Uimara na udhaifu wa Mama Samia

Uimara na udhaifu wa Mama Samia

Mataga utapata tabu sana usipo kubali kubadilika. Falsafa nyingi za magufuki zilikuwa ni outdated! Hii ni Karne ya 21 moja! Ni karne ya Utandawazi! Ni kituko mtu upo kwenye karne ya 21, lakini mawazo yako yapo karne ya 20!

Karne ya akina Nyerere ya kuwaita Wazungu Mabeberu! Ni wakati sahihi sasa kusbirikiana na matifa mengine kwa manufaa ya pande zote mbili. Kunitenga na Dunia ya utandawazi, ni uwendawazimu wa kiwango cha ajabu!
Binafsi najua Mwendazake ni kiongozi ambae amefanya mengi mazuri kwa ajili ya taifa lake hawezi kuwa perfect alikua na weakness lkn amejitahidi kwenye mengi nawajua binadamu huwezi kuwafurahisha makundi yote na wamejaa unafiki ataondoka mama simu moja Sasa hivi wanamsifu kwa kuachia Uhuru wa vyombo vya habari watakuja na agenda nyingine kumponda na kukashfu uongozi wake.This people they will never satisfy.Yesu nwenyewe alisalitiwa na wanafunzi wake Tena akiwepo na anashuhudia ,Mwendazake anasalitiwa baada ya kwenda zake , Gaddafi alifanya kila alichoweza lkn alionekana hafai na wakamsaliti huwezi kuja kuwaridhisha binadamu huwezi huwezi huwezi.
 
Ni zamu yenu sasa kuhama nchi kama hamridhishwi na utendajivwa Raus wa sasa! Ila ukweli utabakia pale pale! Mabeberu siyo watu wa kushindana nao.

Ukiwa kiongozi wa nchi maskini kama Tanzania, unatakiwa kuishi nao kwa umakini na siyo kwa kuwatishia nyau! Dakika 0 tu wanakupoteza.
Usishindane nao lakini waonyeshe na wewe una akili na maamzi juu ya raslimali zako. sio waje wachote tu na watanzania wanyonge waishie kutopata service zozote na maafisa wa serikali wanufaike wenyewe! Ndio maana tulimpenda JPM alikuwa jiwe (maskini jeuri) kwa ajili ya watanzania na kafanya so much. Hapa tutakuwa legelege kwa wazungu na service kwa umma kama elimu na miundombinu vitakuwa historia pamoja na kujichekesha kwao!
 
Usishindane nao lakini waonyeshe na wewe una akili na maamzi juu ya raslimali zako. sio waje wachote tu na watanzania wanyonge waishie kutopata service zozote na maafisa wa serikali wanufaike wenyewe! Ndio maana tulimpenda JPM alikuwa jiwe (maskini jeuri) kwa ajili ya watanzania na kafanya so much. Hapa tutakuwa legelege kwa wazungu na service kwa umma kama elimu na miundombinu vitakuwa historia pamoja na kujichekesha kwao!
Acha uoga wewe! Hii nchi itaendelea tu hata bila ya huyo magufuli wako.
 
Acha uoga wewe! Hii nchi itaendelea tu hata bila ya huyo magufuli wako.
bila shaka itaendelea. Iliendelea Sokoine alipokufa; Nyerere alipostaafu; na Mrema alipofukuzwa kazi na Sasa itaendelea tu! Lakini Mama asipoangalia unafiki na uroho wa wanasiasa waliokuwa wameficha kucha zao, basi JPM atakumbukwa na wengi kwa machozi yasiyoisha!
 
bila shaka itaendelea. Iliendelea Sokoine alipokufa; Nyerere alipostaafu; na Mrema alipofukuzwa kazi na Sasa itaendelea tu! Lakini Mama asipoangalia unafiki na uroho wa wanasiasa waliokuwa wameficha kucha zao, basi JPM atakumbukwa na wengi kwa machozi yasiyoisha!
Hata wakati wake, bado hao wanasiasa wanafiki walikuwa ni wengi! tena kuliko wakati mwingine wowote ule! Kama ni kumpotosha, wamempotosha sana! Kiasi cha kusababisha watumishi wa umma tulio wengi, kumchukia kwa maamuzi yake ya kibabe na kikatili aliyo yachukua dhidi yetu, kwa nyakati tofauti.

Wanafiki wapo tu karne na karne! Kama unavyosema, anatakiwa kweli kuwa makini. Mimi ningemshauri awekeze zaidi kwenye ujenzi wa mifumo imara ya kiutendaji kupitia Katiba Mpya! Badala ya kupambana yeye kama yeye. Kwa sababu nchi itabakia milele! Ila sisi tunapita tu. Hata enzi za Magufuli, tulimtahadharisha kuhusu jambo hili, ila yeye alidhani ataishi milele.

