Uhuru una mipaka Jiheshimu Mkuu

Uhuru una mipaka Jiheshimu Mkuu

Sawa Mkuu.

HILI BANDIKO LIMENIFANYA NIJUE NADILI NA WATU WA NAMNA GANI.
Unadili na watu wa aina gani?

Unakubali kwamba, ingawa inawezekana ni kweli inatubidi tufanye mazungumzo kwa staha fulani, kwa sababu bila staha yoyote tutatukanana na mazungumzo hayatawezekana, lakini pia, kuna mstari mwembamba sana kati ya kusisitiza staha na kuwanyamazisha watu wasitoe maoni yao kwa kutumia hoja ya staha?

Unakubali kwamba hoja za staha, kuheshimu dini, kuheshimu utamaduni wa Mtanzania, kuheshimu viongozi, kuheshimu wakubwa, etc., zinaweza kutumika kunyamazisha hoja muhimu tu ambazo zinapaswa kuzungumzwa kwa uhuru?
 
nachukia sana kuambiwa nimelamba asali
Usichukie. Pinga tu kwa hoja.

Kwa mfano. Mimi ikiwa nimetoa hoja ya kimantiki kusifia kitu, halafu akaja mtu kuni dismiss tu kwamba nimelamba asali, naweza kumwambia huyo mtu kuwa anafanya logical fallacy ya ad hominem.

Anaacha kujadili hoja, anamtukana mtoa hoja.

Hiyo ni dalili ya kukosa hoja.
 
Unadili na watu wa aina gani?

Unakubali kwamba, ingawa inawezekana ni kweli inatubidi tufanye mazungumzo kwa staha fulani, kwa sababu bila staha yoyote tutatukanana na mazungumzo hayatawezekana, lakini pia, kuna mstari mwembamba sana kati ya kusisitiza staha na kuwanyamazisha watu wasitoe maoni yao kwa kutumia hoja ya staha?

Unakubali kwamba hoja za staha, kuheshimu dini, kuheshimu utamaduni wa Mtanzania, kuheshimu viongozi, kuheshimu wakubwa, etc., zinaweza kutumika kunyamazisha hoja muhimu tu ambazo zinapaswa kuzungumzwa kwa uhuru?
Upo sahihi Mkuu.
 
Usichukie. Pinga tu kwa hoja.

Kwa mfano. Mimi ikiwa nimetoa hoja ya kimantiki kusifia kitu, halafu akaja mtu kuni dismiss tu kwamba nimelamba asali, naweza kumwambia huyo mtu kuwa anafanya logical fallacy ya ad hominem.

Anaacha kujadili hoja, anamtukana mtoa hoja.

Hiyo ni dalili ya kukosa hoja.
inawezekana wew umeona ina mantiki, yeye kaiona kero na imemkera

kumbuka mazingira tunamoishi unaweza chukiwa au ukawa kero bila sababa ila imetokea tu
 
inawezekana wew umeona ina mantiki, yeye kaiona kero na imemkera

kumbuka mazingira tunamoishi unaweza chukiwa au ukawa kero bila sababa ila imetokea tu
Sasa hayo ni mapungufu yake, watu wengi wenye hekima wa JF wakipima kwa mizani wataona tu, huyu hapa kahemka kihisia tu.

Huwezi kumaliza mapungufu ya kila mtu.
 
Sasa hayo ni mapungufu yake, watu wengi wenye hekima wa JF wakipima kwa mizani wataona tu, huyu hapa kahemka kihisia tu.

Huwezi kumaliza mapungufu ya kila mtu.
Yes,
Apo tunaelewana. Ukitoa bandiko lako jamaa akitukana au kubeza kwa namna yeyote ile mchukulie poa tu, tambaa na reply za maana, chota maarifa, ufahamu, uelewa na ujuzi....

Muache na mitusi na mihemko yak kwa uhuru na nafasi yake...
 
Habari zenu Wakuu,

Kumekuwa na Uhuru mbovu kwa baadhi ya watu linapokuja suala la kuchangia mada au Bandiko la mtu.

Nimeona sio mara moja, ni mara nyingi sana mtu analeta mada halafu anatokea mtu from nowhere ana-comment upuuzi au kumdharau mleta mada.

Hii hali nimekuwa naiona kwenye mabandiko yanayohusiana na Siasa au Dini, kiukweli sio jambo jema mnalolifanya kwa watoa Mada. Kukejeli au kumdharau mtu kwa Siasa au udini ni Ubaguzi na unapaswa kukemewa.

