Uharibifu wa mazingira ni janga kubwa sana, shule na vyuo vitumike kusaidia kupambana na janga hili

Uharibifu wa mazingira ni janga kubwa sana, shule na vyuo vitumike kusaidia kupambana na janga hili

Robert S Gulenga

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2013
Posts
2,255
Reaction score
1,565
Hakuna shaka kuwa janga la uharibifu wa mazingira ni tatizo la Dunia nzima, athari za janga hili ni kubwa sana, Tanzania kama sehemu ya Dunia tumeanza/tunaendelea kupitia maafa ikiwa ni pamoja na ukosefu wa mvua, kupungua kwa vyanzo vya maji, mafuriko, kukauka kwa mabwawa etc ambavyo vyote hivi vina athari kubwa kwenye uchumi wa Nchi na Mtanzania mmoja.

Kama Taifa, moja ya njia za kupambana na janga hili ni kupanda miti, natambua kampeni zinazofanywa na Taasisi mbali mbali za Serikali pamoja na Wadau wa Mazingira, lakini uhalibifu bado ni mkubwa.

Tunaweza kutumia Shule za Msingi , Shule za Sekondari pamoja na vyuo kuhakikisha tunapambana kwa nguvu zote katika upandaji wa miti. Mh Waziri (anayeshughulikia Mazingira), Mh Waziri -OR TAMISEMI- MMK, tukiazisha mashindano ya upandaji miti kwa Shule zote na vyuo , kisha shule 10 (mfano) zitakazoshinda zipewe hata milioni 200, amabazo mgao wake unaweza kuwa nusu ya fedha hizo ziende kuboresha mazingira na nusu iende kwa Walimu na Wanafunzi, kwa Idadi ya Shule na vyuo vilivyopo, baada ya miaka kumi, Tanzania itakuwa GREEN TENA.

Tunaweza kujifunza kwa Shule ya Sekondari Longido- ukifika hapo, hakika utaiona Tanzania ile yenye miti na uoto wa asili.

MWENYEZI MUNGU IBARIKI TANZANIA
MWENYEZI MUNGU MBARIKI RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
 
Mimi naona ikiwa binadamu wanaishi basi mazingira HAYAWEZI kuwa salama

Tutafika tu mahali dunia haikaliki na itabidi tuhame sayari ama tutoweke
 
tumeanza/tunaendelea kupitia maafa ikiwa ni pamoja na ukosefu wa mvua, kupungua kwa vyanzo vya maji, mafuriko, kukauka kwa mabwawa etc ambavyo vyote hivi vina athari kubwa kwenye uchumi wa Nchi na Mtanzania mmoja.
Mbongo namuaminia kwa kuharibu anatisha eg miti aina ya miembe sio kwa kukatwa huko yaani mikaa hizi yaani mimi mtanzania mimi kwa kuharibu mazingira naongoza 🙆🙆😭
 
Nitafika nikajifunze chiziwafursa
Yaani hivi,,,ujue form one pale walikuwa 200 mwaka 2020 huwezi amini wote walipewa miti lakini hadi walipo fika form four miti iliopita haizidi 30 yaani basi😭😭😭 kama ya unataka kwenda it's okay 🆗 ila kampeni hio iko good sema uangalizi na ukaguzi hakuna 😭😭😭
 
tukiazisha mashindano ya upandaji miti kwa Shule zote na vyuo , kisha shule 10 (mfano) zitakazoshinda zipewe hata milioni 200, amabazo mgao wake unaweza kuwa nusu ya fedha hizo ziende kuboresha mazingira na nusu
Ila kwa ushauri washindanishe wilaya na wilaya au mikoa na mikoa shuleni impact inaweza kuwa ndogo
 
Back
Top Bottom