Uhusiano wangu kimapenzi na "Hamida"

Uhusiano wangu kimapenzi na "Hamida"

1. Wakwe walishatangulia mbele za haki. (Wazazi wa Ruth pia)

2.Unguja nimeshaenda tena na tena hadi Pemba nimefika, tena hadi Konde.

3. Similizi iliishia miaka ya 1980 huko. (84-85). Hivyo kuna maisha yaliendelea baada yake. Napo kuna simulizi za kusisimua, tatizo muda tu wa kuandika na MODs kuvunja moyo wasimuliaji...

4. Kwa atakayesoma post hii napenda ajue kuwa kumbe kweli Rose alishika ujauzito, na ana binti yangu ambaye nimeshawasiliana naye, wanaishi Botswana. Natafakari sijui nilete uzi wa "Hatimaye Rose aniPM JF"?
Mkuu Shikamoo.

Kama Mwenyezi Mungu akakujalia na ukapata muda tunaomba japo kwa kiduchu hii ya Hatimaye Rose ameniPM

Kuna funzo kubwa sana nalipata hapa kupitia hizi simulizo zako.

Asante
 
Shikamoo baba mkubwa (umempita miaka michache baba yangu ) nilianza hii story kutokea kwenye uzi wa rikiboy ila jana usiku nikasoma sehemu zilizobakia huku mpaka usingizi ukanipitia. Nilipoamka nikaendeleza mpaka nimemaliza sijutii muda hata kidogo maana mafunzo niliyopata hapa ni mengi.
Nashukuru Mungu kwa kunifikisha hapa mpaka nikaweza kupata simulizi hii yenye mafunzo mazuri. Nashukuru sana kwa elimu nilioipata inanipa nguvu ya kupambana na changamoto ninazopata za mahusiano na za kifedha.
Nawasilisha
 
1. Nimeulizwa na mmoja wa mdau aliyesoma uzi huu, pm:-

"Je zamani mke ikijulikana hana bikra baada ya ule usiku inakuaje?"

Nimeamua majibu pia niyaweke hapa kwa faida ya wengine.

____

Enzi hizo kuna 'kitu' kilikuwa kinaitwa HARUSI KUJIBU.

Ukisikia harusi imejibu maana yake bibi harusi amekutwa bikra na bwana harusi wakati harusi yenyewe.

Kama harusi HAIJAJIBU maana yake bibi harusi amekutwa hana bikra siku ya ndoa.

Nini hutokea baada ya harusi kutojibu inategemea na bwana harusi ama upande wa bwana harusi watakavyo lichukulia swala hilo kwa uzito upi.

Ikimbukwe kuwa kuna bikra fake pia wakati wa harusi, hii inaweza kutokea bila bwana harusi kujuwa na zipo zinazopangwa akishirikishwa bwana harusi.

Enzi hizo, kama bibi harusi alikuwa hajawahi kuolewa na hakuwa na mtoto na siku ya harusi akakutwa hana bikra, kulikuwa na uwezekano mkubwa wa ndoa kuvunjia kwa baadhi ya maeneo...

Lakini wengine ndoa huendelea lakini thamani ya bibi harusi haitokuwa kama angekutwa na bikra...

Wengine hawakujali huendelea na ndoa kwa thamani ile ile lakini wengi wao ni wale ambao nao walionja kwa bibi harusi mhusika kabla ya ndoa.

Harusi ISIYOJIBU huwa gumzo mtaani kiasi cha kuleta fedheha (enzi hizo)

Harusi ISIPOJIBU, somo wa bibi harusi hupata aibu, ikumbukwe kuwa somo na kungwi kwa mukhtadha huu ni watu wawili tofauti, ingawaje kungwi aweza kuwa huyohuyo ndio somo. Bibi harusi pia huwaibisha wazazi wake na yeye mwenyewe pia.

Aidha, Somo ni yule 'aliyemuokota' kigoli alipovunja ungo, ama yule aliyekabidhiwa amfundishe baada ya 'kuokotwa'

Kuokotwa ni msemo tu wa kwamba 'kuonwa mwanzo'

Yaani, binti alipovunja ungo basi yule mwanamke aliyemuona ama kujuwa kabla ya wengine ndio anakuwa 'amemuokota' na automatically anakuwa somo yake.

Enzi hizo, hata sasa ni fahari sana kwa wazazi pindi wakimuozesha binti yao akiwa bikra.

Kuna siri nzito juu ya kuoa bikra, hili linahitaji uzi wake, maana siku hizi imekuwa siyo ishu tena. Lakini jaribu kuuliza tu walio oa bikra, watakumegea baadhi ya siri hizo.

Nikipata muda nitaanzisha uzi huo.


2. Nimeombwa na wasomaji wapya wa uzi huu niipandishe stori yote kwenye post ya mwanzo ili waisome kwa urahisi.

Nitafanya hivyo, lakini nawasihi pia wapitie uzi wote kwa maana kuna yatokanayo ambako kuna mafunzo mengi yapo ambayo hayapo kwenye simulizi.
 
1. Nimeulizwa na mmoja wa mdau aliyesoma uzi huu, pm:-

"Je zamani mke ikijulikana hana bikra baada ya ule usiku inakuaje?"

Nimeamua majibu pia niyaweke hapa kwa faida ya wengine.

____

Enzi hizo kuna 'kitu' kilikuwa kinaitwa HARUSI KUJIBU.

Ukisikia harusi imejibu maana yake bibi harusi amekutwa bikra na bwana harusi wakati harusi yenyewe.

Kama harusi HAIJAJIBU maana yake bibi harusi amekutwa hana bikra siku ya ndoa.

Nini hutokea baada ya harusi kutojibu inategemea na bwana harusi ama upande wa bwana harusi watakavyo lichukulia swala hilo kwa uzito upi.

Ikimbukwe kuwa kuna bikra fake pia wakati wa harusi, hii inaweza kutokea bila bwana harusi kujuwa na zipo zinazopangwa akishirikishwa bwana harusi.

Enzi hizo, kama bibi harusi alikuwa hajawahi kuolewa na hakuwa na mtoto na siku ya harusi akakutwa hana bikra, kulikuwa na uwezekano mkubwa wa ndoa kuvunjia kwa baadhi ya maeneo...

Lakini wengine ndoa huendelea lakini thamani ya bibi harusi haitokuwa kama angekutwa na bikra...

Wengine hawakujali huendelea na ndoa kwa thamani ile ile lakini wengi wao ni wale ambao nao walionja kwa bibi harusi mhusika kabla ya ndoa.

Harusi ISIYOJIBU huwa gumzo mtaani kiasi cha kuleta fedheha (enzi hizo)

Harusi ISIPOJIBU, somo wa bibi harusi hupata aibu, ikumbukwe kuwa somo na kungwi kwa mukhtadha huu ni watu wawili tofauti, ingawaje kungwi aweza kuwa huyohuyo ndio somo. Bibi harusi pia huwaibisha wazazi wake na yeye mwenyewe pia.

Aidha, Somo ni yule 'aliyemuokota' kigoli alipovunja ungo, ama yule aliyekabidhiwa amfundishe baada ya 'kuokotwa'

Kuokotwa ni msemo tu wa kwamba 'kuonwa mwanzo'

Yaani, binti alipovunja ungo basi yule mwanamke aliyemuona ama kujuwa kabla ya wengine ndio anakuwa 'amemuokota' na automatically anakuwa somo yake.

Enzi hizo, hata sasa ni fahari sana kwa wazazi pindi wakimuozesha binti yao akiwa bikra.

Kuna siri nzito juu ya kuoa bikra, hili linahitaji uzi wake, maana siku hizi imekuwa siyo ishu tena. Lakini jaribu kuuliza tu walio oa bikra, watakumegea baadhi ya siri hizo.

Nikipata muda nitaanzisha uzi huo.


2. Nimeombwa na wasomaji wapya wa uzi huu niipandishe stori yote kwenye post ya mwanzo ili waisome kwa urahisi.

Nitafanya hivyo, lakini nawasihi pia wapitie uzi wote kwa maana kuna yatokanayo ambako kuna mafunzo mengi yapo ambayo hayapo kwenye simulizi.
Kama wanavyosema kuwa wajinga huzeeka,,,naamini pia wenye busara na hekima huzeeka pia,mkuu nakupa hongera sana kwa kuzeeka na hekima zako.
 
SEHEMU YA SABA
*******************

Alarm ya saa ya mezani iliniamsha saa kumi na mbili asubuhi, ndio nikajuwa kuwa nilikunywa kupita kiasi, turntable ilijizima yenyewe (changer), taa sikuzima, na nilishtuka nikiwa sebuleni kwenye kochi.

Kumbe niligigida mzinga wote wa Cognac Brandy. Kichwa kilikuwa kizito, na ilikuwa Jumanne.

Niliamka kujiandaa kwenda kazini.

=

"Habari za asubuhi Marry?" Nilimsalimia mhudumu ofisini kwangu .

"Nzuri boss, karibu" alinijibu huku akipokea mkoba wangu mdogo.

"Leo najisikia vibaya kidogo, hivyo napumzika ofisini kwangu hadi saa nne, baada ya hapo utaruhusu watu kuonana nami" nilimwambia.

"Sawa boss" alijibu huku akiendelea na usafi.

Niliingia ofisini na kukaa kwenye dawati langu huku nimeinama.

"Karibu chai boss" Marry alinistua...

"Oh, ahsante, eeeeh hebu nenda pale mgahawani kaniletee supu maridadi" nilisema huku nikijiweka sawa.

