Ugumu anaoupitia Harmonize ni kielelezo tosha kwanini sanaa yetu haikui. WCB inaua wasanii nje ya lable yao

Ugumu anaoupitia Harmonize ni kielelezo tosha kwanini sanaa yetu haikui. WCB inaua wasanii nje ya lable yao

mtu yuko nje ya wcb alafu unasema inamuua, kivipi? unataka wao ndo wamsaidia kupost au? sasa hizo chanel kutopost show za harmonze vinaingiliana vp na wcb? au ndo unamtafutia kiki kupitia hiyo wcb?
 
Ye apige kazi tu atakubalika.

Shida inayotokea anataka awe top ghafla huku watu wameshashtukia hawezi kihivyo kama simba.

Kitu nachosema kila siku aache kujilinganisha na simba na kuiga swag zake. Hii itamwangusha. Yani yule simba mi tembo, kila kitu kuiga!


Ye ajenge brand watu wamjue yeye kama yeye.

Hao top wa nigeria ukiangalia kila mmoja ana ka staili tofauti si kuigana igana kila kitu!!!
 
Japo mimi sio shabiki wa Diamond lakini huwa nashangaa sana mtu anaposema sijui Diamond mbinafsi, anataka kuwa juu peke yake, anatengeneza beef na wasanii wengine nk. Msanii anabaniwa vipi na Diamond kama yeye mwenyewe hajitumi, hana uthubutu, hajui kuutangaza mziki wake, hatafuti angalau collabo na wasanii wakubwa wa nje ambapo watamtangaza zaidi au muziki wake kuvuka border.

Muziki ni biashara kila mtu anahangaikia upande wake unabaniwa vipi na msanii mwingine? Harmonize kuondoka WCB binafsi hata mimi nilipongeza nikijua ataleta changamoto kubwa katika mziki wa bongo. Sasa iweje aonekane anabaniwa wakati lebo aliyokuwepo mwanzo ndio inaongoza kubaniwa na media nyingi?

Wakati yupo WCB anatoa hit songs haikua Clouds Media, East Africa Radio/TV, eFM, Millard Ayo ambazo zilikua zikimsampoti leo hii media hizo zinamsapoti Harmonize hapa anabaniwa vipi? Tayari wakati yupo WCB alishafanya International Collabo nyingi ambazo zimeshafanya atambulike zaidi Africa hapa napo nini kinamzuia asiwe mkubwa zaidi ya Diamond?

Pengine hii ndio ingekuwa fursa kwake kutoa hit songs nyingi na kujiongezea fan base kwasababu yupo huru, hebu nielewesheni labda sielewi wakuu maana ya msanii kubaniwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu umetiririka ataeshindwa kuelewa basi tena
 
Tatizo ninaloliona ni kuwa konde boy anataka ajilinganishe na mond kitu ambacho kwa namna moja ama nyingine hakiwezekani kama ataamua afanye music bila kushindana na mtu atatoboa ila akiendelea hivi na mafumbo kwenye music atapotea kingine sie mashabiki hatuwambii ukweli wasanii wetu tunawapa sifa zilizo nje ya uwezo wao
Menejment yake inabidi wamwambie asisikilize kabisa nyimbo za mondi na asiangalie kabisa social media za mondi. Ana obsession na mondi na akiendelea kuiga iga hivi hatakuwa na chochote kinachomtambulisha yeye kama brand zaidi ya tofauti ya majina tu. Huku konde music worldwide kule WCB miziki kila kitu kile kile wakati anajua konde worldwide haiwezi kuifikia wcb chiniya mondi!!!
 
kinachomkuza m2 ni his or her perfomance so kukubalika kwa harmonize.... it depends to his perfomance and how he make an interaction to others
Then jarbu kujifunza kuhusu youtube channels... WCB haiwez ku run youtube chennels zote zisipost show ya huyo harmonize...
Note: karudie uchunguz wako then urud hapa useme kitu
 
WCB ni Diamond peke yake, ukiwa katika Lebal hiyo mashabiki wake ndio watakua wako, ukiondoka unabakia na mashabiki wa Muziki pekee, wale wenhine wanabaki nae na kukuchukia wewe.

