Ujenzi wa barabara na reli viende sambamba na uchumi wa maeneo

Ujenzi wa barabara na reli viende sambamba na uchumi wa maeneo

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Kama barabara hizi hazitatumika kusafirisha mazao, mifugo na bidhaa kwenda na kutoka zinakopita zitatumiwa na wananchi kusafirisha vyuma vya madaraja na alama za barabarani vya barabara hizo vilivyokatwa na kung'olewa na wananchi kwenda kuuza na kujipatia fedha ya kujikimu.

Tunapomimina hela za kujenga barabara tumimine fedha wakati huohuo fedha za kuboresha kilimo, ufugaji na bidhaa ningine.

Kugawa ardhi ya mashamba makubwa yaliyokuwa ya mifugo, katani, ngano, mpira, nk kwa wakulima wadogo wanaolima kwa jembe la mkono na mbegu za kizamani ni kuendeleza umaskini wao na taifa.

Mashamba makubwa (plantations and ranches) yataajiri vijana wengi zaidi kuliko kugawa ardhi kwa mtu mmojammoja. Mashamba madogo yawepo lakini mashamba makubwa ya wawekezaji wakubwa yawepo pia.
 
Kama barabara hizi hazitatumika kusafirisha mazao, mifugo na bidhaa kwenda na kutoka zinakopita zitatumiwa na wananchi kusafirisha vyuma...
Sisi tulipaswa tuwe wasambaji wakubwa wa ngano, mafuta ya alzeti na gesi duniani lakini kwa uongozi mbovu wa CCM sisi ndiyo ombaomba wakubwa
 
Sisi tulipaswa tuwe wasambaji wakubwa wa ngano, mafuta ya alzeti na gesi duniani lakini kwa uongozi mbovu wa CCM sisi ndiyo ombaomba wakubwa
kiongozi uchwara anaamua kugawia wapiga kura mashamba ya katani, kahawa, ngano, mifugo badala ya kuyafufua yazalishe kisasa yatoe ajira kwa vijana wengi na kuongeza pato la taifa.
 
Back
Top Bottom