Ndugu zangu badala ya kutoa ushauri naomba mniruhusu nimhukumu Mama Samia kwa hotuba zake na teuzi zake japo ni mapema saana kufanya hivyo. Ameanza vizuri kwa ujumla lakini inabidi ajue mapema uimara wake na udhaifu wake:
Uimara wake (strengths):
1. Alimtendea haki sana JPM wakati wa msiba wake. Alimheshimu sana na kuongoza mamilioni ya watanzania kumuaga. katika hili ana Alama A+
2. Uamzi wake wake wa "kuwapa" watu na vyombo vya habari uhuru wa kuongea kwa mujibu wa sheria ni jambo jema. Kuna wakati maafisa wa serikali walikuwa wanatafuta tu sifa kwa kutotenda haki. Katika hili Alama A.
3. Kuahidi kuendeleza nidhamu kazini na matumizi mazuri ya serikali na kuwatumbua wabadhilifu - Alama B (kwa vile ni ahadi tu).
4. Kujiamini na kufanya mabadiliko ya mawaziri na makatibu kwa vigezo vya 'ujuzi/ubobezi' wao - Alama A.
5. Kuahidi kuendeleza miradi mikubwa na midogo ya kimkakati - Alama B (Ahadi tu bado)
Udhaifu (weaknesses)
1. Kujaribu kuwafurahisha wawekezaji/Wazungu - Magufuli "was not a fool" hawa watu si wa kuchekea na kujirahishisha kwao. Kikwete alikuwa Rais mzuri sana lakini tuliishia kuwa na mikataba ya kinyonyaji sana. Anafanya makosa yale yale!
2. Kujaribu kuwafurahisha Wafanyabiashara - ataishia kukusanya mapato kiduchu na mengi yataishia mifukoni mwa TRA
3. Suala la Covid-19 - Kujaribu kuturudisha nyuma tulikotoka wakati tumefika mbali sana. Kwa nini tulizuia takwimu? Kwa nini tunakataa barakoa na chanjo zao? Je tiba zetu za asili azikutusaidia? Je sasa tufanye wazungu wanavyotaka? - Anakosea sana!
4. Kujivua wajibu wake kwa maamzi ya serikali iliyopita wakati yeye alikuwa mshauri mkuu wa JPM. - Uwezi kuwa juzi tu ulikuwa makamu wa Rais na leo unafanya U-turn ya mambo mengi ambayo ulikuwa sehemu ya maamzi yake.
5. Kutupa dalili kuwa tunarudi katika unyonge wa kuwapigia magoti wazungu na ile jeuri aliyotupa Mwl.JK na JPM ianze kupotea!
Siku nyingine:
Baadhi ya teuzi hazikuwa 'fair' au zilikuwa za kuumiza sana kwa wahusika. By the way "CCM inaongozwa na nani?" - Haya yatakuwa ya siku nyingine.
Uimara wake (strengths):
1. Alimtendea haki sana JPM wakati wa msiba wake. Alimheshimu sana na kuongoza mamilioni ya watanzania kumuaga. katika hili ana Alama A+
2. Uamzi wake wake wa "kuwapa" watu na vyombo vya habari uhuru wa kuongea kwa mujibu wa sheria ni jambo jema. Kuna wakati maafisa wa serikali walikuwa wanatafuta tu sifa kwa kutotenda haki. Katika hili Alama A.
3. Kuahidi kuendeleza nidhamu kazini na matumizi mazuri ya serikali na kuwatumbua wabadhilifu - Alama B (kwa vile ni ahadi tu).
4. Kujiamini na kufanya mabadiliko ya mawaziri na makatibu kwa vigezo vya 'ujuzi/ubobezi' wao - Alama A.
5. Kuahidi kuendeleza miradi mikubwa na midogo ya kimkakati - Alama B (Ahadi tu bado)
Udhaifu (weaknesses)
1. Kujaribu kuwafurahisha wawekezaji/Wazungu - Magufuli "was not a fool" hawa watu si wa kuchekea na kujirahishisha kwao. Kikwete alikuwa Rais mzuri sana lakini tuliishia kuwa na mikataba ya kinyonyaji sana. Anafanya makosa yale yale!
2. Kujaribu kuwafurahisha Wafanyabiashara - ataishia kukusanya mapato kiduchu na mengi yataishia mifukoni mwa TRA
3. Suala la Covid-19 - Kujaribu kuturudisha nyuma tulikotoka wakati tumefika mbali sana. Kwa nini tulizuia takwimu? Kwa nini tunakataa barakoa na chanjo zao? Je tiba zetu za asili azikutusaidia? Je sasa tufanye wazungu wanavyotaka? - Anakosea sana!
4. Kujivua wajibu wake kwa maamzi ya serikali iliyopita wakati yeye alikuwa mshauri mkuu wa JPM. - Uwezi kuwa juzi tu ulikuwa makamu wa Rais na leo unafanya U-turn ya mambo mengi ambayo ulikuwa sehemu ya maamzi yake.
5. Kutupa dalili kuwa tunarudi katika unyonge wa kuwapigia magoti wazungu na ile jeuri aliyotupa Mwl.JK na JPM ianze kupotea!
Siku nyingine:
Baadhi ya teuzi hazikuwa 'fair' au zilikuwa za kuumiza sana kwa wahusika. By the way "CCM inaongozwa na nani?" - Haya yatakuwa ya siku nyingine.