Nikaiangalia ile chai, nikaona haipandi kabisa asubuhi ile. Hivyo nikaanza kupekua mafaili yangu wakati nikisubiri supu, huku nawaza mambo mawili makuu, kusilimu na kuanza kumtongoza Hamida.
******

Haikupita muda mrefu nikaletewa supu ya ng'ombe ya moto safi kabisa, nikainywa na kula nyama, nikaanza kujisikia ahueni.

Niliendelea kufanya kazi kivivu vivu huku nikiwaza mengi kichwani...

Niliwaza jinsi harusi za kwetu utaturuni zinavyokuwa, niliwaza jinsi wanawake wa kitaturu wanavyojuwa kuwanyenyekea wanaume, niliwaza kuhusu sherehe zinavyokuwa, niliwaza msisimko wa nyimbo na hamasa zenye kuamsha hisia kali... Ilimradi niliwaza mambo mengi kuhusiana na mambo ya harusi.

"Kweli sasa nimekua" nilijikuta nasema kwa sauti.

"Vipi boss, leo mbona uko hivyo? siyo kawaida yako!" Marry aliniuliza alipokuja kuchukuwa vyombo pamoja na kuleta mafaili mengine ya kuyapitia...

"Eeeeh, nafikiri muda wangu wa kuoa sasa umewadia" nilimjibu huku nikitabasamu

"Heheeee!" Alicheka kiumbea

"Vipi, huamini?" Nilimuuliza huku natabasamu

"Hapana, naamini ila najiuliza ni nani huyo aliyekukamata hadi umetangaza ndoa" alisema.

"Hapana, sijatangaza ndoa, wala mchumba mwenyewe hajui kama atatongozwa..." Nikasita kidogo kisha nikaendelea...

"Nataka nioe Mwarabu" nilimalizia.

"He!" Alishangaa na kuondoka.
**********

Marry ni mfanyakazi hodari sana, ni Katibu muhtasi wa siku nyingi (nilimkuta kazini) na anapenda sana utendaji wangu.

Huwa namshirikisha mambo yangu mengi, na huwa ananishauri vizuri.

=

Jioni baada ya kutoka kazini moja kwa moja nilielekea kwa Alimaua kumtembelea mzee Katibu Kata.

Nilimkuta ana nafuu sana kuliko juzi yake. Nikamweleza maamuzi niliyofanya ya kuanza kubadili dini na kisha muanza kumpa maneno ya mapenzi mchumba mtarajiwa.

Alifurahia uamuzi wangu wa kuamua kuingia katika 'dini yake', lakini hakuwa na matumaini kama nitafanikiwa kumuoa Hamida kwa jinsi alivyokuwa anazifahamu familia za Kiarabu.
*****

Mzee Burhani ana asili ya Oman, Babu yake alikuja miaka mingi kabla ya uhuru, alikuwa anaishi kisiwani Unguja. Baba yake mzee Burhan marehemu alhaj Ahmed Said alihamia Dar es Salaam katika harakati za kibiashara na yeye mzee Burhani alizaliwa hapo Dar.

Mke wake ni half-cast wa kingazija na kihindi, yaani baba yake alikuwa mgazija na mama yake alikuwa ana asili ya kihindi waliolowea Comoro.

Mchangachiko huo ulitoa matunda mazuri ya watoto wa kike ambaye kitinda mimba wao ndio nafikiria jinsi ya kumuingia na kumtongoza.

Kaka yake Hamida aitwaye Yasir pamoja na rafikiye Abdul wote ni madereva wanaendesha malori (Scania 81). Wiki hiyo magari yao yalikuwa Kibaha (Sub-Scania) kwa ajili ya service kubwa, ndiyo maana walikuwa wanaonekana mjini muda mwingi.

Warda ameolewa na mtoto wa baba yake mdogo, yupo Mwanza, Sabra ameolewa pia na ndugu yao wapo Oman, Yasir bado hajaoa.
********

Tuliongea mengi na mzee Katibu Kata, akanitia moyo japo alikuwa anahisi 'nitagonga mwamba' katika harakati zangu za kumchumbia Hamida.

Nilivyotoka Mwananyamala moja kwa moja nilielekea nyumbani, baada ya kupumzika nilielekea Butiama Restaurant, tayari ilikuwa jioni, nilienda kwa mzee Burahan kurudisha 'coolbox' yao, na kuchukuwa juisi nzuri ya mikomamanga iliyochanganywa na embe ng'ong'o.

Aliyenipokea alikuwa Yasir, kaka yake Hamida, alipokea lile boksi kisha akamwita Hamida apeleke jikoni.

Hamida alivyokuja alinikuta bado nimesimama ukumbini (koridoni)...

"Huingii varandani leo" Hamida aliuliza huku anakuja

"Hapana, leo nina haraka..." Kabla sijaendelea alinikatisha...

"Basi subiri nikuletee juisi" alisema.

"Sawa" nilimjibu.

Punde si punde alirejea dumu la lita 3 lililojaa juisi. Nilipokea na kumlipa, nilijifanya sina stori siku hiyo, nikaaga Nilielekea home.
*******

=

Siku tatu baadaye jioni nilipotoka kazini, ilikuwa siku ijumaa, nilitoka mapema kuliko kawaida yangu...

"Naenda kwenye mawindo ya binti mwarabu" nilisema baada ya kumuaga Marry.

"Haya boss, usinisahau kwenye kamati ya maandalizi..." Alijibu kuhu akitabasamu.

Nikaenda nyumbani moja kwa moja, nikaoga na kubadili nguo, (nilivaa 'bora shoes', suruali ya kitambaa, tshirt nyeupe) nikatoka nikaenda moja kwa moja hadi Africa Studio, nikakuta picha zipo tayari (black & white), zilikuwa zimetoka vizuri mno. Wakaziweka kwenye bahasha (B5) nyeupe, nikamalizia malipo nikaelekea Shibam.

Pale Shibam sikumkuta mzee Burhani, niliwapiga round moja ya kahawa kisha nikaelekea nyumbani kwa mzee Burhani.

Nilikaribishwa vizuri na yule mama wa kiafrika na kuingia sebuleni. Sebule yote nikaibadilisha harufu na kuanza kunukia uturi (perfume) ya Gift of Zanzibar. Ilikuwa inanukia vizuri sana, kama udi hivi lakini siyo, kama asmini hivi lakini siyo, ilimradi ni harufu isiyochosha wala kukera.

Baada ya kusalimiana, nikamkabidhi lile dumu la juisi, halafu nikamwambia kuwa nina shida na mzee.

Akanijibu mzee yupo chumbani kwa Hamida wana mazungumzo na wanawe.

"Kuna posa (ya maneno) imeletwa ndio wanajadili mzee, mama Warda, Hamida na Yasir." Alisema.

Ghafla moyo ukaanza kunidunda kwa nguvu, nadhani hata yule mama aligundua.

"Sawa mama, nasubiri wakimaliza watanikuta" nikamjibu.

"Basi ngoja nikuletee kinywaji chako ukipendacho" alisema huku akiinuka

"Sawa mama" nilijibu.

Aliniletea bilauli iliyojaa togwa baridi, akavuta stuli na kuniwekea.

"Karibu" alinikaribisha.

"Ahsante mama" nilisema kisha nikaweka bahasha yangu kwenye stuli.

Nikaanza kunywa mdogo mdogo huku nikiwa na mawazo.

Akatoa ukimya kwa kuniuliza, imekiwaje nalipenda togwa, nilimjibu nilijifunzia kunywa Iramba ambako ni kinywaji cha kawaida.

Akahoji "wewe nyiramba"
Nikamjibu "hapana"

"Mnyaturu?"
"Hapana"

"Ishi, sasa wewe ni kabila gani?" Aliuliza.

"Mimi ni Mtaturu" nilimjibu

"Ahaaaa, nyie ndio Mang'ati eee" alisema kwa kutania

"Hapana, ila tunashabihiana sana, wote asili yetu ni Ethiopia, lakini mababu zetu walihamia miaka mingi sana maeneo ya Arusha - Manyara (wakati huo Manyara ilikuwa sehemu ya Arusha)

" Ahaaa, ndio mkaanza kuwaibia wamasai ng'ombe zao eeee!" Alitania

Nikacheka kisha nimasema "Hapana, sisi ndiyo tulikuja na mifugo kutoka Ethiopia, babu zetu walikuwa wakibadilishana mifugo na wenyeji kupata ruhusa ya kukaa sehemu kabla ya kufika ardhi waliyoipenda ambapo ni kandokando ya ziwa Eyas. Hivyo zote hizo ni ng'ombe zetu...." Nikacheka tena kisha nikaendelea, "Hata zile za Usukumani ni za kwetu pia" nilitania...

Nilikuwa nadhani yeye ni msukuma kwa lafudhi yake wakati anaongea.

"Unafikiri mie msukuma, mie ni Mnyamwezi" alisema na kucheka kiasi

Nami nikacheka. Hakika aliniondoa kwenye mawazo yaliyotaka kuniteka ghafla.

"Basi togwa hilo ni la Tabora" alisema,

"Mie ndio nimewafundisha humu ndani kulitengeneza, niko nao hawa tangia usichana wangu hadi sasa, kuna wakati niliondoka nikaolewa nikazaa watoto 7, lakini ndoa haikuwa ya furaha sana, nikaomba talaka, ndipo niliporudi hapa hadi sasa." Alisema huku akionesha huzuni kiasi.

"Du, pole sana", nilimwambia, na kumuuliza watoto wake wako wapi.

Alinijibu kuwa wote wapo Tabora kwa baba yao.

