Uhafidhina, Deko na kujuana kwa wana CCM, kunamkwaza Rais Mwinyi Zanzibar

Uhafidhina, Deko na kujuana kwa wana CCM, kunamkwaza Rais Mwinyi Zanzibar

Kuondoka kwa JPM na Maalim Seif -------hii ndio sababu nyingine KUBWA
 
Nchi ngumu ile, hapo bado hujazungumzia udini...
 
Mimi Mtanganyika ya Visiwani hayanihusu.
 
Ktk Rais ambaye hana confidence na kiti chake ni Mwinyi. Maana hata watumushi chini yake wanajua Abcd za namna alivyo upata. Hana ubavu hata kidogo wa kuwayumbisha
Exactly, tena ukizingatia wanamchukulia kama ni mbara aliyepandikizwa ndio kabisa.
 
Hivi ulitegemea rais aliyeingia madarakani kwa wizi wa kura na umwagaji damu awe na nguvu zipi za kuhoji, na hata kuchukua hatua? Uzuri ni kuwa rais, pamoja na anaowahoji wanajua kabisa kaingia madarakani kwa mbeleko. Akiwachukulia hatua, uchaguzi unaofuata hawezi kushinda huo urais bila mbeleko.
Sikubaliani na wazo lako
Kwa Afrika Rais anaweza kukuteua umtangaze ku2a Rais ukimaliza unanyea debe gerezani maana hata ukipeleka kesi zako atamteua wa kuzibatilisha.

Tatizo la nchi za kiafrika ni Wizi kwa VIONGOZI wanaingia wakiwa na nia KUPIGA zamu zao, ni mwendonwa KUMEKI.

Jingine ni kukosa UTHUBUTU na UJASIRI bora uwe Mwizi wewe Rais peke yako na kuwathibiti wengine. Wengi wanaona maisha yao , familia na jamaa zao yatakuwa HATARINI hivyo kuamua kujisalimisha na kutumikia KIKUNDI fulani kujitoa mhanga ni jambo ADIMU.

Usaliti wa KIAFRIKA . Waafrika tunatumika na mataifa kutugawa , na miongoni mwetu wapo Agent wako tayari watoe ramani ilimradi tu watahakikishiwa usalama wa maisha yao huko nje au ndani, ukijitoa Mhanga UTANG'OLEWA fasta , utatawala au kuongoza kwa vurugu wanaharakati Uchwara miingoni mwetu wataibuka, hakuna asiye na makosa watayatumia kukumaliza kabisa

Wengi inabidi wanyweee
 
Sikubaliani na wazo lako
Kwa Afrika Rais anaweza kukuteua umtangaze ku2a Rais ukimaliza unanyea debe gerezani maana hata ukipeleka kesi zako atamteua wa kuzibatilisha.

Tatizo la nchi za kiafrika ni Wizi kwa VIONGOZI wanaingia wakiwa na nia KUPIGA zamu zao, ni mwendonwa KUMEKI.

Jingine ni kukosa UTHUBUTU na UJASIRI bora uwe Mwizi wewe Rais peke yako na kuwathibiti wengine. Wengi wanaona maisha yao , familia na jamaa zao yatakuwa HATARINI hivyo kuamua kujisalimisha na kutumikia KIKUNDI fulani kujitoa mhanga ni jambo ADIMU.

Usaliti wa KIAFRIKA . Waafrika tunatumika na mataifa kutugawa , na miongoni mwetu wapo Agent wako tayari watoe ramani ilimradi tu watahakikishiwa usalama wa maisha yao huko nje au ndani, ukijitoa Mhanga UTANG'OLEWA fasta , utatawala au kuongoza kwa vurugu wanaharakati Uchwara miingoni mwetu wataibuka, hakuna asiye na makosa watayatumia kukumaliza kabisa

Wengi inabidi wanyweee
Specific Kwa Zanzibar. Hali ni tofauti na maelezo mengine. Kule chama kinatumika kama kichaka.

Mifumo yote imedhibitiwa kichama na si uweledi. System yote imejazwa makada ambao hata kama Rais ana nia njema wanamuhujumu kimtindo.

Kwanza siri zinavuja na kujadiliwa vijiweni Kwa CCM. Mila mtu ni mwanamapinduzi.

Wizi na kulindana Tu.
 
Mwinyi, alikuwa anatembelea gia ya Magufuri,na sio Mwinyi tu hata mawaziri wengi wamepotea, Sasahivi mambo yameanza kurudi kawaida,hata maofisini nyodo zimerudi kila saa wako kwenye vikao,Wakina Mwinyi wote ulikuwa moto wa mabua tu.
Magufuli huyu jambazi ama
 
Veting system Haifai. Ukitaka kuleta mabadiliko Zanzibar inabidi uanzie mbali.

Kila kitu kimefujwa Kwa zaidi ya miongo minne sasa, Kama miaka 35 hivi na kuja Kwa vyama vingi.

Zanzibar imeathiriwa na siasa mno.

Wataalamu wengi walifukuzwa makazini, hakukuwa na succession plan. Wat u wakapachikwa kisiasa na kujazwa makazini hapo ndipo tatizo lilipoanzia.

