Ujio wa Obama: Kashfa ya kupokwa ulinzi, vyombo vya habari vinavyoiona Tanzania

Ujio wa Obama: Kashfa ya kupokwa ulinzi, vyombo vya habari vinavyoiona Tanzania

Candid Scope

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
11,897
Reaction score
6,925
article-0-1A9D8EEB000005DC-962_634x384.jpg

United in remembrance: The two presidents bowed their heads as a Marine placed the wreath of red,
white and blue flowers in front of the large stone memorial to the Tanzanian victims of the
simultaneous attacks at the U.S. embassies here and in Kenya masterminded by
Osama bin Laden

Mara kadhaa tumetembelewa na Viongozi wa juu wa Taifa la Marekani, lakini hatujapata kuona mfumo wa ulinzi na usalama wa viongozi hao kuwa wa pekee na kufikia kutoaminika kwa vyombo vya usalama nchini. Mara zote ulinzi ulikuwa shirikishi tofauti na ulinzi wa Obama ambapo hata tu viongozi wa juu serikalini kama mawaziri kuambiwa watachujwa watakaokaribia na kusalimiana na Obama. Nini nyuma ya pazia kwa vigezo vipya kwa ulinzi na usalama wa viongozi wa Marekani kuwepo nchini kipindi hiki tofauti na miaka ya nyuma? Wingi wa baraza la mawaziri nchini umechangia kuchujwa?

Vyombo vya usalama vya Marekani kupokonya majukumu ya vyombo vya usalama vya Tanzania
Ilielezwa kwamba vyombo vya usalama kutoka marekani vilipokonya jukumu la ulinzi wa viongozi wa msafara wa Rais Obama na delegates wake hapa nchini na kuonyesha kila dalili ya kutoamini vyombo vya usalama vya nchi mwenyeji Tanzania. Pamoja na Rais Obama kuanzia ratiba ya huko West Afrika na kisha South Afrika jambo la vyombo vya usalama vya huko kupokonywa haki za kukendesha usalama hazikusikika kama ilivyotokea hapa.

Mapokezi ya viongozi wa awali wa Marekani kutembelea hapa nchini hapakuwa na hali iliyojitokeza safari hii kwani kulikuwepo ushirikiano zaidi na kuaminiana zaidi. Jambo kubwa na la msingi serikali kulitathmini kwa nini imetokea hivyo leo tofauti na siku za nyuma. Rais Obama anapokeleka zaidi ulimwenguni kuliko ilivyokuwa Rais wa zamani wa marekani George Bush, lakini kwa nini itokee hivyo kwa Obama tena Mwafrika mwenzetu?

Mchujo wa viongozi wa Serikali kumpokea na kumwaga Obama
Habari ambazo hazikufichwa kwenye mafaili maofisini juu ya jopo la viongozi wa kumpokea Obama uwanjani ni kwamba vyombo vya usalama vya Marekani kuiwekea ngumu Serikali katika orodha ya viongozi wa kujumuika kumpokea Obama. Mbali zaidi kwamba orodha ya viongozi watakaojumuika kumpokea itatolewa na Wamarekani wenyewe na kwamba hata mawaziri so wote watakaobahatika kumshika Mkono Obama atakapotua uwanjani. Kiwango hicho si cha kawaida, pengine Wamarekani kuwa na hisia mbaya kwa baadhi ya viongozi waandamizi serikalini na hivyo kuwawekea ngumu?

Utekelezaji wa mpango huko unaonekana kufana kutokana na baadhi ya viongozi waandamizi serikalini waliozoeleka kuwa karibu na Mkulu latika mtukio kama haya kutoonekana, sina maana waliwekwa kando na vyombo vya usalama Marekani, labda waliamua kuondokana na udhia huo. Hata katika safu ya utambulisho wa viongozi wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar Makamu wa Kwanza wa Rais hakujumuishwa, labda tu ratiba ziliingiliana kwa tafsiri nyepesi.

Mood ya uwajibikajia vyombo vya usalama Marekani tofauti na vya hapa nchini vinavyokandamiza raia
Tukio ambalo limeanikwa hadharani na chombo kimojawapo cha habari nchini juu la purukushani iliyotoka Makumbusho kwa Mwanausalama mzawa kumdhalilisha mwandishi wa Gazeti la Uhuru, na kisha dada huko mwandishi kuokolewa na Mwanausalama wa Marekani kwa kumtetea na kulinda haki zake za msingi kama binadamu na mwandishi akiwa kazini ni jambo ambali limezidi kuvichafua vyombo vya usalama nchini katika kile kilichozoeleka juu ya udhalilishaji.

