Uhakiki wa Wanachama Chama Kipya Cha Siasa 1993

Uhakiki wa Wanachama Chama Kipya Cha Siasa 1993

Mama...
Fikra zangu si za kidini.

Huu ni uchambuzi ambao mtu yeyote huru anaweza kuwa nao.

Hivi ni vibaya kuuliza kwa nini Bunge na Serikali imehodhiwa na watu wa imani moja?

Au ni vibaya kuuliza mbona historia ya kweli ya uhuru ilifutwa hatuwasomi wazalendo waliopigania uhuru?

Sijui kama hizi ni harakati wala sijui unaposema ningekuwa mbali unakusudia nini.

Unakusudia hapa Tanzania kwetu niko nyuma?

Labda nikufahamishe.

Hapa JF nimepokea Certificate of Appreciation kwa uandishi wangu.

Waislam wa Tanzania wamenipa nishani mara mbili pia kwa uandishi wangu na kwa kusahihisha historia ya uhuru.

Naamini unakijua kitabu changu: "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968)The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika," (London 1998).

Hivi karibuni hapa JF walikuwa wanapiga kura kuchagua mwandishi bora kwq kila jukwaa.

Wapiga kura 14 kwa mfululizo walinichagua mimi.

Baada ya hivyo ikasimamishwa na wapiga kura walikuwa wakisema sina mshindani.

Huenda hufahamu ni vipi mimi nimejua sana historia hii kuwapita watu wengi.

Babu zangu ndiyo walianzisha harakati hizi za kudai uhuru 1929 na najua historia yao.

Si kwa kuisoma vitabuni bali kwa kuwa harakati hizi zilikuwa ndani ya familia na ndani ya nyumba zetu.
Utalalamika sana ila ndo ishatokea babu zako kufutwa kwenye historia. Waasisi walijua udini mlio nao ndo maana historia inaanza na kuishia kwa Nyerere na Karume tu.
 
Utalalamika sana ila ndo ishatokea babu zako kufutwa kwenye historia. Waasisi walijua udini mlio nao ndo maana historia inaanza na kuishia kwa Nyerere na Karume tu.
Mama...
Hapana mimi si mlalamishi wala si mdini.

Ningekuwa hivyo tayari hapa tushagombana.

Mimi hueleza fikra zangu kwa nia ya kuelimishana.

Historia ilifutwa lakini tumeirejesha na haitopotea kamwe.

Hapa JF nimesomesha wengi.
Kwenye group nina wanafunzi wengi sana.

Nimetiwa kwenye miradi mingi ya kuandika historia na vitabu vyangu vimechapwa na vinasomwa.

Nimeshirikishwa katika uandishi wa kitabu cha historia ya Zanzibar (2010).

Nimeshirikishwa pia katika kuandika maisha ya Mwalimu Nyerere (2020).

1678335107325.jpeg

Mohamed Omari Mkwawa akiwa ameshika kitabu alichosaidia utafiti wake kwa kutoa taarifa ambazo kabla zilikuwa siri kubwa kuhusu kambi ya Kipumbwi iliyotoa Wamakonde walioshiriki katika mapinduzi ya Zanzibar 2010.

1678335455094.jpeg

Jopo la Prof. Shivji waandishi wa Nyerere Biography wakinihoji kuhusu maisha ya Julius Nyerere 2013
Yaliyokuwa hayafahamiki leo yako hadharani na ni sehemu ya historia ya Tanzania.

1678338864080.jpeg

Mtangazaji wa TBC1 akinihoji kuhusu kitabu cha maisha ya Mwalimu Julius Nyerere​
 
Back
Top Bottom