Uhamiaji Arusha kuambiwa na Makonda watoe pasipoti kwa siku saba: Tuna tatizo la siasa nchi hii…

Passport inachukua muda gani mpaka kuipata mimi sina uzoefu!

Pasiport hata siku moja inawezekana tu wee tu ndo huelewi
Mfano ukienda lita kule wanakwambia kupata cheti cha kuzaliwa kuanzia siku 14na kuendelea. Lakini kam huna mkono wa birika siku tatu hadi Tano utapata cheti na kama unaharaka sama siku tati tu wemaliza kazi
 
Mnapenda kuteseka sana sana..Mimi nilipata passport yangu ndani ya siku nne na wala si Arusha!
Watanzania huwa mnataka nini? Wewe kwani ni uhamiaji mpaka ubishe? Inashindikana nini passport kutolewa ndani ya siku saba kama mtu ana kila kitu? Hivi unajua kinachochelewesha passport?
Mtu anawasidia mnaanza kulalamika tena hahahhaha
 
Lita ni wapi?
 
Taarifa zako unajaza Online Uhamiaji wanazi link na mifumo mingine.bkuna watu wanapata chini ya siku 2 kama mkoani kwako wame verify taarifa zako unataka tena ukae mwaka. Siku 7 zinatosha. Kama unaona chache kaa hata mwezi uende kuchukua shida iko wapi. Watu tunapenda taabu
 
Makonda anakitu sema chuki uliyonayo kwa makonda hata akiongea kitu gani huwezi kumuelewa.
Makonda hakuna kitu, tunashangazwa na hao wanaomteua kila kukicha. Hana mikakati yoyote yenye kuleta tija, zaidi ya kiki za kitoto.
 
Mimi mwaka jana passport nilipata siku nne baada ya kusubmit docs zangu, ilikuwa Morogoro mjini.
 
Kama Ukiwa na pesa nzuri, Passport Dar unaipata siku hiyo hiyo....!

Kama ukatoa pesa kidogo ila sio ndefu, Passport Dar unaipata kwa siku 3....! Hata kama zinakua printed Dar es salaam, inawezekana kuipata passport Arusha baada ya siku 7.
 
Labda katumwa na mama usishangae kesho akiwa waziri wa mambo ya ndani uhamiaji zote zinakua chini yake na passport tunapata kwa siku mbili!
Utashangaa kapangiwa ukuu wa Wilaya Gairo huko kutoka RC mpaka DC, shukhrani kwa Mama anaupiga mwingi
 
uzuri makonda anaujua huo mkoa nje ndani

wanaarusha kaeni mkao wa kula
 
Ndio maana nimesema sina uzoefu lakini haya maujanja ulionipa wallah iddi ikimalizika naenda kukamata kinyago!
 
Kwenye watu 10 wasiomkubal P C Makonda ni wawili tu, kwhyo idadi ya wanaomchukia ni ndogo sana fanyeni jambo waongezeke mkuu
 
Muachen Makonda afanye kazi yke ng'ombe nyie ,wenyewe hapo hamna hata ubalozi wa nyumba 1 na mnajikuta miambaa.

Mkiona hamumuelewi wekeni Mama zenu wakawe wakuu wa mkoa huo.
 
makonda hana shida ila kuna watu wanakinyongo nae sana ingekuwa vzuri zaidi hata paspot zitolewe hata baada ya siku mbili mambo yaende chapu chapu ila kwa kufata utaratibu...mtoa maada kwani dar ndo nn hicho kitu inatakiwa kinamalizika mkoani
MiTanzania mingne jau sana mzee, yan hayaeleweki yanataka nn akipatkana kiongoz wakuyasemea yanamuona mnyanyasaji haya wakipata zuzu bdo watayasema
 
Muachen Makonda afanye kazi yke ng'ombe nyie ,wenyewe hapo hamna hata ubalozi wa nyumba 1 na mnajikuta miambaa.

Mkiona hamumuelewi wekeni Mama zenu wakawe wakuu wa mkoa huo.
Ndugu yangu tuweke itikadi pembeni; zipo huduma siyo za kufanyia siasa. Tukiforce bila utafiti utakaribisha banyamulenge tuanze kuishi kwa mitutu ya bunduki humu.

Lakini pia nimesema ukitaka kupata ushahidi ; Mhe. Makonda alipokwenda Tunduma akiwa Katibu wa Uenezi alitamka kwamba pasipoti zitolewe bure kwa Madereva.

Niliweka uzi hapa nikasema haitekelezeki na hakuna Rais anaweza kutoa huduma kwa upendeleo ; leo hii ni Dreva gani anapewa pasipoti bure?

Mwisho, pasipoti siyo kitambulisho ni utaifa lazima tunapoitoa tuonyeshe tunaipa ulinzi mkubwa. Tukiweka siasa tunapewa lakini huko Duniani tutazuiwa kuingia kwa sababu itashuka thamani.

Duniani kote pasipoti ni silaha kubwa sana, leo hii mzungu akipoteza pasipoti anaacha shughuli zote anakwenda kuomba ubalozini ifutwe na apewe nyingine.

Hivyo tunapojadili pasipoti tunajadili Utanzania wetu nje ya mipaka ya nchi. Wao kama serikali wazungumze ndani lakini siyo jambo la kuzungumza kwenye majukwaa ya siasa litatuzibia riziki wengine tunaosafiri.

Kutoa pasipoti hata siku moja is not a big deal kwa sababu hata leo ukiwa na emergency wanatoa; ila kusema kila anayewakilisha maombi apewe NO
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…