Mbaya zaidi lugha aliyotoa yule Mwanausalama wa Marekani kwa mwanausalama mzawa kwamba:
"Hivi ndivyo mnavyofundishwa katika uwajibikaji kazini," ni aibu kubwa kiasi kwamba mwanausalama wa Marekani uvumilivu ulimshinda na kuamua kumwambia wazi na kumruhusu dada aendelee na shughuli iliyomfikisha pale Makumbusho.

Vyombo vya kimataifa vinanyoshea kidole CCM na Serikali na kuisafisha CHADEMA
Uwepo wa Rais Obama nchini kwa vile anatoka Taifa kubwa duniani, vyombo mbalimbali vya habari vikubwa duniani vilikuwepo nchini. Kama ilivyo ada vyombo hivyo havifutatilii ziara hiyo tu, ila pia kuisoma nchi yetu kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni nk.

Pamoja na vyombo hivyo kuisifia Tanzania katika makaribisho ya Rais Obama yasiyo ya kawaida na kuzidi sehemu nyingine alizotembelea hapa Afrika, vyombo hivyo vya habari havikuchelea kusoma hali ya kisiasa nchini na matukio ya uvunjaji wa amani ikiwa ni pamoja na matukio ya mabomu Arusha kwenye kanisa na mkutano wa Chadema. Vyombo hivyo tofauti na mtazamo wa serikali ya Tanzania pamoja na CCM inavyoitazama Chadema na vyama vingine vya upinzania, vimeonyesha dalili ya kwamba vyama vya upinzani vinakandamizwa. Vyombo hivyo vimegusia kuhusu kufungiwa Gazeti la Mwanahalisi, Kuuawa Mwangosi, Kutekwa na kuteswa Mwenyekiti wa madaktari nchini na Mwandishi wa Habari Kibanda.

Magazeti mbalimbali ya Marekani New York Time, Washington Post, USA Today, na mengineyo, Magazeti ya UK, vyombo vya habari vingine kama CNN, BBC, FOX, Yahoo, Microsoft, ABC, Nk vimeonyesha jinsi demokrasia inavyokandamizwa nchini kwa njia mbalimbali na kuonyesha dalili ya serikali ya Tanzania kuifanyia kazi ili kulinda amani ya nchi.

OB-YB148_obamas_G_20130702100658.jpg

Obama receives a pass from Tanzania’s President Jakaya Kikwete during the demonstration at the Ubungo Power Plant

Marekani imeacha ujumbe serikali inatakiwa kufunguka kuuelewa ujumbe huo

Nchi zilizoendelea huwa hazitoi jumbe zao kama kufundisha chekechea, hutumia mfumo wa kifalsafa zaidi iwe kimatendo, maoni ya vyombo vya habari na hotum\ba za viongozi wao.
Rais Obama
Pamoja na kutumia sana diplomatic language, amesema wazi maendeleo Afrika yataletwa na Waafrika wenyewe si na wageni. Ujumbe huo ni mzito ingawa tunaujadili mara kwa mara. Pengine misafara ya viongozi wetu kuzungukia dunia kila kukicha kusingepewa uhimu zaidi, bora kutulia nchini na kuwa karibu zaidi na wananchi ili kujadiliana namna bora ya kuleta maendeleo kwa kutumia zaidi tulicho nacho kuliko pesa tunayopata toka nje wakati tunapoenda kuitafuta tunatumia gharama kubwa kuliko pesa tunayopata.​

Vyombo vya kumataifa kuanika madudu ya hapa nchini
Muhimu serikali ikatafakari juu ya kinachoendelea nchini hasa amani na utulivu ambao unaelekea ukingoni. Matumizi ya nguvu kutoka vyombo vya usalama, kauli tata za viongozi ni moja na viashiria vya kuchochea vurugu kama:​


  • [*=2]Rais Kikwete Mkutano Mkuu Dodoma - Nitahakikisha na kufanya kila niwezalo nakabidhi kiti cha urais kwa CCM
    [*=2]Waziri Mkuu Pinda Bungeni - Tumeagiza vyombo vya usalama viwapige wananchi tumechoka kuvumilia
    [*=2]Tamko kwa Tanzania Daima Jeshi la Wananchi - Tumeagizwa na serikali kuwachapa wananchi kulinda amani
Marekani licha ya Ziara ya Obama, Bush pia ameingia, yote kwa kiongozi mahiri na mwenye tafakari angeweza kujua mema ambayo Marekani inaitakia nchi hii, lakini kutotilia maanani asishangae hao hao Marekani kesho wakimgeuka, muhimu kusoma yasemwayo na vyombo vya kimataifa kwa kianchoendelea nchini.

