Uhusiano wangu kimapenzi na "Hamida"

Uhusiano wangu kimapenzi na "Hamida"

SEHEMU YA TISA
*******************

Ahamis ile ilipita vizuri. Niliamua 'kumuua' Hamida kwa kutumia 'sumu ya kuua taratibu', sikuwa na papara na sijui uvumilivu ule ulitoka wapi!

Kuanzia Ijumaa hadi Jumapili ilikuwa siku za mimi kupumzika kufundishwa masomo ya dini, hivyo nilipanga Ijumaa hii niende sinema.

Sikuwa napata nafasi ya kuongea na Hamida nje ya nyumbani kwao, tena akiwa amejihifadhi mwili wote kasoro sehemu ya uso, lakini nilikuwa nafurahia uwepo wake karibu nami hasa siku ya 'jana' ambapo alipokuwa akinirekebisha kusoma vizuri.

"Hivi wewe kwani huwa huendi matembezini? Mie kesho usiku nitaenda sinema Cameo kuna filamu nzuri nimeona kwenye gazeti. Kesho Ijumaa nikitoka kazini nitakuja kununua juisi, bila shaka nitakukuta angalau nikuone maana kesho hadi Jumapili nilichaguwa kupumzika na kufanya mambo mengine"

Hili lilikuwa ni shambulizi dogo na hafifu lakini lenye sumu inayoweza kuua taratibu, ni barua (memo) niliyompatia Hamida kabla hajaondoka kwenye kile chumba kuelekea sebuleni.
*********

Ijumaa nikiwa kazini nilimuaga Marry kuwa naelekea msikitini. Nilitoka saa sita kamili kuelekea maeneo ya mtaa wa mkunguni kisha nikaenda msikiti wa Manyema.

Miaka hiyo maeneo ya mtaa wa Living stone, mkunguni ilikuwa imechangamka sana, katika harakati zangu nilikuwa naonekana maeneo ya kjiwe cha mabaharia (sea men's coner), enzi hizo kazi ya ubaharia ilikuwa ya ujiko sana kwa vijana na wengi walijifunza kuzamia meli (stowaway) kutokea kijiwe hicho... Biashara za jeans kali (used), bidhaa zingine za 'mamtoni' (nje ya nchi) zilikuwa zinafanyika maeneo hayo , siyo kwa maduka maalumu bali mkononi tu, unapata info, Baharia fulani anauza cheni za gold apate nauli arudi 'Belgium', unamvizia, unampa hela anakupa cheni, ama bidhaa nyingine kama alivyotangazia 'wasela' (sikuhizi mnasema masela), Sela lilitokana na ubaharia, Sail, Sailer yani baharia hususan wale wa vyombo vitumiavyo upepo kama nguvu ya kusafirisha chombo (Jahazi, Dau, Mashua, na ngalawa)

Mabaharia wengine walikuwa wanashinda pale Forodhani Atiman House (barabara ya Sokoine na Kivukoni)

Maeneo hayo (Mkunguni / Living stone) kulikuwa na biashara zisizo rasmi za kubadilisha hela yetu na kuwa dola, madini, udalali na kadhalika.

Nikiwa maeneo hayo mida ya waislamu kuswali nilikuwa nasikia adhana kwa ukaribu na pia mawaidha wakati mwingine unayasikia hata ukiwa mita kadhaa kutoka eneo la msikiti, hivyo nilichaguwa msikiti wa Manyema kusalia swala za Ijumaa.

"Hongera, umekuwa mswaliina, katuombee na sisi" alisema Marry wakati natoka

"Ahsante, nitarudi saa saba na nusu hivi maana leo ni siku ya kusikiliza hotuba mbili za Ijumaa" nilisema na kuongeza maneno kidogo kuonesha kuwa dini imeanza kunikolea.

Marry alitamasamu, mie nikaondoka.

Marry kama nilivyozoea kumwita alikuwa ni mtu wa kutoka Kilimanjaro, ana mume na watoto wawili. Nilimzoea sana, lakini sikuwahi 'kumtokea' (kumtongoza) licha ya yeye kunionesha dalili zote za kutaka 'nitembee naye', dalili zilikolea pale naye aliponishirikisha mambo yake ya nyumbani... Hakuwa na ndoa yenye furaha..., ila kuna siku alinitega sana hadi uzalendo ukanishinda, ilikuwa kabla ya kumuona Hamida.

