thisdayes
JF-Expert Member
- Oct 28, 2016
- 3,610
- 4,556
Kilimo Tz kinalipa sana na mifano ipo hai bahati mbaya kama wewe ulipata hasara, hao wataalamu unao wapuuza ndiyo wanasema Kenya inasonga na Tz pia inasonga sasa kwanini hukatae waki sema vizuri Tz! Ndiyo maana nikakwambie ulete takwimu. Ninachojua Kenya inaongoza kwa kukumbwa na njaa kwa EA, inaongoza kwa ukosefu wa ajira, Miradi ambayo inachukua pesa nyingi na kuiingiza kwenye madeni yasiyo eleweka, kodi kubwa zinaongezwa ili kulipa madeni e.t.cNadhani kuna vitu vingine inafaa kuona kwa macho pia inasaidia na nitaangalia huko zaidi.Kuliko hizi Propaganda pamoja na majarida ya theory ya kiuchumi ambayo tunamezeshwa Watanzania kuaminishwa kwamba tunasonga.
Kenya wana kila kitu ambacho Tanzania tunajaribu kuwa nacho kwa sasa. Miundo mbinu ya Kenya Kuanzia Nairobi na miji mingine ni ndoto kwetu ya miaka 20. Mambo ya Ndege kwao Bandari na usafiri wa Umma sisi tunafuata.
Viwanda Kenya sio swala jipya wakati sisi tunafikiria Cherehani nne kama kiwanda. Biashara ya Kimataifa kuhusu Export nadhani unajua sisi tunachofanya hapa ni hakuna.
Kilimo Kenya mtu akilima au akifuga anaona kabisa maisha yakibadilika hapa tunaishia bei elekezi na kuzuia yasitoke.
Makaazi ya watu kuanzia Isibania mpaka Lunga Lunga au Namanga mpaka Isiolo ni tofauti na kwetu .
Elimu yetu wakati vitabu vinasema kazi ya kichwa ni kubeba mizigo huwezi kulinganisha ufahamu wa Darasa la nane Kenya na Form six wetu.
Tz inaongoza kwa uchumi shirikishi Africa, chakula cha kutosha mpaka ku export. Matumizi mazuri ya pesa za miradi na miradi inayo tekelezeka. Nimejitahidi kukujibu kadri ya nafasi ilivyo tosha, ila mwisho siwezi kuku lazimisha uamini. Ila siku si nyingi vitu vitajiweka wazi