matumizi ya dawa za NSAIDs kwa ajili ya kuondoa uwezekano wa damu kuendelea kutoka kwa vile kama ilivyoonekana hapo awali, matumizi ya dawa hizi huweza kusababisha uvujaji wa ndani kwa ndani ya mwili.
  3. Wagonjwa sugu, hufanyiwa baadhi ya upasuaji ambao huitaji utaalamu wa hali ya juu katika kuondoa neva na mishipa ya fahamu yenye kuhusika na uzalishaji wa tindikali katika tumbo.
Madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo
  1. Uvujaji wa damu ndani ya utumbo: Hali hii yaweza kusababishwa na vidonda kuenea hadi kwenye mishipa ya damu na hivyo kufanya damu kuanza kuvuja. Hali hii ni hatari sana na inahitaji tiba ya dharura.
  2. pen.jpg
    Vidonda vya tumbo huweza kusababisha tundu (kutoboka kwa ukuta wa tumbo) na kufanya vitu vilivyo ndani ya utumbo kutapakaa katika tumbo (abdomen) Hali hii huitwa peritonitis na ni hatari sana na inahitaji matibabu ya dharura. Aidha, kuenea huko kunaweza pia kuathiri tezi kongosho na kusababisha madhara katika tezi hiyo, ugonjwa unaojulikana kama pancreatitis.
  3. Vidonda vya tumbo vinaweza pia kuenea na kuathiri pia viungo vya jirani kama vile ini au kongosho (pancrease)
  4. Kuvimba kwa kuta za tumbo pamoja na makovu yasababishwayo na vidonda hivi huweza kusababisha kuziba kwa njia ya kupitishia chakula kutoka kwenye tumbo (stomach) kwenda sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (duodenum) hali ambayo kitaalamu huitwa gastric outlet obstruction.
  5. Iwapo vidonda vya tumbo vimesababishwa na H. pylori, kuna uwezekano wa kati ya mara tatu hadi ya sita ya mgonjwa kupata kansa ya tumbo (stomach cancer).
chanzo. Ugonjwa wa Vidonda Vya Tumbo (Peptic Ulcer Disease)
 
Nimesikia tetesi kuwa kuna dawa ya vidonda vya tumbo,mwenye kujua wana JF naomba anijuze!
 
Dawa ya Vidonda vya tumbo, Chukua maganda ya komamanga mengi tu uyaanike juani kwa muda wa siku 3 yakisha kauka Uyatwange mpaka yatowe unga uchekeche upate unga wake,kipimo cha kikombe cha kahawa na Uchukue Asali ya nyuki mbichi kipimo cha

kikombe cha kahawa Uchanganye pamoja na unga wa maganda ya komamanga Utengeneze hivyo kila siku Unywe
Asubuhi kabla ya kula kitu kikombe kimoja na jioni kabla ya kula kitu kikombe kimoja kwa muda wa mwezi mmoja Inshaallah kwa uwezo wa Mwenyeezi Mungu utapona. Tumia kisha unipe
Feedback.
 
Nimesikia tetesi kuwa kuna dawa ya vidonda vya tumbo,mwenye kujua wana JF naomba anijuze!

Dawa za vidonda vya tumbo zipo kwa muda mrefu sana mkuu. kama una shida hiyo waone madaktari watakupatia dawa za aina tatu zinazoitwa kwa ujumla triple therapy.
 
Dawa ya Vidonda vya tumbo, Chukua maganda ya komamanga mengi tu uyaanike juani kwa muda wa siku 3 yakisha kauka Uyatwange mpaka yatowe unga uchekeche upate unga wake,kipimo cha kikombe cha kahawa na Uchukue Asali ya nyuki mbichi kipimo cha

kikombe cha kahawa Uchanganye pamoja na unga wa maganda ya komamanga Utengeneze hivyo kila siku Unywe
Asubuhi kabla ya kula kitu kikombe kimoja na jioni kabla ya kula kitu kikombe kimoja kwa muda wa mwezi mmoja Inshaallah kwa uwezo wa Mwenyeezi Mungu utapona. Tumia kisha unipe
Feedback.

Nashukuru ndugu kwa ushauri wako ntaufanyia kazi na ntakupa feedback,but hayo makomamanga yanpatikan wapi?
 