(Stori yake ni fupi sana, nitaelezea kwenye uzi wa kula kimasihara pamoja na stori nyingine ya shindano la kufikisha bao 12)

=

Baada ya Ibada ya Ijumaa nilirudi ofisini kumalizia siku.

"Umependeza kweli na kanzu yako" alisema Mary wakati naingia ofisini huku nimevaa kanzu juu ya nguo nilizovaa asubuhi, kabla sijaenda msikitini, nilipitia Kariakoo mtaa wa pemba kwenye duka moja hivi la mhindi nikanunua kanzu na kofia ya mkono (waliziita kofia za Zanzibar) ndio nikaelekea Manyema.

"Ahsante Marry", nimeamua kubadilika, karibu nawe nianze kukuona ukivaa baibui (buibui), nilisema kisha nikaingia ofisini kwangu.

Enzi hizo mabaibui yalikuwa tofauti na ya sasa, yalikuwa kama yana kikofia hivi (ushungi) halafu lazima ukivute upande mmoja ukibane kwapani kuepuka kulikanyaga ama kuburuza (ilikuwa ndio fashen), rangi nyeusi tii, 'texture' nzuri ajabu. Ilikuwa ni kawaida kwa wanawake kuvaa hayo mabaibui wakitaka 'kutoka' (yaani kwenda sehemu)
********

Marry alicheka akionesha (kwa kumaanisha) kuwa ni vigumu yeye kubadili dini.

Mezani nilikuta bahasha (barua) kutoka wakala la pijot. Saa tisa na nusu nilitoka ofisini moja kwa moja hadi nyumbani pamoja na mambo nipate kuisoma vizuri ile barua
******

Wakati nipo mwaka wa mwisho Uingereza niliwaandikia Peugeot Ufaransa nikitaka wanipatie profoma invoice ya kununua 504 GL pickup. Walinijibu kuwa nipitie wa wakala waliomuidhinisha aliyepo Dar es Salaam.

Hivyo nilivyofika Dar kutoka masomoni nilinunua Batavuz kwa jamaa mmoja wa kutoka Zanzibar pale Mkunguni, ilikuwa kama mpya tu, kisha ndio nikaenda Peugeot house pale mtaa wa Ali Hassan Mwinyi (Bibi titi / Ohio) nikaagiza kupitia wakala wao. Masomo ya post graduate diploma hayakuwa yananichukulia muda sana hivyo nilifanya kazi za part time na kutengeneza hela ya kutosha kununua gari na mazagazaga mengine...

Meli zilikuwa zinachelewa sana kuwasili kutoka ulaya hasa zile zinazozungukia Atlantic hadi South Africa kisha ndio kuja mashariki ya Africa, zile zilizopitia upenyo wa Gibralta kisha upenyo wa Suez zilikuwa zinawahi.

Kwenye ile barua niliambiwa gari yangu imeshafika na ipo afisini kwao hivyo niende kukamilisha taratibu zingine ili nikabidhiwe...

Nilifurahi sana, nikajisema hili litakuwa jambo la kwanza siku ya jumatatu.

Saa kumi na nusu nikaenda kwa akina Hamida, baada ya Mama Warda kunikaribisha nilimuambia leo sikai, sina kipindi bali nilimuagiza juisi Hamida..

"Hamidaaaa" mama Warda aliita huku yeye akirudi sebuleni na kuniacha nimesimama kwenye karido...

"Abee mama" aliitikia Hamida kwa sauti yake nyororo kama ya mama yake, sauti inayonifanya niwe 'mgeni' nyumbani kwao kila siku...

Hamida alitoka chumbani kwake, aliponiona tu, alirudi ndani tena kisha akatoka na kuelekea kwenye jokofu kubwa kuchukuwa juisi niliyomuagiza...

Lengo halikuwa juisi bali majibu ya barua (ki-memo) nilichomuachia jana...

Mapigo ya moyo yananidunda kuliko kawaida, nawaza sijui atajibu namna gani...

