Ujenzi wa nyumba za kuficha paa/contemporary/ hidden roof

Ujenzi wa nyumba za kuficha paa/contemporary/ hidden roof

Habari waungwana na wadau wa ujenzi.
Nawajaribisha tushirikiane kujadiliana aina hii ya ujenzi kwa wataalam na wadau wa ujenzi wa aina hii....karibuni
1.Je una changamoto katika ujenzi wa nyumba tajwa hapo juu?

2. Umejengewa nyumba ukakutana na changamoto ya kuvuja?

3. Wewe ni mjenzi na hujui namna ya kujenga kwa usahihi nyumba za kuficha paa?

4. Una ndoto ya kujenga nyumba za aina hii lkn hujui gharama zake?

Niko hapa kutoa ushauri bure kabisa.

View attachment 1803969View attachment 1803971


......................................................................................
Chukua haya yafuatayo;
1. Msingi uinuke
2. Boma liwe na tofali laini 11
3. Baada ya lenta hakikisha unatengeneza sehemu ya kupokelea maji
4. Pawepo na ducts za kupitishia maji na sio bomba
5. Upake bitumen pamoja na mebrane cloth maeneo ya wazi ya kupokelea maji.

6. Epuka slop ndefu za paa bali livunje vunje vipande vipande ili maji yashukie sehemu tofauti

Ukizingatia haya nyumba hii hsivuji na utaifurahia na haina gharama kubwa
Tafadhali tufahamishe kimo kilichopo kati ceiling board na paa/bati.
Wiring ya hizi nyumba kwenye roof hufanyikia wapi ukilinganisha na nyumba za kawaida?
 
Kwa utafiti wangu mdogo nimeufanya, wengi wanaosema hazifai wapo na maneno ya kuambiwa. Hawajawahi hata kujenga hizo nyumba. Ni kama wale wanaokwambia usinunue Nissan haifai kabisa, ukiuliza kama amewahi hata kumiliki utagundua ni maneno ya kijiweni.

Nakubaliana na wanaosema tatizo ni mafundi. Nyumba hizi zinahitaji fundi anayezijua. Tatizo lipo kwa wenye nyumba, unamuamini fundi aliyekufanyia kazi za tofali akuezekee na bati tu kwa sababu gharama amefanya ndogo.

Contemporary ni zaidi ya kuezeka na mafundi wazuri wapo.
Weka uzuri na ubaya wa hizo nyumba ili watu wapate kifahamu.
 
Mafundi wengi hawawezi kuziezeka japo kwa tamaa zao watakupa moyo na maneno mengiijj, mwisho Wa siku kuvuja kupo pale pale mnaanza kuzungushana. Mafundi wanaozimudu wapo ila ni wachache sana
Kiufupi hakuna fundi anayezimudu kwenye upauaji uezekaji .
 
Kiufupi hakuna fundi anayezimudu kwenye upauaji uezekaji .
Hakuna fundi anayezimudu kupaua au wewe ndio huwajui mafundi mkuu??

Tatizo kinachowacost watu ni kutokujua
Hizi nyumba sio kwamba gharama inapungua kama wengi wanavyodhania, ile gharama inayopungua kwenye bati na mbao utaifidia pale kwenye gata, na ikitokea fundi wako amejenga gata la kubana matumizi hapo sasa ndio utavujiwa mpaka akili ikukae sawa.
 
Weka uzuri na ubaya wa hizo nyumba ili watu wapate kifahamu.
Uzuri au Ubaya wa kitu chochote upo kwa mtu anayehitaji hicho kitu. Ndiyo maana pamoja na watu kusikia kwamba nyumba za namna hiyo huvuja sana (Mabaya) lakini hawaachi kujenga.
Ila kwa upande wangu naweza sema, uzuri wa nyumba hizi kwa uchache

1. Zina muonekano mzuri kama mchora ramani yako alikuwa vyema kwenye kuinakshi hiyo ramani na ukapata mtu sahihi wa kufanya finishing.
2. Inaokoa gharama ya mbao kwa kiasi fulani
3. Inaokoa gharama ya bati kwa kuwa bati unayoweka yaweza kuwa ya kawaida kimuonekano lakini ni bati bora.

Ubaya
1. Ni nyumba inahitaji maintainance kubwa zaidi ukilinganisha na aina ingine.

Kumbuka, pamoja na huo unaitwa ubaya wa kuvuja kwa nyumba hizi, hata ukipiga bati kawaida na usipopata fundi mzuri lazima zivuje.

Asante
 
Mbona swali lako hili pia ni la kijinga! Kwani elimu ndo inajenga nyumba au ujuzi wa mtu! Hujifunzi kwa mainjia wale wa majengo wanavoharibu kazi na mavyeti yao!
Jamaa anadhani vyeti ndio kila kitu.. nina watu si chini ya watano nawafahamu hawajamaliza hata darasa la 7 ila ni mafundi wazuri mno mno mno kuliko graduates wengi tu
 
Tafadhali tufahamishe kimo kilichopo kati ceiling board na paa/bati.
Wiring ya hizi nyumba kwenye roof hufanyikia wapi ukilinganisha na nyumba za kawaida?
Mkuu komaa kwanza na kujulishwa namna ya kuzuia kuvuja mengine baadae,mana hilo ndio tatizo kuu la hizo nyumba. Nazipenda sana ilazishaanza kunikaatishaa tamaa. Fundi wengi wanaashindwa kuezeka vema, hivyo zinavuja sana
 
Kuna post moja juzi
Mvua imenyeshaa bati imeshukia ndani
Chumbani kumegeuka bwawa

Nkasema hii style basi tena
Ngja tuendelee na style zinazojulikana
 
Back
Top Bottom