Mazungumzo yetu yalikatishwa pale Yasir alipoingia sebuleni, alisalimia na kuketi. Haikupita muda mama Warda naye akaingia, tukasalimiana, kisha akatania "umefuata ice cream na leo?", nikamwambia hapana, leo nina shida nyingine na mzee, mara mzee naye akaingia. Tukasalimiana kisha akasema "samahani, nimekusikia umekuja muda kidogo, lakini tulikuwa tuna mazungumzo ndani, binti yangu ameposwa, lakini hataki kuolewa ndiyo tulikuwa tunayajenga..."

Da! Kimoyomoyo nilifurahi sana, nikaona hii ni dalili njema kwangu, hofu na wasiwasi juu ya kumkosa Hamida ukaniondoka.

"Ahaa, haina neno, mie nilikuwa na mama huyu sikuwa mpweke" nilijibu.

"Naam, twaib, nakusikiliza, au ni faragha niwaombe hawa watuachie nafasi?" Mzee Burhani alisema.

"Hapana, siyo siri, nimekuja naomba unisilimishe, nimeshakata shauri" nilisema.

"Allahu akbar" alisema mzee Burhani.

"Hamidaaaa" mzee Burhani alimuita binti yake.

Mara Hamida akaingia, kimyakimya, macho mekundu, sura imemvimba kama alikuwa analia. Akaketi jirani na yule mama wa kiafrika.

Pakawa na ukimya fulani hivi wa sekunde chache, kisha mzee Burhani akakata ukimya kwa kusema...

".... Eeeh bila shaka nyote mnamfahamu James, wiki iliyopita tulikuwa hapa tunazungumza, alikuja kuomba muongozo akitaka kusilimu. Nilimpa mawili matatu na leo amekata shauri na kutaka kusilimu."

Alitulia kidogo kisha akaendelea...

"Binadamu wote kwa asili tunazaliwa waislamu, lakini wazazi wetu ndio hutubadili dini na kufuata dini nyingine ama kubaki katika dini ya asili ambayo ni uislamu..."

Aliendelea na hotuba isiyo rasmi...

"Uislamu ni Amani, kama lilivyo neno lenyewe, ni kujisalimisha kwa Mola Muumba wa mbingu na nchi na kunyenyekea kwake, hivyo basi umefanya uamuzi sahihi kurejea katika dini ya asili ambayo ina mfumo mzima wa maisha ya mwanadamu wa namna ya kuyaendea mambo yake hapa duniani, kaburini, siku ya ufufuo na hukumu na baada ya hukumu." Alisimama kidogo kumeza mate kisha akaendelea...

"Shahada mbili ni mkusanyiko wa matamko mawili ya ahadi anayoichukua kiumbe (mwanadamu) mbele ya Muumba wake na viumbe wenzake; mbapo mtamkaji hula kiapo cha utii kwa Mwenyezi Mungu (Allah) na Mtume wake katika maisha yake yote kwa kufuata maamrisho na makatazo yake."

"Shahada ya kwanza ni tamko la utii kwa Allah, na shahada ya pili ni tamko la utii wa mtume wa Allah..."

"Sasa nitasema maneno nawe utafuatisha..."

Nikaitikia sawa.

"Nitaanza kusema kwa kiarabu kisha tutarudia kwa kiswahili ili uelewe maana yake" alisema, kisha akaanza kutamka...

Wakati huo wote sebuleni palikuwa kimya, nami namsikiliza mzee Burhani kwa makini huku nikiibia kumuangalia Hamida, alikuwa amejitanda uso wote kwa mtandio kasoro macho tu ambayo yalionekana kuwa mekundu kuliko kawaida.


“ASH-HADU"
Nikafuatisha,
(Ash-hadu)

"AN LAA"
(An-laa)

"ILAAHA"
(Ilaaha)

"ILLAL-LAAHU”
(Illal-laahu)

“WA ASH-HADU"
(Wa ash-hadu)

"ANNA MUHAMMADAN"
(Anna Muhammadan)

"RASUULU LLAH”
(Rasuulu llah)

"NASHUHUDIA KWA MOYO NA KUTAMKA KWA ULIMI KWAMBA"

Nikaendelea kufuatisha...
(Nashuhudiabkwa moyo na kutamka kwa ulimi kwamba)

"HAKUNA MOLA APASWAYE KUABUDIWA KWA HAKI ISIPOKUWA ALLA"
(Hakuna Mola apaswaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allah)

"PIA NASHUHUDIA KWA MOYO NA KUTAMKA KWA ULIMI KWAMBA"
(Pia nashuhudia kwa moyo na kutamka kwa ulimi kwamba"

"MUHAMMADI NI MJUMBE WA ALLAH"
(Muhammad ni mjumbe wa Allah)

"kama alivyo Yesu, Mussa, Ibrahimu" alimalizia kisha wote mle ndani wakasikika wakisema, Allahu akbaru, Allahu akbaru, Mungu ni Mkubwa, Mungu ni Mkubwa.

Walisema maneno hayo (Allahu akbaru) hata kabla sijayafuatisha maneno ya mwisho ya mzee Burhani.

Kisha nikamuona Hamida, Yasir na mama Warda wanalia kwa kutokwa na machozi bila kutoa sauti...

Pakawa na ukimya kidogo...

Nikawa nawaza, hivi hawa wanaolia, wanalia kwa sababu nimesilimu ama kuna jambo jingine!

Nilikuja kujuwa baadaye sana wakati mtu mwingine aliposilimu nikishuhudia, kuna hali fulani ya utii na unyenyekevu wa imani (emotions) hujaa...

"Sasa James umeshakuwa mwislamu, inabidi uchague jina zuri ulipendalo ili uitwe kwa jina hilo" mzee Burhani alitoa ukimya uliokiwepo.

Tayari kichwani nilikuwa nina jina nililolipenda ambalo lilianzia na herifi J kama jina langu.

"Jamaal" nilitamka

"Maa shaa Allah, Jamaal maana yake ni mzuri, wa kupendeza yaani handsome..." Alidakia mzee Burhani.

"Kuanzia sasa tutakuwa tunakuita Jamaal" aliendelea...

"Sasa kuna mambo muhimu ambayo unapaswa kujifunza ili uyajuwe ukishakuwa mwislamu, nitakupatia vitabu ili uweze kujisomea mambo muhimu, yameandikwa kwa kiswahili pia vipo vitabu vya kwa lugha ya kiingereza..." Aliendelea

"Kwakiwa wewe ni mtu mzima, inabidi upate mafunzo ya dini kwa njia tofauti siyo kama watoto wanavyofundishwa, chaguwa siku za kujifunza nami nitakutafutia mwalimu"

Nikamjibu

"Mie nipo tayari siku nne kwa wiki, yaani Jumatatu hadi Alhamis baada ya kutoka kazini nakuwa huru, hivyo nakusikiliza wewe mzee"

"Yasir hebu kalete kile kitabu cha swala na mafundisho / maamrisho yake" mzee Burhani alimwambia kaka yake Hamida

"Naona muda wa swala umewadia, sasa twende wote msikitini" alisema mzee Burhani huku akiwa mwenye furaha.

Mie sikuwa na hofu wala kipingamizi, nilishayavulia nguo maji inabidi niyaoge.

Yasir alirudi na kitabu kidogo kiitwacho Sala na maamrisho yake na kunipatia.

Kwakuwa kilikuwa kidogo sana, nilikiingiza mfukoni mwa suruali.

Mzee Burhani akasimama, nami nikasimama tukatoka tukawa tunaelekea msikitini. Tulielekea msikiti wa Mkauni, siyo mbali kutoka kwa mzee Burhani.

Nyuma yetu Yasir alitufuata, tukawa tunaambatana naye, tulivyofika msikitini, tukavua viatu kama kawaida, tukavi hifadhi sehemu ya kuhifadhia, kisha mzee Burhani akamwambia Yasir anifunidhe namna ya kuchukuwa udhu ili niwe tayari kwa ibada ya swala.

Yasir alinielekeza msalani, baada ya kutoka msalani akanipeleka sehemu maalum ya kutawadhia (kuchukuwa udhu), yaani kuosha viganja vya mikono, kusukutua, kusafisha pua, uso, mikono yenyewe hadi viwikoni, kupaka maji kwenye kichwa na masikio kisha kumalizia na kuosha miguu.

Nilifanya kwa kumuigiza afanyavyo, tulipokuwa tayari tuliingia ndani tayari kwa ibada...

Baada ya kuswali (inachukuwa dakika tano hivi) nikasikia tangazo...

"Kuna kijana amesilimu, alikuwa akiitwa James Jasson na sasa ataitwa Jamaal Jason, alikuwa dhehebu la Roman Catholic, tunamuomba asimame ili waislamu tumuone tumjue kuwa ni ndugu yetu katika imani"

Ni imamu (kiongozi wa ibada) alikuwa akitangaza.

Wakati nainuka nilisikia Allahu akaru nyingi hadi nilisisimkwa mwili, nikaombewa dua, kishwa waumini wakaambia wawe wananisaidia katika mambo ya ibada na kadha wa kadha.

Baada ya tasbihi (kama kusoma rozali vile) na dua, watu walianza kutoka, mzee Burhani alikuwa anaongea na Imamu, bila shaka ndiye aliyempa taarifa za kusilimu kwangu.

Kisha nikaona mzee Burhani amesimama tena peke yake akawa anaswali.

Mie na Yasir tukatoka nje tukawa tunamsubiri.

"Eti, mbona nilimuona Hamida akilia, kulikoni" niliuliza kiuchokozi

"Aaaa ni stori ndefu nitakuhadithia kesho in shaa Allah" alijibu kifupi namna hiyo, na mara mzee Burhani akawa anatoka nje.

