Uhujumu Uchumi, Utakatishaji Fedha

Uhujumu Uchumi, Utakatishaji Fedha

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Mara nyingi binadamu walio wengi, wanapoyasikia mabaya, kama hayawagusi moja kwa moja, ni rahisi kufikiria kuwa hayawahusu, na wale wanaopatwa nayo wanawaona ama ni wajinga ama hawana uthamani kama walio nao wao.

Leo hii, kama kuna mtu au anakuwa ametekwa au kukamatwa na vyombo vya usalama, unakuwa na uhakika wa karibu wa 70% juu ya anachokuwa ametenda, na utakuwa na uhakika wa zaidi ya 95% juu ya mashtaka atakayoshitakiwa nayo mahakamani.

Wahalifu wa kweli hawatekwi bali wanakamatwa au kutakiwa kuripoti Polisi. Lakini ukisikia ametekwa, unaanza kufuatilia ili kujua kama mtu huyo siku za karibuni aliwahi kuwakosoa watawala, serikali au vyombo vya usalama. Kama ametekwa:

1) Utakuwa na uhakika kama wa 70% hivi kuwa mtu huyo atakuwa amewakosoa watawala, vyombo vya dola au serikali

2) Kama atabahatika kufikishwa mahakamani, makosa atakayoshtakiwa nayo ni uhujumu uchumi na/au utakatishaji fedha haramu.

Mashtaka hayo yanamfanya mtuhumiwa kutopewa dhamana, na hivyo kukaa rumande wakati wote.

Waliotunga na kupitisha sheria ya kuwanyima dhamana watuhumiwa wa makosa hayo mawili, nina uhakika kuwa hawakufikiria kuwa kuna siku sheria hiyo itatumika kuwatesa au kuwakomoa watu wasio na makosa.

Watunga sheria waliamini kuwa watawala watakuwa genuine, vyombo vya usalama vitakuwa genuine na mahakama pia zitakuwa genuine.

Hali ya sasa inatoa funzo kubwa kwa sisi sote, watunga sheria, wananchi wa kawaida na hata watawala wa sasa.

Sheria inayomnyima mtu haki ya dhamana kwa tuhuma yoyote ile ni mbaya kwa sababu kuna watu wanaweza kuitumia sheria hiyo vibaya kwa dhamira mbaya ya kutaka kuwakomoa watu ambao kisheria hawajatenda makosa ya jinai.

Ni wakati sahihi sasa wa kuifuta hiyo sheria kwa sababu inatoa mwanya kwa vyombo vya dola na watawala kuitumia vibaya tofauti na ilivyokusudiwa.

Sheria hii mbaya ya kuwanyima watuhumiwa dhamana, kama itaendelea kuwepo, hata wanaoitumia leo, kuna siku itawageuka, na watajutia kwa nini walipokuwa kwenye nafasi za kuifuta hawakuchukua hatua.

Sheria hii kama itaendelea kuwepo, hakika nawaambieni kuna siku, baadhi ya wenye mamlaka leo, iwe ni wakuu wa mikoa, wilaya, mawaziri, polisi, usalama wa Taifa na hata wanajeshi, watauona na kujutia ubaya wake.

Leo ninapoyanena maneno haya, kuna wengi watayaona ni maneno ya kijinga kutoka kwa mtu mjinga asiye na mamlaka kwa sababu leo wapo kwenye nafasi ambazo, kauli zao tu, mtu anafurahi au kuumia, awe anastahili au hastahili.

Wanachosahau ni kuwa mamlaka hayo siku nyingine hayatakuwa mikononi mwao, na wengine watayatumia dhidi yao.

Ukiwa na nafasi yoyote iwe ya kuongoza, kutawala au kusimamia, ufahamu kila tendo unalolitenda kwa dhamira mbaya, litalipwa kwako kwa namna tofauti, kama siyo ya moja kwa moja kwako, itakuwa kwa mtu wa karibu yako ambaye akitendwa, utaumia kama Mfalme Daud alivyoumizwa na mateso na kifo cha mwanae ambaye alikuwa zao la uovu, japo mtoto hakuwa ametenda uovu wowote.

