TUKANA UONE
JF-Expert Member
- Jan 3, 2018
- 2,345
- 6,970
Ubaya Ubwela & Nyie Hamuogopi vimepita,tujikite kwenye mada kuntu!
Kuna mshikaji wangu mmoja tulimaliza wote Sekondari na bahati nzuri hata chuo tukasoma wote,Mimi na yeye tulitokea Kuwa marafiki sana na hata hapo nyuma Kuna Uzi niliuweka hapa unaohusu maisha ya Ughaibuni nilimzungumzia!
Baada ya sote kumaliza chuo hatukuwa vizuri kiuchumi,hivyo tukaunganisha nguvu Kwa pesa kidogo tulizokuwa nazo tukaona tufanye biashara ya nafaka,Biashara mwanzo ilikuwa na changamoto ila tukakomaa hatimaye tukajipata,nyumbani kwao ilikuwa kama kwetu na kwetu kama kwao!
Mama yake amezoea kuniita pacha wa Mwanaye kwasababu tulikuwa hatuachani!
Kumbe jamaa alikuwa anafanya mipango ambayo alijua yeye alifanyaje fanyaje ghafla anakuja kuniambia amepata Visa ya Kwenda Marekani,so nikamuuliza Marekani anakwenda Kusoma au?,Akaniambia amepata mchongo wa kazi!
Nikamuuliza mbona imekuwa ghafla sana na hakunishirikisha kama rafiki yake?,ok hilo nikaachana nalo maana ilikuwa ni pasheni yake siku nyingi kutimkia huko maana hata wakati tunafanya biashara ndoto zake ilikuwa kutimkia huko!
Ila baada ya yeye kufika huko akaniambia Kuna wabongo wengi wanatimkia huko kupitia Kongo na Burundi,sijui kama ni kweli au alinidanganya maana hata yeye anasema alipewa mchongo na wabongo hivyo akalipa Hela akaenda hadi Burundi ndiko alikoondokea,Sina hakika lakini sikujali sana!
Nakumbuka kabla ya kuondoka siku tukiwa pale kwao,mama yake wakati anamuaga jamaa alikuwa akilia Kwa Uchungu sana na kimhakikishia mama yake kwamba anaenda kupambana na atahakikisha kila Mwezi atakuwa anamtumia Hela ili wajenge nyumba za kiwango Cha Kimataifa!,Binafsi nilimtia moyo nikamwambia asije kuwasahau ndugu zake na mama yake kwasababu amebakiwa na dada 3 na mama yake na yeye ndiye kijana mkubwa na wapekee!
Kweli jamaa aliondoka na baada ya kufika huko tukawa tunawasiliana hadi Leo na bahati nzuri haikuzidi miezi 3 jamaa akaniambia amepata makaratasi (Documents)ambazo pia zimempa kibali Cha kufanya kazi,alipoanza kazi kiukweli alikuwa akimtumia mama yake kila mwezi Dolla 1000 na akaniaomba niwasaidie kuwatafutia kiwanja maeneo ya Tegeta,nilifanikiwa kupata eneo ambalo lilikuwa likiuzwa pesa chafu ambako nikajua fika kwasababu jamaa anajitafuta hawezi kulimudu,nikamshauri nimtafutie eneo mahali pengine ambako ni nje ya mji na bei ambayo ataimudu,baada ya kumwambia jamaa akagoma akasema yeye anataka Tegeta,hivyo nikamwambia Kuna eneo hilo la mara ya kwanza bei yake ni Tsh 150 milioni,nikaona jamaa hashituki,duuuuu nikapatwa maswali sana uenda jamaa kweli kapata kazi ya maana,kwasababu alikuwa akiniambia mahali anapofanya kazi analipwa $ 30 Kwa Siku na anafanya kazi saa 8,hivyo nikapiga hesabu zangu Kwa haraka haraka nikagundua jamaa Kwa mwezi anakunja si chini ya milioni 16 Kwa kipindi hicho!