Tulirudi wote hadi nyumbani kwa mzee Burhani, lakini sikuingia ndani, bali niliagana nao nikapanda batavuz yangu huyooo hadi Butiama restaurant, kisha nyumbani.
**********

Nilivyofika nyumbani nilikipitia kile kitabu na kuona yaliyoandikwa, ni kitabu kidogo sana unachoweza kusoma kwa saa chache tu.

Nilikuta misamiati mingi ambayo sikujuwa maana yake mara moja, lakini kilikuwa kinaeleweka vizuri tu.

Baada ya kujimwagia maji na kujifuta, nikajilaza kitandani chalichali nikiwa nimevaa bukta huku nikitafakari safari ambayo nimeianza.

Nikawa nawaza, hapa pombe tena basi, kuzini tena basi nk hadi nikapitiwa na usingizi.
********

Sikwenda sinema ijumaa hiyo kama ilivyo kawaida yangu. Kesho yake mapema sana nikaenda kwa mzee Katibu Kata, niliwahi ili asije kuondoka nyumbani kabla.

Nilimueleza habari yote ya kusilimu kwangu, akafurahi sana, tukabadilishana maneno mawili matatu kisha nikamuaga huyooo hadi nyumbani.

Niliendelea na shughuli ya usafi hadi niliposikia adhana, nikaacha, nikajitayarisha kwenda msikitini. Kutoka nyumbani hadi msikiti wa mkauni ni mbali kidogo kwa kutembea kwa miguu, hivyo niliwasha batavuz nikaenda.

Nikifuata utaratibu kama wa jana usiku hadi ibada ilipoisha nikatoka na kuelekea Butiama. Hakika Butiama Restaurant nimewachangia sana!

Baada ya hapo nilirudi nyumbani kumalizia usafi na mambo mengine.
****

Saa kumi baada ya swala ya alasiri nilienda Shibamu, siku za Jumamosi watu huwa wengi wakijiburudisha kwa michezo mbalimbali.

Mara mzee Burhani akawasili...

"Ahaaaa sheikh Jamaal, upo?" Alisema baada ya kusalimia watu waliokuwepo pale...

"Jamani eee, kuanzia jana huyu James sasa tumuite Jamaal, amesilimu." Alisema

Allahu akbaru, watu waliokiwepo pale walisema maneno hayo kwa kurudia mara tatu.

"Karibu sana Jamaal" mzee mmoja maarufu sana kijiweni hapo alisema.

Mzee Burhani akaniambia, mwalimu wako wa awali atakuwa mwanangu Yasir, wiki hizi mbili yupo tu anasubiri gari iwe tayari, iko service kubwa.

Sasa basi Jumatatu utaanza naye hadi atakapoondoka kisha nitakuwa nimeshapata mwalimu utakaye endana naye kukusomesha mambo muhimu.

Tuliongea palee hadi magharibi ilipofika, baada ya swala akanikaribisha kwake kwa chakula cha usiku.

"Umri wako unaruhusu kuoa, utakula hotelini mpaka lini" alitania

"Bado natafuta mke muafaka" nilijibu...

Tuliendelea na mazungumzo ya dini hadi ilipowadia muda wa swala ya isha. (Swala ya saa mbili usiku)

Baada ya kuswali, tulirudi nyumbani kwa ajili ya chakula cha usiku.
*****

Sebuleni kuliandaliwa chakula kizuri sana, kulikuwepo viazi mbatata (viazi mviringo), sijui hata wamevifanyaje, maana ni vilaini pia vina kama mbogamboga (nilijuwa baadaye kuwa ni kachori), mchuzi wa nyama ya ng'ombe pamoja na nyama yenyewe, chapati maridadi sana, sikuwahi kuziona kama hizo kabla, wali uliopikwa kwa nazi, mchuzi shatashata wa kamba / kaji (prowns), chai ya maziwa na ya mkandaa (black tea), kisamvu kilichokolea nazi.... Bila kusahau pembeni kulikuwa na jagi la maji ya kunywa.

Mtihani ukawa namna ya kukunja miguu wakati wa kula maana pameandaliwa kwenye busati juu yake paliwekwa mkeka.

Baada ya kujikunja vizuri nikifanikiwa kukaa ipasavyo, ni mkao unaoweza kukaa hivyo kwa muda mrefu bila kuchoka (miguu inakunjwa kwa kupishana kama unaikalia lakini huikalii)

Kwa kuwa sebule ilikuwa kubwa sana, kuliandaliwa sehemu mbili, jirani na pazia la mlango walikaa mama wa Kiafrika, Hamida, Nadya na mama Warda, na upande mwingine tulikuwa mimi, Yasir na mzee Burhani.

Mie nilikaa kwa namna ambayo nilikuwa naangakiana uso kwa uso na Hamida japo kuna ka-umbali hivi.

Nilishazoea kula kwa kijiko, leo najifunza kula kwa mikono, nilisema hivyo wakati Yasir akinimwagilia maji ya kunawa...

"Utaweza tu Jamaal" alijibu.

Sikutaka kuanza kula wali kwa kuwa nimeshauzoea, nilianza kula chapati kwa mchuzi na chai, [emoji39] Hakika kuna watu wanajuwa kupika jamani... Nilijikuta nasema tu kwa sauti...

Nilivyomaliza chapati moja nikahamia kwenye kachori, dah, tamu sana, zina pilipili kwa mbaali, mwisho nikapakuwa 'tuwali' kiduchu ili nimalizie, loh salaleh, kumbe bwana ule wali ndio funga kazi, nikaongeza mwingine mwingi...

Mchuzi wake sasa na prouwns waliokaangwa na kumenywa kisha kuungwa kwa nazi nzito, acha kabisa..., utamu wa kisamvu sijawahi kula popote pale... (Kilitwangwa jana yake na kuchemshwa kwa viungo muafaka, leo ndio kimeungwa vizuri kwa nazi, hii aliniambia Hamida siku nyingine kabisa nilivyomuuliza)
*****

Baada ya kula, tukawa tunazungumza mambo ya kawaida, hali ya uchumi wa nchi, kupungua kwa bidhaa muhimu nk

Wakati huo Hamida alikuwa bize akiondosha vyombo...

Aliporudi alikuja na bahasha yangu niliyoishau jana (kwa makusudi)

"Jana ulisahau mzigo wako" Hamida alisema huku akinipatia bahasha ambayo tangia awali sikuwa nimeifunga kwa lengo maalum.

"Ooh, ahsante, nilishasahau kama zipo hapa" nilijibu

Lengo langu lilikuwa Hamida anione vizuri kwakuwa mara zote niwapo hapo huniangalia kwa kuibia ibia tu.
*******

Niliaga, Yasir akaniambia ngoja nikusindikize....

Nilikokota batavuz huku tukielekea maeneo ya Shabam kutokea nyumbani kwa akina Hamida...

Njiani wakati tunaongea mawili matatu ndipo nikachomekea kuhusu kulia kwa Hamida...

Akanieleza kuhusu posa iliyokuja kutoka Oman, na kwamba muoaji alikuwa mtu mzima sana lakini tajiri... Hamida alikuwa hataki kuolewa na mtu mzima hivyo walikuwa wanajaribu kumsihi akubali kwani ndiyo posa ya kwanza na umri wake ulikuwa umewadia kuolewa...

Hamida alimaliza kidato cha nne miaka miwili iliyopita kisha akaenda Kenya kusomea stashahada ya domestic science na catering (Kenya Utalii College - Campas ya Mombasa).

"Du" nilisema
"Lakini yafaa apewe uhuru wa kuchaguwa ampendaye, kama hamtaki msimlazimishe, asije akachukuwa maamuzi mabaya" nilisema

Kipindi hicho mabinti kuzaga chupa na kumeza kwa ajili ya kujiua ilikuwa tabia iliyoshamiri sana.

Tuliagana yeye akarudi na mie nikapanda batavuz yangu hadi home nikiwa na furaha sana kwa kupiga hatua nyingine kwenda 'mbele'.
*******

ItaendeleaView attachment 1343282View attachment 1343283View attachment 1343284

James Jason
Chief.. huyu Marry hakumla kimasikhara maana ule ufundi wa kile kitabu cha mzungu ulikuwa umekolea [emoji3]
 
SEHEMU YA 11
*************

[Picha zote ni kwa hisani ya google, hazina uhusiano wa moja kwa moja na simulizi hii. Majina yaliyotumika si halisi, bali majina machache sana kwa sababu maalum. Hii ni simulizi ya kweli lakini imeongezwa chumvi kidogo na maji kidogo sehemu nyingine ili kukidhi ladha ya usomaji na kupunguza uhalisia]
*****************
=

Siku hazigandi, mara Ijumaa hii hapa nipo kazini na muda wa kufunga ofisi imekaribia...

Nilimuaga Marry na kutoka na Batavuz yangu. Sikuwa napenda kwenda na gari ofisini.

Wiki hiyo yote nilikuwa namuhadithia Marry maendeleo ya mimi na Hamida, akawa ananiambia kweli umedhamiria...

"Atakuweza kweli na nanihii lako kubwa hivyo!" Alisema huku sasa akiwa anaamini kabisa nipo serious kuhusu Hamida.

"Maana mie mwenyewe niliweza kwa tabu japo nimezaa watoto wawili tena kwa kusukuma, lakini shughuli niliipata..."

Aliendelea kusema huku akionesha dalili za kutamani tena. Zaidi ya siku ishirini sasa sijapata msichana wa kustarehe naye, nami wala sikuwa na 'moto' zaidi ya kumuwaza Hamida.
***

Jumatatu ya wiki hiyo baada ya kuripoti afisini, nilitoka kuelekea peugeot house, nilionana na afisa mhusika na akaniambia yanayopaswa kufanywa ili kukamikisha utaratibu wa kiforodha na kibiashara kwa upande wao.