USHAURI
Kama unapinga mada ya mtu basi tumia hekima na staha kwenye maneno unayoyaandika.
we ni mgeni humu? Kama unaona huwezi kuona ukipingwa na kuzodolewa usiposti kitu. Wenzio tunajua kuwakabili wenye majibu yenye karaha na dharau, tunawanyuka humuhumu mpaka wanakimbia wenyewe na kushika adabu zao
 
Unaomba hurumaaa😂😂😂😂


Yaani mi nile gambe kwa hela zangu alafu uje unilazimishe kucoment vizuri kwenye andiko la hovyo!!!?

aaaa bwana weeee mi laazma nikuchane laaaivuuuu kabisaaa!!!! Kwanzaa Babuu USIFORCE TUFANANEEEE!!!!!!!
 
Habari zenu Wakuu,

Kumekuwa na Uhuru mbovu kwa baadhi ya watu linapokuja suala la kuchangia mada au Bandiko la mtu.

Nimeona sio mara moja, ni mara nyingi sana mtu analeta mada halafu anatokea mtu from nowhere ana-comment upuuzi au kumdharau mleta mada.

Hii hali nimekuwa naiona kwenye mabandiko yanayohusiana na Siasa au Dini, kiukweli sio jambo jema mnalolifanya kwa watoa Mada. Kukejeli au kumdharau mtu kwa Siasa au udini ni Ubaguzi na unapaswa kukemewa.

USHAURI
Kama unapinga mada ya mtu basi tumia hekima na staha kwenye maneno unayoyaandika.
Posa msichana mzuuuuuri hapo ulipo nakulipia mahari 100%.
 
Yaani kuna watu wanatukana humu bila sababu, mpaka unajiuliza hivi kwao ni mama zao ndio wanatukana hivyo?
Maana kuna kina mama wanachamba aisee
Inawezekana wanajifunza toka huko
Haiwezekani mtu anachangia hoja au anaandika mada halafu anatukanwa moja kwa moja
Hawa wanafaa kufungiwa maisha wakatafute jukwaa la matusi [emoji1] [emoji1787]
Hiyo sentensi ya mwisho ndiyo imebeba ufumbuzi wa tatizo.
 
Unaomba hurumaaa😂😂😂😂


Yaani mi nile gambe kwa hela zangu alafu uje unilazimishe kucoment vizuri kwenye andiko la hovyo!!!?

aaaa bwana weeee mi laazma nikuchane laaaivuuuu kabisaaa!!!! Kwanzaa Babuu USIFORCE TUFANANEEEE!!!!!!!
Ukikua kiakili utaacha.

KWASASA TUNAKUPA MUDA UKUE KIAKILI KWANZA (HAUJIELEWI).

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
Kabisa Mkuu, wanakera sana.

YANI INAFIKIA HATUA MPAKA MLETA UZI NAYEYE ANATUKANA KWA KUKOSA UVUMILIVU.
Hapo juu kulia kwa mada kuna vidoti 3, ukivifungua kuna option ya kuripoti bandiko la mchango unaodhani umekiuka maadili. Tatizo hata ukiripoti mara 100 hakuna hatua inayochukuliwa, wakati fulani nadhani natenda dhambi kufikiri kuwa labda hali iko hivyo kutokana na kwamba huenda mmiliki wa jamvi naye kakuzwa kwenye mazingira dhalili kama haya ndiyo maana hawezi kuchukuwa hatua.
 
Kuna watu hawana heshima Mkuu, yani hawachagui maneno ya ku-comment kabisa.

Nimeshuhudia kwenye uzi wa mdau akijibiwa upuuzi mpka nikajihisi vibaya.

Watu wasio na heshima kama hawa wanachangia wadau wasiandike mada kwa kuogopa kutamkiwa maneno ya hovyo.

WABADILIKE AISEE, WANAKERA!
Wewe utakuwa mgeni wa mtandao, karibu mtandaoni...

Actually JF imekuwa ya kistaarabu sana sasa hivi, sababu joto la kisiasa sio kubwa sana, na tension za kidini hazijafikia za wkati ule

miaka ya 2015/2016 hii unayoiona ilikuwa cha mtoto
 
Tena hili la kujadili mada tofauti. Ni 100% lazima kitu kijadiliwe tofauti. Na matusi lazima yawepo.

Mitandao kama quora, ukiona watu wanavyochati utajua tu hawa watu wanafikiri nini na inakupa picha nzima ya watu hao.

Miaka 2006 mpaka 2010 thread nyingi zina staha sana.
Mkuu,

Kama matusi ni lazima yawepo najiuliza ni kwanini mtandao unaweka disclaimer zinazopinga matusi. Wee andika neno la kujaamiana kwa Kiingereza, mfumo wa mtandao utaukataa chap.

Hii pia nadhani mfumo umekaririshwa misamiati bila kujuwa kuwa lugha ina misemo pia.

Mfano, msemo "https://jamii.app/JFUserGuide off" siyo tusi, bali unamaanisha "kuachana na jambo/kitu"
 
Back
Top Bottom