Naamini hivi kwasababu, wanaojitoa WCB sio member wa kundi au Band kusema tuwaone peke yao watafanyaje?

Na kama Nyimbo alizozitoa nje ya WCB angezitoa akiwa hajajitoa amini zingekua habari nyingine, mfano UNO na ingekua na Collable ya Mond ndani yake.

Sisi wabongo ni wavivu so inapotokea mtu kufanikiwa huchukia wengine kuwa juu yake ili kutokana na uvivu wake asije kuanza kutumwa.

Hali hii inasababisha Tasnia nzima kukosa uwazi na yote ni woga wakushuhudia wengine wakipata mafanikio.

Mfano. Thamani ya msanii mmoja mmoja hajulikani, malipo wanayoyapata katika tour, social media au shows hawayaweki wazi. Maisha yao tuu ni siri wengi hatujui wanaishi vp...

kwa vile ni kibongo bongo utaambiwa unafuatilia mambo ya watu ambao wengi wao hawana maisha ya majina yao. Lakini maisha yakina jigga tunayajua hadi mtaa anaoishi na kwa mwaka kaingiza shing ngapi na ni mmoja wa mabilionea.

Kwahiyo naamini katika uwazi kama chachu yakuchochea wengine wapambane zaidi na hatimae kupatikana wasanii wengi wenye mafanikio. Kuliko hivi sasa wenhi wanaogopana kutokana na njaa.




Sent using Jamii Forums mobile app
Ila tukumbuke fan base ya diamond kajenga kwa jitihada kubwa binafsi. Jamaa anatoka kitofauti kila siku watu hawamchoki na ndo maana na fans wanabaki hapo hapo. Hawa wengine wanafurukuta ila wapi kutoka kiupya kila mara inakuwa ngumu.

Nachotaka kusema ni kwamba kukitokea artist mwenye talent kama mondi haitajalisha yuko lebo gani kabaniwa au nini, lazima atatoka tu.
Na brand ya msanii si nyimbo ni pia muonekako, swag zile, nk maana kuna madem wanamfuatilia mondi cause wanampenda tu!!! Jux yule mi sioni anachoimba ila ndo hivo yupo!!!!

Sasa kama kuhujaliwa hivi vitu vingine mbali na sauti utabaki kulaumu tu. Bongo fleva bado ina fan base ndogo kulinganisha na naija au unyamezini. Mtu ana vi-mb vyake kidogo anachagua aangalie kichupa cha nani akiangalia cha mwenzako akiacha chako ujue kuna mengi nyuma ya pazia si kwamba anakuchukia au ngoma yako mbaya!!!
 
Huyu ndugu aliyeleta uzi si ajabu ukakuta yupo kwenye management team ya kondeboy, kwa excuses hizi totatoboa kweli????

Kitu pekee mlishindwa kugundua toka mwanzo ni kuwa kutoboa kiafrica needs alot of efforts accompanied na nyimbo nzuri, katika efforts hizo, collabo na wasanii wa nje haikwepeki mlidhani Mond ni mjinga kufanya collabo nyingi? Diamond aliwahi ingia mkataba na moja ya mameneja wa Wizkid kwa ajili ya kupush mambo fulani fulani huko west mnadhani hakuwa na akili eenhe?? Tanzania ni nchi ambayo iko nyuma kwenye international eyes kwa kila kitu na muziki ukiwepo, hivyo extra efforts zinahitajika kutoboa tusidanganyane.
Kondeboy ametoka WCB akiwa bado mchanga kwa international market, alihitaji menejiment makini izidi kumpush sana. Walifanyie hili kazi ama sivyo wataendelea kulia lia. Kwa maana nyingine alitakiwa apate management ambayo wapo smarter na wana exposure kuliko ya WCB.