Pole kwa matatizo wengi wanaumwa sana ugonjwa huu kutokana sababu ikiwa mawazo au kutokula kwa kutokuwanacho au kuwa katika mahangaiko muda mwingi
Dawa yake ni ghali kidogo lakini rahisi kwa mtu wa shamba na kama una uwezo kidogo na dawa yake ni Parachichi tu
Tengeneza juisi ya parachichi na kunywa kabla ya kula chochote asubuhi na mchana kunywa hata baada ya kula na jion pia tumia
Tumia muda wa wiki mbili hadi tatu kama una uwezo tumia katika maisha yako yote utaepusha familia yako na madhara hayo ya vidonda vya tumbo
Wakati wa dawa usile mara kwa mara dagaa na maharagwe ila unaruhusiwa kula mara moja moja na epuka pia kutumia pilipili wakati wa tiba " UKINGATIA INSHALLAH MUNGU ATAKUPONYA NA WAPE DAWA HII WENZIO MAANA MATAPELI NI WENGI NA WAGONJWA WENGI WANAPOTEZA MAISHA KWA TATIZO HILI LAKINI WANGANGA WAJADI WENGI WANADANGANYA WATU BILA MAFANIKIO YOYOTE"
 
Habarini wanajamii forums nilitaka kujua ukiondoa dagaa na maharage ni vyakula gani vingine ambavyo mgonjwa wa ulcers hatakiwi kula na pia kwa nini hvyo harusiwi kula?
Kingine nilitaka kujua dawa inayotibu ulcers
 
Habarini wanajamii forums nilitaka kujua ukiondoa dagaa na maharage ni vyakula gani vingine ambavyo mgonjwa wa ulcers hatakiwi kula na pia kwa nini hvyo harusiwi kula?
Kingine nilitaka kujua dawa inayotibu ulcers
Salam,
Kama nimekufahamu itakuwa unakusudia "peptic ulcer" (PU) Vidonda vya tumbo ? kama ni hivyo

Masuala yako limejigawa sehemu 3 ambazo ntachangia kwa ufafanuzi kidogo kama ifatavyo:

UFUNGUZI: Ugonjwa wa PU ni ugonjwa unaotokana na kuathirika kwa tumbo aidha kwa kupata vidonda" Ulcer" au michubuko "Gastritis".

SABABU: Ni pamoja na mambo mbali mbali, ikichangiwa na kutokula kwa wakati, kula vyakula vikali/ vichachu, msongomano wa mawazo "tension /enxiety", au uchofu "stress" lakini msingi mkubwa ni kupungua kinga ya tumbo kuhimili tindi kali inayotolewa tumboni kusaga chakula "hydrochloric acid" hivyo badala ya kuyayusha chakula huanza pole pole kuuunguza utumbo aidha kwenye tumbo lenyewe au sehemu ya chini "Duodenum" na ndio maana vidonda hivi vikagawika sehemu mbili ambazo ni i. peptic ulcer na ii. duodenal ulcer.

MATIBABU: yamejigawa katika sehemu kuu kama ifuatavyo

1.Kuachana na sababu inayochangia mfano stress, ugomvi, mawazo, kutokula kwa wakati, kuto pumzika, kuto fanya mazoezi ya mwili.

2. Tabia ya ulaji wa vyakula vikali au vyenye acid, mfano Jamii ya maharage, kunde... nk, Vyakula vya acid kama ndimu , limau, maembe mabichi, ukwaju...nk, achari na vyakula vyoote vichachu, madawa kama asprin, diclofenac na dawa zote jamiii ya NSAD, mavyakula ya mafuta mengi. (Vidagaa vya kupika visivyo ungwa kwa ukali unaweza kula)

3. Anti acid, ni vyakula au dawa za kukata acid, mfano maziwa, vidonge vya Magnesium trisilicate, dawa za kunywa relcer gel, gastrocid...nk

4. Dawa za kuponesha vidonda na za kuua vidudu, zipo nyingi na za kisasa zinauwezo mkubwa wa kutibu lakini hapa si pahala pake kuzitaja kwani zinahitaji utaalam kwa matumizi yake.

SABABU ZA KUTOKULA VYAKULA HIVYO
Kama nilivyosema hapo juu sababu kubwa ya ulcer ni acid ambayo huunguza utumbo na hivyo vyakula vilivyo katwazwa pia vina kiwango kikubwa cha acid ni kusema vikiendelea kuliwa vitaongeza athari ya maradhi na vitaongeza mda wa kupona, au kusababisha hata kutoboa tumbo/ uchango na kusababisha kuvuja damu ambayo na hatari sana.