Alikuja uelekeo wangu, kwa mwendo wa madaha (ndio mwendo wake ) shingo upande kidogo mikono yote ameshika dumu la lita 3 japo angeweza kulishika kwa mkono mmoja..

Alinikabidhi lile dumu kwa mikono yote miwili na mkono wake wa kushoto akiwa amebana karatasi ndogo ambayo haionekani kwa urahisi, akanigusa vidole vyangu vya mkono wa kulia wakati napokea dumu kama ishara ya kutaka kunipatia kitu...

"Haijaganda sana leo..." Alisema huku ameinama chini kidogo, nami nikamjibu kuwa haina neno nikapokea, nigaaka kwa sauti kubwa ili mama na wengine sebuleni wasikie kisha nikatoka.

Wakati ananigusa vidole nilijisikia kama nimepigwa shoti hivi na kusisimka hatari, nikijikaza kwa kutoonesha tofauti.

Nilitoka hadi nyumbani tena na kuanza kuisoma.

Aliandika mwandiko 'mduchu' sana (what we call microscopic words), karatasi ilikuwa ndogo sana na alitaka kuandika mengi...

Mwandiko umelalia kushoto, nafikiri alitumia zile pen aina ya bic zenye rangi ya njano kwa nje (0.6mm)

Kimemo chake hakikuwa cha mahaba, bali aliandika...

"Assalaam aleikum, mie sijambo alhamdulillah. Jana nilisoma ujumbe wako, huwa natoka lakini kwa sababu maalum ambayo wazazi wataielewa, angalau wakati nasoma nilikuwa huru kidogo, lakini maisha yetu ni ya kufungiwa ndani muda mwingi. Nakuona kuwa una busara kuna jambo mie pia nataka nikushirikishe unishauri, maana hapa Kaka yangu baba na mama wote sioni kwa hiki kama wananishauri vyema. Kesho ukija kurudisha dumu nitakuwa nimeshajuwa namna ya kutoka tuweze kuongea, wa billah tawfiq."

Nilirudia kuisoma memo ile kama mara 23 hivi [emoji23]

Ilikuwa inaniondoa wasiwasi, inatuliza mtima, inaondoa joto, inaleta matumaini kwenye harakati zangu za kuongeza dozi ya 'sumu' maana mzee Katibu Kata alinishauri nisiwe na papara la sivyo nitafeli na kujiaibisha.

Kwa siku moja nilipokea barua mbili zenye kunipa furaha, asikwambie mtu, nikikuwa na furaha sana hasa kile kipengele "kesho nitakuwa nimeshajuwa namna ya kutoka..."
******

Baada ya chakula cha jioni nilienda Cameo Cinema kuangalia filamu mpya iitwayo Grease. Ni filamu ya stori ya mapenzi.

Muda wote nikiwa naangalia sinema hiyo nilikuwa najiona kama mimi ndiye Danny Zuko (Starring) na Sandy ni Hamida....

Nilifurahia sana filamu hiyo na kutamani kama Hamida angekuwepo ukumbini siku hiyo.

Tulifurahishwa pia kwa trela za "bad spensa"

Saa tano na nusu usiku tayari nilikuwa nyumbani, filamu za kizungu mara nyingi huchukuwa dakika 90 ama 120.

Nililala kwa furaha siku hiyo huku nikiona kama saa haziendi ili niende kwa Hamida kurudisha dumu la juisi [emoji14]
****

Majira ya saa tano asubuhi nilienda kwa akina Hamida, bahati nzuri ni yeye aliyenipokea na kunikaribisha sebuleni.

Niliwakuta mama wa kiafrika, mama Warda na Nadya pia wakiwa wanasogoa (wanazungumza)

Hamida alipokea lile dumu kisha akaenda nalo, huku akiniambia...

"nimekutengenezea togwa, najuwa unalipenda, leo ma-mkubwa nilimuambia apumzike, ngoja nikuletee..."

Punde si punde alirudi akiwa na dumu dogo lingine la lita moja lenye togwa ndani, wakati akija nami nilikuwa naaga ili nitoke tukutane kwenye korido.

