Ujasiriamali Haujaribiwi Aiseee

Ujasiriamali Haujaribiwi Aiseee

ELAFU

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2014
Posts
410
Reaction score
150
Napenda Kutumia Fursa Hii Kuwajuza Wale Wanaotaka "kujaribu" Ujasiriamali Kwamba Hiyo Ni Moja Kati Ya Wazazi Wa Matatizo Na Changamoto Lukuki! Ukitaka Kufanya Ujasiriamali Ufanye Tu Kwa Moyo Mmoja, Na Si Kujaribu; Na Kama Ukihisi Uwezi Basi Ongeza Juhudi Katika Mambo Yako Mengine Utafanikiwa Vyema Tu. Hata Kama Una Mtaji Wa 100,000/= Tu Amua Kuwa Committed Na Uwe Serious Kweli, Utarudisha Mtaji Wako Wote Na Kupata Faida Lukuki (kipato, Ajira, Uhuru, Muda N.K.). Jiandae Kwa Changamoto Mbalimbali ( Loss, Overworking, Kodi, Hali Ya Hewa, Wateja Wasumbufu, Bidhaa Kuharibika, Mtaji Kupungua Au Kukata, Muda, Price Fluctuations, Sheria Za Nchi HII N.K.) Na Ukaze Msuli Kweli Huku Ukizipatia Changamoto Zote Ufumbuzi Wa Kudumu. Omba Mungu Kwa Imani Thabiti Na Uchape Sana Kazi Hadi Upate Mafanikio Uliyokuwa Unayataka. Ukiingia Kwa Kujaribu Ndugu Yangu Jiandae Kushindwa Changamoto Na Kubwaga Manyanga. Kwa Leo Naomba Niishie Hapa.
 
Mpwa umekuja na mada nzuri sana ila umekuja na vitisho pia! Hakuna kitu duniani kisichokuwa na changamoto... kikubwa ni kuwa committed na kufanya research ya kutosha pia kuwa na interest na hicho unachokitaka na sio kufuata mkumbo!

Kwa mfano umekaa mahali; kijiweni, Bar, Msibani, n.k kwenye story za hapa na pale unakuta watu wanasema ufugaji wa kuku unalipa sana! Unavutiwa na mada hio kwahio unachotakiwa kuangalia ni je ntaweza na sio ku conclude kuwa itanilipa!

Kama kweli imekuvutia unatakiwa kufanya yafuatayo, tulia, jipe muda wa kuwaza kwa kina na kusoma na kuuliza kwa watu ambao ni wafugaji! Wanasemaje? Kisha jihoji wewe mwenyewe.

Pili, andaa mazingira ya kuwezekana na sio ya kujaribu!

Tatu, muda ni muhimu sana kwa kila kitu! Hakikisha una dedicate muda wako mwingi kwenye hio business kuliko kwenye starehe na vitu vingine.

Nne, epuka kujipa excuse za kijinga.

Tano, Usichanganye kazi yako hio au biashara yako na undugu au urafiki uliopitiliza.

Suala la mtaji ni muhimu sana na ukiamua kufanya jambo fanya na sio kujaribu! Hapa wengi ndio tunapotea njia.

Zijue zile main challanges kabla ya kaunza na jinsi unavyoweza kuzikabili.... i am sure tutafanikiwa tukifanya sehemu yetu na Mungu akiwa upande wetu
 
Kwa uvivu wetu watanzania nasapoti lugha/vitisho alivyotumia mtoa mada.
Hongera mtoa mada.
 
Mpwa umekuja na mada nzuri sana ila umekuja na vitisho pia! Hakuna kitu duniani kisichokuwa na changamoto... kikubwa ni kuwa committed na kufanya research ya kutosha pia kuwa na interest na hicho unachokitaka na sio kufuata mkumbo!

Kwa mfano umekaa mahali; kijiweni, Bar, Msibani, n.k kwenye story za hapa na pale unakuta watu wanasema ufugaji wa kuku unalipa sana! Unavutiwa na mada hio kwahio unachotakiwa kuangalia ni je ntaweza na sio ku conclude kuwa itanilipa!

Kama kweli imekuvutia unatakiwa kufanya yafuatayo, tulia, jipe muda wa kuwaza kwa kina na kusoma na kuuliza kwa watu ambao ni wafugaji! Wanasemaje? Kisha jihoji wewe mwenyewe.

Pili, andaa mazingira ya kuwezekana na sio ya kujaribu!

Tatu, muda ni muhimu sana kwa kila kitu! Hakikisha una dedicate muda wako mwingi kwenye hio business kuliko kwenye starehe na vitu vingine.

Nne, epuka kujipa excuse za kijinga.

Tano, Usichanganye kazi yako hio au biashara yako na undugu au urafiki uliopitiliza.

Suala la mtaji ni muhimu sana na ukiamua kufanya jambo fanya na sio kujaribu! Hapa wengi ndio tunapotea njia.

Zijue zile main challanges kabla ya kaunza na jinsi unavyoweza kuzikabili.... i am sure tutafanikiwa tukifanya sehemu yetu na Mungu akiwa upande wetu

Thanx man for the best idea.
 
Back
Top Bottom