Uhafidhina, Deko na kujuana kwa wana CCM, kunamkwaza Rais Mwinyi Zanzibar

Uhafidhina, Deko na kujuana kwa wana CCM, kunamkwaza Rais Mwinyi Zanzibar

KISHADA

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2012
Posts
2,226
Reaction score
3,291
Hio ndio hali inayoendelea. Rais Mwinyi alikuja na nia njema kabisa akitaka kujitofautisha na watangulizi wake. Nia hio ilionekana mapema. Sasa watu wanajiuliza kulikoni ile spidi haionekani kuendana na alichomaanisha hadi sasa kunani?

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu mbali mbali vya tathmini, Rais Mwinyi anakutana na changamoto za kimya kimya kutokana na sababu mbali mbali.

Uhafidhina: Hakuna kipya chini ya uhafidhina Zanzibar. Waliopewa nafasi kwenye Serikali zilizopita wote ni CCM na waliomuweka au kuchangia Rais Mwinyi KUINGIA MADARAKANI NI HAO HAO. Ni kawaida Serikalini Zanzibar, Kusikia kwamba " muache, atatulia mwenyewe" Wanavyotaka wahafidhina unakuwa ndio msimamo wa chama hata kama unavunja sheria. Zanzibar imezoeleka Wahafidhina kuwa juu ya sheria na kuachwa. Hali hii imevikumba hata vyombo vya ulinzi kuwashughulikia wahalifu ambao hujiegemeza kwenye chama na kulindwa.

Nia njema ya Dkt Mwinyi inaishia kwenye matamko na utekelezaji ukishushwa chini kwenye kunasua sua tu. Huo ndio uhalisia.

Kujuana na Deko
Zanzibar kumezidi watu kuajiriwa na kupewa nafasi kwa kujuana. Hata Dkt Mwinyi Mwenyewe anajua hili na amewahi kulisemea. Kila unayemgusa ana mtu na analindwa kwa mwavuli wa undugu na uchama. Bahati mbaya CCM Zanzibar ilibeza uwezo na kutoajiri wenye sifa. Kuna nongwa na visasi kila mtu kumpendelea wake. Kichaka kikubwa ni chama. Ubadhirifu na wizi umeota mizizi kwenye awamu zote na kila aukijaribu kuchukua hatua unakwama.

Ziko wapi Ripoti za Uchunguzi za ubadhirifu za wizi na ajira hewa kwenye SMZ AMBAZO TILIAMBIWA KUMEUNDWA TUME?

Nani wamewajibibishwa kwa dhati kwa upotevu wa mamilioni ya miradi mifano ya ZUSP na Uwekaji Taa barabarani na Ununuzi wa Meli ya MV Mapinduzi II?

Hatua gani zimechukuliwa kuwajibishwa kwa wanaolalamikiwa kote mawizarani, Maashirikani, Halmashauri na manispaa?
Hatua gani zimechukuliwa kwa wanaotajwa kwenye Ile Show ya ONGEA NA RAIS MWINYI? tunazo taarifa malamiko ni mengi mno lkn hatuoni hatua?

KUPWAYA KWA WASAIDIZI WAKE
Hiki nacho kinaonekana kwa UWAZI. Spidi imeyayuka hata kwa mawaziri walioanza kujizolea umaarufu. Wamepotea na mambo ni yale yale. Mzigo wa kuwabeba makada walioharibu na kuwawajibisha ni mzito kwa Dkt Mwinyi maana unawahusu CCM.

Katika hali hio, hakuna mpya maana tatizo linajulikana. Huu ni mzigo wa Chama. Chama kimebeba makondokando na kiko tayari kuyalinda.

Uchambuzi unaonesha Kuondoka kwa JPM na Maalim Seif vile vile kumerudisha nyuma jitihada. Nini kitegemewe?

Jee Rais Mwinyi ataweza ? hilo ndio Suali lililopo. Utamaduni wa kulindana, kupeana vyeo na nongwa ni mgumu mno.

Zanzibar kuna shida iliyolelewa kwa muda mrefu na hadi sasa hakuna tiba kutokana na ushindani wa kisiasa na upinzani wenye nguvu kiasi kwamba huo ndio uchochoro wa kupiga kwa sababu unakuwa na uhakika wa kulindwa.

Tunakaribisha mjadala kwa aliye na la kusema.

Kishada.
 