Kuanzia hapo kilichoendelea ni majanga hadi Leo. Akili za wakubwa ni kuingia ikulu Kwa njia yoyote ile.
Sass kulipana fadhila ndio inakuwa mpango mzima.

Its a long story. Itoshe kusema Dr Mwinyi anakwazwa na mila za CCM za kudekezana, uhafidhina na kupendeleana Zanzibar
 
Kwa tathmini ya haraka inaonesha kuwa Rais Hussein Mwinyi hakuwa amejiandaa kuwa Rais wa Zanzibar,hakuwa na ajenda juu ya nini anakusudia kukifanya katika kuiongoza Zanzibar zaidi ya kutegemea mbeleko ya Rais magufuli, kutoijua kwake Zanzibar na watu wake kwa kiasi kikubwa kunamfanya kuonekana kiongozi mgeni asiejua mfumo na miiko ya uongozi wa Zanzibar ni kweli kwa sasa amepwaya sana na amepoteza ile haiba alioanza nayo siku za awali za uongozi wake,miongoni mwa mambo yanayotajwa kumfelisha ni kusikiliza ushauri wa kikundi cha watu kinachojinasibisha na siasa za Jimbo lake la kwahani,watu hao hawana uwezo wa uongozi wala uzoefu katika kusimamia masuala ya uendeshaji wa nchi, kwa hiyo ukiondoa sababu zilizoelezwa na mleta mada zipo sababu hizi ambazo zinamkwaza dr Mwinyi na matokeo yake anaweza kumaliza muhula wake huku kukiwa hakuna hatua kubwa ya maendeleo iliyopigwa huko Zanzibar.
 
Kuna shida jamani.

Rais Mwinyi alijitahidi kuziba miaNYA. ALIZUIA UAJIRI MPYA NA KUHAKIKI. Ripoti kimya na hawajawajibishwa watu. Fedha zilipigwa mno kwenye mishahara hewa hasa vinavyoitwa VIKOSi. Mlolongo ni mrefu.

Wateule wa zamani wa Dkt Shein hawajaguswa na hawagusiki.

Kuna uchafu kwenye taasisi nyingi. Viongozi wana skendo nyingi hawagusiki yalikuwa mapendekezo ya Chama.

Chama kinamfunga miguu na Mikono.
Unaposema chama kinamfunga miguu sikubaliani nawe kwani kuna maamuzi ya uendeshaji Serikali hayahitaji vikao vya chama, tatizo ninaloliona Urais wa Dr Mwinyi umezongwa na washauri wengi kila mmoja anamvuta rais katika muongozo wake matokeo yake anapoteza dira na kutojua jambo la kufanya, mfano suala la uteuzi wa watendaji hili halihitaji vikao vya chama, suala la kuwajibisha viongozi wazembe hili halihitaji vikao vya chama haya ni mambo yalio ndani ya mamlaka ya Rais
 
Hivi ulitegemea rais aliyeingia madarakani kwa wizi wa kura na umwagaji damu awe na nguvu zipi za kuhoji, na hata kuchukua hatua? Uzuri ni kuwa rais, pamoja na anaowahoji wanajua kabisa kaingia madarakani kwa mbeleko. Akiwachukulia hatua, uchaguzi unaofuata hawezi kushinda huo urais bila mbeleko.
Unawajua CCM au unawasikia wewe? Wako tayari kuendele akumhujumu rais wao kuliko kuitoa Sirikali kwa upinzani 😀

Huyu utawala wake utajaa changamoto mpaka akiamua "kutulia"
 
Kwa hiyo anajitutumua tu.mwisho wa miaka 5 hii utamuona kashazeeka mamvi tele .muulize obama uraisi sio lele mama kuna vitu vingi vipi nyuma ya pazia.
Amewatumbua wale wahasibu 80 waliofukuzwa kazi kwa kuchezea mifumo ya makusanyo.sasa hapo angetaka aendelee angejaza wahasibu kutoka bara huku na wale wazembe awahamishie mikoani ya mbali huku bara kama vile ngara.kiteto.mwanga nk watanyooka tu .lkn kwa kiongea sana wa zenji wanamsikiliza halafu hawatekelezi.mchana wenda kula urojo ndio imetoka hiyo hawarudi tena kazini.
 
Unaposema chama kinamfunga miguu sikubaliani nawe kwani kuna maamuzi ya uendeshaji Serikali hayahitaji vikao vya chama, tatizo ninaloliona Urais wa Dr Mwinyi umezongwa na washauri wengi kila mmoja anamvuta rais katika muongozo wake matokeo yake anapoteza dira na kutojua jambo la kufanya, mfano suala la uteuzi wa watendaji hili halihitaji vikao vya chama, suala la kuwajibisha viongozi wazembe hili halihitaji vikao vya chama haya ni mambo yalio ndani ya mamlaka ya Rais
Mkuu chama ni mwenendo, imani, utashi na utamaduni.

CCM Zanzibar ina huo mwenendo na utamaduni Wa kuleana.