Serikali itafakari kurejesha amani kidipolomasia badala ya matumizi ya nguvu
Serikali itafakari kwa nini inapofanyika mikutano ya vyama vya upinzani nchini bila uwepo wa jeshi la polisi hapajatokea mtafaruku wa uvunjaji amani. Hali kadhalika kuna ugumu gani kukaa na wananchi kuwasilikiza wanachokitaka kama suala ya gas ya Mtwara, maana hawa wananchi ndio wenye serikali, hawa viongozi wanapita, na ipo siku wananchi watatumia haki zao kuwatosa kwa vile hawawasikilizi.

Kikwete amemshauri Rais Wa Rwanda Kagame akae chini pamoja na wapinzani na kujadiliana ili kurejesha amani nchini humo, jambo hilo analiona zaidi Rwanda lakini hapa nchini haoni sababu ya kufanya hivyo ila kutuma vyombo vya usalama kuwapiga wananchi anakubaliana nalo?

Ziara ya Obama kupokonya usalama ni kutoaminika vyombo vya usalama nchini?
Vyombo vya habari nchini Marekani licha ya kutoonyesha moja kwa moja chanzo cha vurugu nchini na kutonyoshea kidole vyama vya upinzani bali kuonyesha kuna kitu kisichokuwa sawa ndani ya mfumo wa vyombo vya usalama nchini, dalili ya kupokonywa haki za kulinda ziara ya Obama huenda inatokana na kile kinachoendelea vyombo vya dola kukandamiza wananchi na pengine kusababisha mtafaruku wa amani. Milipuko ya mabomu yakutupwa kwa mkono Arusha pamoja na kuacha maswali mengi yasiyojibika kwa uwazi kutoka vyombo vya usalama nchini ni dalili tosha kutoaminika 100%.
 
Kabla ya kuja Obama katika hizi nchi Za kiafrika, vyombo vya ulinzi na usalama vya marekani viliweka wazi kuwa ulinzi wa rais wao wataufanya wao kwa 100%, sasa hapo ww ulichoa andika ni kipi?.

Kuna thread aliiandika humu ndani mwanakijiji itafute uisome ndipo utajua ulicho andika ni ----- na ni craaaaaap ndani ya JF.
 
jamaa watakuwa walipewa na ubaloz wao jinsi viongoz wa tz wanavyowatumia usalama wa taifa na vyombo vya dola kutesa na kuua na kulipua mabomu kwa chadema ndo mana wakawapga chini mawaziri kwa kuwa ubaloz wa marekan waliwapa inshu zote wanausalama wao znazoendelea humu na hawakuamin tena vyombo vyetu vya dola na wakawapga chn akna mwema na wasira na makapi mengne
 
jamaa watakuwa walipewa na ubaloz wao jinsi viongoz wa tz wanavyowatumia usalama wa taifa na vyombo vya dola kutesa na kuua na kulipua mabomu kwa chadema ndo mana wakawapga chini mawaziri kwa kuwa ubaloz wa marekan waliwapa inshu zote wanausalama wao znazoendelea humu na hawakuamin tena vyombo vyetu vya dola na wakawapga chn akna mwema na wasira na makapi mengne

Nimeshangaa kuto mwana Wasira na Mwema viongozi ambao mara nyingi wako karibu mno na Kikwete katika matuko mbalimbali. Hata Emmanuel Nchimbi naye sijui alijificha wapi.
 
Kabla ya kuja Obama katika hizi nchi Za kiafrika, vyombo vya ulinzi na usalama vya marekani viliweka wazi kuwa ulinzi wa rais wao wataufanya wao kwa 100%, sasa hapo ww ulichoa andika ni kipi?.

Kuna thread aliiandika humu ndani mwanakijiji itafute uisome ndipo utajua ulicho andika ni ----- na ni craaaaaap ndani ya JF.

Natanguliza shukrani kama utajibu hoja zangu kiufasaha badala ya majibu ya kunipeleka huko unakonielekeza. Hii si nukuru niliyoleta bali ni picha niliyoipata kwa kusoma na kusikiliza vyombo mbalimbali vya habari hali kadhalika kuisoma na kuelewa ziara nzima ya Rais Obama hapa nchini.

Jaribu kunileta utetezi kwa hoja zangu nilizoziweka hapo kwenye mada si kimipasho vile ufanyavyo ndugu yangu. Nchi hii ni yetu sote na waadhirika kama leto mmoja katika familia yako hayajampata ipo siku tageuka na kuikumbuka hoja yangu na kuthamini utaifa zaidi ya itikadi.
 
Nimeshangaa kuto mwana Wasira na Mwema viongozi ambao mara nyingi wako karibu mno na Kikwete katika matuko mbalimbali. Hata Emmanuel Nchimbi naye sijui alijificha wapi.

