Ugumu wa Maisha husababisha Wanaume kuugua kwa wingi matatizo ya Afya ya Akili kuliko Mwanamke

Ugumu wa Maisha husababisha Wanaume kuugua kwa wingi matatizo ya Afya ya Akili kuliko Mwanamke

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Wataalamu wa afya ya akili na wanasaikolojia wametaja sababu 10 zinazochangia wanaume kuongoza kuugua magonjwa ya afya ya akili ikilinganishwa na wanawake.

Sababu hizo ni kuzongwa na majukumu, ugumu wa maisha, utafutaji, malezi, usiri, kukua kwa teknolojia, matarajio ya maisha, sonona, matukio ya nyuma na matumizi ya mihadarati na pombe kupindukia.

Takwimu za Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) zinaonyesha kuna ongezeko la wagonjwa wa afya ya akili kwa asilimia 17 kwa mwaka 2020/21 huku wanaume wakikabiliwa zaidi na tatizo hilo ikilinganishwa na wanawake.

Kati ya wagonjwa wa nje 24,014 walioonwa, wanaume walikuwa 15,205 ikilinganishwa na wanawake 8,809.

Mtaalamu wa Afya ya Akili na Mwanasaikolojia kutoka Taasisi ya Mental Health Tanzania, Dk Philimina Scarion alisema kuna vyanzo vingi vinavyosababisha wanaume wapate msongo mawazo ambao mwishowe hufikia sonona na kujikuta wakipata tatizo la afya ya akili.

“Wanaume wanaoishi katika nchi za uchumi mdogo na kati, kama Tanzania, wengi huwa na msongo wa mawazo mara nyingi ikilinganishwa na wanawake,” alisema Dk Scarion.

Alitaja sababu nyingine kuwa wengi wao ni wazito kuzungumza ya sirini mwao, hivyo hujikuta wakikaa na matatizo moyoni baadaye yanafika hatua ya juu na kuchanganyikiwa.

“Pia, jamii yetu imekuwa na dhana kuwa mwanamume ni mtu mwenye nguvu, hivyo hapaswi kuonyesha udhaifu wa kuumizwa hivyo wanabaki na maswali mengi wakijiuliza na kujijibu wenyewe,” alisema Dk Philimina.

Mtaalamu wa Saikolojia, Saldin Kimangale alitaja baadhi ya sababu hizo ni wanaume kujijengea ukuta na si wepesi kutafuta msaada mapema ukilinganisha na wanawake.

Alisema ongezeko linatokana zaidi na matumizi ya ulevi na dawa za kulevya, tafiti zinaonyesha wanaume ni watumiaji zaidi kuliko wanawake.

Chanzo: Mwananchi
 
Mwanaume ni bulldozer unatafutia mke, watoto na wazazi bado lawama tele.
Mtaani kugumu nyumbani kugumu lzm uwe chizi.
 
Wataalamu wa afya ya akili na wanasaikolojia wametaja sababu 10 zinazochangia wanaume kuongoza kuugua magonjwa ya afya ya akili ikilinganishwa na wanawake.

Sababu hizo ni kuzongwa na majukumu, ugumu wa maisha, utafutaji, malezi, usiri, kukua kwa teknolojia, matarajio ya maisha, sonona, matukio ya nyuma na matumizi ya mihadarati na pombe kupindukia.

Takwimu za Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) zinaonyesha kuna ongezeko la wagonjwa wa afya ya akili kwa asilimia 17 kwa mwaka 2020/21 huku wanaume wakikabiliwa zaidi na tatizo hilo ikilinganishwa na wanawake.

Kati ya wagonjwa wa nje 24,014 walioonwa, wanaume walikuwa 15,205 ikilinganishwa na wanawake 8,809.

Mtaalamu wa Afya ya Akili na Mwanasaikolojia kutoka Taasisi ya Mental Health Tanzania, Dk Philimina Scarion alisema kuna vyanzo vingi vinavyosababisha wanaume wapate msongo mawazo ambao mwishowe hufikia sonona na kujikuta wakipata tatizo la afya ya akili.

“Wanaume wanaoishi katika nchi za uchumi mdogo na kati, kama Tanzania, wengi huwa na msongo wa mawazo mara nyingi ikilinganishwa na wanawake,” alisema Dk Scarion.