"Najuwa utalipenda bila shaka, ma-mkubwa alinifundisha vizuri.." Alisema kwa sauti ili wa sebuleni nao wasikie...

"Ahsante, nashukuru ila mie sikai tutaonana kesho ama Jumatatu..." Nilisema huku nikiipokea memo yake nyingine aliyoibana kama jana.

Niliipokea kisha kiganja changu nikashika vidole vyake kwa sekunde kadhaa, akavivuta kujitoa lakini si kwa hasira, akanifungulia mlango. Matendo hayo yalifanyika ndani ya sekunde chache wakati wa kubadilishana yale maneno ya kuagana.

Nilimuaga kwa kumpungia mkono na kuondoka kuelekea nyumbani.
******

=

"Assalaam aleikum, panapo majaaliwa kesho baada ya kunywa chai nimeaga nitaenda Msasani kwa Shangazi, basi kama una nafasi naomba unisindikize nipate kukueleza yanayonisibu, saa nne asubuhi unisubiri kituo cha Mwanamboka Kinondoni, usikose, wabillah tawfiq"

Hayo yalikuwa meneno kwenye memo ya Hamida.

Ikumbukwe kuwa hadi sasa Hamida sijamtongoza na hajui kiasi gani nimempenda na maamuzi magumu niliyofanya na ninayoendelea kuyafanya.

Jumamosi hii ni siku yangu ya kwenda DDC Kariakoo kwenye dansi, lakini ratiba za ibada nazo zinanibana, hivyo nilienda kwa kuchelewa, na safari hii nilikaa upande ule wa watu waliotulia. Madaraja hadi ndani ya kumbi za starehe.

Bahati nzuri Mziki wa DDC Mlimani Park ulikuwa haujaanza, kulikuwa na maonesho ya Kibisa ngoma troup.

Kwenye kikundi hiki ndipo nilipomuona kijana Amri Athumani ambaye alikuwa akiliza watu sana kwa uigizaji wake, hususani igizo aliloigiza kama mtoto wa kambo aliye lelewa kwa manyanyaso na mateso makubwa lakini baadaye alifanikiwa kuwa na maisha mazuri... (Pumzika kwa amani King Majuto)
************

=

Saa zikawa haziendi, enzi hizo hakuna simu za mkononi, hakuna mitandao ya internet, nilisoma masomo ya kutumia tarakikishi (computer) nikiwa Uingereza, naikumbuka pc yangu chuoni ilikuwa IBM 386 ikitumia mfumo endeshi (operating system) microsoft windows 3.1, hadi nacheka hapa, ilikuwa ni ya kisasa sana wakati huo....

Mzee Burhani alikuwa anayo simu ya mezani, lakini sikuwa na tabia ya kuwapigia. Na hata nikimpigia Hamida kwenye simu ya mezani nitaongea naye vipi maneno ya mapenzi akiwa sebuleni na mara nyingi panakuwa na watu...

Njia zilizobakia ni kuonana naye ana kwa ana ama kuandikiana barua.

Sasa kwa memo ile ya Hamida muda ndio ukawa 'hauendi' kabisa!

Niliamua kufanya kazi zote nizifanyazo Jumapili ili siku hiyo niwe huru, nikapaweka vizuri chumbani, sebuleni na mazingira ya nje, nilikuwa msafi kupitiliza, na kazi nyingi nilikuwa nafanya mwenyewe, mwili wangu ulikuwa umejengeka vizuri, nyama nyama zilikuwepo kidogo siyo kama ilivyokuwa miaka sita iliyopita.
*****

Usiku baada ya kula ndio nilienda DDC kwa ajili ya mziki wa dansi.

Baada ya Kibisa ngoma troup kumaliza maonesho yao ya ngoma za asili, mziki wa dansi ulianza taratibu kwa mpiga solo mmoja kuanza kuchombeza... Kisha wanamziki wengine wakachukuwa nafasi zao na burudani ikaanza kuchanganya.

