Ujasiri wa Hajjat Amina Said?

Ujasiri wa Hajjat Amina Said?

Madabwada

JF-Expert Member
Joined
May 8, 2009
Posts
541
Reaction score
320
Kwa kweli nimependezwa sana na uwajibikaji wa huyu mama, last week aliamuru kufungwa mara moja kwa shule ya sekondari ya Bundikani huko kibaha baada ya kugundulika wanafunzi wa kidato cha kwanza wanakaa chini, lakini pia jana ameamuru kukatwa mishahara kwa watendaji wazembe wa kisarawe.

Naomba tu isiwe just a move to gain popularity ili baadaye atimize azma yake ya kuwa mbunge (ameshatangaza azma yake ya kugombea ubunge katika jimbo la Kiteto mwaka huu - 2010) na pengine kutimiziwa ahadi nyingine alizoahidiwa baada ya kuukwaa huo ubunge. Binafsi nitafurahi kuona huu moto aliouanzisha basi awe ana maanisha. Kwa sasa nakupa hongera mama lakini ......!!


MKUU wa Mkoa wa Pwani, Hajjat Amina Said, sasa ameamua kutoa makucha yake dhidi ya watendaji wazembe ambao amedai kuwa ndio wanaokwamisha maendeleo ya mkoa huo na si kukosekana kwa fedha kama inavyodaiwa na baadhi ya watendaji.
Mkuu huyo alifanya hivyo juzi akiwa wilayani Kisarawe, ambako aliaamuru watendaji sita wa halmashauri ya wilaya hiyo, wakatwe asilimia 15 ya mishahara yao kwa kipindi cha miezi miwili, ikiwa ni adhabu kwa kosa la kuchelewesha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Watendaji hao ambao wataanza kukatwa mishahara yao kuanzia mwezi ujao ni pamoja na Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Alquin Ndungwi.


Wengine ni Ofisa Elimu ya Msingi wa Wilaya ya Kisarawe, Winifrida Mbuya, Ofisa Elimu ya Sekondari Donard Chavila, Ofisa Afya Dk E. Helela, Mhandisi wa Wilaya Ayoub Myaule, Ofisa Mipango, Deus Mbalamwezi, na Mweka Hazina, Isaya Moses.
.
Mkuu huyo wa mkoa alitaja baadhi ya miradi iliyokwama kutokana na uzembe wa watendaji hao kuwa ni ile ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule za sekondari za kata, zahanati na ukosefu wa madawati, jambo linalosababisha wanafunzi kuketi sakafuni.

Hijat Amina alitoa agizo la kukatwa sehemu ya mishahara watendaji hao katika kikao chake cha majumuisho ya ziara ya siku moja aliyoifanya wilayani humo, ziara iliyokuwa na lengo la kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM.

Mkuu huyo wa mkoa alisema kimsingi, wilayani hiyo imeshindwa kutekeleza ipasavyo ilani hiyo.

Alisema serikali ilikwishapeleka fedha za miradi katia vipindi tofauti vya kuanzia Julai mwaka jana na kwamba alichogundua ni kwamba watendaji hao kila mmoja kwa nafasi yake, alikaa nazo hadi Februari na Machi mwaka huu, walipoamua kuzipeleka kwa wananchi.

Mkuu huyo alisema kitendo kukalisha fedha hizo kwa muda wa miezi sita bila kufika kwenye miradi, kinaashiria kuwa zilikuwa zinahifadhiwa katika akaunti za watu binafsi kwa lengo la kupata faida.

"Hapa msinieleze kitu,katika taarifa mlioniletea, mmeonyesha miradi imekamilika sasa leo nimeamua kupita na kujionea hali halisi kuwa nyie ni waongo, na mmeidanganya serikali katika hili simfumbii macho mtu wala sitajali cheo chake,"alisema Mkuu wa wilaya.

Katika ziara hiyo kiongozi huyo alitembelea shule tano za sekondari za kata za Gongoni, Makulunge, Msimbu, Mfuru na Kibuta.
Hijat Amina alielezwa kuwa kwa pamoja shule hizo zina madawati 120 tu kati ya madawati 640 yanayohitajika.
 
kimsingi kama ndivyo alivyo; hafai kuwa Mbunge wa kawaida. Anatakiwa kuwa mbuneg wa kuteuliwa halafu anapewa uwaziri wa kusimamia matokeo.. we need results oriented leadership..
 
Kukata mtu mshahara sio kinyume cha sheria?

Baadhi ya watz watu wa ajabu sana siku hizi,mtu anavunja sheria the great thinkers tunakuja hapa kusifia!