''Ni kwa njia hii, Mungu aliupenda Ulimwengu, hata akamtoa mwanae wa pekee ili Ulimwengu wote upate kuokoka''. Watawala na wenye mamlaka, mnatoa nini kwa watu mnaowaongoza? Mnawapa upendo badala ya chuki? Mnawapa msamaha badala ya visasi? Mnawapa ulinzi badala ya kuwateka? Na mimi kama raia wa kawaida, ninawapa nini wananchi wenzangu?

Ni tafakari ya Noeli. Kristo ni upendo. Azaliwe kwenye mioyo yetu. Azaliwe kwenye mioyo ya watawala. Afute roho za unafiki na hila maana yeye ni Kweli ya Mungu toka kwa Mungu.
 
Sheria ya kutakatisha fedha haina tatizo, tatizo lipo kwetu sisi tunaokaa kimya watu wakionewa!
Screenshot_20191225-213054-picsay.jpeg
 
Halafu kesi ya msingi hata haisikilizwi. Unaweza kaa rumande hata miaka mitatu serikali inasema "uchunguzi haujakamilika".

Sent using Jamii Forums mobile app
Watu wasio na hatia wanateseka. Leo watu wanashtakiwa kuhujumu uchumi wa nchi kwa sh 17m. Kule Segerea wapo watu 4 wanehujumu uchumi kwa sh 20m maana yake sh 5m kila mmoja. Hata makosa ya ukwepaji kodi ambayo yangeshughulikiwa na TRA, yanageuzwa kuwa uhujumu uchumi.

Mtu mmoja anapoonewa na kuteseka, kuna watu su chini ya 100 wanateseka moja kwa moja, na wengine si chini ya 100,000 wanajenga chuki dhidi ya watawala na vyombo vya dola.

Hakuna mahali popote Duniani, nguvu ya polisi au jeshi viliweza kuleta umoja wa wananchi. Tunawahitaji sana polisi, usalama wa Taifa na wanajeshi, kwa sababu hitaji la kwanza la binadamu yeyote ni usalama wake na mali zaje. Lakini vyombo hivi vikitumika vibaya huua umoja wa kitaifa na huweza kusababisha machafuko.
 
Halafu kesi ya msingi hata haisikilizwi. Unaweza kaa rumande hata miaka mitatu serikali inasema "uchunguzi haujakamilika".

Sent using Jamii Forums mobile app
Wakati huo huo mahakama nazo hazishinikizi kwa watawala kuharakisha upelelezi!

Mtu anaendelea kusota ndani kwa kukosa dhamana, miaka na miaka!
 
Wacha iendelee kuwepo ili iwakute hawa waliyoiweka. Ipo siku tu
Inaendelea kuumiza wasiohusika kuitunga na ikibidi tuipinge isijewumiza hata walioitunga,nao labda hawakufahamu madhara yake au wanaoitekeleza hawaelewi au wanaipindisha kwa kuwa inakubali kupinda(Haina Checks and Balance) maana ni sheria mbaya yenye kuwekwa kwa nia ovu za watawala kujimwambafy.
Kiujumla nchi yetu ya Tanzania inahitajika izaliwe upya(Full Reformation) maana wameihairibu beyond repair. We have to do it.
 
Lengo la hizo kesi ni kukukomoa sio kwamba wanakesi ya kukufunga maana wanajua miaka mi3 mahabusu ukitoka kichwa kimevurugika
Wakati huo huo mahakama nazo hazishinikizi kwa watawala kuharakisha upelelezi!

Mtu anaendelea kusota ndani kwa kukosa dhamana, miaka na miaka!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa naanza kuamini wanaitumia hiyo sheria ya kutakatisha fedha kuonea watu, wanachungulia kwenye akaunti za watu wakiona una pesa nyingi wanakubambikia hilo kosa ili baadae ukiri kwa DPP uombe msamaha halafu eti urudishe, issue sio kurudisha, ni uoga wa wahanga, infact wananyan'ganywa pesa zao kijanja, na wao wanajua sema ndio wanaogopa kusema ukweli.

Wengine ni wale wanaoshtakiwa kwa uhujumu uchumi ili wafungwe midomo, kwa kuwa hilo kosa halina dhamana wanajua wataozea jela tu, hawa hata wakijaribu kuongea na DPP ili wasamehewe hawasamehewi, ni uonevu mtupu.