US-NSA wanajua kila kitu, kifupi ni kwamba nchi iko uchi.
 
Naomba tuwe wazi Mkuu Candid Scope,

Unataka kusema kuwa Tanzania ina uwezo wa kufikia US Intelligence? Habari za Obama na Usalama kuwa mikononi mwa The US Intelligence zimekua ni habari ulizozisikia sana Tanzania sababu ni nchi yako una access ya kila habari inayotolewa. Pia na udhaifu wa baadhi ya Waandishi kushabikia na kuweka headlines katika hilo katika Obama's visit katika vitu viiingi ambavyo si msingi badala ya yale yenye msingi na yenye manufaa kwa maslahi ya nchi.

Ni aibu sana... Wananchi Uzalendo haupo kabisa, mtu anajitazama yeye na Chama anacho shabikia. Raisi anatoa hotuba badala ya kujadili kile anacho ongea rais kama kina mantiki ama hakina mtu anajadili kiingereza Kibovu. So Sad. Mwambie sasa yeye aongee Kiingereza.

Imefika wakati suala linapo husu taifa la Tanzania liangaliwe kwa Uzalendo na Upendo juu ya nchi na si kwa Unafiki na Ubinafsi. Kuna suala ambalo wengi wanajidanganya juu ya sifa ya Tanzania.... Mtu anadhani kuwa Tanzania ikiongelewa vibaya pamoja na Serikali basi CCM ndiyo inachekwa! Si kweli... Sikilizeni vyombo vya habari, hakuna anae jua CCM ni nini Ki mataifa hasa nchi za Ughaibuni! Wao wanajua kuwa Tanzania ni nini.

Baadhi ya watu/taasisi/Wanaharakati/Wanasiasa wamekosa misimamo na mbaya zaidi kudhihirisha ubinafsi wa hali ya juu! Serikali ya Kikwete na CCM in general ni wazi imeshindwa kuingozoa nchi. Kikwete amekuwa akisemwa, tukanwa, kashifiwa kwa safari za ovyo ovyo kuwa anajipendekeza... Wakati hapo hapo wao Wasemaji, Watukanaji na watoa Kashfa wanawapongeza the other side kwa kwenda kulia nje ya nchi jinsi Kikwete na Serikali yake inashindwa kuiongoza nchi. Haya ni kati ya makundi pakee ambayo yanaweza kuwa mkombozi wa Mtanzania ambaye hajui hata pa kuanzia kuweza kuikomboa nchi... Hapo kuna matumaini kweli?

It is time Upinzani uache kushindana na CCM, It is time waache kuingia kwenye mitego wazi, Maana sasa hivi inakuwa kama wote wapo sawa na tofauti ni kuwa tu CCM ina nguvu ya dola na Jeshi la polisi na Upinzani hawana.

Ujio wa Obama kuna ya Msingi ambayo inapaswa kuhoji, kujadili na kuelewa. BUT habari zilizo jaa ni ambazo tayari zimepita na wala hazina tija; habari zimejaa za - Obama ndege yake hivi, Malia Obama kabinti kazuri sana, Obama na Jk wacheza mpira, Obama hivi, Obama vile, Obama pale na Obama kibao!

Muda umefika sasa wa kuweka hayo pembeni na kutafakari Ujio wa Rais ambaye anakuwa Considered wa dunia kaja hapa Tanzania. What do we expect? Kikwete anatuambia nini? Wamekubaliana nini? Sisi Watanzania tunanufaika vipi? Na kutulia na kutafakari ile Conference Ikulu was it what it seems to be?

Tujenge nchi jamani... Nchi haijengwi na viongozi pekee bali na wananchi pia.
 
Serikali ya kipumbavu na watawala wake wapumbavu

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
...hata kama ni mimi ndo ningelikuwa nahusika na usalama wa raisi Obama,siwezi kuliamini jeshi linalo safirisha bangi,pembe za ndovu...jeshi linalo wababikizia raia kesi za fuvu la binadam...jeshi lililoshidwa hata kumwona twiga akitoloshwa kwa ndege pamoja na urefu na ukubwa wake...jeshi linalo ng'oa watu kucha,meno na kuwatoboa macho...jeshi lililoshindwa kuzuia wizi wa mabilioni ya pesa benki kuu(EPA) na kushidwa kujua mafisadi walioficha pesa nchi za nje(USWIS)...jeshi linalotumika kama kiwanda cha kutengeneza kesi kuwakandamiza watu wenye mawazotofauti na serikali...jeshi linalopokea na kutekeleza mawazo ya "M.P.u.m.b.a.v.u" bila kupima hathari zake...KULIAMINI JESHI LA AINA HII INGELIKUWA NI KUWEKA REHANI YA USALAMA WA RAISI WA MAREKANI...
 
