Uhusiano wangu kimapenzi na "Hamida"

Uhusiano wangu kimapenzi na "Hamida"

Nimeweka kisa cha "bao 12 challenge" kule kwenye uzi wa kula kimasihara

Nikipata muda nitaweka cha Mary, japo ilikuwa kwa makubaliano ya mara moja tu tusirudie tena... Very short story!

Cha "Hamida" endelea kufuatilia, huku ukiweka LIKE, yani kila nikipata like 23 mzuka wa kuandika unakuja!

James Jason
Post namba ngapi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA SITA
******************

Nilikaa kwa mzee Katibu Kata hadi saa tatu usiku, hakuwa katika afya nzuri, malaria ilikuwa inamsumbua na alikuwa amemeza klorokwin (Chloroquine), dawa chungu kama muarobaini lakini pia zilikuwa zinamuwasha...

Tuliongea mambo mengi, lakini suala langu la kumchumbia Hamida lilichukuwa nafasi kubwa.

Aliniambia kuwa siwezi kufanikiwa kumpata binti Burhani, na sababu zake niliona zina mashiko. Kwamba, kwanza mimi ni mkristo, siwezi kufunga ndoa na binti Burhani ambaye baba yake ni mtu wa msimamo katika dini yake. Pia aliniambia kuwa Waarabu wana utaratibu wa kuoana wao kwa wao kama ilivyo kwa Wahindi. Ni nadra sana kukuta ndoa iliyo tofauti na hivyo, aliniambia.

Pia alinishauri kama kweli nimedhamiria basi kwanza kabisa nianze kumteka kimapenzi Hamida; Hamida ambaye hata hajui kwamba James 'amemzimikia'

Yaani nijitahidi nipate nafasi ya kuongea naye ili ajue nia yangu, nijue kama atanikubali ama la. Kisha ndio nianze mashambulizi kupitia Mshenga. Lakini pia alinishauri nijiweke sawa kisaikolojia na kuanza kufikiria kubadili dini.

Nilirudi home nikiwa na ahueni ya fikra, nilala vizuri usiku huo huku nikiwaza mambo mengi hususani pa kuanzia 'kumteka' Hamida kimapenzi.

Kwa wakati huo tayari nilikuwa mbobezi katika kufanya ngono na suala zima la mahaba, nikawaza sijui nitumie mbinu kama ya kwenye kitabu cha "Captive Bride"? Mwandishi Johanna Lindesy alisimulia kisa cha kusisimua sana katika kitabu hicho na harakati za kumteka umpendaye kisha atakupenda baadaye... [emoji23]

Wakati huo tayari nilikuwa nimeshasoma vitabu vingi vya falsafa ya mapenzi nk, nilikuwa najuwa nama ya kummiliki nimpendaye ipasavyo, sikuwa na hofu juu ya namna ya kuonesha mahaba yangu kwa Hamida, bali hofu ilikuwa namna ya kupata wasaa naye na kuanza kueleza 'neno la mapenzi'

Nilijimwagia maji (kuoga) na kulala huku nikiwa na ahueni.
*******

Kulipokucha kama kawaida ya siku za kazi huwa nawahi kazini kwa ajili ya kulisukuma gurudumu la maendeleo...

Nilifanya kazi nikiwa mwenye furaha sana kuliko mwanzo wa mwisho wa juma lililopita.

Baada ya kutoka kazini nilienda moja kwa moja hadi Magomeni Mwembe chai ambapo kulikuwa na kinyozi mzuri chini ya mwembe. (Alikuwa anatumia mikasi misafi, vitambaa vyake ni visafi na pia ananijulia kuninyoa)

Wakati huo nilikuwa nafuga nywele nyingi (afro / mchicha), hivyo nilienda kuziweka vizuri.

Baada ya kutoka hapo nilienda nyumbani kuoga na kubadili mavazi, chini nilivaa raba mtoni (raba toka Ulaya), nikavaa jeans ya bluu iliyokolea ya Levi Straus 501, mkanda mweusi wenye backle kubwa, nikavaa shati langu la picha ya ndege (a.k.a. Juliana), ndani nilikuwa nimetanguliza vest ya matobo matobo madogo (ilikiwa fasheni), mkonono nikavaa saa yangu Motima, nywele zangu afro nikazichana baada ya kuzipaka mafuta safi (hairtonic) Nilijipulizia pafyumu pendwa 'YU for Men', kisha nikatoka kuelekea Magomeni mapipa, pale yanapogeuzia Ikarus kwa pembeni kulikuwa na studio ya kupigia picha iitwayo Africa Studio.

