Ujenzi wa Msalato international airport wazidi kunoga –PAC yaridhishwa na maendeleo, yaagiza ukamilike kwa haraka na ubora

Ujenzi wa Msalato international airport wazidi kunoga –PAC yaridhishwa na maendeleo, yaagiza ukamilike kwa haraka na ubora

Venus Star

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2018
Posts
26,519
Reaction score
78,311
Mradi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato jijini Dodoma umeendelea kuonyesha maendeleo makubwa, huku kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) ikieleza kuridhishwa na hatua zilizofikiwa hadi sasa. PAC imeitaka serikali na wakandarasi kuhakikisha mradi huu unakamilika haraka lakini pia kwa kuzingatia ubora wa viwango vya kimataifa.

View: https://youtu.be/NMnvY1Skd0w?si=b1fHED1mTmyBNQhr
Uwanja wa Msalato, unaojengwa kwa gharama ya zaidi ya Shilingi trilioni 1.7, ni miongoni mwa miradi mikubwa ya kimkakati inayotarajiwa kubadilisha sura ya mji wa Dodoma na kuitangaza Tanzania kimataifa. Uwanja huu unalenga kukidhi mahitaji ya usafiri wa anga yanayoendelea kuongezeka kutokana na ongezeko la shughuli za kiserikali, biashara, na uwekezaji katika makao makuu ya nchi.

Faida za Uwanja wa Msalato:

  1. Kuongeza kasi ya maendeleo ya kiuchumi kwa Dodoma na mikoa jirani.
  2. Kukuza sekta ya utalii kwa kuwarahisishia watalii kutoka nje kufika kwenye vivutio vya Kati na Kusini mwa Tanzania.
  3. Kuwavutia wawekezaji wa kimataifa kupitia miundombinu bora ya usafiri wa anga.
  4. Kuboresha usafirishaji wa mizigo hasa mazao ya kilimo na bidhaa nyingine kutoka Kanda ya Kati.
PAC imesisitiza umuhimu wa kuzingatia ratiba ya mradi huu na kuhakikisha kuwa fedha zinazotumika zinaleta thamani kwa wananchi. Aidha, imeipongeza serikali kwa kusimamia vyema mradi huu huku ikiahidi kufuatilia maendeleo hadi pale uwanja utakapokamilika rasmi.

Wananchi wameendelea kufuatilia mradi huu kwa matumaini makubwa, wakiamini kuwa uwanja huu utafungua fursa mpya kwa kila sekta na kuipa Tanzania heshima kimataifa.

#MsalatoInternationalAirport
#DodomaMakaoMakuu
#MiradiYaKimkakati
#MaendeleoKwaVitendo
 
Pac wao Huwa wanaridhishwa tu Kila mradi wa aina yeyete?Sijawahi kuwasikia kabisa waliona mapungufu kwenye mradi wowote wanaoutembelea lakini CAG akiupitia unakuta madudu mengi kabisa.
 
Pac wao Huwa wanaridhishwa tu Kila mradi wa aina yeyete?Sijawahi kuwasikia kabisa waliona mapungufu kwenye mradi wowote wanaoutembelea lakini CAG akiupitia unakuta madudu mengi kabisa.
Tupatie mfano wa mradi mwingine. Tanzania ipo na miradi zaidi ya 100,000 hebu tupatie orodha ya miradi 10 tu ambayo PAC wameridhishwa nayo.
 
Hivi airport ya Mwanza imefikia wapi? Mara ya mwisho nimepita pale aisee inasikitisha sana ukiangalia yale majengo
 
Hivi airport ya Mwanza imefikia wapi? Mara ya mwisho nimepita pale aisee inasikitisha sana ukiangalia yale majengo
Nchi ya wajinga hii! Kiwanja chenye abiria wengi wa ndani hakijengwi wanajenga Dodoma kisa makao Makuu!
 
Nchi ya wajinga hii! Kiwanja chenye abiria wengi wa ndani hakijengwi wanajenga Dodoma kisa makao Makuu!
Wewe upo naakili nyingi kuliko watanzania zaidi ya 60m? 🤣 🤣 🤣 🤣
Utoto raha sana
 
Wewe upo naakili nyingi kuliko watanzania zaidi ya 60m? 🤣 🤣 🤣 🤣
Utoto raha sana
Utoto gani? Kujenga Dodoma sio shida shida je Dodoma ina abiria wengi kuzidi Mwanza?
Usiongee kama chawa ongea uhalisia!
 
Hivi airport ya Mwanza imefikia wapi? Mara ya mwisho nimepita pale aisee inasikitisha sana ukiangalia yale majengo
Mwenye mradi kashaondoka, kwani ule wa Chato umefikia wapi sasa?
 
Haukuwa mradi wake, ni mradi wa nchi.
Mbon hiyo miradi pamoja na ule wa Chato-Burigi national parks imedorora baada ya yeye kuondoka. Mbona hata zile taa za barabani na miradi mingine mingi tu kule Chato imesimama? Mwenye miradi hayupo.
 
Ukiachana na airport dodoma, Inatakiwa wawekeze kwenye kumbi za kimataifa za mikutano kama 10. Wawekeze kwenye sekta ya utalii wa kimikutano, inaitwa MICE Tourism

Meetings, incentives, conferences and exhibitions tourism (MICE tourism) is a type of tourism in which large groups, usually planned well in advance, are brought together. Recently there has been an industry trend toward using the term "meetings industry" to avoid confusion from the acronym.[1] Other industry educators[who?] are recommending the use of "events industry" to be an umbrella term for the vast scope of the meeting and events and profession
 
Back
Top Bottom