Kabla ya kuja Obama katika hizi nchi Za kiafrika, vyombo vya ulinzi na usalama vya marekani viliweka wazi kuwa ulinzi wa rais wao wataufanya wao kwa 100%, sasa hapo ww ulichoa andika ni kipi?.

Kuna thread aliiandika humu ndani mwanakijiji itafute uisome ndipo utajua ulicho andika ni ----- na ni craaaaaap ndani ya JF.

Ni mjinga tu anayeweza kutetea haya yaliyotekea sasa.Bush amewahi kuja,mkewe amekuja,Clinton amewahi kuja mbona hapo awali haikua hivyo?Na kwanini hadi mawaziri wachujwe?Usilete siasa kila mahali.Nchi hii kuna upuuzi mwingi sana unaoendelea na mnautetea kwa kila hali kulindsa matumbo yenu, badala ya kuangalia ustawi wa Taifa mnaangalia ustawi wa chama,na kupoteza nuda mwingi kupambana na wapinzani badala ya kuangalia maendeleo yetu.
 
Kweli Watanzania tunahitaji kujiangalia upya kama watanzania wazalendo, mm nimefuatilia kwa karibu coverage ya vyombo vyetu vya habari tangu kuwasili kwa Obama mpaka anaondoka kwa kweli hakuna kipya kilichoripotiwa kwa minajili ya kumfanya Mwananchi kuelewa nini hasa kimezungumzwa na viongozi hao (maudhui ya ziara ya Obama) sanasana nimeishia kuelimishwa watu wengi wamejitokeza kumpokea Obama, mara eti kiingereza,mara Watanzania watumie fursa ya ziara ya obama,mke was Obama ameeleza yeye ni alikuwa maskini na upuuzi mwingine mwingi tu. Hakuna wakati ambapo nimepata kuudhika na utendaji wa vyombo vya Habari kama hizi siku mbili.WATANZANIA TUBADILIKE TUACHE UZUZU TUJADILI MAUDHUI YA SAFARI SIO SUTI WALIZOVAA, CHAKULA WALICHOKULA N.K vYOMBO VYETU VYA HABARI NA WAANDISHI WAHABARI MJISAHIHISHE NAMNA YA KURIPOTI HABARI ZENU ACHENI USHABIKI.
 
Nimeshangaa kuto mwana Wasira na Mwema viongozi ambao mara nyingi wako karibu mno na Kikwete katika matuko mbalimbali. Hata Emmanuel Nchimbi naye sijui alijificha wapi.
kwani Candid Scope unataka kusema ni lazima watu wote ambao ni viongozi kwenda kumwona Obama?? kumbuka kwamba wakati obama yupo pia viongozi wengine wa nchi za nje walikuwepo na walihitaj mwenyeji. mfano kulikuwa na GLOBAL 2013 SMART PARTNERSHIP na watu kama Mfalme Mswati, waziri mkuu wa Malysia, vice president wa Botswana etc sasa je unafikiri hawa hawakutakiwa kuwa na company?? nijuavyo kwa wakubwa kama hawa hata dinner hupangiwa watu wa kula nao so to me nafikri kutokuwepo kwa baadhi ya viongozi sishangai.

Nakupa mfano mdogo tu Chissano siku anakuja Obama alikuwa na Dinner na baadhi ya watu katika hotel aliyofikia na najua baadhi ya watu ambao walidine naye so usishangae sana juu ya hili.
 
Last edited by a moderator:
Ni mjinga tu anayeweza kutetea haya yaliyotekea sasa.Bush amewahi kuja,mkewe amekuja,Clinton amewahi kuja mbona hapo awali haikua hivyo?Na kwanini hadi mawaziri wachujwe?Usilete siasa kila mahali.Nchi hii kuna upuuzi mwingi sana unaoendelea na mnautetea kwa kila hali kulindsa matumbo yenu, badala ya kuangalia ustawi wa Taifa mnaangalia ustawi wa chama,na kupoteza nuda mwingi kupambana na wapinzani badala ya kuangalia maendeleo yetu.


Mkuu suala si kutetea... Suala ni kutambua nini wakati wake wa kujadili. Tupo hali mbaya ki nchi kuanza ku entertain masuala ambayo yanaweza kuwa na tija but si Msingi. Suala ni kuwa Wazalendo na kupunguza Ushabiki kwa vitu ambavyo vinatuathiri kama Watanzania bila kujalisha kuwa unashikilia Itikadi zipi na wala bila kujalisha chamba unachotoka! Tanzania kwanza, CHADEMA, CCM na Vyama vingine baadae!