Alitaja sababu nyingine kuwa wengi wao ni wazito kuzungumza ya sirini mwao, hivyo hujikuta wakikaa na matatizo moyoni baadaye yanafika hatua ya juu na kuchanganyikiwa.

“Pia, jamii yetu imekuwa na dhana kuwa mwanamume ni mtu mwenye nguvu, hivyo hapaswi kuonyesha udhaifu wa kuumizwa hivyo wanabaki na maswali mengi wakijiuliza na kujijibu wenyewe,” alisema Dk Philimina.

Mtaalamu wa Saikolojia, Saldin Kimangale alitaja baadhi ya sababu hizo ni wanaume kujijengea ukuta na si wepesi kutafuta msaada mapema ukilinganisha na wanawake.

Alisema ongezeko linatokana zaidi na matumizi ya ulevi na dawa za kulevya, tafiti zinaonyesha wanaume ni watumiaji zaidi kuliko wanawake.

Chanzo: Mwananchi
Sisi Wanaume ni viumbe wavumilivu sana.Ndio maana kadiri siku zinavyoenda tunabaki wachache Sana.

Sent from my Infinix X688C using JamiiForums mobile app
 
Wataalamu wa afya ya akili na wanasaikolojia wametaja sababu 10 zinazochangia wanaume kuongoza kuugua magonjwa ya afya ya akili ikilinganishwa na wanawake.

Sababu hizo ni kuzongwa na majukumu, ugumu wa maisha, utafutaji, malezi, usiri, kukua kwa teknolojia, matarajio ya maisha, sonona, matukio ya nyuma na matumizi ya mihadarati na pombe kupindukia.

Takwimu za Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) zinaonyesha kuna ongezeko la wagonjwa wa afya ya akili kwa asilimia 17 kwa mwaka 2020/21 huku wanaume wakikabiliwa zaidi na tatizo hilo ikilinganishwa na wanawake.

Kati ya wagonjwa wa nje 24,014 walioonwa, wanaume walikuwa 15,205 ikilinganishwa na wanawake 8,809.

Mtaalamu wa Afya ya Akili na Mwanasaikolojia kutoka Taasisi ya Mental Health Tanzania, Dk Philimina Scarion alisema kuna vyanzo vingi vinavyosababisha wanaume wapate msongo mawazo ambao mwishowe hufikia sonona na kujikuta wakipata tatizo la afya ya akili.

“Wanaume wanaoishi katika nchi za uchumi mdogo na kati, kama Tanzania, wengi huwa na msongo wa mawazo mara nyingi ikilinganishwa na wanawake,” alisema Dk Scarion.

Alitaja sababu nyingine kuwa wengi wao ni wazito kuzungumza ya sirini mwao, hivyo hujikuta wakikaa na matatizo moyoni baadaye yanafika hatua ya juu na kuchanganyikiwa.

“Pia, jamii yetu imekuwa na dhana kuwa mwanamume ni mtu mwenye nguvu, hivyo hapaswi kuonyesha udhaifu wa kuumizwa hivyo wanabaki na maswali mengi wakijiuliza na kujijibu wenyewe,” alisema Dk Philimina.

Mtaalamu wa Saikolojia, Saldin Kimangale alitaja baadhi ya sababu hizo ni wanaume kujijengea ukuta na si wepesi kutafuta msaada mapema ukilinganisha na wanawake.

Alisema ongezeko linatokana zaidi na matumizi ya ulevi na dawa za kulevya, tafiti zinaonyesha wanaume ni watumiaji zaidi kuliko wanawake.

Chanzo: Mwananchi
Miss Zomba
 
Mfano unaweza kuta familia ya watoto wa kike na wakiume ambao ni wakubwa wanaishi nyumba moja, lakini wakike wakawa na furaha na kucheka muda wote hata kama kuna shida.
Lakini wakiume ndio utakuta wenye mawazo na huzuni muda wote sababu hakuna sababu ya kucheka ilhali kuna tatizo bali unafikiria njia ya kutatua hilo tatizo.

Lazima kichwa kipasuke sababu hata ukisema wanawake hawajali wala kuwa na msaada wowote, hivyo hapo ni haki yako kuwa kichaa.
 
Back
Top Bottom