Aliamini kwenye Tanzania ya Magufuli badala ya ile Tanzania yenye mifumo imara ya kiutawala. Mwisho wa siku, amekwenda zake katika mazingira ambayo hakuna aliye tarajia.
 
Nawalipa gharama za simu yao. Lakini wao wanataka kuchukua resources zetu kwa wizi.
Ndugu yangu, kaa na resources zako uone kama zitakusaidia. Suala si kuwachukia wazungu kwa sababu ndio watumiaji wakubwa wa hizo resources unazosema kwani kama ni kulaliana hata huku uswahilini ukizubaa waswahili wenzio wanakulalia tu. Kama alivyosema yeye Mama Samia, ukitaka kwenda mbali nenda na wenzio na ukitaka kufika haraka nenda peke yako na sisi tunahitaji kufika mbali hivyo ni lazima twnde na wenzetu. Waangale Wachina waliporuhusu uwekezaji lakini kwa uangalifu sana wameweza kuwa mshindani mkubwa wa Marekani. Hivyo basi hatupaswi kuwasideline wazungu ila ni kwenda nao kwa umakini tukijua tunataka nini na tutakipataje tunachotaka kupata toka kwao.
 
Ndugu zangu badala ya kutoa ushauri naomba mniruhusu nimhukumu Mama Samia kwa hotuba zake na teuzi zake japo ni mapema saana kufanya hivyo. Ameanza vizuri kwa ujumla lakini inabidi ajue mapema uimara wake na udhaifu wake:

Uimara wake (strengths):
1. Alimtendea haki sana JPM wakati wa msiba wake. Alimheshimu sana na kuongoza mamilioni ya watanzania kumuaga. katika hili ana Alama A+

2. Uamzi wake wake wa "kuwapa" watu na vyombo vya habari uhuru wa kuongea kwa mujibu wa sheria ni jambo jema. Kuna wakati maafisa wa serikali walikuwa wanatafuta tu sifa kwa kutotenda haki. Katika hili Alama A.

3. Kuahidi kuendeleza nidhamu kazini na matumizi mazuri ya serikali na kuwatumbua wabadhilifu - Alama B (kwa vile ni ahadi tu).

4. Kujiamini na kufanya mabadiliko ya mawaziri na makatibu kwa vigezo vya 'ujuzi/ubobezi' wao - Alama A.
5. Kuahidi kuendeleza miradi mikubwa na midogo ya kimkakati - Alama B (Ahadi tu bado)

Udhaifu (weaknesses)

1. Kujaribu kuwafurahisha wawekezaji/Wazungu - Magufuli "was not a fool" hawa watu si wa kuchekea na kujirahishisha kwao. Kikwete alikuwa Rais mzuri sana lakini tuliishia kuwa na mikataba ya kinyonyaji sana. Anafanya makosa yale yale!

2. Kujaribu kuwafurahisha Wafanyabiashara - ataishia kukusanya mapato kiduchu na mengi yataishia mifukoni mwa TRA

3. Suala la Covid-19 - Kujaribu kuturudisha nyuma tulikotoka wakati tumefika mbali sana. Kwa nini tulizuia takwimu? Kwa nini tunakataa barakoa na chanjo zao? Je tiba zetu za asili azikutusaidia? Je sasa tufanye wazungu wanavyotaka? - Anakosea sana!

4. Kujivua wajibu wake kwa maamzi ya serikali iliyopita wakati yeye alikuwa mshauri mkuu wa JPM. - Uwezi kuwa juzi tu ulikuwa makamu wa Rais na leo unafanya U-turn ya mambo mengi ambayo ulikuwa sehemu ya maamzi yake.

5. Kutupa dalili kuwa tunarudi katika unyonge wa kuwapigia magoti wazungu na ile jeuri aliyotupa Mwl.JK na JPM ianze kupotea!

Siku nyingine:
Baadhi ya teuzi hazikuwa 'fair' au zilikuwa za kuumiza sana kwa wahusika. By the way "CCM inaongozwa na nani?" - Haya yatakuwa ya siku nyingine.

Muhaya wa hovyo! Muda wa kuchukia mataifa mengine ni wakati wa vita au kugombea uhuru. Sasa hivi hatuna vita na tuna uhuru karibia miaka 60 sasa.

Ni wakati wa kuinua national interests zetu. Huwezi kusema USA inagombea korosho, kahawa na pamba ya Tz. CCM wametuingiza kwenye mikataba iliyoua maslahi ya kitaifa, kama Magufuli alidhibiti hilo - Sasha nae afanye hivo. Tuache ujinga na chuki kwa wazungu wakati unataka waje kutalii upate pesa, unataka kuuza mazao yao kwao, unatumia teknolojia yao katika uzalishaji na mawasiliano.
 