Jana kwenye taarifa ya habari UTV (Azam) nimemwona Mh. Rais ametembelea shamba la serikali amekutana na changamoto na kero za kutosha, akamuuliza Mkurugenzi wa shamba mwaka jana 2019 mmekusanya mapato kiasi gani jumla, mkurugenzi akamwambia Mheshimiwa kwa kweli sifahamu mimi nilikuwa likizo ndio nimerudi, anajichekesha wala hana wasiwasi, Rais naye anamcheki tu, nikajiuliza hivi Mkurugenzi mzima unashindwa kujua hata kwa range tu mmekusanya kiasi gani, nikahisi Rais atamwambia wewe hufai ktk hiyo nafasi lakini wala maisha yakaendelea. Mtoa mada usimacho naona kina ukweli kwa asilimia kubwa tu.
 
Kati ya Rais na Kisiwandui, hapa Zanzibar Kisiwandui ndio ina nguvu. Kasi imepotea, wa Kisiwandui wameshasema "atatulia mwenyewe" na tayari ameshatulia. Ukipewa ushindi na Kisiwandui, basi utatii tu watakavyo kisiwandui. Ndio maana huwa nasema CCM hata akae nani, ndo yale yale!
 
Kwa kifupi usultani umehamia CCM toka kwa ukoo ukoo wa Sultan Jamshid.

Kila aliyenasibishwa na uhusika wa Baraza la Mapinduzi kupindua serikali ya Sultan Jamshid sasa ndiyo wao wanamapinduzi , watoto wao ,vijukuu na vitukuu ndiyo wanapewa vyeo, teuzi, scholarships za masomo Tanganyika au nje ya nchi n.k n.k
 
Kuna shida jamani.

Rais Mwinyi alijitahidi kuziba miaNYA. ALIZUIA UAJIRI MPYA NA KUHAKIKI. Ripoti kimya na hawajawajibishwa watu. Fedha zilipigwa mno kwenye mishahara hewa hasa vinavyoitwa VIKOSi. Mlolongo ni mrefu.

Wateule wa zamani wa Dkt Shein hawajaguswa na hawagusiki.

Kuna uchafu kwenye taasisi nyingi. Viongozi wana skendo nyingi hawagusiki yalikuwa mapendekezo ya Chama.

Chama kinamfunga miguu na Mikono.
 
Kati ya Rais na Kisiwandui, hapa Zanzibar Kisiwandui ndio ina nguvu. Kasi imepotea, wa Kisiwandui wameshasema "atatulia mwenyewe" na tayari ameshatulia. Ukipewa ushindi na Kisiwandui, basi utatii tu watakavyo kisiwandui. Ndio maana huwa nasema CCM hata akae nani, ndo yale yale!
Mwinyi, alikuwa anatembelea gia ya Magufuri,na sio Mwinyi tu hata mawaziri wengi wamepotea, Sasahivi mambo yameanza kurudi kawaida,hata maofisini nyodo zimerudi kila saa wako kwenye vikao,Wakina Mwinyi wote ulikuwa moto wa mabua tu.
 
Jana kwenye taarifa ya habari UTV (Azam) nimemwona Mh. Rais ametembelea shamba la serikali amekutana na changamoto na kero za kutosha, akamuuliza Mkurugenzi wa shamba mwaka jana 2019 mmekusanya mapato kiasi gani jumla, mkurugenzi akamwambia Mheshimiwa kwa kweli sifahamu mimi nilikuwa likizo ndio nimerudi, anajichekesha wala hana wasiwasi, Rais naye anamcheki tu, nikajiuliza hivi Mkurugenzi mzima unashindwa kujua hata kwa range tu mmekusanya kiasi gani, nikahisi Rais atamwambia wewe hufai ktk hiyo nafasi lakini wala maisha yakaendelea. Mtoa mada usimacho naona kina ukweli kwa asilimia kubwa tu.

Hivi ulitegemea rais aliyeingia madarakani kwa wizi wa kura na umwagaji damu awe na nguvu zipi za kuhoji, na hata kuchukua hatua? Uzuri ni kuwa rais, pamoja na anaowahoji wanajua kabisa kaingia madarakani kwa mbeleko. Akiwachukulia hatua, uchaguzi unaofuata hawezi kushinda huo urais bila mbeleko.
 
Hili linchi alikuwa analiweza mwenda zake tu.
Watanzania tuna utamaduni mbovu sana kwenye swala la uwajibikaji.

Dhalimu alikuwa anaweza nini, yeye mwenyewe alikuwa ni muendesha miradi ya hasara. Alichofanikiwa ni kudhibiti vyombo vya habari na kutangazwa kwa propaganda alizozitaka yeye.
 
Hio ndio hali inayoendelea. Rais Mwinyi alikuja na nia njema kabisa akitaka kujitofautisha na watangulizi wake. Nia hio ilionekana mapema. Sasa watu wanajiuliza kulikoni ile spidi haionekani kuendana na alichomaanisha hadi sasa kunani?