Kesho yake taratibu zote zikikamilika, nikapewa kadi ya gari (ilikuwa ya rangi ya orange iliyokolea, kadi ilikuwa ya kukunja mara moja.)

Niliwafuata maafisa wa bima makao makuu kwa ajili ya kupatiwa bima kubwa. Nilikamilisha siku hiyo hiyo na kuitoa gari yangu.

=

Mwaka 1976 baada ya kutoka NMC kabla sijaingia RTC nilipata mafunzo ya udereva mkoa wa Tanga (Tanga Driving School), wakati huo kilikuwa chuo bora sana, sijui kama bado kipo au kilichakufa.., nilipata cheti cha umahiri (CC) baada ya majaribio ya nadharia na vitendo nilivyofanyiwa na afisa mkaguzi msaidizi (Assistant Inspector) wa Polisi. Tulitumia Landrover 109 na baadaye alinijaribu kwa pikipiki ya Polisi kwa umbali mfupi.

Hivyo sikuhitaji usaidizi wa dereva mwingine, niliitoa gari pale na kuchukuwa njia ya Bibi titi (sasa) na kupinda kulia kufuata barabara ya Morogoro, huyoo mdogo mdogo hadi nyumbani.

Miaka hiyo usalama ulikuwa mkubwa sana, watu wengi walikuwa wanapaki magari yao nje ya nyumba zao usiku kucha bila hofu wala wasiwasi. Nami nilikuwa naipaki nje ya nyumba lakini pia bahati nzuri kwa jinsi nyumba zile zilivyojengwa kulikuwa na nafasi kubwa kutoka njia ya mtaa hadi kuufikia mlango wa mbele wa nyumba.
***

Ratiba yangu ya mwisho wa juma hili Marry alikuwa anaijuwa yote kwa kuwa nilimshirikisha.

=

Nilifika nyumbani, kabla sijaingia ndani nilifungua mlango wa gari na kuiwasha (baada ya ukaguzi wa kawaida), kwa kuwa asubuhi nilichelewa kuamka hivyo sikuiwasha.

Nikaingia ndani huku gari inaunguruma nje. Ilikuwa pijo ya kisasa wakati huo, ilikuwa na 'staff gear lever', yaani ile gia liva ya kwenye usukani pembeni. Ilikuwa inatumia petroli supa, ilikuwa inatumia kitu kinaitwa distributor, pistoni nne, cc 1,796 , gia nne ya tano 'rivas'

Nikawa naendelea kupitia user's manual, ambayo nimekuwa nikiipitia tangia Jumanne kila siku jioni baada ya kutoka madrasa (isiyo rasmi) kwa akina Hamida.

Baada kama ya dakika thelethini hivi niliona tayari inatosha niliamua kwenda kuizima.

Baada ya kuizima kabla sijaingia ndani naona Marry huyu hapa anakuja...

"Karibu" nilisema huku nikiwa nawaza kuna kitu gani kimetokea, maana si kawaida yake kuja kwangu bila kunijulisha.

"Karibu sana" nilisema tena huku nikifungua mlango wa nyumba.

"Nimekuja kuiangalia kwa karibu pijo yako" alisema kwa kutania.

"Aaaaah, hiyo hapo, mwari mpya kabisa" nilisema kwa kulisifia gari.

Hii ilikuwa ni mara ya nne kwa Marry kufika nyumbani, mara ya kwanza ilikuwa kwa nia ya kupafahamu, mara ya pili ilikuwa kwa kunielezea matatizo ya nyumbani kwake (ndoa), mara ya tatu tulikuja wote kwa ajili ya 'one night stand'. Tulikubaliana tusirudie tena.
***

Aliketi kwenye kochi (yale ya mninga na cussion), mimi nikaenda kwenye friji nikamtolea pilsiner (ndio nilikuwa namaliIa bia za mwisho zilizokiwepo home, ila Brand bado zilikuwepo chupa kadhaa ambazo nilikuwa nazipata kule mtaa wa Mkwepu / Jamuhuri. Nilikuwa napenda Cognac kwa sababu ndiyo niliyo jifundishia kunywa nikiwa Uingereza.

"Karibu Marry" nilisema huku nikimmiminia pombe kwenye bilauli (hosco brand)

"Ahasate" alisema na kukaa kimya.

Mie kwa kuwa baadaye nilitaka kwenda kwa akina hamida kumfikishia memo niliyoiandaa, sikunywa pombe, bali nilimalizia juisi ambayo nilikuja nayo jana kutoka kwa mama Warda.

"Mbona wewe hunywi" aliuliza Marry

"Si nilikuambia mimi nimeanza kuacha, nimesilimu hivyo wewe enjoy, ukiweza beba zote hizi uende nazo (zilibakia kama tano hivi kwenye friji)

"Hahahhah, yani hadi pombe umeacha! We kiboko! Hamida anakupeleka puta eee"

Alisema kilevilevi, maana Marry ni mbovu kwa pombe, bia mbili tu anachangamka.

"Ukisikia mwisho wa reli basi ndio pale, Hamida nadhani ndio itakuwa 'Kigoma yangu'

Nilisema huku nikionesha msisitizo.

" Enhe, kulikoni umekuja bila taarifa badala ya kumuwahi Mangi nyumbani?" Nilimuuliza huku nikichagiza

"Mmhhh!"
Alishusha pumzi kisha akaendelea

"Mwezi wa tatu huu sasa tangia nipate haki yangu ya ndoa, tena mara ya mwisho wala sikufika, nguvu zake zinazidi kupungua na kisukari nacho kinazidi kumkondesha"
Alisema kisha akachukuwa chupa na kumimina bia kwenye glasi yake.

Mume wa Marry alipata maradhi ya kisukari kiasi ya kumsababishia upungufu wa nguvu za kiume, kukawa na mgogoro sana kwenye ndoa yake, bado anaendelea na dawa za kila siku huku akihudhuria kliniki.

"Leo nimezidiwa, ndio maana nimekuja ili unisaidie, maana hata wewe wajuwa kuwa mimi si malaya na sipendi kuanzisha uhusiano na mwanamume mwingine bora wewe ulinisaidia siku ile basi nakuomba na leo tafadhali nimezidiwa"

Alisema huku akilegeza macho kwa ulevi na nye*ge.

"Marry Hapana, si tulikubaliana kuwa ni mara moja tu siku ile na nilikutimizia!!, mie nimebadilika siku hizi, siyo kito*mbi kama zamani, nilifikiri umekuja na jambo muhimu la kikazi kumbe...."

Akanikatisha

"Tafadhali Boss, hebu angalia..."

Akajipekenyua na kuingiza vidole viwili, kisha akatoa ulendaulenda (ule ute transparent mzito unaoteleza na usiokatika haraka)

Macho hayana pazia, kitumbua nikakiona kilivyotuna, mashavu ya papuchi yaleee, amenyoa fresh, lakini huu ute si yupo heat period huyu! Nikiwaza kimya kimya faster.

"Ona nilivyo" alinionesha tena baada ya kuingiza vidole tena.

Moyoni nikawa na mawazo mkingamo, nina ukame wa karibu wiki tatu, lakini nilitaka nimuwekee Hamida, mara mawazo ya kishetani yakanijia (yani sina shaka hapa ni Shetani kabisa alini-push)

"Aaah, kwanza Hamida ni bikira kama anasema kweli, siku ya kumpata atasumbua sana ninaweza kujichafua hata kabla sijamuingilia na hamu ikapungua, ngoja nizipunguze kwa huyu..."

Niliwaza haraka haraka kisha nikamuuliza...

"Wewe si upo danger period?"

"Ndiyo, lakini ninatumia majivu tangu juzi na pia nitameza pills just incase" alijibu kwa kujihamini.

"Okay, basi nenda kaoge"

Nilisema huku nikiinuka na kuzitoa chupa za bia na glasi pale mezani na kuzipeleka jikoni.

Nyumba ina vyumba viwili vikubwa, vyote havina vyoo vya ndani, lakini bafu na choo pia vipo ndani kama unaelekea nje kwa mlango wa nyuma.

Aliingia chumba kingine (tulichokitumia mara ya mwisho) kwa ajili ya kubadilisha nguo aende kuoga.
**

=

Saa moja na nusu jioni nilikuwa tayari niko safi na fresh kutoka. Nilimsindikiza Marry hadi kwao Mabibo (mabwawa 7, siku hizi wanapaita 'beach' ama maji machafu), kisha nikarudi moja kwa moja hadi kwa mzee Burhani.

Nikapaki gari nje, nikabisha hodi.

"Nimeleta dumu hili" nilimuambia Hamida huku nikimpatia dumu pamoja na ile memo kama ambavyo tumekuwa tukipeana. Kisha nikamuaga na kumwambia awasalimie ndani maana nina haraka kuna sehemu naenda.

Huyoo nikatoka hadi Moroco, kisha nikachukuwa njia ya kwenda mjini (Ali Hassan Mwinyi rd), vuuuu hadi ikafika 60kph, nikapita taa za kuongozea mahari za Namanga nikiwa 80kph, vuuuuuu hadi taa za Ohio/Bibi titi nikiwa nimebalansi 80kph, vuuuu hadi taa za Nkruma / Lumumba, bado nipo 80kph, vuuuu hadi taa za Tazara, 80kph bado, vuuuu hadi Airport. Nikazunguka kugeuza (ilikuwa terminal one wakati huo) na kurudi kwa mtindo ule ule...

Kuna rafiki yangu wa kisingasinga aliwahi kuniambia kuwa hizi taa kutokea airpot hadi Moroco kama ukipita kwa spidi ya 80kph, utapita taa zote zikiwa kijani kama taa za awali ulipita kwa spidi hiyo...