Muhaya wa hovyo! Muda wa kuchukia mataifa mengine ni wakati wa vita au kugombea uhuru. Sasa hivi hatuna vita na tuna uhuru karibia miaka 60 sasa.

Ni wakati wa kuinua national interests zetu. Huwezi kusema USA inagombea korosho, kahawa na pamba ya Tz. CCM wametuingiza kwenye mikataba iliyoua maslahi ya kitaifa, kama Magufuli alidhibiti hilo - Sasha nae afanye hivo. Tuache ujinga na chuki kwa wazungu wakati unataka waje kutalii upate pesa, unataka kuuza mazao yao kwao, unatumia teknolojia yao katika uzalishaji na mawasiliano.
Hatupo huru. Kuna neo colonialism since 1961.
 
Ndugu zangu badala ya kutoa ushauri naomba mniruhusu nimhukumu Mama Samia kwa hotuba zake na teuzi zake japo ni mapema saana kufanya hivyo. Ameanza vizuri kwa ujumla lakini inabidi ajue mapema uimara wake na udhaifu wake:

Uimara wake (strengths):
1. Alimtendea haki sana JPM wakati wa msiba wake. Alimheshimu sana na kuongoza mamilioni ya watanzania kumuaga. katika hili ana Alama A+

2. Uamzi wake wake wa "kuwapa" watu na vyombo vya habari uhuru wa kuongea kwa mujibu wa sheria ni jambo jema. Kuna wakati maafisa wa serikali walikuwa wanatafuta tu sifa kwa kutotenda haki. Katika hili Alama A.

3. Kuahidi kuendeleza nidhamu kazini na matumizi mazuri ya serikali na kuwatumbua wabadhilifu - Alama B (kwa vile ni ahadi tu).

4. Kujiamini na kufanya mabadiliko ya mawaziri na makatibu kwa vigezo vya 'ujuzi/ubobezi' wao - Alama A.
5. Kuahidi kuendeleza miradi mikubwa na midogo ya kimkakati - Alama B (Ahadi tu bado)

Udhaifu (weaknesses)

1. Kujaribu kuwafurahisha wawekezaji/Wazungu - Magufuli "was not a fool" hawa watu si wa kuchekea na kujirahishisha kwao. Kikwete alikuwa Rais mzuri sana lakini tuliishia kuwa na mikataba ya kinyonyaji sana. Anafanya makosa yale yale!

2. Kujaribu kuwafurahisha Wafanyabiashara - ataishia kukusanya mapato kiduchu na mengi yataishia mifukoni mwa TRA

3. Suala la Covid-19 - Kujaribu kuturudisha nyuma tulikotoka wakati tumefika mbali sana. Kwa nini tulizuia takwimu? Kwa nini tunakataa barakoa na chanjo zao? Je tiba zetu za asili azikutusaidia? Je sasa tufanye wazungu wanavyotaka? - Anakosea sana!

4. Kujivua wajibu wake kwa maamzi ya serikali iliyopita wakati yeye alikuwa mshauri mkuu wa JPM. - Uwezi kuwa juzi tu ulikuwa makamu wa Rais na leo unafanya U-turn ya mambo mengi ambayo ulikuwa sehemu ya maamzi yake.

5. Kutupa dalili kuwa tunarudi katika unyonge wa kuwapigia magoti wazungu na ile jeuri aliyotupa Mwl.JK na JPM ianze kupotea!

Siku nyingine:
Baadhi ya teuzi hazikuwa 'fair' au zilikuwa za kuumiza sana kwa wahusika. By the way "CCM inaongozwa na nani?" - Haya yatakuwa ya siku nyingine.
Nonsense!

The obvious can not be proved!

Tatizo lako unawaza kizamanizamani hivyo huwezi kumuelewa mama yetu.

Acha mama aongoze nchi kwa umahiri wake. Usimpangie.

Uraisi wake hauna ubia na Magufuli. Magufuli alitawala bila kupangiwa na hakusikiliza ushauri wa mtu yeyote. Hatukumuingilia.

Unataka mama yetu asisikilize kilio cha walipakodi aendelee kudhulumu wafanyabiashara kama Magufuli alivyokuwa anafanya? Pathetic!

Kazi iendelee...
 
Mama anahitaji kujua tunawaza nini kwa vile japo ni Rais awamu yake ni awamu inayoendeleza kile alichoahidi na mgombea mwenza wake JPM
Kwa hiyo waliahidi pamoja kudhulumu wafanyabiasha kwa kuwabambikia kodi kubwa na kuwafungulia kesi za uhujumu uchumi na utakatishaji fedha?

Waliahidi pamoja kuzuia uhuru wa vyombo vya habari?

Mwacheni mama yetu aongoze nchi kwa kuzingatia misingi ya sheria na utawala bora kama alivyoanza. Hatutaki kutawaliwa kidikteta kama Magufuli alivyokuwa anafanya.
 
Back
Top Bottom