Ukija suala la mifano ya Viongozi ambao wamewahi kuja nchini Ikiwemo Bush, Clinton na hata Bibi Clinton (Kama US Secretary of State). Hawa woote walikuja kabla ya event ya September 11. Baada ya terror hiyo iliyoshutua dunia na kuitikisa US Security imekuwa tight zaidi. Obama/US ina maadui zaidi (hiyo ni sababu ndani ya sababu za msingi), Technology na Science imekua na haichagui kuwa unaitumia kwa niya njema ama wewe ni gaidi.

Sasa hapo yapaswa kujiuliza.... Kunani? Clinton, Bush, na sasa Obana (tena na Bush) wamekuja katika hii nchi. We have to stop underestimating the power of our nation! [On top of Xi Jimping rais wa nchi ambayo inakuwa kwa kasi na ni tishio kwa US alikuja hapa] tha Kuna maswali ya msingi yanahitaji majibu na majibu so far mimi toka nimeanza kusoma articles hakuna yanayo ridhisha...

So inabaki kuwa tuanze kuhoji masuala ya Msingi ambayo yatakuwa na manufaa sisi kama Watanzania an Tanzania.
 
AshaDii nakubaliana na wewe ka sehemu kubwa lakini ningependa kuweka angalizo moja kwa faida yako na kwa faida ya watanzania wenzangu.

Tumefika hapo tulipo leo kwa sababu ya serikali ya CCM, kwamba kila wanachokifanya wanakifanya kwa kofia ya CCM hata masuala ambayo ni ya kitaifa ambayo hayahitaji kuyavika kofia ya chama wao wanayavika kofia ya uchama.

Serikali hii ya Kikwete imefika mahali imetengeneza uadui kati ya watanzania kwa misingi yao ya itikadi za kidini na kisiasa.Kama wanasiasa wa ccm wameamua kuwachukulia wanachama wa vyama vya upinzani kuwa ni second class citizens, kwa uhakika hawa watu hawawezi kukubvali kirahisi kuwa second class citizens, ni lazima wapiganie haki yao ya utanzania na ubinadamu wao.

Katika mazingira kama haya ambayo viongozi wa serikali pamoja na chama tawala wanatugawa kiasi hiki cha kupandikiza chuki za kidini na kisiasa hata mara moja tusitegemee kuwa na taifa lenye watu wenye uzalendo na nchi yao, zaidi tunajenga taifa la watu wenye uzalendo na vyama vyao, watu wenye uzalendo na dini zao, watu wenye uzalendo na makabila yao kwakuwa serikali na chama tawala wameamua kututambulisha hivyo.

Kama kweli tunataka tuwe na nchi yenye mshikamano ambayo sote tutajivunia kuwa wazalendo kwa nchi yetu na tutamheshimu na kumuunga mkono raisi ama waziri kutoka katika chama chochote cha siasa, ni lazima viongozi wa serikali na chama tawala wabadilike kifikra na kuwajali wananchi wote katika usawa. Haiingii akilini kuona watu tunabaguliwa wazi wazi kwa sababu tu ya misimamo yetu ya kisiasa ambayo ni haki yetu ya kikatiba.

Kwanini mikutano ya CHADEMA na CUF ivamiwe na jeshi la polisi na kupiga wananchi wasiokuwa na hatia na wasiofanya vurugu yoyote? ni kwanini jeshi la polisi liwapige waandamanaji wasiokuwa na hata kisu kwa risasi za moto na kuwaua? ni kwanini mikutano ya CHADEMA inavurugwa na polisi na kisha kuua wananchi wasio na hatia kisha jeshi la polisi linakimbilia kwenye vyombo vya habari kufanya propaganda dhidi ya CHADEMA? Kama kweli CHADEMA wanahusika na matukio ya mauaji ya wananchi katika mikutano yao mbona hakuna hata kiongozi mmoja ama mwananchama mmoja wa CHADEMA aliyeshitakiwa kwa mauaji ya Ally Zona Morogoro? mbona hakuna mwanaCHADEMA aliyeshitakiwa kwa mauaji ya Mwangosi Iringa?