Nilipiga picha tatu matata sana, moja nikiwa nimekaa kwenye kiti, nyingine nimesimama pembeni ya stuli ndefu ya studio na ya mwisho ilikuwa ni passport size. "Kwa hizi picha, Hamida hachomoi", niliwaza.

Wakati huo ilibidi kusubiri picha kwa siku nne ama tano hivi ili ziwe tayari. Hivyo sikukaa sana pale nikaelekea Shibam kwenye kijiwe cha Keram.

Niliwakuta watu wengi kama kawaida, niliwasalimia (vizuri safari hii), nikakaribishwa, kawaida yangu nikifika pale lazima niwapige round moja kwanza huku burudani zinaendelea...

Walikuwa wananipenda sana kwa hilo lakini pia kwa nafasi yangu RTC.

Wakati burudani, mabishano / mijadala inaendelea, nikaenda jirani na mzee Burhan (alikuwa hakosi hapo kila baada ya swala ya alasir) na kuanza kumdodosa...

" Mzee, nimeyafikiria maneno yako ya siku ile nimeona leo nije unipe muongozo" nilimuambia.

"Maneno gani tena?" Aliuliza.

Nikamkumbusha jinsi nilivyokosea kusalimia na kusema "salama leko" badala ya assalaam aleikum"

Akasemaa "ahaaaaa", kisha akacheka...

"Sasa mzee nafanyaje ili niwe mwislamu?" Nilimuuliza.

"Hebu twende nyumbani tukaongee vizuri" alisema huku akiwa amefurahi na kuanza kuinuka"

Moyoni nikasema "yes!, mwanzo huoo!

Kwakuwa hapakuwa mbali na hapo, batavuz yangu niliiacha nimeifunga vizuri, tukaanza kuelekea kwa nyumbani kwa mzee Burhan taratiib huku tukiongea mawili matatu.

Tukiwa njiani alinifundisha maana ya assalaam aleikum. Akaniambia kuwa maana yake ni 'amani iwe nanyi', na wa aleikum salaam maana yake ni ' nanyi iwe kwenu' yani hiyo amani. Nilifurahi sana kufahamu maana ya salamu hiyo na majibu yake.

Nikamwambia kuwa sisi waroma tunasalimiana 'tumsifu Yesu kristu' na tunajibu kwa kusema milele amina. Akaniambia kuwa anajuwa kwa kuwa kuna wakati aliwahi kwenda pale Moroco Hotel, Kanisani na kuwasikia waumini wakisalimiana hivyo mara kwa mara.

Tukafika kwake, akausukuma mlango kwa ndani bila hodi, ila akaniambia karibu sana kijana. Nikasema starehe.

"Karibu varandani" alisema huku akivua sandles zake na kutambuka (kuruka) kizingiti kuingia sebuleni.

Nami nikavua raba zangu kisha nikaingia. Mle ndani tuliwakuta watu watano wakiongea, alikuwepo yule mama Mwarabu, mama wa kiafrika, kijana wa makamo wa kiarabu, kijana mwingine wa kiafrika na mtoto mdogo (wa umri wa miaka mitano hivi)

Mzee Burhan alianza...

"Karibu sana James, huyu hapa ni mke wangu, maarufu kama mama Warda, yule pale ni mdogo wake (nilikuja kujuwa baadaye kuwa alikuwa msaidizi wa kazi aliyeishinao kwa miaka mingi sana), yule pale ni mwanangu anaitwa Yasir na rafiki yake..."

"Anaitwa Abdul" alidakia Yasir.

"Nashukuru kuwafahamu" nilijibu

"Eeee na huyu anaitwa James..." Mzee Burhani alimalizia akinioneshea mimi kidole....

"Tunamfahamu" walijibu wale vijana (Yasir na Abdul) kwa pamoja.

"Samahani, naomba mtupishe tuna maongezi nyeti kidogo" alisema mzee Burahani.
Yasir na Abdul walitoka nje kabisa ya nyumba, mama Warda na mdogo wake wakaenda chumba kingine...

Mzee akachukuwa Radio cassete recorder (Memory Q), akasogeza nilipokaa akaweka juu ya stuli kisha akaniambia kuwa atarikodi mazungumzo yetu ili awe na ushahidi...