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu mbali mbali vya tathmini, Rais Mwinyi anakutana na changamoto za kimya kimya kutokana na sababu mbali mbali.

Uhafidhina: Hakuna kipya chini ya uhafidhina Zanzibar. Waliopewa nafasi kwenye Serikali zilizopita wote ni CCM na waliomuweka au kuchangia Rais Mwinyi KUINGIA MADARAKANI NI HAO HAO. Ni kawaida Serikalini Zanzibar, Kusikia kwamba " muache, atatulia mwenyewe" Wanavyotaka wahafidhina unakuwa ndio msimamo wa chama hata kama unavunja sheria. Zanzibar imezoeleka Wahafidhina kuwa juu ya sheria na kuachwa. Hali hii imevikumba hata vyombo vya ulinzi kuwashughulikia wahalifu ambao hujiegemeza kwenye chama na kulindwa.

Nia njema ya Dkt Mwinyi inaishia kwenye matamko na utekelezaji ukishushwa chini kwenye kunasua sua tu. Huo ndio uhalisia.

Kujuana na Deko
Zanzibar kumezidi watu kuajiriwa na kupewa nafasi kwa kujuana. Hata Dkt Mwinyi Mwenyewe anajua hili na amewahi kulisemea. Kila unayemgusa ana mtu na analindwa kwa mwavuli wa undugu na uchama. Bahati mbaya CCM Zanzibar ilibeza uwezo na kutoajiri wenye sifa. Kuna nongwa na visasi kila mtu kumpendelea wake. Kichaka kikubwa ni chama. Ubadhirifu na wizi umeota mizizi kwenye awamu zote na kila aukijaribu kuchukua hatua unakwama.

Ziko wapi Ripoti za Uchunguzi za ubadhirifu za wizi na ajira hewa kwenye SMZ AMBAZO TILIAMBIWA KUMEUNDWA TUME?

Nani wamewajibibishwa kwa dhati kwa upotevu wa mamilioni ya miradi mifano ya ZUSP na Uwekaji Taa barabarani na Ununuzi wa Meli ya MV Mapinduzi II?

Hatua gani zimechukuliwa kuwajibishwa kwa wanaolalamikiwa kote mawizarani, Maashirikani, Halmashauri na manispaa?
Hatua gani zimechukuliwa kwa wanaotajwa kwenye Ile Show ya ONGEA NA RAIS MWINYI? tunazo taarifa malamiko ni mengi mno lkn hatuoni hatua?

KUPWAYA KWA WASAIDIZI WAKE
Hiki nacho kinaonekana kwa UWAZI. Spidi imeyayuka hata kwa mawaziri walioanza kujizolea umaarufu. Wamepotea na mambo ni yale yale. Mzigo wa kuwabeba makada walioharibu na kuwawajibisha ni mzito kwa Dkt Mwinyi maana unawahusu CCM.

Katika hali hio, hakuna mpya maana tatizo linajulikana. Huu ni mzigo wa Chama. Chama kimebeba makondokando na kiko tayari kuyalinda.

Uchambuzi unaonesha Kuondoka kwa JPM na Maalim Seif vile vile kumerudisha nyuma jitihada. Nini kitegemewe?

Jee Rais Mwinyi ataweza ? hilo ndio Suali lililopo. Utamaduni wa kulindana, kupeana vyeo na nongwa ni mgumu mno.

Zanzibar kuna shida iliyolelewa kwa muda mrefu na hadi sasa hakuna tiba kutokana na ushindani wa kisiasa na upinzani wenye nguvu kiasi kwamba huo ndio uchochoro wa kupiga kwa sababu unakuwa na uhakika wa kulindwa.

Tunakaribisha mjadala kwa aliye na la kusema.

Kishada.
Mwinyi hana anachoweza kuwafanya yeye mwenyewe ameingia kwa Mbeleko ya hao wahafidhina. Amekwenda na atawaacha
 
Hivi ulitegemea rais aliyeingia madarakani kwa wizi wa kura na umwagaji damu awe na nguvu zipi za kuhoji, na hata kuchukua hatua? Uzuri ni kuwa rais, pamoja na anaowahoji wanajua kabisa kaingia madarakani kwa mbeleko. Akiwachukulia hatua, uchaguzi unaofuata hawezi kushinda huo urais bila mbeleko.
Ktk Rais ambaye hana confidence na kiti chake ni Mwinyi. Maana hata watumushi chini yake wanajua Abcd za namna alivyo upata. Hana ubavu hata kidogo wa kuwayumbisha
 
Huyu ni Dr wa binadamu aachie avae gwanda zakazi muhimbili pale kazi iendelee
 
Back
Top Bottom