Kila mmoja anamuogopa Mwenzake na kuhofu makundi. Chama kinashindwa kumpa full sapoti ya kushughulikia walaji na wazembe ma a na wote ni CCM. Wapo hapo Kwa mgongo Wa chama na kujuana Ki familia.

Ukimgusa mtu umegusa maslahi ya chama na Mapinduzi.

Huo ndio mkwazo wenyewe na hio ndio CCM ilivyo Zanzibar.
 
Tatizo la Zanzibar ni CCM, Zanzibar hakuwezi kutokea mabadiliko as long as CCM ndio inaongoza. Mwinyi hawezi fanya chochote kwa kupitia CCM.
 
Magufuli huyu jambazi ama
Jambazi alikuwa Baba yako,muuza unga, ndio maana alikuwa na chuki na Magufuri, kwenye uko wenu wote mpaka mwisho wa dunia unafika, akuna mtu atakeyefikia cheo cha Magufuri,Jaribu kueshimu watu hata kama umpendi,wewe mbwa.
 
Hio ndio hali inayoendelea. Rais Mwinyi alikuja na nia njema kabisa akitaka kujitofautisha na watangulizi wake. Nia hio ilionekana mapema. Sasa watu wanajiuliza kulikoni ile spidi haionekani kuendana na alichomaanisha hadi sasa kunani?

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu mbali mbali vya tathmini, Rais Mwinyi anakutana na changamoto za kimya kimya kutokana na sababu mbali mbali.

Uhafidhina: Hakuna kipya chini ya uhafidhina Zanzibar. Waliopewa nafasi kwenye Serikali zilizopita wote ni CCM na waliomuweka au kuchangia Rais Mwinyi KUINGIA MADARAKANI NI HAO HAO. Ni kawaida Serikalini Zanzibar, Kusikia kwamba " muache, atatulia mwenyewe" Wanavyotaka wahafidhina unakuwa ndio msimamo wa chama hata kama unavunja sheria. Zanzibar imezoeleka Wahafidhina kuwa juu ya sheria na kuachwa. Hali hii imevikumba hata vyombo vya ulinzi kuwashughulikia wahalifu ambao hujiegemeza kwenye chama na kulindwa.

Nia njema ya Dkt Mwinyi inaishia kwenye matamko na utekelezaji ukishushwa chini kwenye kunasua sua tu. Huo ndio uhalisia.

Kujuana na Deko
Zanzibar kumezidi watu kuajiriwa na kupewa nafasi kwa kujuana. Hata Dkt Mwinyi Mwenyewe anajua hili na amewahi kulisemea. Kila unayemgusa ana mtu na analindwa kwa mwavuli wa undugu na uchama. Bahati mbaya CCM Zanzibar ilibeza uwezo na kutoajiri wenye sifa. Kuna nongwa na visasi kila mtu kumpendelea wake. Kichaka kikubwa ni chama. Ubadhirifu na wizi umeota mizizi kwenye awamu zote na kila aukijaribu kuchukua hatua unakwama.

Ziko wapi Ripoti za Uchunguzi za ubadhirifu za wizi na ajira hewa kwenye SMZ AMBAZO TILIAMBIWA KUMEUNDWA TUME?

Nani wamewajibibishwa kwa dhati kwa upotevu wa mamilioni ya miradi mifano ya ZUSP na Uwekaji Taa barabarani na Ununuzi wa Meli ya MV Mapinduzi II?

Hatua gani zimechukuliwa kuwajibishwa kwa wanaolalamikiwa kote mawizarani, Maashirikani, Halmashauri na manispaa?
Hatua gani zimechukuliwa kwa wanaotajwa kwenye Ile Show ya ONGEA NA RAIS MWINYI? tunazo taarifa malamiko ni mengi mno lkn hatuoni hatua?

KUPWAYA KWA WASAIDIZI WAKE
Hiki nacho kinaonekana kwa UWAZI. Spidi imeyayuka hata kwa mawaziri walioanza kujizolea umaarufu. Wamepotea na mambo ni yale yale. Mzigo wa kuwabeba makada walioharibu na kuwawajibisha ni mzito kwa Dkt Mwinyi maana unawahusu CCM.

Katika hali hio, hakuna mpya maana tatizo linajulikana. Huu ni mzigo wa Chama. Chama kimebeba makondokando na kiko tayari kuyalinda.

Uchambuzi unaonesha Kuondoka kwa JPM na Maalim Seif vile vile kumerudisha nyuma jitihada. Nini kitegemewe?

Jee Rais Mwinyi ataweza ? hilo ndio Suali lililopo. Utamaduni wa kulindana, kupeana vyeo na nongwa ni mgumu mno.

Zanzibar kuna shida iliyolelewa kwa muda mrefu na hadi sasa hakuna tiba kutokana na ushindani wa kisiasa na upinzani wenye nguvu kiasi kwamba huo ndio uchochoro wa kupiga kwa sababu unakuwa na uhakika wa kulindwa.

Tunakaribisha mjadala kwa aliye na la kusema.

Kishada.
Ya Zanzibar hayatuhusu, kwenye matatizo yenu mnataka tujadili lakini kwenye kula keki yenu hamtaki kutushirikisha
 
Back
Top Bottom