SN.BARRY
JF-Expert Member
- Oct 12, 2012
- 4,038
- 8,929
1. Kazi yenu ni kutoa passport sio kujua mtu anaenda wapi. Passport ni haki ya kila mtu. Jifunzeni kutoka nchi nyingine.
2. Sasa hivi Tanzania ajira hamna. Mnanyima watu passport maana yake wafe na njaa wakiwa Tanzania. Jifunzeni kwa nchi jirani. Kenya, Uganda hata Rwanda raia wao wanafanya kazi nchi mbalimbali kama Dubai, Qatar, Canada, South Africa, Botswana, Namibia, Ubelgiji, Norway n.k Nyie mmekuwa mwiba kwa watanzania.
3. Sio kila recruitment agency inayopeleka watu kufanya kazi Ulaya, America na Asia ni matapeli. Acheni kukariri. Dunia ya leo huwezi kupata kazi nje ya nchi bila kutumia agent. Badilikeni. Kila kampuni mnaita matapeli hivi hamuwezi kutrace kujua uhalali wa kampuni? Jiongezeni.
4. Mnapenda sana makamera kudhalilisha watu wanaoenda nje kupambana na maisha. Nyie mpo ofisini mnakula mishahara muwaache vijana wakapambane nje. Tanzania kazi hamna hata hizo za saidia fundi hamna.
5. Mnasema mtu akienda kufanya kazi nje ananyanyaswa. Mnajua manyanyaso yapo kila mahali ni bora mtu akanyanyaswe nje alipwe milioni kwa mwezi kuliko unyanyaswe na makampuni ya Tanzania halafu ulipwe laki na nusu. Hivi mnajua mishshara wanayolipwa wafanyakazi wa Bakhresa, Mohamed Enterprises, viwanda vya pale mikocheni kama Frostan n.k, mnajua hata hapo Ubungo EPZ watu wanaingia saa 1 asubuhi kutoka saa 11 na mshahara ni laki na nusu? Huo sio unyanyasaji?
6.Kampuni ya G4S Security imeajiri watu kutoka Uganda wanafanya kazi ya Ulinzi Asia na Ulaya na wanalipwa mamilioni. Na hizo kazi lazima agent atumike. Fatilieni makampuni ya ajira kisha mtoe orodha ili vijana wajue kampuni ipi ni genuine sio kuzuia tu vijana wasitoke nje ya nchi.
ACHENI WATU WAKAFANYE KAZI NJE YA NCHI.
2. Sasa hivi Tanzania ajira hamna. Mnanyima watu passport maana yake wafe na njaa wakiwa Tanzania. Jifunzeni kwa nchi jirani. Kenya, Uganda hata Rwanda raia wao wanafanya kazi nchi mbalimbali kama Dubai, Qatar, Canada, South Africa, Botswana, Namibia, Ubelgiji, Norway n.k Nyie mmekuwa mwiba kwa watanzania.
3. Sio kila recruitment agency inayopeleka watu kufanya kazi Ulaya, America na Asia ni matapeli. Acheni kukariri. Dunia ya leo huwezi kupata kazi nje ya nchi bila kutumia agent. Badilikeni. Kila kampuni mnaita matapeli hivi hamuwezi kutrace kujua uhalali wa kampuni? Jiongezeni.
4. Mnapenda sana makamera kudhalilisha watu wanaoenda nje kupambana na maisha. Nyie mpo ofisini mnakula mishahara muwaache vijana wakapambane nje. Tanzania kazi hamna hata hizo za saidia fundi hamna.
5. Mnasema mtu akienda kufanya kazi nje ananyanyaswa. Mnajua manyanyaso yapo kila mahali ni bora mtu akanyanyaswe nje alipwe milioni kwa mwezi kuliko unyanyaswe na makampuni ya Tanzania halafu ulipwe laki na nusu. Hivi mnajua mishshara wanayolipwa wafanyakazi wa Bakhresa, Mohamed Enterprises, viwanda vya pale mikocheni kama Frostan n.k, mnajua hata hapo Ubungo EPZ watu wanaingia saa 1 asubuhi kutoka saa 11 na mshahara ni laki na nusu? Huo sio unyanyasaji?
6.Kampuni ya G4S Security imeajiri watu kutoka Uganda wanafanya kazi ya Ulinzi Asia na Ulaya na wanalipwa mamilioni. Na hizo kazi lazima agent atumike. Fatilieni makampuni ya ajira kisha mtoe orodha ili vijana wajue kampuni ipi ni genuine sio kuzuia tu vijana wasitoke nje ya nchi.
ACHENI WATU WAKAFANYE KAZI NJE YA NCHI.