Niliwahi kujaribu kwa batavuz lakini sikufanikisha kwa sababu ya uwezo wake, hivyo siku hiyo nilipata fursa ya kujaribu na nili-prove kuwa ni kweli.

Nilirudi hadi nyumbani na kupumzika. Sikwenda kuangalia sinema, nilitaka kupumzika baada ya kumsaidia Marry ipasavyo.
***
=

"Tafadhali, fanya ufanyavyo kesho asubuhi uje tumalizie mazungumzo yetu, muhimu sana, usikose"

Hiyo ndiyo nilikuwa memo niliyomuandikia Hamida na kumpatia kabla sijaenda kufanya fujo barabarani kuelekea airport.

Nilipumzika chumbani huku nikiwaza, je Hamida atafanikiwa kuja? Kama akija nimshauri nini au nimuambie nini?

Nikawa nawaza weee mara taa ya idea mpya ikawaka [emoji362]

Roho ikatulia nikaanza kutafuta usingizi. Zile pilsner nne zilizobakia nilimpatia Marry. Kwenye kabati nilibakiwa na chupa tatu ya brand.
******

Baada ya kutoka kumsindikiza Hamida kwa shangazi yake Jumpili iliyopita, Jumatatu nilihudhuria kipindi kwa mzee Burhani kama kawaida.

Mwalimu maalum bado alikuwa hajapatikana hivyo Hamida aliendelea kunifundisha.

Alianza kunifundisha kusoma baadhi ya 'sura' katika juzuu ili nizitumie katika ibada ya swala.

Niliipenda sana 'suratil fatha', maana niliona kama inafanana na sala ya Baba yetu uliye Mbinguni...

Aliniambia kuwa suratil fatha (maarufu kama alhamdu) ni sura ya ufunguzi katika Qur'an. Ndiyo sura ya mwanzo kabisa katika msahafu. Ikisomwa mara moja kwa dhati kabisa inakuwa na uzito kuliko sura nyingine zote zilizobakia kwa pamoja. Ni sura ambayo ibada ya swala haikamiliki bila kusomwa, hivyo alinisistizia sana niijuwe kwa kuihifadhi moyoni (kukariri)

Siku hiyo Jumatatu alianza kwa kunikaririsha aya nne za mwazo. Nilizihifadhi haraka tu, akanikazania nizurudie rudie akiwa ameniacha peke yangu...

Kwakuwa mashuleni na vyuoni tulishazoea ‘kumeza’ maandishi, haikuwa tabu kwangu kumeza sura ile kwa siku ile moja kwa saa chache nilizo kaa pale...

Ila nilikuwa nafanya ujanja, nasoma aya nne za mwanzo kwa sauti kisha zilizofuata nasoma kimya kimya.

Aliporudi alitaka anisikilize kama nimehifadhi zile aya nne.

Nikazisoma, akafurahi.

Kumbuka katika kukaa, yeye anakaa kulia kwangu halafu kwa nyuma kidogo, hivyo nilikuwa simfaidi sana. Na hata mie wakati huo sikuwa mwenye papara ya kuonesha ubazazi. Nilikuwa mwanfunzi mtulivu kwelikweli.

"Iyaaka na'abudu wa iyaaka na stai'n" alianza kusoma aya ya tano na kunitaka niisome.

"Maana yake nini" nilimuuliza

"Ni wewe tunakuabudu na ni wewe tunakuomba msaada" alijibu kisha akasisitiza nihifadhi kwanza kwakuwa mzee Burhani alisema kwa kuwa naendelea vizuri ataniletea msahafu wa tafsiri ya Kiswahili cha Sheikh Abdullah Saleh Farsi.

Nikaanza kusoma aya ya tano hadi mwisho!

Akashangaa sana, nikamwambia nimeshahifadhi. Akafurahi kisha akaniambia nisome kuanzia mwanzo hadi mwisho, nikaanza kusoma na akawa yeye anasoma kwa tafsiri yake:-

1. Kwa jina la Mwenyezi Mungu, mwingi wa Rehema, mwenye kurehemu,

2. Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, Mola mlezi wa viumbe vyote,

3. Mwingi wa Rehema, mwenye kurehemu,

4. Mwenye kumiliki siku ya malipo,

5. Wewe tu tunakuabudu, na wewe tu tunakuomba msaada,

6. Tuongoze njia iliyo nyooka,

7. Njia ya ulio waneemesha, siyo ya walio kasirikiwa, wala walio ghadhibikiwa (waliopotea)

Amin.
***

Alinifundisha hivyo japo tafsiri sikuhifadhi yote siku hiyo. Katika kukaa naye sikugusia habari za kwa aunt yake hata kidogo.
***

Siku ya Jumanne niliendelea na masomo, nikafanikiwa kuhifadhi tafsiri ya surat'l fatha.

Taarifa zikamfikia mzee Burhani, Jumatano baba yake Hamida aliniletea msahafu wa kijani wenye kiarabu na tafsiri ya kiswahili, nilifurahi sana na bila shaka mzee Burhani alikuwa anafurahia maendeleo yangu.

Siku hiyo Hamida alianza kunifundisha sura tatu za mwisho katika Qur'an tukufu, yaani surat'l Ikhlaas, surat'l Falaq na surat' Nnaas. (Sura ya 112, Sura ya 113 na Sura ya 114). Hivyo Qur’an ina Sura 114 tu.

Hadi kufikia alhamisi tayari nilikuwa nimeshaweza kuzisoma na kuzihifadhi, ila tafsiri nikawa najisomea nyumbani, kisha kupata ufafanuzi kwa Hamida.
***

Asubuhi niliamka mapema sana na kuanza kufanya usafi wa mazingira nje, kisha ndani, hadi kufikia saa mbili asubuhi nilikuwa tayari kwenda kuoga.

Mara ghafla mawazo ya jinsi nilivyo mtekelezea haja yake Marry yakanijia...

Hakika ilikuwa 'show ya kibabe' maana nilipiga mashine hadi alisema tayari nimeshamtoa ny*ege zote. Kwa kuwa sikuwa na mzuka naye sana, wazungu walikuwa wanachelewa kuja, jambo ambalo kwa upande wake ilikuwa faida na kumfanya 'afike' mara kadhaa. Bao zangu mbili tu zilimtosha.

Mara mawazo ya ujio wa Hamida yakaja, nikachukuwa mafuta ya kupikia (supa-ghee), nikaandaa mayai, nikaandaa vitunguu, pilipili mboga, chumvi, pilipili zile ndefu za kijani pia, carot, bila kusahau chupa ya cognac.

Katika ile memo niliyompajia jana, sikutaja muda wa yeye kuja maana sikujuwa mchakato wa kupata ruhusa ungekuwaje.

Kwangu hakuwahi kufika, lakini katika mazungumzo ya kila siku niliwahi kumuelekeza, na sasa ataona alama ya gari yangu nje na pia akiulizia kwa majirani ataelekezwa.

Nafasi yangu RTC ilinifanya nijulikane na watu wengi japo mie wengine sikuwafahamu.

Nikatoka kwa miguu kwenda duka la ushirika la jirani na kununua mkate wa siha. Tanbond na zesta red-palm jam zilikuwepo nyumbani.

Niliharakisha ili niwahi isije ikatokea Hamida amefika mie sipo.

Saa tatu na nusu bado bila bila, sioni dalili ya Hamida. Nikataka nikoroge simu nipige nyumbani kwao lakini roho ikasita. Nikajipa moyo kwamba atakuja tu kama ana nia kweli ya ushauri wangu, Jamaal mwenye busara [emoji4] nilijisemea na kutabasamu.

Saa nne asubuhi njaa ikaanza kuniuma, nikaanza kutengeneza chai. Majani ya chai ya wakati ule yalikuwa mazuri sana, Green-Lebel, chai ilivyokuwa tayari niliiweka kwenye chupa ya chai (thermos) iliyosalia kwenye surufia nilimimina kwenye kikombe, nikaweka maziwa (B&B condensed milk) kisha nikaanza kupooza njaa.

Awali nilikuwa nataka akija tunywe wote chai, kama akija mchana tule wote ili mradi wakati wa maongezi tuwe tunakula.

Nilivyomaliza kunywa chai, tano kasoro hiyo, si Simba wala Yanga, nikaenda kwenye meza ya music system, nikaangalia angalia santuri kisha nikachukuwa santuri mbili, moja ya Kenny Roggers na nyingine ya Bob Marley.

Nikaiweka ya Bob, Legend Colletion, ya Kenny ilikuwa nimeinasisha kwa juu (standby), Bob akaanza kuimba taratiiibu huku mie moyo kila mara unanilipuka kwa kuhisi Hamida anakuja...

Nyimbo zile za Bob na chai niliyokunywa zikanifanya nisinzie...
***

"Ngongongo" nilisikia sauti ya mlango ukigongwa

"Karibu" Nilijibu kwa sauti nzito ya kuzinduka usingizini

Nikainuka na kwenda kufungua mlango

"Karibu Hamida" nimwambia.

"Ahsante" alijibu huku akivua sandals zake na kuingia. Mie nikazichukuwa na kuziingiza ndani nikaziweka kwenye ‘rack’ ya viatu.

"Karibu uketi" nilisema huku nimwonesha kochi lililo kaa angle nzuri.

"Karibu sana Hamida, hapa ndiyo nyumbani." Nilimwambia kwa kujiamini, na kweli palikuwa pametulia, yaani pameenea kasoro mke tu, na leo ndio namuona huyu hapa kwangu japo hajui chochote kuhusu mimi kumtaka kimapenzi sembuse kumposa na kumuoa.

