Mama...
Fikra zangu si za kidini.
Huu ni uchambuzi ambao mtu yeyote huru anaweza kuwa nao.
Hivi ni vibaya kuuliza kwa nini Bunge na Serikali imehodhiwa na watu wa imani moja?
Au ni vibaya kuuliza mbona historia ya kweli ya uhuru ilifutwa hatuwasomi wazalendo waliopigania uhuru?
Sijui kama hizi ni harakati wala sijui unaposema ningekuwa mbali unakusudia nini.
Unakusudia hapa Tanzania kwetu niko nyuma?
Labda nikufahamishe.
Hapa JF nimepokea Certificate of Appreciation kwa uandishi wangu.
Waislam wa Tanzania wamenipa nishani mara mbili pia kwa uandishi wangu na kwa kusahihisha historia ya uhuru.
Naamini unakijua kitabu changu: "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968)The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika," (London 1998).
Hivi karibuni hapa JF walikuwa wanapiga kura kuchagua mwandishi bora kwq kila jukwaa.
Wapiga kura 14 kwa mfululizo walinichagua mimi.
Baada ya hivyo ikasimamishwa na wapiga kura walikuwa wakisema sina mshindani.
Huenda hufahamu ni vipi mimi nimejua sana historia hii kuwapita watu wengi.
Babu zangu ndiyo walianzisha harakati hizi za kudai uhuru 1929 na najua historia yao.
Si kwa kuisoma vitabuni bali kwa kuwa harakati hizi zilikuwa ndani ya familia na ndani ya nyumba zetu.