"Hamidaaa" aliita yule mzee Burhani

"Abee baba" nilisikia sauti hafifu kisha nikasikia mlango unafunguliwa na hatua za kivivu zikawa zinasikika kuja upande wa sebuleni.

"Abee baba" alirudia kuitikia, safari hii sauti ilikuwa kama ile ya siku ya kwanza kumuona.

"Katuletee soda" Mzee Burhani alimuambia...

Kabla hajaondoka nikaijikuta nasema "Mie niletee togwa kama lipo"

Hamida hakusena neno, akaondoka...

"Huyu ni binti yangu wa mwisho, anaitwa hamida, ndio ametoka college juzi juzi, alikuwa akisomea mambo ya upishi." Aliendelea mzee Burhani.

"Nilikuwa watoto watano, Watatu wakike na wawili wakiume, dada yao mkubwa anaitwa Warda, kisha amefuatia Sabra halafu Yasir na Hamida ndio kitinda mimba. Mmoja alifariki. Huyo mtoto mdogo unayemuona ni mjukuu, mtoto wa binti yangu wa kwanza Warda" alinifahamisha.

Mara Hamida akaingia na chupa moja ya fanta na bilauli tatu.

Akaifungua ile soda na kumimina kwenye bilauli ndogo ambayo alimpa yule mtoto.

"Nadya, usimwage mwage eee!" Sauti nyororo ya Hamida ilisikika.

Kisha akamimina soda iliyobakia kwenye bilauli ya baba yake. "Karibu baba" alisema kisha akatoka tena.

Aliporudi alikuja na magi yenye togwa baridiii!, akasogeza redio pembeni kidogo, akachukua ile bilauli iliyosalia akaiweka kisha akamimina... " Karibu kaka" alisema na kuondoka.

Mie hapo moyo wangu burdani, nilikuwa nafurahia kila sekunde aliyokuwepo Hamida.

"Karibu James..." Mzee alisisitiza na kunitoa kwenye mawazo yaliyonijia ghafla.

"Enhe, umesema unataka muongozo kuhusu kubadili dini!" Alisema huku akibofya kitufe cha kuchezea kaseti sanjari na kitufe chekundu cha kurekodia.

"Ndio mzee, nipe muongozo" nilijibu baada ya kugida (kunywa) fundo (puff) moja ya togwa.

Akasema, sasa nitakuhoji maswali ambayo utakavyojibu itanipa mwelekeo...

"Je umelazimishwa ama kushawishiwa na mtu kubadili dini na kuwa mwislamu?" aliuliza

"Hapana mzee" nilijibu.

"Je huogopi kutengwa na jamii yako wakigundua kuwa umewahama?" Aliendelea kuuliza...

Niliinua bilauli ya togwa na kunywa tena, kisha nikamjibu, hapana, nimeshafikisha umri wa kuamua nitakalo, hivyo sina hofu yoyote.

Mzee Burhani akaniangalia kwa makini kisha akaniuliza kama najuwa uwepo wa mtu aliyeitwa Muhammad (s.a.w), nikamjibu, ndiyo nasikia alikiwepo mtu huyo.

Mzee aliendelea kunihoji imani yangu kuhusu Mungu. Nikamjibu "Sisi tunaamini Mungu ni mmoja na yupo katika nafsi tatu, yani Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho mtakatifu"

Akaniambia wao waislamu wanaamini kwamba Mungu ni mmoja tu na hakuna Mungu mwana wala Mungu Roho mtakatifu...

Kwa kuwa nilishayavulia maji ilibidi nikubaliane naye katika kila alilozungumza, nilikuwa naona kama ananichelewesha...

"Sasa ili uwe mwislamu inabidi ukiri kwa moyo na kutamka kwa ulimi kwamba hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allah na Muhammad ni mjumbe wake" alisema.

Aliniambia mengi ya awali kuhusu imani ya kiislamu ikiwemo kutosulubiwa kwa Yesu ambapo wao wanamuita Nabii Issa na mambo mengine kadha wa kadha.

Nikapata ugumu wa kiimani, kwani kusulubiwa kwa Yesu ndiyo msingi wa imani yetu ilipolala, lakini nikapiga moyo konde.

Akaniambia, nikajifikirie, kama nitakuwa tayari basi nimtafute ili anisilimishe rasmi na kunipeleka msikitini kwa ajili ya utambulisho.

Nikamjibu, sawa. Kisha nikamalizia togwa iliyobakia kwenye bilauli.

