Ujenzi wa nyumba za kuficha paa/contemporary/ hidden roof

Ujenzi wa nyumba za kuficha paa/contemporary/ hidden roof

Kaka hebu nieleweshe wakati naanza ujenzi sikuwaza ujenzi wa namna hii lakini nyumba imefika saiz ya lenta inawezekana nisiezeke bâti?
Paua kawaida tu, nyumba nyingi wanazochange huwa contempo huwa hazina muonekano mzuri
 
Paua kawaida tu, nyumba nyingi wanazochange huwa contempo huwa hazina muonekano mzuri
Inategemea mkuu maana ukiacha mbwembwe zingine,huo muonekano utatafutwa kwa kuezeka mapaa yanayomwaga maeneo tofauti..

Nimeona nyumba ya hivyo haina marembo ya nje ila baada ya ku design mapaa ikawa na muonekano mzuri.

Ishu ya hizo nyumba ni kupata fundi mtaalamu.
 
Kaka hebu nieleweshe wakati naanza ujenzi sikuwaza ujenzi wa namna hii lakini nyumba imefika saiz ya lenta inawezekana nisiezeke bâti?
Inawezekana sana mkuu japo inaweza kuhitaji kuongezea vionjo kidogo.

Ninaomba radhi sikuingia jf muda nilikuwa nje kikazi na mazingira hayakuwa na internet access ya ihakika
 
Kuna post moja juzi
Mvua imenyeshaa bati imeshukia ndani
Chumbani kumegeuka bwawa

Nkasema hii style basi tena
Ngja tuendelee na style zinazojulikana
Tatizo sio muundo bali nani kajenga mkuu.
Si kila anayeitwa fundi anaweza kupaua au kujenga nyumba hii
 
Hakuna fundi anayezimudu kupaua au wewe ndio huwajui mafundi mkuu??

Tatizo kinachowacost watu ni kutokujua
Hizi nyumba sio kwamba gharama inapungua kama wengi wanavyodhania, ile gharama inayopungua kwenye bati na mbao utaifidia pale kwenye gata, na ikitokea fundi wako amejenga gata la kubana matumizi hapo sasa ndio utavujiwa mpaka akili ikukae sawa.
Uko sahihi sana.
Kuna kitu tunaita Duct hii ni muhimu sana tena ziwe zaidi ya 4 hii hupokea maji kutoka gata
 
Uzuri au Ubaya wa kitu chochote upo kwa mtu anayehitaji hicho kitu. Ndiyo maana pamoja na watu kusikia kwamba nyumba za namna hiyo huvuja sana (Mabaya) lakini hawaachi kujenga.
Ila kwa upande wangu naweza sema, uzuri wa nyumba hizi kwa uchache

1. Zina muonekano mzuri kama mchora ramani yako alikuwa vyema kwenye kuinakshi hiyo ramani na ukapata mtu sahihi wa kufanya finishing.
2. Inaokoa gharama ya mbao kwa kiasi fulani
3. Inaokoa gharama ya bati kwa kuwa bati unayoweka yaweza kuwa ya kawaida kimuonekano lakini ni bati bora.

Ubaya
1. Ni nyumba inahitaji maintainance kubwa zaidi ukilinganisha na aina ingine.

Kumbuka, pamoja na huo unaitwa ubaya wa kuvuja kwa nyumba hizi, hata ukipiga bati kawaida na usipopata fundi mzuri lazima zivuje.

Asante
Unajua sababu ya kuvuja?
 
Fikiria umelala zako usingizi mzito, mvua kubwa inanyesha, ni saa saba usiku alafu inaanza kuvuja na hapohapo umeme unakatika.
Kwanini uvujiwe?

Tatizo wengi mnadharau taaluma za watu mnachozingatia ni bei nafuu huko ndiko mnalizwaga mkuu
 
Unajua sababu ya kuvuja?
Cyanee naomba kama utanisaidia kupata Ka ramani kazuri ka chumba kimoja na choo chake,chumba kikubwa wastani ila kachumba kawe na paa la kuficha kama hilo,ikikupendeza unipe gharama za ujenzi na gharama za nyumba mpaka nahamia.

Kama Mungu akipenda na wewe ukipenda pia nitafurahi ukiwa fundi wangu kwenye hako ka master single room.

Bei ujumuishe kila kitu kuanzia material mpk Ufundi ikikupendeza hapahapa kwa faida ya wengi,ya ufundi ndio unaweza nitumia Inbox kama utaona soo kuiweka hapa.Asante.
 
Cyanee naomba kama utanisaidia kupata Ka ramani kazuri ka chumba kimoja na choo chake,chumba kikubwa wastani ila kachumba kawe na paa la kuficha kama hilo,ikikupendeza unipe gharama za ujenzi na gharama za nyumba mpaka nahamia.

Kama Mungu akipenda na wewe ukipenda pia nitafurahi ukiwa fundi wangu kwenye hako ka master single room.

Bei ujumuishe kila kitu kuanzia material mpk Ufundi ikikupendeza hapahapa kwa faida ya wengi,ya ufundi ndio unaweza nitumia Inbox kama utaona soo kuiweka hapa.Asante.
Ramani nitakuandalia mkuu.
Kuhusu kukujengea zaidi nitakupa ushauri
Utumie fundi wako mkuu.

Na usijali nitakushauri viziri fundi yeyote mwenye akili kwa maelekezo yangu atafanya kazi nzuri kabisa...najijua mimi ni zaidi ya mwalimu katika taaluma hii
 
Back
Top Bottom