Kwani huyu mama ndiye Waziri mkuu wetu?Huyu mama hivi sasa ndiye waziri wa UTUMISHI?huyu mama ndiye waziri wa TAMISEMI?

kama hana nafasi hizo 3 nilizotaja juu,basi kwa madaraka gani ndani ysa katiba ya jamhuri ya tz inayompa nguvu kufanya haya aliyoyafanya kwa maafisa wenzake wa serikali kuu?

Namshauri kama lengo lake ni kujitutuma aonwe na wananchi wa kiteto ili wampe ubunge afanye hivyo bila kuvunja katiba,na kama anataka sana kukata watumishi mishahara yao basi afanye hivyo kwa house girl/boy wake(kama anao),maana hao ndiyo wapo chini yake kiuajiri !
 
Baadhi ya watz watu wa ajabu sana siku hizi,mtu anavunja sheria the great thinkers tunakuja hapa kusifia!

Kwani huyu mama ndiye Waziri mkuu wetu?Huyu mama hivi sasa ndiye waziri wa UTUMISHI?huyu mama ndiye waziri wa TAMISEMI?

kama hana nafasi hizo 3 nilizotaja juu,basi kwa madaraka gani ndani ysa katiba ya jamhuri ya tz inayompa nguvu kufanya haya aliyoyafanya kwa maafisa wenzake wa serikali kuu?

Namshauri kama lengo lake ni kujitutuma aonwe na wananchi wa kiteto ili wampe ubunge afanye hivyo bila kuvunja katiba,na kama anataka sana kukata watumishi mishahara yao basi afanye hivyo kwa house girl/boy wake(kama anao),maana hao ndiyo wapo chini yake kiuajiri !

Sasa hivi hata ukisimamishwa kazi unakula msahara full...sasa hawa si wako kazini?Halafu DED unamchambua mbele ya kikao...kazi kwelikweli..wakikakwa hiyo mishahara anapewa nani hayo makato?
 
nadhani tutakuwa tumetimiza wajibu wetu pia kama tutaweza kumshauri endapo tu hii motive yake ina nia njema na nchi hii .... tusiishie tu kukatisha watu tamaa, kulalamika na kulialia hovyo ... we need solutions jamani!
 
Namshauri kama lengo lake ni kujitutuma aonwe na wananchi wa kiteto ili wampe ubunge afanye hivyo bila kuvunja katiba,na kama anataka sana kukata watumishi mishahara yao basi afanye hivyo kwa house girl/boy wake(kama anao),maana hao ndiyo wapo chini yake kiuajiri!

malafyale ... you can do better than this ... !!
 
nadhani tutakuwa tumetimiza wajibu wetu pia kama tutaweza kumshauri endapo tu hii motive yake ina nia njema na nchi hii .... tusiishie tu kukatisha watu tamaa, kulalamika na kulialia hovyo ... we need solutions jamani!

Bahataji mbaya watendaji wetu hawa hawaendi na nayakati.Haya ni maamuzi ya 1980s...kama sikosei huyu mama alikuwa Iringa kabla ya pwani na alileta taabu na mabo ya lumbesa na vipimo vya mazao...yeye ni mtu wa statistics nadhani..jaribu kufikiri mkuu wa mkoa(sio huyu) anapoamuru kila mwanakijiji alime ekari 4 za muhugo..halafu waupeleke wapi..hawawezi uziana maana kila mtu anao...hawawezi safirisha barabara hakuna...matokeo yake kuozea shamba..ukilima mahindi ukavuna mabichi unakamatwa...unazuiwa lumbeza wakati tatizo ni upungufu wa magunia
 
malafyale ... you can do better than this ... !![/QUOTE

Please accept my apologetic attitudes(if any)kwa habari hii hasa kama imekukukwaza mwana jf mwenzangu Madabwada!

Huyu Coastal Region RC alinikera sana na ha-make sense at all,kama ndiyo ingekuwa ukiwa mtendaji mbaya unakatwa mshahara basi angekatwa toka Jk na baraza lake lote na wengine wengi aliowateua akiwemo yeye maana hakuna walilowatendea kuwapa maisha bora watz;achilia wabunge wetu wengi ambo ni gvt rubber stamp!

kwanza suluhisho la kuwaondoa wafanyakazi inefficient sio kuwakata mishahara bali ni kuwafukuza kazi jambo ambalo litafanywa na mwajiri wao na huyu mama sio mwajiri wa watumishi hawa!

kukatwa mtu mshahara ni kinyume na utawala bora na hapo labda ndipo nikakasirika hadi nikateleza kuandika ndugu madabwada-nisamehe sana!
 
Interesting..

Najiuliza watakataje mishahara wakati inapitia Benki kutoka Hazina...Nasikia dalili ya sarakasi na muwasho wa upupu hapa.
 
kimsingi kama ndivyo alivyo; hafai kuwa Mbunge wa kawaida. Anatakiwa kuwa mbuneg wa kuteuliwa halafu anapewa uwaziri wa kusimamia matokeo.. we need results oriented leadership..