Alisisitiza kuwa kuwa muislamu ni rahisi sana, unatamka shahada mbili basi tayari unakuwa mwislamu.

Kwa kuwa jua lilizama tukiwa bado tunaongea, akaniambia anaenda kuswali (ndani) hivyo nimsubiri, kisha akatoka mle sebuleni.

Mara sauti za miguu ikitembea nikasikia ikija upande wa sebuleni.

Waooo! Hamida huyo! Nikijisemea kimoyomoyo, akakusanya zile bilauli na magi iliyobakia togwa shinda (kiasi) na kutaka kuondoka...

"Angalia usiangushe bilauli kama siku ile..." Maneno yalinitoka mdomoni...

Akatabasamu kisha akasema "hizi chafu hazitoanguka kwakuwa nimezibebanisha... Halafu siku ile ule mtandio ulikuwa unateleza sana..." Alijibu huku akimfuta Nadya alipojimwagia soda.

"Pole" nilimwambia kisha nikamuuliza "Eti malai (icecream) zipo?"

Akajibu kuwa zimebakia chache. Nikamwambia, nikitaka kuondoka naomba uniletee zote.

Akashangaa na kuuliza "sasa utazibebaje?"

Niwekee kwenye chombo kesho nitakuletea, naenda kuzihamishia kwenye chombo kingine ili niziponde ponde nitengeneze juisi.

Akacheka kisha akasema "si bora ungesema tu tukutengenezee juisi"

"Ewaaaaa (aiwaa) hilo pia ni wazo zuri, lakini leo nifungie, halafu naomba unitengenezee juisi nzuri ili nikinywa niwe nakukumbuka muangusha bilauli" nikasema.

"Mmh" akaguna na kuondoka.

Baada kama ya dakika kumi hivi nikamsikia mzee Burhani akikohoa huku akija uelekeo wa sebuleni.

"Samahani nilikuacha peke yako" alisema huku akiingia.

"Bila samahani, sikuwa peke yangu, Hamida alikuwepo na huyu Nadya pia..." Nilisema huku nikikaa vizuri kwenye kochi.

Hatukuongea sana baada ya pale, nikaaga na kutaka kuondoka, nikamuambia nimeagiza niletewe malai...

"Hamidaaaa" Mzee Burhani aliita.

"Mgeni anataka kuondoka"

Mara akaja na kiboksi kidogo cha kuhifadhi joto (ama baridi), akanipatia.

"Shilingi ngapi?" Nikamuuliza kwa sauti ya chini.

"Shilingi nne, zipo nane humo" alijibu.

Nikatoa gwala (dala/ shilingi tano) nikampatia, nikamwambia chenji nitachukuwa kesho.

Akasema "in shaa Allah."

Tukasimama na mzee Burhani kwa pamoja, nikachukuwa kiboksi chenye malai na kutoka sebuleni, nikavaa ndaba (raba mtoni) zangu na mzee Burhani akanifungulia mlango, akanisindikiza hadi Shibam (siyo mbali), nikamwacha hapo, nikachukuwa batavuz yangu huyoo hadi Butiama restaurant kisha nyumbani.
*******

Nilikuwa na furaha kubwa sana, kupata wasaa wa kuongea na mzee Burhani na kubadilishana maneno na Hamida.

Ghafla tafakari za imani ya dini yangu ikanijia, nikaanza kuwaza mabadiliko yatakayojitokeza kama nikisilimu.

Kupoteza mawazo nikachukuwa zile icecream na kuzipondaponda kisha nikaweka kwenye friji. Nikachukuwa sehemu ya ile juisi(vibarafu vidogo vidogo) na kuweka kwenye glasi kisha nikachukuwa brandy kabatini na kumiminia kwa wingi hadi glasi ikajaa.

Kiukweli wala sikuwa nahitaji icecream, nilitaka tu nipate wasaa wa kubadilishana maneno ya Hamida, "nimefanikiwa hivyo ngoja nishangilie ushindi wa awali." Nikijisemea kisha nikaanza kunywa taratiibu huku nikisikiliza santuri ya Kool and the Gang, wimbo wa 'Celebration'
************

Itaendelea...View attachment 1341386View attachment 1341388

James Jason
Mkuu unaweza nipatia na list ya vitabu kuna moja niliona umeitaja "the perfumed garden"... Nilikisoma nimefaidika sana.
 
Back
Top Bottom