Natumai ntakuwa nimechangia angalau kidogo, kwa uchangia zaid karibu tena
Asante
 
Salam,
Kama nimekufahamu itakuwa unakusudia "peptic ulcer" (PU) Vidonda vya tumbo ? kama ni hivyo

Masuala yako limejigawa sehemu 3 ambazo ntachangia kwa ufafanuzi kidogo kama ifatavyo:

UFUNGUZI: Ugonjwa wa PU ni ugonjwa unaotokana na kuathirika kwa tumbo aidha kwa kupata vidonda" Ulcer" au michubuko "Gastritis".

SABABU: Ni pamoja na mambo mbali mbali, ikichangiwa na kutokula kwa wakati, kula vyakula vikali/ vichachu, msongomano wa mawazo "tension /enxiety", au uchofu "stress" lakini msingi mkubwa ni kupungua kinga ya tumbo kuhimili tindi kali inayotolewa tumboni kusaga chakula "hydrochloric acid" hivyo badala ya kuyayusha chakula huanza pole pole kuuunguza utumbo aidha kwenye tumbo lenyewe au sehemu ya chini "Duodenum" na ndio maana vidonda hivi vikagawika sehemu mbili ambazo ni i. peptic ulcer na ii. duodenal ulcer.

MATIBABU: yamejigawa katika sehemu kuu kama ifuatavyo

1.Kuachana na sababu inayochangia mfano stress, ugomvi, mawazo, kutokula kwa wakati, kuto pumzika, kuto fanya mazoezi ya mwili.

2. Tabia ya ulaji wa vyakula vikali au vyenye acid, mfano Jamii ya maharage, kunde... nk, Vyakula vya acid kama ndimu , limau, maembe mabichi, ukwaju...nk, achari na vyakula vyoote vichachu, madawa kama asprin, diclofenac na dawa zote jamiii ya NSAD, mavyakula ya mafuta mengi. (Vidagaa vya kupika visivyo ungwa kwa ukali unaweza kula)

3. Anti acid, ni vyakula au dawa za kukata acid, mfano maziwa, vidonge vya Magnesium trisilicate, dawa za kunywa relcer gel, gastrocid...nk

4. Dawa za kuponesha vidonda na za kuua vidudu, zipo nyingi na za kisasa zinauwezo mkubwa wa kutibu lakini hapa si pahala pake kuzitaja kwani zinahitaji utaalam kwa matumizi yake.

SABABU ZA KUTOKULA VYAKULA HIVYO
Kama nilivyosema hapo juu sababu kubwa ya ulcer ni acid ambayo huunguza utumbo na hivyo vyakula vilivyo katwazwa pia vina kiwango kikubwa cha acid ni kusema vikiendelea kuliwa vitaongeza athari ya maradhi na vitaongeza mda wa kupona, au kusababisha hata kutoboa tumbo/ uchango na kusababisha kuvuja damu ambayo na hatari sana.

Natumai ntakuwa nimechangia angalau kidogo, kwa uchangia zaid karibu tena
Asante

Nashukuru sana kwa mchango wako hakika mchango wako siyo kidogo kwangu ni mkubwa sana asante sana na kuhusu dawa ya kuponyesha nilikuwa naomba mawasiliano yako sababu naihitaji sana
 
Mi pia nina tatizo hilo. Baadhi ya dawa za Ulcers ni OMEPRAZOLE, RANITIDINE na CIMETIDINE[TAGAMENT]. Kuhusu dozi, wasiliana na Doctor au Pharmacist.
 
Mi pia nina tatizo hilo. Kwa faida ya wote wanaohitaji, Baadhi ya dawa za Ulcers ni OMEPRAZOLE, RANITIDINE na CIMETIDINE[TAGAMENT]. Kuhusu dozi, wasiliana na Doctor au Pharmacist.
 
Nashukuru sana kwa mchango wako hakika mchango wako siyo kidogo kwangu ni mkubwa sana asante sana na kuhusu dawa ya kuponyesha nilikuwa naomba mawasiliano yako sababu naihitaji sana mawasiliano yangu ni e-mail ni luzubamkono@yahoo.com
simu ni 0763692416

