Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Wataalamu wa afya ya akili na wanasaikolojia wametaja sababu 10 zinazochangia wanaume kuongoza kuugua magonjwa ya afya ya akili ikilinganishwa na wanawake.
Sababu hizo ni kuzongwa na majukumu, ugumu wa maisha, utafutaji, malezi, usiri, kukua kwa teknolojia, matarajio ya maisha, sonona, matukio ya nyuma na matumizi ya mihadarati na pombe kupindukia.
Takwimu za Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) zinaonyesha kuna ongezeko la wagonjwa wa afya ya akili kwa asilimia 17 kwa mwaka 2020/21 huku wanaume wakikabiliwa zaidi na tatizo hilo ikilinganishwa na wanawake.
Kati ya wagonjwa wa nje 24,014 walioonwa, wanaume walikuwa 15,205 ikilinganishwa na wanawake 8,809.
Mtaalamu wa Afya ya Akili na Mwanasaikolojia kutoka Taasisi ya Mental Health Tanzania, Dk Philimina Scarion alisema kuna vyanzo vingi vinavyosababisha wanaume wapate msongo mawazo ambao mwishowe hufikia sonona na kujikuta wakipata tatizo la afya ya akili.
“Wanaume wanaoishi katika nchi za uchumi mdogo na kati, kama Tanzania, wengi huwa na msongo wa mawazo mara nyingi ikilinganishwa na wanawake,” alisema Dk Scarion.
Alitaja sababu nyingine kuwa wengi wao ni wazito kuzungumza ya sirini mwao, hivyo hujikuta wakikaa na matatizo moyoni baadaye yanafika hatua ya juu na kuchanganyikiwa.
“Pia, jamii yetu imekuwa na dhana kuwa mwanamume ni mtu mwenye nguvu, hivyo hapaswi kuonyesha udhaifu wa kuumizwa hivyo wanabaki na maswali mengi wakijiuliza na kujijibu wenyewe,” alisema Dk Philimina.
Mtaalamu wa Saikolojia, Saldin Kimangale alitaja baadhi ya sababu hizo ni wanaume kujijengea ukuta na si wepesi kutafuta msaada mapema ukilinganisha na wanawake.
Alisema ongezeko linatokana zaidi na matumizi ya ulevi na dawa za kulevya, tafiti zinaonyesha wanaume ni watumiaji zaidi kuliko wanawake.
Chanzo: Mwananchi
Sababu hizo ni kuzongwa na majukumu, ugumu wa maisha, utafutaji, malezi, usiri, kukua kwa teknolojia, matarajio ya maisha, sonona, matukio ya nyuma na matumizi ya mihadarati na pombe kupindukia.
Takwimu za Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) zinaonyesha kuna ongezeko la wagonjwa wa afya ya akili kwa asilimia 17 kwa mwaka 2020/21 huku wanaume wakikabiliwa zaidi na tatizo hilo ikilinganishwa na wanawake.
Kati ya wagonjwa wa nje 24,014 walioonwa, wanaume walikuwa 15,205 ikilinganishwa na wanawake 8,809.
Mtaalamu wa Afya ya Akili na Mwanasaikolojia kutoka Taasisi ya Mental Health Tanzania, Dk Philimina Scarion alisema kuna vyanzo vingi vinavyosababisha wanaume wapate msongo mawazo ambao mwishowe hufikia sonona na kujikuta wakipata tatizo la afya ya akili.
“Wanaume wanaoishi katika nchi za uchumi mdogo na kati, kama Tanzania, wengi huwa na msongo wa mawazo mara nyingi ikilinganishwa na wanawake,” alisema Dk Scarion.
Alitaja sababu nyingine kuwa wengi wao ni wazito kuzungumza ya sirini mwao, hivyo hujikuta wakikaa na matatizo moyoni baadaye yanafika hatua ya juu na kuchanganyikiwa.
“Pia, jamii yetu imekuwa na dhana kuwa mwanamume ni mtu mwenye nguvu, hivyo hapaswi kuonyesha udhaifu wa kuumizwa hivyo wanabaki na maswali mengi wakijiuliza na kujijibu wenyewe,” alisema Dk Philimina.
Mtaalamu wa Saikolojia, Saldin Kimangale alitaja baadhi ya sababu hizo ni wanaume kujijengea ukuta na si wepesi kutafuta msaada mapema ukilinganisha na wanawake.
Alisema ongezeko linatokana zaidi na matumizi ya ulevi na dawa za kulevya, tafiti zinaonyesha wanaume ni watumiaji zaidi kuliko wanawake.
Chanzo: Mwananchi