Unaweza kuniambia imekuwaje viongozi na wanachadema wameshinda kesi ya mkusanyiko usio halali uliofanyika Nyololo Iringa?unaweza kuniambia imekuwaje wana-CHADEMA wameshinda kesi Ndago Singida? Unafikiri huu mfululizo wa viongozi na wanachama wa CHADEMA kufunguliwa kesi za kugushi na serikali ya CCM unaweza kuwaacha wana-CHADEMA wakiwa na uzalendo kwa nchi yao? unadhani hali hii ya kuwapiga risasi za moto wana-CHADEMA katika mkutano wa kufunga kampeni Arusha unaweza kuwaacha wanachadema wakiwa na uzalendo kwa nchi yao? hapa ni lazima tuuseme ukweli bila kutafuna maneno "HAKUNA UZALENDO KAMA SERIKALI YA CCM HAIWATENDEI HAKI WANANCHI WAKE HASA WANAOUNGA MKONO VYAMA VYA UPINZANI".

Tunashuhudia sasa JWTZ nao wakiwa wameingizwa katika mkumbo wa kutumiwa na wanasiasa. Wakati tunapambana kutaka vyombo vya ulinzi na usalama kama polisi na usalama wa taifa waache kutumika kisiasa, ghafla tunashuhudia na JWTZ ambayo angalau wananchi walikuwa na imani nayo sasa imeanza kufanya mambo ya kisiasa, inateka wananchi nankwenda kuwatesa,tumeshuhudia viongozi wakubwa wa cuf walivyotekwa na kuteswa, pia imeripotiwa kwamba hawa jamaa wa JWTZ wamevuka mipaja hata kufikia hatua ya kuwabaka akina mama wa kitanzania wasiokuwa na hatia yoyote.

Raisi Kikwete amewahi kunukuliwa akiwaambia wanaccm sasa wawe tayari kukabiliana na wapinzani na wasitegemee kusaidiwa na jeshi la polisi. Hivi karibuni waziri mkuu Pinda amesema wao viongozi (wa CCM na serikali) wamechoka sasa wanalitaka jeshi la polisi liwapige an liendelee kuwapiga wananchi wasiokubaliana na matakwa yao watawala. Je huo ndio utawala wa kisheria wanaouhubiri kila siku? je hayo ndio matamko ya kujenga na kuimarisha uzalendo wa watanzania?

Nimalizie kwa kusema kwamba uzalendo wa watanzania kwa nchi yetu utaendelea kumomonyoka hadi hapo viongozi wetu watakapojitambua na kutambua thamani ya kuwa na taifa lenye mshikamano na upendo, lakini kwakuwa wanafanya hivi iki kujihakikishia kuendelea madarakani basi na sisi wengine tulipo upande wa upinzani ni lazima tuendelee kupambana hadi hapo haki zetu za kiraia zitakapoheshimiwa na watawala waliopo.

Na kwa kumalizia hoja ya Candid Scope juu ya wamarekani kujitwalia shughuli za ulinzi kwa raisi wao, mojawapo ya sababu ninayoifikiria mimi ni hizi kesi za kutunga za ugaidi zinazofunguliwa na serikali ya CCM dhidi ya CHADEMA. Vyombo vya habari vinapokuwa vinaripoti kuwa kuna kesi za ugaidi nchi basi wamerakani wanapata wasiwasi kuwa Tanzania si nchi salama tena kwahiyo wanalazimika kujichukulia majukumu yote ya ulinzi na usalam wa kiongozi wao.

Hawa jama zetu wa vyombo vya ulinzi na usala wa hapa nchini JWTZ, TISS na Polisi wao waendelee tu kupamba na CHADEMA kwakuwa ndiyo kazi waliyokabidhiwa na CCM kwa sasa huku wakisahau kabisa majukumu yao ya msingi ya ulinzi na usala kwa nchi yetu matokeo yake ni kudhalilishwa tu kwa viongozi wetu, kwamba hata mawaziri wetu hawaaaminiki hadi wanalazimika kukaguliwa na walinzi wa kimarejani kabla ya kuruhusiwa kuingia katika shughuli ya raisi Obama.
 
Kwa mimi binafsi, sikutegemea kama angekuja Obama Tanzania na Kova or whoever ndio akatoa vikosi vya maaskari kuwa karibu naye kwa ajili ya ulinzi wake. Je kwa nchi nyingine zozote ambako rais wa Marekani anatembelea ulinzi wa karibu unatoka kwa nchi inayotembelewa?

Kwa vyombo vya habari, hususani magazeti, nafikiri hawakukidhi mahitaji yetu waTZ kutueleimisha juu ya ujio huu hasa kwenye sekta ya kiuchumi. Kuna magazeti yalipamba karibu gazeti zima yakielezea undani wa habari za familia yake rather than faida na hasara za ujio wake.

Ambacho naona kina msingi sana, ni hoja yake ya kuwa maendeleo ya nchi za Afrika yataletwa na waafrika wenyewe na si vinginevyo. Mfano mzuri alipoongelea vita ya Kongo, kuwa ni wao wenyewe ndio watasema kuwa enough is enough. Na pia kuwa Marekani inataka tuanze kufanya kazi in the form of partnership, jamani kutoa grant kila siku inawezekana kuwa sasa wanachoka.