Tukija kwa market ya ndani, anatakiwa awe na mashabiki loyal wengi sana , be it wapuuzi kama mnavowa-name au smart ones. Business wise mashabiki ni mashabiki as long as wanasupport unachofanya. Kibongo bongo mashabiki ambao ni loyal ni wa Diamond, Mpira, CCM, CDM, Wema (kwa kipindi chake) na Zari. Wengine wote au kwingine kote wanajaribu kugawana gawana waliobaki ambao hata sio loyal. Watu walimis-look wakati Konde anajitoa WCB kwa kudhani ana mashabiki wa kutosha ukweli ni kuwa hana mashabiki mnaodhani anao, mashabiki zake wengi ni wa Diamond na wamebaki na Diamond wao. Tulishauri miaka ya nyuma ufanyike mpango mkakati wa kuwatengeneza mashabiki loyal kwa Harmonize, Rayvanny na mavoko kipindi hicho WCB hawajamsajili mboso na lavalava. Sasa kondeboy hana mashabiki loyal wengi, na hajatoa nyimbo nzuri tangu atoke WCB graph lazima ishuke tu hakuna uchawi hapo.

Nimezungumzia loyal fanbase kwa uzito kuliko hata support ya media houses sababu sote tunajua impact ya social media ambayo ni uwanja huru, kuna muda unaingia kwa social media unashangaa kumechafuka posts za yanga ,simba au za Diamond etc unaanza kujiuliza kwani nini kinafanyika leo! Unajikuta umepata hamu ya kufuatilia.

Mashabiki wanaplay role kubwa sana ya kupost na kurepost kusababisha kitu kiende viral. Mfano mwingine unakuta wimbo umetoka unafanyiwa challenge Dunia nzima mfano ule “Kiki”(in my feelings) wa Drake, hata kama mtu huna interest nao unajikuta umefuatilia na umefahamu.

binti kiziwi hongera sana sina la kuongeza! Kumbe unatema madini hivi sema huwa una kaa kimya na kutoa like tuu......

Aiseee umenena
 
Bado cjaelewa WCB wanahusika vp hapo.
pia nshawai sikia Harmonize ndiye msanii mkubwa Tanzania anakwamishwa vp na hawa WCB
na vp kuhusu clouds waliompeleka Diamond international wanashindwa kumpiga tafu harmonize..?

Naomba muongozo kwa aliyeelewa
 
Nimefatilia kwa undani mikiki anayopitia Konde Boy toka ajiengue WCB. Kiukweli hajashuka Kama tunavyolazimishwa tuamini. Kwanza official songs katoa UNO na KUSHOTO KULIA na zote zimefanya vyema you tube. Hainshtui na Hujanikomoa ni bonus track wakati anajiandaa kuachia album yake.


Inashangaza sana kuwa Nchi yenye watu million 50 tunataka msanii awe Diamond Platnumz tu. Wenzetu Nigeria, International Artist ni wengi kwa sababu wanaachiana nafasi. Huku Tz tunapambana kushushana yaani mpaka media za YouTube hazipost show za Harmonize ili tu akose mvuto. Wenzetu wamefanikiwa kwa kuachiana nafasi.

Sasa hivi wamemwachia nafasi BURNABO. Hata hapa watu watakavyojibu ni kwa kumkatisha tamaa Konde Boy.
Mmeshindwa kujua kinavhomporomosha mnamsingizia Diamond? Muulizeni Diamond mwenyewe alipokubali kuwa Msukule nini kilimtokea, mpaka aliposhituka?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aendelee kupambana hapa hakuna atakayemuonea huruma......Diamond babalao yy saaizi ni kati ya wale sugu kawaita wajinga kaenda ccm Aendelee kutunga nyimbo za kumsifu magufuli
 
Japo mimi sio shabiki wa Diamond lakini huwa nashangaa sana mtu anaposema sijui Diamond mbinafsi, anataka kuwa juu peke yake, anatengeneza beef na wasanii wengine nk. Msanii anabaniwa vipi na Diamond kama yeye mwenyewe hajitumi, hana uthubutu, hajui kuutangaza mziki wake, hatafuti angalau collabo na wasanii wakubwa wa nje ambapo watamtangaza zaidi au muziki wake kuvuka border.

Muziki ni biashara kila mtu anahangaikia upande wake unabaniwa vipi na msanii mwingine? Harmonize kuondoka WCB binafsi hata mimi nilipongeza nikijua ataleta changamoto kubwa katika mziki wa bongo. Sasa iweje aonekane anabaniwa wakati lebo aliyokuwepo mwanzo ndio inaongoza kubaniwa na media nyingi?