Tulifaidi sana kusikikiza, kucheza na kuwaona mubashari wanamuziki... Upangiliaji wa vyombo, mpangilio wa sauti, maudhui, solo guitar kusikika vizuri, ridhim (rhythm) guitar kusikika bila kumezwa, bass guitar kuchombeza ipasavyo, organ kuchukuwa nafasi yake, saxafone na trumpets kusikika wakati muafaka, drums kuongoza mziki mzima, uchezaji wa wanamziki na wapenzi wa muziki na kadhakika ni burudani safi kabisa iliyotufanya tufurahie na kutokosa kila weekend...
*****

Nitaweka wimbo mmoja kwenye attachment ili wewe kijana wa sasa usikilize kwa makini...

=

Siku ilipita hivyo, nilirudi nyumbani nikiwa mwenye furaha na kupumzika.

Saa mbili asubuhi alarm iliniamsha, nilipitiwa na usingizi hata ibada ya swala asubuhi sikufanya.

Niliamka na kufanya yapaswayo kufanywa asubuhi kisha nikatengeneza chai ya maziwa ya BB condensed milk, slesi za mikate na mayai ya kukaanga.

Saa tatu kamili nipo tayari, nikachukuwa ile memo tena na kuanza kuisoma upyaaaa kama vile sijaisoma....

"...saa nne uwepo Mwanamboka.... Usikose..." Nilijikuta nafurahi kwa mara nyingine tena japo si kwa mtoko wa kimapenzi, kwanza Hamida hajui kama 'nimekufa nimeoza juu yake' nilijisemea.

Nilachukuwa juzuu na kudurusu herufi hadi nilipoishia Alhamisi ili nipate sehemu za kumuuliza ama sababu za kuanzia kuvunja ukimya rasmi...

Saa tatu na robo nilianza safari mdogo mdogo hadi magomeni kituo cha taksi, sikuchukuwa batavuz, nikakodi taksi hadi Kindondoni, akanishusha kituo cha Mwanamboka.

Saa nne kasoro kumi mie nipo kituoni. Nilisimama tu hapakuwa na benchi wala kivuli cha paa.

Hali ya hewa ilikuwa si joto wala baridi, watu wachache barabarani, wengi wao bado wapo makanisani...

Kila baada ya dakika najikuta naangalia motima (saa) yangu, muda hauendi! Mara saa nne hii hapa! Hakuna dalili ya Hamida...

Ilipofika saa nne na dakika ishirini na tano hivi nikaona UDA ya kwenda Mwenge imesimama na kushusha abiria, ilikuwa basi kubwa, na abiria wote walikuwa wakishukia mlango wa mbele, mlango wa nyuma ulikuwa wa kuingilia tu. Na ukiingia tu unakutana na mkatisha tiketi (amekaa) anakukatia kwa mashine flani hivi ndogo kama efd kwa sasa ila ilikuwa mechanical. Kupanda kwenye basi ni kwa foleni.
****

Mara paap nikamwona Hamida anashuka mlango wa mbele na kuja upande wangu...

Alikuwa amevaa gauni la rangi ya pink, mtandio uliofungwa vizuri wa rangi pink, viatu fulani vinavyoziba vidole vya mbele hadi nusu mguu vya pink, mkononi ameshika begi dogo la mkononi nalo rangi ya pink, hakika mavazi yalimpendeza.

"Assalaam aleikum" alinisalimia bila kunipa mkono.

"Wa aleikum salaam Hamida", umechelewa

" Nisamehe, nilichelewa kuaga maana nimebadilisha ilikuwa nirudi baadaye magharibi lakini nimeomba ruhusa nilale huko Msasani, nimekubaliwa" alijibu.

"Batavuz yako umeiweka wapi" aliuliza huku akiangaza huku na huko

" Aaa, leo sikuja nayo, nimekuja kwa teksi" nilijibu

"We nawe, pale na hapa tu unapoteza hela kwa teksi" alisema huku akimaanisha

"Kwakuwa sijui mazingira tuendako ndio nikaona bora niiache ili tutumie usafiri wa jumuiya ama teksi" nilijibu kwa kujiamini.

Nami siku hiyo nilikuwa nimepigilia hasa, nilivaa safari buti, kadet, shati pia kadet, kichwani nywele nimechana vyema (mchicha / afro).