Hii ni pointi nzuri ya kuanzia kama viongozi wetu watabeba maneno hayo na kuyafanyia kazi.
 
kwani Candid Scope unataka kusema ni lazima watu wote ambao ni viongozi kwenda kumwona Obama?? kumbuka kwamba wakati obama yupo pia viongozi wengine wa nchi za nje walikuwepo na walihitaj mwenyeji. mfano kulikuwa na GLOBAL 2013 SMART PARTNERSHIP na watu kama Mfalme Mswati, waziri mkuu wa Malysia, vice president wa Botswana etc sasa je unafikiri hawa hawakutakiwa kuwa na company?? nijuavyo kwa wakubwa kama hawa hata dinner hupangiwa watu wa kula nao so to me nafikri kutokuwepo kwa baadhi ya viongozi sishangai.

Nakupa mfano mdogo tu Chissano siku anakuja Obama alikuwa na Dinner na baadhi ya watu katika hotel aliyofikia na najua baadhi ya watu ambao walidine naye so usishangae sana juu ya hili.

Kwahiyo IGP Saidi Mwema alikuwa anakula dinner na nani siku hiyo? akili mnazo lakini saa nyingine sijui mnazitumiaje...
 
Last edited by a moderator:
Kama ulikosa tathmini ya kitaalamu kheri ungenyamaza ulichoandika ni tathmini ya mbumbumbu
 
Naomba tuwe wazi Mkuu Candid Scope.....Tujenge nchi jamani... Nchi haijengwi na viongozi pekee bali na wananchi pia.

Kuhusu suala la ulinzi wa Marekani hapa kwetu hata usiliongelee.Hatuhitaji kuongelea kwa wenzetu kuliuaje.Tuna mifano ya ndaniBUsh ,aliwahi kuja,tena kipindi ambacho kilikua hatarishi,na alikaa siku nyingi zaidi,Clinton,Mama Bush,lakini vyombo vyetu vilishirikishwa kwa kila hali.Lakini safari hii,vimewekewa kando kabisa,hadi kufikia kutawala na Airport yetu halafu wewe unaona hali hii ni kawaida.Tuache hayo imefikia hadi wamarekani kuchuja mawaziri wewe unaona hilo ni kawaida?
Suala la kuhusu uzalendo hilo serkali ndiyo imeliharibu yenyewe kwa kutoweka mazingira sawa na haki katika kuendesha mambo yake.Kwamfano,suala la vyama vingi ni la kidemokrasia na tulilichagua wenyewe.Iweje inapokuwa wapinzani wakifanya mambo yao ,mpaka wapigwe ,wawekewe vigingi kama vile sio raia?yaani uwanyanyase watu kwa haki yao kwa sababu tu wanamtizamo tofauti na wewe, then utegemee wakuunge mkono kwenye mapungufu yako?Umoja na mshikamano unatakiwa utoke pande zote,raia kwa upande mmoja na serikali upande mwingine bila kujali ni wa upinzani au tawala.Imekua ni kawaida serikali kuwanyanyasa wapizani ,kana kwamba sio raia na hawachangii kodi ya maendeleo ya nchi hii ambayo serikali,au chama tawala kinajisifia ,wakati ni kodi zetu wenyewe.Ambazo viongozi wa nchi hii hawataki kuzilipa huku wakiendelea kujilimbikizia mali.Hivi unaweza kunijibu kwa nini viongozi nchi hii hawalipi kodi?Wakati nchi zilizoendelea sifa mojawapo ya kuwa kiongozi ni pamoja na Kulipa kodi?Kwani kodi ni tozo inayotokana na mapato halali.Hivyo linapofika suala la kodi kuanzia viongozi hadi raia ni lazima walipe kodi.Hii haipaswi kuwa na msamaha.

Kwa kifupi mazingira yaliyopo kwa sasa nchi hayaruhusu hayo unayoyataka,hayawezekani kwa sasa mpaka marekebisho ya nayopaswa yafanyike,ikiwa ni uhuru wa kujiamulia mambo yetu kama hatuvunji sheria.Ulichokua unakifanya hapa,ni kuuma na kupuliza na kujaribu kubalance maoni yako.
 
Blacklisted; Magaidi, nyara za serikali, pesa uswis, Wapigwe tu; haki za binadamu na demokrasia!? who knows?
 
Hivi mwwingulu Nchemba alialikwa kwenye tafrija ikulu?
 
Back
Top Bottom