Wakati yupo WCB anatoa hit songs haikua Clouds Media, East Africa Radio/TV, eFM, Millard Ayo ambazo zilikua zikimsampoti leo hii media hizo zinamsapoti Harmonize hapa anabaniwa vipi? Tayari wakati yupo WCB alishafanya International Collabo nyingi ambazo zimeshafanya atambulike zaidi Africa hapa napo nini kinamzuia asiwe mkubwa zaidi ya Diamond?

Pengine hii ndio ingekuwa fursa kwake kutoa hit songs nyingi na kujiongezea fan base kwasababu yupo huru, hebu nielewesheni labda sielewi wakuu maana ya msanii kubaniwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa maneno mafupi alipokuwa WCB nyimbo zake zilikuwa chache ila ametoka nyimbo zake zinapigwa media zote mpaka Wasafi hivyo wigo wake umetanuka apambane tu
 
Huyu ndugu aliyeleta uzi si ajabu ukakuta yupo kwenye management team ya kondeboy, kwa excuses hizi totatoboa kweli????

Kitu pekee mlishindwa kugundua toka mwanzo ni kuwa kutoboa kiafrica needs alot of efforts accompanied na nyimbo nzuri, katika efforts hizo, collabo na wasanii wa nje haikwepeki mlidhani Mond ni mjinga kufanya collabo nyingi? Diamond aliwahi ingia mkataba na moja ya mameneja wa Wizkid kwa ajili ya kupush mambo fulani fulani huko west mnadhani hakuwa na akili eenhe?? Tanzania ni nchi ambayo iko nyuma kwenye international eyes kwa kila kitu na muziki ukiwepo, hivyo extra efforts zinahitajika kutoboa tusidanganyane.
Kondeboy ametoka WCB akiwa bado mchanga kwa international market, alihitaji menejiment makini izidi kumpush sana. Walifanyie hili kazi ama sivyo wataendelea kulia lia. Kwa maana nyingine alitakiwa apate management ambayo wapo smarter na wana exposure kuliko ya WCB.

Tukija kwa market ya ndani, anatakiwa awe na mashabiki loyal wengi sana , be it wapuuzi kama mnavowa-name au smart ones. Business wise mashabiki ni mashabiki as long as wanasupport unachofanya. Kibongo bongo mashabiki ambao ni loyal ni wa Diamond, Mpira, CCM, CDM, Wema (kwa kipindi chake) na Zari. Wengine wote au kwingine kote wanajaribu kugawana gawana waliobaki ambao hata sio loyal. Watu walimis-look wakati Konde anajitoa WCB kwa kudhani ana mashabiki wa kutosha ukweli ni kuwa hana mashabiki mnaodhani anao, mashabiki zake wengi ni wa Diamond na wamebaki na Diamond wao. Tulishauri miaka ya nyuma ufanyike mpango mkakati wa kuwatengeneza mashabiki loyal kwa Harmonize, Rayvanny na mavoko kipindi hicho WCB hawajamsajili mboso na lavalava. Sasa kondeboy hana mashabiki loyal wengi, na hajatoa nyimbo nzuri tangu atoke WCB graph lazima ishuke tu hakuna uchawi hapo.

Nimezungumzia loyal fanbase kwa uzito kuliko hata support ya media houses sababu sote tunajua impact ya social media ambayo ni uwanja huru, kuna muda unaingia kwa social media unashangaa kumechafuka posts za yanga ,simba au za Diamond etc unaanza kujiuliza kwani nini kinafanyika leo! Unajikuta umepata hamu ya kufuatilia.

Mashabiki wanaplay role kubwa sana ya kupost na kurepost kusababisha kitu kiende viral. Mfano mwingine unakuta wimbo umetoka unafanyiwa challenge Dunia nzima mfano ule “Kiki”(in my feelings) wa Drake, hata kama mtu huna interest nao unajikuta umefuatilia na umefahamu.
Point zako zimeshiba nadhani zimemsaidia hata Komando Jide maana ana mashabiki wake ambao amekuwa nao tangu anaanza muziki pamoja na mashabiki wapya ambao wanapatikana kutokana na uwepo wa wale wengine
 
Back
Top Bottom