Mkononi alikuwa ameshika kikapu kidogo, ndani yake ameweka pochi yake kubwa ya rangi sawa na gauni, amevaa gauni la light blue, ushungi wake wa kadri mweupe, ananukia vizuri ili mradi kila sifa ya mwanamke mrembo naiona kwake. (Kupenda buana!)

"Kumbe unapenda nyimbo za Bob Marley" alisema.

Wakati huo wimbo uitwao "stir it up" ulikuwa ukiimba (ukicheza)

"Yes, mie napenda miziki, hasa yenye jumbe nzuri, Bob nyimbo zake zina maana na hisia kali sana.
***

Hakika wimbo huo ulicheza muda muafaka, maana lyrics zake ni mahaba tosha, hebu angalia:-

Stir it up, little darlin', stir it up.

Come on, baby
Come on and stir it up, little darlin', stir it up. O-oh!

It's been a long, long time, yeah! (Stir it, stir it, stir it together)

Since I've got you on my mind (oh-oh-oh-oh) Oh-oh!

Now you are here (stir it, stir it, stir it together), I said,

It's so clear
To see what we could do, baby, (oh-oh-oh-oh)
Just me and you

Come on and stir it up, little darlin'!
Stir it up, come on, baby!
Come on and stir it up, yeah!
Little darlin', stir it up! O-oh!

I'll push the wood (stir it, stir it, stir it together)

Then I blaze ya fire
Then I'll satisfy your heart's desire. (Oh-oh-oh-oh)

Said, I stir it together (stir it, stir it, stir it together)

Every minute
All you got to do, baby, (oh-oh-oh-oh)
Is keep it in, and oh…
********



*******

=

Wakati huo wimbo ndio ulikuwa unaishia...

"Ngoja ni rewind uusikilize vizuri" nilisema huku tayari nimesha nyanyuka na kurudisha nyuma kidogo ukaanza upya kuimba [emoji443]

"Eee ngoja nikuandalie chochote jikoni..."
Nilisema,

"Hapana mie nimeshakula nyumbani" alijibu kwa kunikatisha

"Hapana, umekula kwenu, ngoja nikioneshe nami ukarimu wangu" nikaingika jikoni.

Nilikiwa na jiko la umeme (TANALEC) sahani mbili (two plates), nikawasha, na kuweka kikaangio (kikaago) kipate moto, nikaweka mafuta (supa-ghee) yakaanza kuyeyuka, kisha nikaweka vitunguu kiasi, nikawa napiga (koroga) mayai matano, vitunguu vilipokuwa brown kidogo nikaweka kwenye kikaangio mchanganyiko wa mayai, chumvi kiasi, vitunguu vingine, carot, pilipili ndefu na hoho...

Kabla ya kuiva nikaongeza drops kadhaa za brand, kisha nikakunja (half circle) na kukandamiza na kijiko cha kukaangia...

Nikageuza kisha nikakandamiza tena ikiwa vivyo hivyo nusu duara.

Nilisubiri ikaiva vizuri nikaipua na kuiweka katika sahani flat ya udongo, nikapeleka alipo Hamida.

Nikaleta thermos yenye chai, na vikombe viwili, asali, sukari jam, maziwa ya kopo (ya maji mazito) pamoja na tanbond. Kisha nikaleta sles sita za mkate wa siha.

Hamida ametulia tu.

"Karibu Hamida " nilisema huku nikimpatia maji ya kunawa. Akanawa bila kusema kitu.

Nikamuuliza unapenda chai ya rangi au ya maziwa, akajibu ya maziwa, nikamuwekea kwa kikombe chake maziwa kidogo (kiduchu), kisha nikamimina chai, na kumuambia, onja sukari maana hayo maziwa yana sukari, kisha nikamwambia ukitaka asali hiyo hapo na sukari hiyo hapo.

Mie nikawa napaka jam na tanbond kwenye slesi za mikate, nilipaka slesi nne tu, mbili jam na mbili tanbond kisha nikazigawa nusu (mshazali) na kuwa vipande vinne viwili vilivyoshikana kwa kila mtu.

Nami nikakoroga chai ya rangi tukaanza kunywa.

"Kumbe nawe ni mpishi mzuri hivi!?" Alisema alipoonja sehemu ya yai...

"Halafu yana ladha nzuri, umeweka nini humu?" Aliuliza huku akiongeza kipande kingine kikubwa.

"Nimeweka libwata la kukufanya kila jumamosi na jumapili uje kunywa chai hapa, hahahaha" nilijibu kwa kutania na kukwepa swali lake la msingi.

Tuliendelea kunywa na maongezi ya hapa na pale, mziki ulikuwa unaendelea kuimba na safari hii santuri ilianguka ile ya Kenny Roggers... Wimbo "Lady"
******



*******

"Lady"

Lady, I'm your knight in shining armor and I love you

You have made me what I am and I am yours

My love, there's so many ways I want to say I love you

Let me hold you in my arms forever more

You have gone and made me such a fool

I'm so lost in your love
And oh, we belong together

Won't you believe in my song

Lady, for so many years I thought I'd never find you

You have come into my life and made me whole

Forever let me wake to see you each and every morning

Let me hear you whisper softly in my ear

In my eyes I see no one else but you

There's no other love like our love

And yes, oh yes, I'll always want you near me

I've waited for you for so long

Lady, your love's the only love I need

And beside me is where I want you to be

'Cause, my love, there's something I want you to know

You're the love of my life, you're my lady
**********

Tuliendelea kunywa chai pale huku akisifia ladha ya mayai... Moyoni najisema angejuwa nilichoweka wala asingekula... Lakini nikakumbuka naye ni mpishi aliyesomea bila shaka anajuwa lakini asichojuwa ni pombe gani niliyoweka... Niliwaza tu...

Tulivyomaliza, nikainuka nikawa naanza kutoa vyombo, naye akasimama akanisaidia kupeleka jikoni, alitaka kuviosha lakini nilimkataza, moyoni niliona muda unapotea... Pia aliiona chupa ya pombe kali kule jikoni ikiwa imetumika kiasi.

"Enhee, nyumbani umeagaje?" Nilimuuliza baada ya kuwa tumerudi na kukaa kwenye makochi yanayo angaliana huku tukitenganishwa na cofee table.

"Nimeaga kuwa naenda kwa aunt Msasani, na nimewaambia nitarudi kesho" alisita kisha akaendelea...

"Wiki hii yote nimekuwa na kisirani tangia walivyoanza kunilazimisha nikubali posa, hivyo hawakuwa wagumu kuniruhusu na wanajuwa kuwa aunt ananipenda" Alisema

Nikamuuliza kuhusu siku ile Shangazi yake alisemaje, akanijibu kuwa yupo upande wake kwa maana ameniambia nifuate moyo wangu kwa kuwa mimi ni mtu mzima sasa, ningekuwa chini ya miaka 18 sawa, lakini nimepevuka na ninaweza kuona napenda nini na nini sipendi. Alimalizia hivyo.

Nikamwambia basi nitakupeleka kwa aunt yako baada ya chakula cha mchana, hapo ni mida ya saa sita kasoro hivi.

Ndani nina mchele, nina samaki wa kopo kwenye friji (saladin), viungo vingine vyote vipo kasoro mboga za majani tu. Hivyo sikuwa na waaiwasi wa kupoteza muda kutafuta vya kupika.

"Enhe, ulisema nije kupata ushauri ulioufanyia kazi, ndio nausubiri" alisema na kukaa vizuri kwenye kochi.

"Mbona leo tuna muda mrefu, nitakuambia tu usijali, pia usafiri tunao, utachaguwa batavuzi ama pijo" nilimjibu kibaharia..

Nikasimama nikachukuwa photo albam iliyokuwepo kwenye 'shelfu' la vitabu nikampatia.

Akaanza kupekuwa huku akiuliza hapa ni wapi, hapa ni wapi...

Baada ya hapa ni wapi ya tatu nikasimama na kuhamia upande wake nikakaa kwenye mbao ya juu ya kochi nikawa namjibu vizuri, na hata bila kuuliza nikawa natoa maelezo ya kutosha, akawa anafurahia sana nchi ya Uingereza ilivyo...

"Na huyu nani? Aliuliza alipomwona Sue binti wa Hispania.

" Aaa huyo alikuwa mate wangu chuoni, actually alikuwa girl friend wangu..." Nikameza mate kisha nikaendelea...

"Tulishaachana miaka zaidi ya miaka miwili iliyopita..." Nilisema huku yeye bado akikodolea picha nyingine za huyo binti Paterson.

Kukawa na ukimya fulani hivi, muziki ulikuwa tayari umesimama, mara akasema, nioneshe msalani.

Nikatangulia nikamuonesha...

Nikamuacha humo mie nikarudi na kuwaza nianzeje.

Plani ya awali ilikuwa nimleweshe akichangamka nitumie faida hiyo kumteka kimapenzi, lakini akili ikawa inakataa, badala yake inaniambia nimtongoze akiwa yupo fresh bila pombe, naanzaje sasa! Mara [emoji362][emoji362][emoji362]
***

Aliporudi kutoka maliwatoni, akaketi nami nikawa upande wa wangu...

Nikajikuta nimesimama na kuzunguka meza na kukaa juu ya meza ile ndogo (cofee table) nikiangaliana naye uso kwa uso, magoti yanakaribia kugusana.

Yeye akachukuwa albam akawa anaendelea kupekua...

"What is love?!" Nilimuuliza huku nikimtazama usoni!

Kabla hajajibu nikampachika swali la pili

"Do you believe in love?!"

Nikamuona amekaa kimya! Akameza mate kisha akajibu kwa ufupi...