[FONT=georgia, serif]Salam Mkuu, Naona kuna mchango hapo juu bali nimeona ni bora nikuchagulie regime moja mana dawa zipo nyingi zinaweza kukuchanganya,[/FONT][FONT=georgia, serif]Sijajua uko serious kiasi gani kwa hili tatizo la vidonda vya tumbo, lakini kwa kuanzia ningekuandikia dawa zifuatozo ambazo natumai zinapatikana Nyumbani.[/FONT]
[FONT=georgia, serif]Utafiti mpya na uzoefu umeonesha kuwa maradhi haya yanaaambatana na uambukizo wa vidudu viitwavyo helicobacter pylori (H. pylori) hivyo matibabu mazima ni lazima kuviua vidudu hivyo ili ufanikiwe vizuri.[/FONT]
[FONT=georgia, serif]Hivyo nitatumia regime inayoitwa Triple therapy ambayo ni:[/FONT]
[FONT=georgia, serif]
[/FONT]
[FONT=georgia, serif]Tratment[/FONT]
[FONT=georgia, serif]1. Caps amoxycillin 500mgs tds for 14 days[/FONT]
[FONT=georgia, serif]2. Tabs flagyl 400mgs tds for 14 days[/FONT]
[FONT=georgia, serif]3. Caps omeprazole 20mgs od for 30 days (dakika 30 kabla chakula)[/FONT]
[FONT=georgia, serif]4. Mxt Relcer gel 15 mls tds for 14 days (baada ya chakula)[/FONT]
[FONT=georgia, serif]
[/FONT]
[FONT=georgia, serif] Utaacha na vile vyakula vikali kama tulivyoongea awali[/FONT]
[FONT=georgia, serif][/FONT]
[FONT=georgia, serif]Tahadhari [/FONT]
[FONT=georgia, serif]Unapotumia dawa hususan flagyl (ambazo nimekuandikia) usitumie pombe yeyote inakuwa ni sumu kali[/FONT]
[FONT=georgia, serif]Utapokua na suala la ziada tumia hii personal E mail[/FONT]
[FONT=georgia, serif]
[/FONT]
[FONT=georgia, serif]If like it let me know[/FONT]
[FONT=georgia, serif]Thank you [/FONT]
[FONT=georgia, serif]Li[/FONT]
[FONT=georgia, serif]
[/FONT][FONT=georgia, serif]
[/FONT]

 
[FONT=georgia, serif]Salam Mkuu, Naona kuna mchango hapo juu bali nimeona ni bora nikuchagulie regime moja mana dawa zipo nyingi zinaweza kukuchanganya,[/FONT][FONT=georgia, serif]Sijajua uko serious kiasi gani kwa hili tatizo la vidonda vya tumbo, lakini kwa kuanzia ningekuandikia dawa zifuatozo ambazo natumai zinapatikana Nyumbani.[/FONT]
[FONT=georgia, serif]Utafiti mpya na uzoefu umeonesha kuwa maradhi haya yanaaambatana na uambukizo wa vidudu viitwavyo helicobacter pylori (H. pylori) hivyo matibabu mazima ni lazima kuviua vidudu hivyo ili ufanikiwe vizuri.[/FONT]
[FONT=georgia, serif]Hivyo nitatumia regime inayoitwa Triple therapy ambayo ni:[/FONT]
[FONT=georgia, serif]
[/FONT]
[FONT=georgia, serif]Tratment[/FONT]
[FONT=georgia, serif]1. Caps amoxycillin 500mgs tds for 14 days[/FONT]
[FONT=georgia, serif]2. Tabs flagyl 400mgs tds for 14 days[/FONT]
[FONT=georgia, serif]3. Caps omeprazole 20mgs od for 30 days (dakika 30 kabla chakula)[/FONT]
[FONT=georgia, serif]4. Mxt Relcer gel 15 mls tds for 14 days (baada ya chakula)[/FONT]
[FONT=georgia, serif]
[/FONT]
[FONT=georgia, serif] Utaacha na vile vyakula vikali kama tulivyoongea awali[/FONT]
[FONT=georgia, serif][/FONT]
[FONT=georgia, serif]Tahadhari [/FONT]
[FONT=georgia, serif]Unapotumia dawa hususan flagyl (ambazo nimekuandikia) usitumie pombe yeyote inakuwa ni sumu kali[/FONT]
[FONT=georgia, serif]Utapokua na suala la ziada tumia hii personal E mail[/FONT]
[FONT=georgia, serif]
[/FONT]
[FONT=georgia, serif]If like it let me know[/FONT]
[FONT=georgia, serif]Thank you [/FONT]
[FONT=georgia, serif]Li[/FONT]
[FONT=georgia, serif]
[/FONT][FONT=georgia, serif]
[/FONT]


Mkuu tunahitaji sana msaada wako ila hiyo personal E mail haionekani hapo natanguliza shukrani za dhati kwako mkuu,huu ni mwaka wa 13 nateseka na hii kitu,tafadhali sana mkuu!!
 
Back
Top Bottom