Utawala mbaya sana huu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watawala wajue kuwa hata wakifanya mambo 1000 mazuri lakini wakafanya matendo 10 ya uonevu wa dola dhidi ya raia, yanafuta chochote kilichofanywa. Utakuja wakati ambao watu hawatataka hata kuvigusa vitu vizuri vilivyofanywa kwa sababu wataona ni kushiriki uibilisi.

Ni aheri kula mchunga ukiwa umekalia kigoda kuliko kula biriani ukiwa umekatilia michongoma.

Watawala wakitaka wanaweza kuendelea kuyaamini maneno ya wanafiki kuwa wananchi wanafurahia mambo yanayofanywa. Lakini ukweli ni kuwa ni awamu hii pekee watu wengi hawana furaha, wanaishi katika mashaka makubwa, siyo kwa sababu ni wahalifu bali ni kwa sababu mtu yeyote anaweza kufanywa kuwa mhalifu wakati wowote. Hali hii siyo ya kuikumbatia.
 
Watawala wajue kuwa hata wakifanya mambo 1000 mazuri lakini wakafanya matendo 10 ya uonevu wa dola dhidi ya raia, yanafuta chochote kilichofanywa. Utakuja wakati ambao watu hawatataka hata kuvigusa vitu vizuri vilivyofanywa kwa sababu wataona ni kushiriki uibilisi.

Ni aheri kula mchunga ukiwa umekalia kigoda kuliko kula biriani ukiwa umekatilia michongoma.

Watawala wakitaka wanaweza kuendelea kuyaamini maneno ya wanafiki kuwa wananchi wanafurahia mambo yanayofanywa. Lakini ukweli ni kuwa ni awamu hii pekee watu wengi hawana furaha, wanaishi katika mashaka makubwa, siyo kwa sababu ni wahalifu bali ni kwa sababu mtu yeyote anaweza kufanywa kuwa mhalifu wakati wowote. Hali hii siyo ya kuikumbatia.
Wanaofaidi huu uovu wanashangilia wakati Watanzania mamilioni wakilia na kusaga meno.Tuliambiwa tutalimia meno,na kweli tunayaona mambo moto moto.Tupo kama vifaranga vya kuku ambaye kafa baada ya kuviangua,hatufahamu pa kwenda au cha kufanya.Hali hii ni sawa na MTU kulazimishwa kutabasamu msibani na Julia machozi harusini.
Watanzania tuamke,hakuna aliye salama hata kidogo.
 
Jamal Malinzi kakaa rumande miaka miwili, siku ya hukumu anaambiwa alipe shilingi laki tano.

Pesa ya kumtoa jela ni ndogo kulinganisha na gharama za yeye kuwa rumande kwa miaka miwili!!.

Peter Mselewa na wanasheria mlio humu ndani, mmesoma vyuoni kwa nguvu kubwa ili muweze kuleta mabadiliko.

Sikukuu njema waungwana.
 
Watu wasio na hatia wanateseka. Leo watu wanashtakiwa kuhujumu uchumi wa nchi kwa sh 17m. Kule Segerea wapo watu 4 wanehujumu uchumi kwa sh 20m maana yake sh 5m kila mmoja. Hata makosa ya ukwepaji kodi ambayo yangeshughulikiwa na TRA, yanageuzwa kuwa uhujumu uchumi.

Mtu mmoja anapoonewa na kuteseka, kuna watu su chini ya 100 wanateseka moja kwa moja, na wengine si chini ya 100,000 wanajenga chuki dhidi ya watawala na vyombo vya dola.

Hakuna mahali popote Duniani, nguvu ya polisi au jeshi viliweza kuleta umoja wa wananchi. Tunawahitaji sana polisi, usalama wa Taifa na wanajeshi, kwa sababu hitaji la kwanza la binadamu yeyote ni usalama wake na mali zaje. Lakini vyombo hivi vikitumika vibaya huua umoja wa kitaifa na huweza kusababisha machafuko.
Sheria ni msumeno mkuu
Unapotaka kupambana na serikali yoyote duniani hakikisha kuwa ni msafi na huachi alama yoyote chafu
 
Back
Top Bottom