JumaKilumbi
JF-Expert Member
- Sep 7, 2022
- 432
- 507
Hapa umesema kweli, ila zile sifa za kuwa mfalme kazisema nani?Hicho kitu wanaita constitutional monarch ni usanii mtupu. Walipoona wamepoteza uwezo wa kuendesha ufalme wakaanzisha hicho kufanya brain washing.
Hizo ni sifa zilizokuwepo tangu enzi na enzi. Hata hao UK walizitumia mpaka ilipofika mahali hawawezi tena kutawala ndio wakafanya mabadiliko ili waendelee kuwepo.Hapa umesema kweli, ila zile sifa za kuwa mfalme kazisema nani?
Kuhusu namna ya ufalme wa Uingereza tulifundishwa shuleni jinsi ulivyotofauti na Ufalme kama wa Eswatini nahisi wewe ulikua huingii darasani.
Kwa msingi huo ndio una ‘m-disqualify’ mfalme Charles III kutokuwa mfalme sababu tu hivi sasa hanazo sifa hizo?Hizo ni sifa zilizokuwepo tangu enzi na enzi. Hata hao UK walizitumia mpaka ilipofika mahali hawawezi tena kutawala ndio wakafanya mabadiliko ili waendelee kuwepo.
Kwasasa yule sio mfalme bali yeye na familia yake ni watu wabinafsi wanaotumia wengine kuwa na mafanikio.Kwa msingi huo ndio una ‘m-disqualify’ mfalme Charles III kutokuwa mfalme sababu tu hivi sasa hanazo sifa hizo?
Ni habari kubwa kwako. Lakin europe us na members wake hili wanalijua muda sana. Ndio maana huwasikii wakihangaika nalo.Sasa hivi imekuwa muda muafaka kuliongelea kwasababu ndio habari kubwa duniani.
Mkuu ni ukweli mchungu ila yeye ni Mfalme na familia yake ni ya Kifalme.Kwasasa yule sio mfalme bali yeye na familia yake ni watu wabinafsi wanaotumia wengine kuwa na mafanikio.
Mfalme ana say but majority ya choice zinatoka bungeni na wananchi.Lakini mfalme anaweza kumchagua waziri?? Nasikia hata bungeni kuna viti maalumu vya royal family
Mkuu, nakuombea ije, pengine nami ntakumbukwaR. I. P queen Elizabeth II. Dah lakini kifo chake kimenikosesha dili la billion 3.2 yaani limesogea mbele [emoji17]
Baada ya kufundishwa ishu ya demokrasia na haohao uwaitaoUfalme Zama Hizi NI ujinga mtupu!
Hili sio suala dogo. US hawezi kuwahoji kwasababu hao ni washirika wake. Halafu raia wengi pale UK wanalihoji hili. Ni suala la muda kabla moto haujawaka pale.Ni habari kubwa kwako. Lakin europe us na members wake hili wanalijua muda sana. Ndio maana huwasikii wakihangaika nalo.
Ni ww tu ndio unahangaika nalo. Nchi wanachama wana mambo ya muhim ya kufanya kuliko kupoteza muda kuhoji kwa suala dogo kama hilo
Ufalme huo ume evolve kiujanjaujanja tu maana walishapiteza ile control ya kifalme. Walifanikiwa sana kuwa-brain wash watu wa UK kwa miaka mingi. Watu wamebakia na ile prestige tu lakini hawanufaiki na uwepo wao.Mkuu ni ukweli mchungu ila yeye ni Mfalme na familia yake ni ya Kifalme.
Sifa za kuwa mfalme ‘zina-evolve’ kutokana na mahali na muda, watu wa jamii husika ndiyo huamua mtu mwenye sifa zipi anafaa kuwa kiongozi wao na yupi hafai, Mfalme huyo atakuwa na mamlaka gani? Hilo ni wao kuamua hivyo hakuna sifa ‘fixed’ kuhusu sifa za Mfalme.
Ila nami nina imani kama yako kuwa ile taasisi ya kifalme imepitwa na wakati, haifai tena kuwepo pale.
Hizi si zama zile, kazi inazozifanya zinaweza fanywa na kiongozi yoyote mwenye kuchaguliwa na raia.
Nimesema anayo influence ya kidiplomasia kwa kiasi fulani. Nguvu kwenye hizo nchi ipo kwa wananchi wenyewe kupitia bunge na mahakama.Hizo nchi zote head of state wao ni Mfalme wa Uingereza sasa utasemaje hana nguvu??
Mfalme hana say yoyote binafsi isipokuwa bunge na mahakama ndio zina nguvu pale.Mfalme ana say but majority ya choice zinatoka bungeni na wananchi.
Bunge la hawa watu lina nguvu
A naweza mfuta kazi waziri mkuu akitaka.Sawa mkuu, lakini vigezo hapo juu vya mfalme hana. Ukiangalia vizuri hana mamlaka ya kuwafuta kazi hao uliowataja bila consent ya bunge au halmashauri ya kanisa la anglikana.
Hujui kwamba kuna tofauti kati ya Constitutional Monarchy and Absolute Monarchy. Anyway, tuongee ya kwetu kwani tunaumia sana na kodi nyingi ambazo hatuoni faida yake, serikali imekuwa msalaba kwa wananchi.Sifa za mtu anayetambulika kama mfalme:
1. Awe anamiliki ardhi yote anayotawala.
2. Awe na amri juu ya watu wote wa eneo lake kila wakati
3. Awe anamiliki mali zote katika eneo lake na kwamba kila raia awe anafanya kazi kwa ajili ya mfalme
4. Tamko la mfalme linakuwa sheria ambayo inatekelezwa mara moja
5. Mfalme ndio mwongozo wa tabia, mwenendo na tamaduni ya kila raia kwenye eneo lake
6. Mfalme anayo haki ya kumpatia au kumnyang'anya yeyote kitu chochote bila kuulizwa
7. Hukumu ya mfalme ni mwanzo na mwisho wa mabishano.
8. Mfalme anawajibika kiulinzi na kuhakikisha watu wake wanapata mahitaji yao ya kila siku.
Haya yote hayapo pale Uingereza. Kinachoendelea pale ni raia masikini wanakubali kuitunza familia isiyokuwa na mamlaka ya kiutawala juu yao.
Only kama hana uungwaji mkono wa bunge. Kwahiyo hana nguvu isipokuwa bunge ambalo linawakilisha wananchi.A naweza mfuta kazi waziri mkuu akitaka.
Acha jazba, huyo ni "mlokole" mwenzio.haikuwa sehem ya roman empire bali walitawaliwa kimabav na warumi , hlf akil yako inaonesha ww ni mvaa kobaz , hujui kuwa wenzetu huji update kuendana na muda