Kweli nikaona jamaa ana kiburi kwasababu vumba lipo,Kile kiwanja hakukipenda tukatafuta kingine tukaambiwa ni Tsh 100 milioni,hivyo jamaa akamwambia mama yake pesa anayomtumia kila mwezi hiyo $ 1000 iwe Niya matumizi,kuhusu kiwanja atatuma Hela Kwa mkupuo!
Wakati huo jamaa alikuwa ananimbia anaishi chumba kimoja tu chenye choo ndani na kabati la nguo na kisehemu Cha jiko analipa $ 2000 Kwa mwezi!
Siku za hivi karibuni mama yake amekuwa akilalamika jamaa hamtafuti na hata Hela ya kula tu inawapiga Chenga,hivyo anakuwa akiniambia ninapowasiliana naye nimkumbushe kuhusu hilo,lakini kila nikiongea na jamaa naye anakuwa mkali sana na kulalama kwamba hao ndugu zake wanadhani maisha ya huko ni mepesi kihivyo?,au wanadhani Hela anachota?
Kwa namna jamaa ambavyo huwa anaongea Kwa ukali,Mimi binafsi huwa naingia mfukoni mwangu nachukua pesa yangu nampelekea au namtumia mama yake na kumwambia imetoka Kwa jamaa lakini ukweli naujua Mimi namna jamaa anavyokuwaga mkali!
Kuna kipindi aliniambia Ile apartment aliyokuwa akikaa alihama na alihamia kijichumba kikubwa ambacho amekitenganisha kimekuwa chumba sebule ambacho analipa $ 4000 Kwa mwezi!,Nikamwambia kwanini asingeendelea tu kukaa pale pale kwenye Kodi ndogo Ili atimize malengo yake ila unajua unajua ndo zinakuwa nyingi!,nikamuuliza uenda kapata kazi mahali pengine palipo mlazimu yeye kuhama pale akasema kazi anafanya pale pale ila kaamua tu kubadiri makazi!
Kila nikimwambia ishu za maisha ya mama yake na ndugu zake jamaa anakuwa mkali kinoma na kuniambia ishu kibao ikiwemo Bills kitu ambacho kinafanya maisha kwake yasiwe rahisi na rafiki kuwatumia ndugu zake na mama yake pesa!
Swali ninalojiuliza,Je wakati amefika anaanza kazi na kila mwezi alipokuwa akimtumia mama yake pesa,Je hakuzijua hizo Bills?
Labda niwaulize swali ndugu zetu mnapokaa huko Marekani Kiranga na wengineo,Je ishu za Bills huko ni kubwa kiasi gani?
1.Je,ugumu wa bills upo kwenye Umeme?
2.Je ugumu wa Bills upo kwenye Maji?
3.Je Ugumu wa Bills upo kwenye Gesi?
4.Je Ugumu wa Bills upo kwenye Usafiri?
5.Je Ugumu wa bills upo kwenye Misosi?
6.Je Ugumu wa Bills upo kwenye Nyumba?
7.Je Ugumu wa Bills upo kwenye Internet?
Je,Bills ni kubwa sana kiasi kwamba msibaki na chochote kitu hata kusevu mnashindwa?,Kama ndivyo kwanini mnaendelea kuteseka huko?
Hebu nieleweaheni ndugu zangu Ugumu wa Maisha uko upo kwenye kitu gani?maana jamaa amekuwa akiwa mkali kama pilipili kila nikimgusia suala la kumtumia mama yake pesa,na kumbuka kila mwezi anapata zaidi ya $ 7000
Mmekuwa mkituambia kwamba huko kazi zipo za kutosha labda ushindwe wewe tu,Sasa kama kazi zipo za kutosha Ugumu wa Maisha unasababishwa na kitu gani?,Tumezoea kuona Watanzania wengi wanalia kuhusu Ugumu wa Maisha Kwasababu hakuna kazi zenye kipato kizuri,kama huko kazi zipo tena zenye kipato kizuri,Ugumu wa Maisha unasababishwa na kitu gani?