"Yes, I do believe in love, and love is tender feelings"

Baharia nikaona mwanzo huooooo! Nashangilia kimoyo moyo.

Nilikuwa naweza kumlazimisha na kumbaka, lakini sina tabia hizo, huwa napata mzuka pale mwanamke anaporidhia mwenyewe lakini hata kama anasema hapana (hapana ila ya mdomoni)

Nikaamua nimuanzie mbali, na wala sikuwa na wazo la kuunganisha naye vikojoleo siku hiyo, nilikuwa na malengo naye ya mbali, sikutaka ani-discredit hata kidogo...

"Hebu niambie, dini inasemaje kuhusu kuchaguwa mchumba" nilipachika swali lingine

"Imehimizwa kuangalia mambo muhimu kama nasaba (koo/ukoo), uchumi, tabia njema, maumbile na dini, lakini papohapo imesisitizwa kuangalia dini zaidi kwani kuna faida ya kupata mengine yote Allah akitaka. Hivyo muolewaji akiendewa na muoaji kama amempenda basi aangalie mambo mawili tu, yaani tabia njema na awe mwislamu"

Akasita kidogo kama kajistukia hivi kisha akaendelea...

"Na muoaji akimpenda mwanamke basi azingatie dini yake tu kwa maana mengine yanaweza kuondoka wakati wowote isipokiwa kama ni mcha Mungu basi atafaulu, na imeruhusiwa kwa muoaji kumuangalia mchumba wake uso na viganja vya mikono..."

Alisema maneno hayo huku akionesha kwa mkono wake sehemu ya uso inayotakiwa kuonekana na kuonesha kwenye kiganja pia.

Nikasema vizuri, nimeelewa, kisha nikmuuliza...

"Sasa huyo mchumba wako wa Omani ana tabia njema? Je ni Muislamu?, Je ameona uso wako na viganja vyako?

" Mchumba wa nani, hebu usiniudhi, siyo mchumba wangu yule...'" Aling'aka

"Sawa, sina maana hiyo, hebu jibu swali..." Nilimkazia macho

"Hapana, hajaniona, labda amepewa picha yangu kupitia kwa da-Sabra ila hanijui wala simjui..."

Baada ya jibu hilo nikamuuliza

"Kwani ili ndoa ikamilike mambo gani lazima yatimie (yatimizwe)?

Alijibu kwa kirefu kwamba...

“Ili ndoa ikamilike lazima mambo haya yawepo:-
1. Idhini ya Walii (Baba mzazi ama msimamizi halali),
2. Kuridhika kwa bibi harusi mtarajiwa,
3. Kutimia kwa tamko la ndoa,
4. Kuwepo kwa mashahidi wawili waadilifu,
5. Kubalighe na kuwa na utambuzi baina ya wanandoa’’

“Je wewe umeridhika kuolewa na huyo mu-Oman?”nilimuuliza japo jibu nalijuwa

Akasema

“Hapana, sijaridhika”

Nikamwambia, basi poa moyo, maana hapo hakutokuwa na ndoa, ili ndoa itimie lazima bibi harusi mtarajiwa aridhie.

Nikaona kama amepata nguvu Fulani hivi. Nikawaza kumbe unaweza ukawa daktari wa magonjwa lakini siku ukipatwa na ugonjwa wewe daktari unaweza kusahau hata dawa za kutumia hadi ukumbushwe..

Hamida kiumri nimepishana naye kama miaka minne hivi, hivyo tunaendana sana. Nikamuuliza swali la uchokozi...

”Ulisema bikra yako utamzawadia mtu umpendaye, unaonaje ukinizawadia mimi?”

Kimyaaa! Akawa anaangalia chini.

”Ulisema pia bikra yako huwezi kuweka rehani kwa mbabu, mie si mbabu, mie ni kijana mwenzio...”

Kimyaaaa huku anachezesha vidole vya miguuni.

”Pia ulisema kuwa bikra yako utampa mumeo mtarajiwa, mie pia nafaa kuwa mumeo, maana nimesilimu juzi juzi tu, tabia zangu tangia unifahamu wazijuwa, mengine hayo ndiyo ulisema si ya kuzingatia sana lakini uwezo wa kukulisha, kukuvisha, kukupa malazi na jimai ninao”

Hamida yupo kimya tu amejiinamia na sasa vidole vyake vya mikononi navyo vimeanza kusuguana suguana...

Nikamshika mkono wake wa kushoto, kasha wa kulia, tukawa tumeshikana kama tunasalimiana...

“Hamida”nilimuita

“Abee” aliitika kwa sauti ya chini iliyonipa nguvu zaidi ya kushambulia...

“Jamaal anakupenda, Jamaal anakupenda sana. Tangia alipokuona mara ya kwanza hajaacha kukupenda wala kuacha kukuwaza. Jamaal amefanya jithada kubwa ili awe nawe muda wote, Jamaal ameweka uteja kwa kunywa juisi na togwa ili isipite siku bila kukuona, hakika Jamaal anakupenda sana. Jamaal amebadilisha dini kwa ajili yako, ili ukumkibalia akuoe. Jamaal yupo tayari kwa changamoto zote zitakazo jitokeza kwa sababu ya tofauti ya asili zetu. Najuwa kuwa wapo wengi waliojitokeza ama watakaojitokeza kukuposa, lakini sina uhakika kama utawapenda kwa kuwa wengi wanakuwa ni ndugu zenu. Pia tumefundishwa mashuleni kuchanganya nasaba ili kupata vizazi bora.”

Hamida kainama tu, bado nimemshika mikono. Nikamuachia mkono wake wa kushoto na kumshika bega lake la kushoto...

“Tafadhali Hamida nipe nafasi katika moyo wako. Love is tender feelings according to your definition, and I do have those feelings to you, so please accept my request”

Nikamshika mabega yake yote mawili huku yeye akizidi kuinama chini.

Nikasimama, nikamshika makwapani na kumuinua, aliinuka wala sikutumia nguvu, palikuwa kimya bado, hakuna mziki wala kelele zozote, pumzi zetu tu zinasikika...

Nikamkumbatia mikono yangu ikiwa mabegani mwake, nikauchukuwa mkono wangu wa kulia na kuushika wake wa kushoto na kumfanya anishike mgongoni, nikafanya hivyo na mkono wake wa kulia kasha mimi nikashusha mikono yangu hadi kiunoni mwake...

Lo salale! Manguo haya wanayovaa waislamu wa kike yanaficha mengi, mikono yangu iligunduwa kuwa Hamida ana mat*ako na hips balaa!

Tuliendelea kukumbatiana kwa sekunde kadhaa, mara shetani akanikumbusha kuwa akili zitamrudia Hamida, mpeleke chumbani...

Nikamwita, Hamida! Akatitia abee! Kwa sauti ile ya kuonesha hana ujanja tena, nikamwambia, twende huku, wala hata hakuuliza, nikamkokota hadi chumbani kwangu (siyo kule kwa jana na Marry)

Moja kwa moja hadi kitandani, shuka jeupe safi, nikawa nimesimama mbele yake yeye akekaa kitandani, nikamwita tena...

“Hamida”

Akaitikia

“mmh, abee!”kwa sauti ya mahaba sasa

Nikamwambia simama huku namuinua, akasimama, nikaanza kumbusu kwenye paji la uso, kisha puani, kisha kwenye lips (just short kisses), kisha shingoni, akahema sana..., nakarudia mdomoni sasa ni ile french kiss, taratiiibu na kuongeza kasi kadri tulivyokuwa tunaendelea, mikono yangu ndio ikawa haitulii kabisa, nikaanza kutalii mgongoni, kiunoni hadi mat*akoni, nikafika kifuani, Hamida naye akaanza kutoa ushirikiano... nikaacha kumkiss mdomoni, nikahamia shingoni maana nilipagundua kuwa ndipo nywila ilipo, alianza kuguna miguno ya ajabu ajabu...

Itaendelea...View attachment 1347835View attachment 1347836View attachment 1347838View attachment 1347839

James Jason
Chief hapa uliikatisha kikatili sana [emoji3]
 
Taarifa kwa tuliokuwa tunawasiliana telegram na whatsapp.

Sipatikani kwenye namba ya DRC tena, nipo Tz kwa muda mrefu sasa namba ya DRC haifanyikazi tena.

Nitawa contact kwa namba nyingine. ASAP.
 
Taarifa kwa tuliokuwa tunawasiliana telegram na whatsapp.

Sipatikani kwenye namba ya DRC tena, nipo Tz kwa muda mrefu sasa namba ya DRC haifanyikazi tena.

Nitawa contact kwa namba nyingine. ASAP.
Asante kwa taarifa Mzee
 
Taarifa kwa tuliokuwa tunawasiliana telegram na whatsapp.

Sipatikani kwenye namba ya DRC tena, nipo Tz kwa muda mrefu sasa namba ya DRC haifanyikazi tena.

Nitawa contact kwa namba nyingine. ASAP.
Nimerudi hewani

Tutaonana soon kwenye social media
 
Kongole mzee wangu sifa nyingi zimetajwa ila ww ni jabari tafadhari ukipata walau kijinafasi jaribu kutupa na story nyingine for sure umepitia mengi na tuna mengi ya kujifunza kupitia wewe unakipawa kikubwa sana cha uandishi sambamba na kumbukumbu Mungu akutunze
Amen
 
Vijana jitahidini msome vitabu hivi vitatu, mtajifunza mengi:-

1. "The Perfumed Garden" - Umar ibn Muhammad Nefzawi - 15th Century

2. "French Sex Art Manners" - Georges Valensin - 1970

3. "Kama Sutra' - Vatsyayan Richard Francis Burton

James Jason
Thanks
 
Back
Top Bottom