"Nisubiri ngoja nikachukue teksi" nilisema huku naondoka

Dakika chache tu nilirudi nikiwa ndani ya teksi siti ya nyuma upande wa kulia...

Niliinama na kumfungulia mlango...

"Karibu, twende!" Nilisema naye akatii na kuingia kwenye teksi.

"Kituo cha kwanza wapi?" Nilimuuliza Hamida ili atoe ramani kwa dereva

"Katuache Morogoro super market" alidakia Hamida...

Moyoni nikashangaa, mbona tunaelekea huko badala ya Msasani... Ila sikumuuliza.

Kulikuwa na ukimya fulani hivi hadi dereva alipoweka mziki wa Boney M, Dad cool.

Nikaanza kutingisha kichwa, Hamida ananiangalia tu katulia.

Tulivyofika Moroco dereva akapinda kulia na kufuata Bagamoyo road kuelekea mjini (siku hizi inaitwa Ali Hassan Mwinyi rd, tulivyofika mbuyuni mbele kidogo dereva akachukiwa njia ya kushoto barabara ya Haile Selasie moja kwa moja hadi Morogoro supermarket.

Nikamlipa dereva ujira wake kisha tukashuka, Hamida akawa anaelekea ndani ya supermarket, nikamfuata, nikamuuliza mbona tumekuja hapa, akanijibu anataka amnunulie shangazi yake zawadi, hivyo tukaingia ndani kwa ajili ya shopping.
*************

Itaendea...View attachment 1345778View attachment 1345779View attachment 1345781View attachment 1345782



James Jason
Hapo kwenye kusoma barua mara nyingi, pamenifurahisha sana
Umenikumbusha barua niliisoma kwa miaka 7 (sio kila siku kwa vipindi tofauti) bila kuichoka pamoja na kua alieniandikia barua nipo nae ndani na tuna mtoto miaka m4 baada kuniandikia hiyo barua adi alivyokuja kuificha yeye mwenyewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kusoma sehemu hii ya 14 ndo najua kuwa chefs pride ilikuwepo toka kipindi hicho,nilikuwa najua zahir hotel pekee maeneo yale.Je ni kweli chef ilikuwepo kipindi hicho !!!!??
 
Kwa kusoma sehemu hii ya 14 ndo najua kuwa chefs pride ilikuwepo toka kipindi hicho,nilikuwa najua zahir hotel pekee maeneo yale.Je ni kweli chef ilikuwepo kipindi hicho !!!!??
 
Kwa kusoma sehemu hii ya 14 ndo najua kuwa chefs pride ilikuwepo toka kipindi hicho,nilikuwa najua zahir hotel pekee maeneo yale.Je ni kweli chef ilikuwepo kipindi hicho !!!!??
Ni "decoy" mkuu, ungeunganisha dot kama ulikuwepo miaka hiyo kwa kuwa sehemu husika stori yangu ilivuma sana.

Actual restaurant ilikuwa jirani na jumba la sinema maeneo hayo, sasa hivi pameota ghorofa. Ni mgahawa uliokuwa na harakati nyingi za kisiasa.

Naomba niishie hapo.

James Jason
 
Ni "dcoy" mkuu, ungeunganisha dot kama ulikuwepo miaka hiyo kwa kuwa sehemu husika stori yangu ilivuma sana.

Actual restaurant ilikuwa jirani na jumba la sinema maeneo hayo, sasa hivi pameota ghorofa. Ni mgahawa uliokuwa na harakati nyingi za kisiasa.

Naomba niishie hapo.

James Jason
Baba saa ngapi tena unakuja au tukalale

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mitishamba muhimu babu, nafikiri mizizi niliyokula utotoni athari yake ilionekana kuanzia kidato cha tano 1974. Nilisumbua sana.

Hadi leo hii makali yapo japo panga lilelile za zamani. (Chapa mamba if you know!)

Pia mila mila kama tutakavyoona kwenye stori mbele.
___

Endeleeni kunionesha kuwa mnasoma. Kuuliza ruhsa.

James Jason
Babu shikamoo! Tupo pamoja tulikusubiri kwa hamu
 
Wadau naombeni link ya ule uzi wa kula tunda kimasihara
 
Back
Top Bottom