Kuna mshikaji wangu mmoja tulimaliza wote Sekondari na bahati nzuri hata chuo tukasoma wote,Mimi na yeye tulitokea Kuwa marafiki sana na hata hapo nyuma Kuna Uzi niliuweka hapa unaohusu maisha ya Ughaibuni nilimzungumzia!
Baada ya sote kumaliza chuo hatukuwa vizuri kiuchumi,hivyo tukaunganisha nguvu Kwa pesa kidogo tulizokuwa nazo tukaona tufanye biashara ya nafaka,Biashara mwanzo ilikuwa na changamoto ila tukakomaa hatimaye tukajipata,nyumbani kwao ilikuwa kama kwetu na kwetu kama kwao!
Mama yake amezoea kuniita pacha wa Mwanaye kwasababu tulikuwa hatuachani!
Kumbe jamaa alikuwa anafanya mipango ambayo alijua yeye alifanyaje fanyaje ghafla anakuja kuniambia amepata Visa ya Kwenda Marekani,so nikamuuliza Marekani anakwenda Kusoma au?,Akaniambia amepata mchongo wa kazi!
Nikamuuliza mbona imekuwa ghafla sana na hakunishirikisha kama rafiki yake?,ok hilo nikaachana nalo maana ilikuwa ni pasheni yake siku nyingi kutimkia huko maana hata wakati tunafanya biashara ndoto zake ilikuwa kutimkia huko!
Ila baada ya yeye kufika huko akaniambia Kuna wabongo wengi wanatimkia huko kupitia Kongo na Burundi,sijui kama ni kweli au alinidanganya maana hata yeye anasema alipewa mchongo na wabongo hivyo akalipa Hela akaenda hadi Burundi ndiko alikoondokea,Sina hakika lakini sikujali sana!
Nakumbuka kabla ya kuondoka siku tukiwa pale kwao,mama yake wakati anamuaga jamaa alikuwa akilia Kwa Uchungu sana na kimhakikishia mama yake kwamba anaenda kupambana na atahakikisha kila Mwezi atakuwa anamtumia Hela ili wajenge nyumba za kiwango Cha Kimataifa!,Binafsi nilimtia moyo nikamwambia asije kuwasahau ndugu zake na mama yake kwasababu amebakiwa na dada 3 na mama yake na yeye ndiye kijana mkubwa na wapekee!
Kweli jamaa aliondoka na baada ya kufika huko tukawa tunawasiliana hadi Leo na bahati nzuri haikuzidi miezi 3 jamaa akaniambia amepata makaratasi (Documents)ambazo pia zimempa kibali Cha kufanya kazi,alipoanza kazi kiukweli alikuwa akimtumia mama yake kila mwezi Dolla 1000 na akaniaomba niwasaidie kuwatafutia kiwanja maeneo ya Tegeta,nilifanikiwa kupata eneo ambalo lilikuwa likiuzwa pesa chafu ambako nikajua fika kwasababu jamaa anajitafuta hawezi kulimudu,nikamshauri nimtafutie eneo mahali pengine ambako ni nje ya mji na bei ambayo ataimudu,baada ya kumwambia jamaa akagoma akasema yeye anataka Tegeta,hivyo nikamwambia Kuna eneo hilo la mara ya kwanza bei yake ni Tsh 150 milioni,nikaona jamaa hashituki,duuuuu nikapatwa maswali sana uenda jamaa kweli kapata kazi ya maana,kwasababu alikuwa akiniambia mahali anapofanya kazi analipwa $ 30 Kwa Siku na anafanya kazi saa 8,hivyo nikapiga hesabu zangu Kwa haraka haraka nikagundua jamaa Kwa mwezi anakunja si chini ya milioni 16 Kwa kipindi hicho!