MM,
Hata akipitia kwetu Wananchi, si bado Muhusika wa wakati huo anaweza kumtunuku hiyo nafasi kulingana na uwezo wake? au taratibibu zinasemaje!
 
malafyale ... you can do better than this ... !![/QUOTE

Please accept my apologetic attitudes(if any)kwa habari hii hasa kama imekukukwaza mwana jf mwenzangu Madabwada!

Huyu Coastal Region RC alinikera sana na ha-make sense at all,kama ndiyo ingekuwa ukiwa mtendaji mbaya unakatwa mshahara basi angekatwa toka Jk na baraza lake lote na wengine wengi aliowateua akiwemo yeye maana hakuna walilowatendea kuwapa maisha bora watz;achilia wabunge wetu wengi ambo ni gvt rubber stamp!

kwanza suluhisho la kuwaondoa wafanyakazi inefficient sio kuwakata mishahara bali ni kuwafukuza kazi jambo ambalo litafanywa na mwajiri wao na huyu mama sio mwajiri wa watumishi hawa!

kukatwa mtu mshahara ni kinyume na utawala bora na hapo labda ndipo nikakasirika hadi nikateleza kuandika ndugu madabwada-nisamehe sana!

malafyale tuko pamoja mkuu ... tuendelee kutaka issues kwa manufaa ya taifa letu ... naheshimu sana michango yako humu ndani ndio maana nikashtushwa na tamshi lako ... lakini sio issue .. naomba tuendelee na mjadala
 
Interesting..

Najiuliza watakataje mishahara wakati inapitia Benki kutoka Hazina...Nasikia dalili ya sarakasi na muwasho wa upupu hapa.

mkuu inawezekana pia alitamka hivyo akiwa anaamini kuwa wana-share the same opinion na ngazi husika za maamuzi za hao maafisa na hivyo atalifikisha hilo suala huko e.g waziri husika and the like.
 
mkuu inawezekana pia alitamka hivyo akiwa anaamini kuwa wana-share the same opinion na ngazi husika za maamuzi za hao maafisa na hivyo atalifikisha hilo suala huko e.g waziri husika and the like.

But that is neither the procedure nor permitted by the new labour act....I hope that it was just a blip of the tongue
 
Interesting..

Najiuliza watakataje mishahara wakati inapitia Benki kutoka Hazina...Nasikia dalili ya sarakasi na muwasho wa upupu hapa.

Ab,
Ikiwa ana Dhamira ya kweli , ni kiasi tu cha kuwaandikia Hazina. Tatizo laweza kuwa la kisheria (pengine) Je ana mamlaka ya kufanya hivyo kisheria?
 
mkuu inawezekana pia alitamka hivyo akiwa anaamini kuwa wana-share the same opinion na ngazi husika za maamuzi za hao maafisa na hivyo atalifikisha hilo suala huko e.g waziri husika and the like.

Binafsi ningemuona wa maana kama angawakatalia safari na fedha za vikao hususan kwenye ile miezi ya kufunga mwaka wa fedha lol...maana hapo ndo hawa wahishimiwa wanapopiga bao la kisigino. Unambana mhasibu akupe mahesabu ktk kipindi cha utekelezaji wa adhabu..

Otherwise hizo ni kauli tu za kuelekea uchaguzi, kila mtu anaangalia atoke vipi.
 
Baadhi ya watz watu wa ajabu sana siku hizi,mtu anavunja sheria the great thinkers tunakuja hapa kusifia!

Kwani huyu mama ndiye Waziri mkuu wetu?Huyu mama hivi sasa ndiye waziri wa UTUMISHI?huyu mama ndiye waziri wa TAMISEMI?

kama hana nafasi hizo 3 nilizotaja juu,basi kwa madaraka gani ndani ysa katiba ya jamhuri ya tz inayompa nguvu kufanya haya aliyoyafanya kwa maafisa wenzake wa serikali kuu?

Namshauri kama lengo lake ni kujitutuma aonwe na wananchi wa kiteto ili wampe ubunge afanye hivyo bila kuvunja katiba,na kama anataka sana kukata watumishi mishahara yao basi afanye hivyo kwa house girl/boy wake(kama anao),maana hao ndiyo wapo chini yake kiuajiri !

kweli umefulia saaana kisiasa na nadhani una homa ya uchaguzi... hata kama anakosea, umeiweka vibaya!!!

Ninajua unaelewa role na nafasi ya mkuu wa wilaya au mkoa!! na unaelewa vyeam decentralization ya utawala wetu --- you disappoint me on this argument
 
Back
Top Bottom