Kweli nikaona jamaa ana kiburi kwasababu vumba lipo,Kile kiwanja hakukipenda tukatafuta kingine tukaambiwa ni Tsh 100 milioni,hivyo jamaa akamwambia mama yake pesa anayomtumia kila mwezi hiyo $ 1000 iwe Niya matumizi,kuhusu kiwanja atatuma Hela Kwa mkupuo!
Wakati huo jamaa alikuwa ananimbia anaishi chumba kimoja tu chenye choo ndani na kabati la nguo na kisehemu Cha jiko analipa $ 2000 Kwa mwezi!
Siku za hivi karibuni mama yake amekuwa akilalamika jamaa hamtafuti na hata Hela ya kula tu inawapiga Chenga,hivyo anakuwa akiniambia ninapowasiliana naye nimkumbushe kuhusu hilo,lakini kila nikiongea na jamaa naye anakuwa mkali sana na kulalama kwamba hao ndugu zake wanadhani maisha ya huko ni mepesi kihivyo?,au wanadhani Hela anachota?
Kwa namna jamaa ambavyo huwa anaongea Kwa ukali,Mimi binafsi huwa naingia mfukoni mwangu nachukua pesa yangu nampelekea au namtumia mama yake na kumwambia imetoka Kwa jamaa lakini ukweli naujua Mimi namna jamaa anavyokuwaga mkali!
Kuna kipindi aliniambia Ile apartment aliyokuwa akikaa alihama na alihamia kijichumba kikubwa ambacho amekitenganisha kimekuwa chumba sebule ambacho analipa $ 4000 Kwa mwezi!,Nikamwambia kwanini asingeendelea tu kukaa pale pale kwenye Kodi ndogo Ili atimize malengo yake ila unajua unajua ndo zinakuwa nyingi!,nikamuuliza uenda kapata kazi mahali pengine palipo mlazimu yeye kuhama pale akasema kazi anafanya pale pale ila kaamua tu kubadiri makazi!
Kila nikimwambia ishu za maisha ya mama yake na ndugu zake jamaa anakuwa mkali kinoma na kuniambia ishu kibao ikiwemo Bills kitu ambacho kinafanya maisha kwake yasiwe rahisi na rafiki kuwatumia ndugu zake na mama yake pesa!
Swali ninalojiuliza,Je wakati amefika anaanza kazi na kila mwezi alipokuwa akimtumia mama yake pesa,Je hakuzijua hizo Bills?
Labda niwaulize swali ndugu zetu mnapokaa huko Marekani Kiranga na wengineo,Je ishu za Bills huko ni kubwa kiasi gani?
1.Je,ugumu wa bills upo kwenye Umeme?
2.Je ugumu wa Bills upo kwenye Maji?
3.Je Ugumu wa Bills upo kwenye Gesi?
4.Je Ugumu wa Bills upo kwenye Usafiri?
5.Je Ugumu wa bills upo kwenye Misosi?
6.Je Ugumu wa Bills upo kwenye Nyumba?
7.Je Ugumu wa Bills upo kwenye Internet?
Je,Bills ni kubwa sana kiasi kwamba msibaki na chochote kitu hata kusevu mnashindwa?,Kama ndivyo kwanini mnaendelea kuteseka huko?
Hebu nieleweaheni ndugu zangu Ugumu wa Maisha uko upo kwenye kitu gani?maana jamaa amekuwa akiwa mkali kama pilipili kila nikimgusia suala la kumtumia mama yake pesa,na kumbuka kila mwezi anapata zaidi ya $ 7000
Mmekuwa mkituambia kwamba huko kazi zipo za kutosha labda ushindwe wewe tu,Sasa kama kazi zipo za kutosha Ugumu wa Maisha unasababishwa na kitu gani?,Tumezoea kuona Watanzania wengi wanalia kuhusu Ugumu wa Maisha Kwasababu hakuna kazi zenye kipato kizuri,kama huko kazi zipo tena zenye kipato kizuri,Ugumu wa Maisha unasababishwa na kitu gani?